< Luka 14 >

1 Ikawa siku moja Yesu alipokuwa amekwenda kula chakula kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo siku ya Sabato, watu walikuwa wakimchunguza kwa bidii.
Ühel hingamispäeval, kui Jeesus läks tuntud variseri koju sööma, jälgiti teda tähelepanelikult.
2 Papo hapo mbele yake palikuwa na mtu mmoja mwenye ugonjwa wa kuvimba mwili.
Tema ees oli üks mees, kes kannatas vesitõve käes.
3 Yesu akawauliza wale Mafarisayo na walimu wa sheria, “Je, ni halali kuponya watu siku ya Sabato au la?”
Jeesus küsis variseridelt ja kirjatundjatelt: „Kas hingamispäeval tohib tervendada või mitte?“
4 Wakakaa kimya. Hivyo Yesu akamshika yule mgonjwa mkono na kumponya, akamruhusu aende zake.
Nemad aga vaikisid. Ta puudutas meest, tegi ta terveks ja saatis ära.
5 Kisha akawauliza, “Kama mmoja wenu angekuwa na mtoto au ngʼombe wake aliyetumbukia katika kisima siku ya Sabato, je, hamtamvuta mara moja na kumtoa?”
Siis ta küsis neilt: „Kui teist kellegi poeg või härg kukub kaevu hingamispäeval, kas te siis ei tõmba teda kohe välja?“
6 Nao hawakuwa na la kusema.
Ja neil ei olnud midagi öelda.
7 Alipoona jinsi wageni walivyokuwa wanachagua mahali pa heshima wakati wa kula, akawaambia mfano huu:
Kui ta märkas külalisi laua ääres aulisemaid istekohti valimas, rääkis ta neile tähendamissõna:
8 “Mtu akikualika arusini, usikae mahali pa mgeni wa heshima kwa kuwa inawezekana amealikwa mtu mheshimiwa kuliko wewe.
„Kui sind keegi kutsub pulma, ära võta endale aulist kohta, sest võib-olla on keegi kutsutu sinust auväärsem.
9 Kama mkifanya hivyo yule aliyewaalika ninyi wawili atakuja na kukuambia, ‘Mpishe huyu mtu kiti chako.’ Ndipo kwa aibu utalazimika kukaa katika nafasi ya chini kabisa.
Ja siis tuleb peremees, kes teid mõlemaid kutsus, sinu juurde ja ütleb: „Anna koht temale!“Ja sa pead häbistatuna võtma kõige viimase koha.
10 Badala yake, unapoalikwa, chagua nafasi ya chini, ili yule mwenyeji wako atakapokuona atakuja na kukuambia, ‘Rafiki yangu, nenda kwenye nafasi iliyo bora zaidi.’ Kwa jinsi hii utakuwa umepewa heshima mbele ya wageni wenzako wote.
Aga kui sa oled kutsutud, siis võta kõige tagasihoidlikum koht, et kui peremees tuleb ja sulle ütleb: „Sõber, tule paremale kohale!“, siis sind austatakse kõigi teiste külaliste juuresolekul.
11 Kwa maana kila mtu ajikwezaye atashushwa, naye ajishushaye atakwezwa.”
Sest igaüht, kes ennast ise ülendab, alandatakse, ja kes ennast ise alandab, seda ülendatakse!“
12 Kisha Yesu akamwambia yule aliyewaalika, “Uandaapo karamu ya chakula cha mchana au cha jioni, usialike rafiki zako au ndugu zako au jamaa zako au majirani zako walio matajiri tu. Ukifanya hivyo, wao nao wanaweza kukualika kwao, nawe ukawa umelipwa kile ulichofanya na kupata thawabu yako.
Siis ütles Jeesus oma võõrustajale: „Kui sa pakud lõuna- või õhtusööki, siis ära kutsu oma sõpru, vendi ja õdesid, sugulasi või rikkaid naabreid, sest kui sa seda teed, võivad nad tasuks sind vastu kutsuda.
13 Bali ufanyapo karamu, waalike maskini, vilema na vipofu,
Vaid kui sa pakud pidusööki, siis kutsu vaeseid ja vigaseid ja jalutuid ja pimedaid,
14 nawe utabarikiwa kwa sababu hawa hawana uwezo wa kukulipa. Mungu atakulipa wakati wa ufufuo wa wenye haki.”
ja sa saad õnnistatud. Sest nemad ei saa sulle tasuda, vaid see tasutakse sulle õigete ülestõusmisel.“
15 Mmoja wa wale waliokuwa pamoja naye mezani aliposikia hivi akamwambia Yesu, “Amebarikiwa mtu yule atakayekula katika karamu ya Ufalme wa Mungu!”
Kui aga üks nendest lauas istujatest seda kuulis, ütles ta Jeesusele: „Õnnistatud on see, kes sööb pidulauas Jumala riigis!“
16 Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anaandaa karamu kubwa, akaalika watu wengi.
Jeesus vastas: „Üks mees valmistas suure pidusöögi ja kutsus palju külalisi.
17 Wakati wa karamu ulipofika, akamtuma mtumishi wake akawaambie wale walioalikwa, ‘Karibuni, kila kitu ki tayari sasa.’
Määratud tunnil saatis ta sulased kutsutuile ütlema: „Tulge! Kõik on valmis!“
18 “Lakini wote, kila mmoja, wakaanza kutoa udhuru: Wa kwanza akasema, ‘Nimenunua shamba, lazima niende kuliona. Tafadhali niwie radhi.’
Aga nemad kõik hakkasid vabandama. Esimene ütles: „Ma just ostsin põllu ja pean minema seda vaatama. Palun vabanda!“
19 “Mwingine akasema, ‘Ndipo tu nimenunua jozi tano za ngʼombe wa kulimia, nami ninakwenda kuwajaribu, tafadhali niwie radhi.’
Teine ütles: „Ma just ostsin viis paari härgi ja lähen neid proovima. Palun vabanda mind!“
20 Naye mwingine akasema, ‘Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.’
Ja veel üks ütles: „Ma just abiellusin ega saa tulla!“
21 “Yule mtumishi akarudi, akampa bwana wake taarifa. Ndipo yule mwenye nyumba akakasirika, akamwagiza yule mtumishi wake, akisema, ‘Nenda upesi kwenye mitaa na vichochoro vya mjini uwalete maskini, vilema, vipofu na viwete.’
Siis sulane tuli tagasi ja teatas sellest peremehele. Majaperemees vihastas ja ütles sulasele: „Mine ruttu linna väljakutele ja tänavatele ja too siia vaesed, vigased, pimedad ja jalutud!“
22 “Yule mtumishi akamwambia, ‘Bwana, yale uliyoniagiza nimefanya, lakini bado ipo nafasi.’
„Isand, “ütles sulane, „mis sa käskisid, on tehtud, aga veel on ruumi.“
23 “Ndipo yule bwana akamwambia mtumishi wake, ‘Nenda kwenye barabara na vijia vilivyoko nje ya mji na uwalazimishe watu waingie ili nyumba yangu ipate kujaa.
Ja peremees ütles: „Mine välja teedele ja radadele ja veena inimesi tulema, et mu maja oleks täis!“
24 Kwa maana nawaambia, hakuna hata mmoja wa wale walioalikwa atakayeionja karamu yangu.’”
Ma ütlen teile, ükski kutsutuist ei saa minu pidusööki maitsta!“
25 Umati mkubwa wa watu ulikuwa ukisafiri pamoja na Yesu, naye akageuka, akawaambia,
Jeesust saatis suur rahvahulk. Ta ütles nende poole pöördudes:
26 “Mtu yeyote anayekuja kwangu hawezi kuwa mwanafunzi wangu kama hatanipenda mimi zaidi ya baba yake na mama yake, mke wake na watoto wake, ndugu zake na dada zake, naam, hata maisha yake mwenyewe.
„Kui keegi minu juurde tuleb ega vihka oma isa ja ema, naist ja lapsi, vendi ja õdesid, ega tõepoolest ka omaenese elu, see ei saa olla minu jünger.
27 Yeyote asiyeuchukua msalaba wake na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
Kes ei kanna oma risti ega järgne mulle, ei saa olla minu jünger.
28 “Ni nani miongoni mwenu ambaye kama anataka kujenga nyumba, hakai kwanza chini na kufanya makisio ya gharama aone kama ana fedha za kutosha kukamilisha?
Kui keegi teie seast tahaks ehitada torni, kas ta ei istuks esmalt maha, et arvutada välja maksumus, ja kas tal selle lõpetamiseks raha jätkub?
29 La sivyo, akiisha kuweka msingi, naye akiwa hana uwezo wa kuikamilisha, wote waionao wataanza kumdhihaki,
Sest kui ta rajab vundamendi, aga ei suuda ehitust lõpetada, hakkab igaüks seda nähes teda pilkama:
30 wakisema, ‘Mtu huyu alianza kujenga lakini hakuweza kukamilisha.’
„See mees hakkas ehitama, aga ei suutnud lõpetada!“
31 “Au ni mfalme gani atokaye kwenda kupigana vita na mfalme mwingine, ambaye hakai chini kwanza na kufikiri iwapo akiwa na jeshi la watu 10,000 ataweza kupigana na yule anayekuja na jeshi la watu 20,000?
Või kui kuningas läheb sõtta teise kuninga vastu. Eks ta siis istu esmalt maha ja mõtle, kas ta on võimeline minema kümne tuhandega selle vastu, kes talle peale tuleb kahekümne tuhandega?
32 Kama hawezi, basi wakati yule mwingine akiwa bado yuko mbali, yeye hutuma ujumbe wa watu na kuomba masharti ya amani.
Ja kui ta ei ole võimeline, eks ta läkita saadikuid paluma rahutingimusi, kui vastane on veel kaugel.
33 Vivyo hivyo, yeyote miongoni mwenu ambaye hawezi kuacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
Samamoodi ei saa ükski teie seast, kes ei loobu kõigest, mis tal on, olla minu jünger.
34 “Chumvi ni nzuri, lakini chumvi ikiwa imepoteza ladha yake, itafanywaje ili iweze kukolea tena?
Sool on küll hea, aga kui sool kaotab maitse, kuidas siis sellele maitse tagasi anda?
35 Haifai ardhi wala kwa lundo la mbolea, bali hutupwa nje. “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
See ei kõlba mulda ega sõnnikuhunnikusse. See visatakse ära. Kel kõrvad on kuulda, see kuulgu!“

< Luka 14 >