< Luka 13 >

1 Wakati huo huo, kulikuwa na watu waliomwambia Yesu habari za Wagalilaya ambao Pilato aliwaua, na damu ya hao watu akaichanganya na dhabihu yao waliyokuwa wanatoa.
Now some were present at the same time who informed him about the Galileans whose blood Pilate mingled with their sacrifices.
2 Yesu akawauliza, “Mnadhani kwamba hawa Wagalilaya ambao walikufa kifo cha namna hiyo walikuwa na dhambi kuwazidi Wagalilaya wengine wote?
And having answered, Jesus said to them, Do ye suppose that these Galileans became sinful above all the Galileans because they have suffered such things?
3 La hasha! Ninyi nanyi msipotubu, mtaangamia vivyo hivyo.
I tell you, no, but if ye do not repent, ye will all perish similarly.
4 Au wale watu kumi na wanane waliokufa walipoangukiwa na mnara huko Siloamu: mnadhani wao walikuwa waovu kuliko watu wote waliokuwa wanaishi Yerusalemu?
Or those eighteen upon whom the tower in Siloam fell and killed them. Do ye think that these became debtors above all the men who dwell in Jerusalem?
5 Nawaambia, la hasha! Ninyi nanyi msipotubu, wote mtaangamia vivyo hivyo.”
I tell you, no, but if ye do not repent, ye will all likewise perish.
6 Kisha Yesu akawaambia mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini uliopandwa katika shamba lake la mizabibu, akaja ili kutafuta tini kwenye mti huo, lakini hakupata hata moja.
And he spoke this parable. A certain man had a fig tree planted in his vineyard, and he came seeking fruit on it, and found none.
7 Hivyo akamwambia mtunza shamba: ‘Tazama, kwa muda wa miaka mitatu sasa nimekuwa nikija kutafuta matunda kwenye mtini huu, nami sikupata hata moja. Ukate! Kwa nini uendelee kuharibu ardhi?’
And he said to the vine workman, Behold, three years I come seeking fruit on this fig tree, and find none. Cut it down, why also waste the ground?
8 “Yule mtunza shamba akamjibu, ‘Bwana, uache tena kwa mwaka mmoja zaidi, nami nitaupalilia na kuuwekea mbolea.
And having answered, he says to him, Sir, allow it this year also until I may dig around it and cast manure.
9 Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vyema, la sivyo uukate.’”
Although surely it should bear fruit, and if not, in the coming year thou will cut it down.
10 Basi Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo siku ya Sabato.
And he was teaching in one of the synagogues on the sabbath day.
11 Wakati huo huo akaja mwanamke mmoja aliyekuwa na pepo mchafu, naye alikuwa amepinda mgongo kwa muda wa miaka kumi na minane, wala alikuwa hawezi kunyooka wima.
And behold, there was a woman who had a spirit of infirmity eighteen years. And she was bent over, and not being able to straighten up completely.
12 Yesu alipomwona, akamwita, akamwambia, “Mwanamke, uwe huru, umepona ugonjwa wako.”
And when Jesus saw her, he called out, and said to her, Woman, thou are loosed from thine infirmity.
13 Yesu alipomwekea mikono yake, mara akasimama wima akaanza kumtukuza Mungu.
And he laid his hands upon her, and immediately she was made straight, and glorified God.
14 Lakini kiongozi wa sinagogi akakasirika kwa sababu Yesu alikuwa ameponya mtu siku ya Sabato. Akaambia ule umati wa watu, “Kuna siku sita ambazo watu wanapaswa kufanya kazi. Katika siku hizo, njooni mponywe, lakini si katika siku ya Sabato.”
And having responded, the synagogue-ruler, being indignant because Jesus healed on the sabbath, answered and said to the multitude, There are six days in which he ought to work. Therefore coming in these, be healed, and not on the day of the sabbath.
15 Lakini Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Je, kila mmoja wenu hamfungulii ngʼombe wake au punda wake kutoka zizini akampeleka kumnywesha maji siku ya Sabato?
But the Lord therefore answered him and said, Ye hypocrites, does not each of you on the sabbath loose his ox or his donkey from the stall, and after leading away, give to drink?
16 Je, huyu mwanamke, ambaye ni binti wa Abrahamu, aliyeteswa na Shetani akiwa amemfunga kwa miaka yote hii kumi na minane, hakustahili kufunguliwa kutoka kifungo hicho siku ya Sabato?”
And ought not this woman, being a daughter of Abraham whom Satan has bound, lo, eighteen years, be loosed from this bond on the day of the sabbath?
17 Aliposema haya, wapinzani wake wakaaibika, lakini watu wakafurahi kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyoyafanya.
And as he said these things all those opposing him were shamed, and all the multitude rejoiced for all the glorious things that were done by him.
18 Kisha Yesu akauliza, “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaufananisha na nini?
And he said, What is the kingdom of God like, and to what will I compare it?
19 Umefanana na punje ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake. Nayo ikakua, ikawa mti nao ndege wa angani wakatengeneza viota vyao kwenye matawi yake.”
It is like a grain of a mustard plant, which having taken, a man cast into his own garden. And it grew and developed into a great tree, and the birds of the sky lodged in the branches if it.
20 Yesu akauliza tena, “Nitaufananisha Ufalme wa Mungu na nini?
And again he said, To what will I compare the kingdom of God?
21 Unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”
It is like leaven that a woman having taken, hid in three measures of meal, until the whole was leavened.
22 Yesu akapita katika miji na vijiji, akifundisha wakati alisafiri kwenda Yerusalemu.
And he went through by cities and villages, teaching, and making a journey toward Jerusalem.
23 Mtu mmoja akamuuliza, “Bwana, ni watu wachache tu watakaookolewa?”
And a certain man said to him, Lord, are they few who are being saved? And he said to them,
24 Yesu akawaambia, “Jitahidini sana kuingia kupitia mlango mwembamba, kwa maana nawaambia wengi watajaribu kuingia, lakini hawataweza.
Compete to enter in by the narrow gate, because many, I say to you, will seek to enter in, and will not be able.
25 Wakati mwenye nyumba atakapoondoka na kufunga mlango, mtasimama nje mkibisha mlango na kusema, ‘Bwana! Tufungulie mlango!’ “Lakini yeye atawajibu, ‘Siwajui ninyi, wala mtokako.’
From the time the house-ruler has risen up, and has closed the door, and ye begin to stand outside, and to knock the door, saying, Lord, Lord, open to us, and having answered, he will say to you, I know not where ye are from,
26 “Ndipo mtamjibu, ‘Tulikula na kunywa pamoja nawe, tena ulifundisha katika mitaa yetu.’
then ye will begin to say, We ate and drank in thy presence, and thou taught in our thoroughfares.
27 “Lakini yeye atawajibu, ‘Siwajui ninyi, wala mtokako. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’
And he will say, I tell you, I know not where ye are from. Depart from me, all ye workmen of unrighteousness.
28 “Ndipo kutakuwako kilio na kusaga meno, mtakapowaona Abrahamu, Isaki, Yakobo na manabii wote wakiwa katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi mkiwa mmetupwa nje.
There will be the weeping and the gnashing of teeth, when ye will see Abraham and Isaac and Jacob and all the prophets in the kingdom of God, and you being thrust out.
29 Watu watatoka mashariki na magharibi, kaskazini na kusini, nao wataketi kwenye sehemu walizoandaliwa karamuni katika Ufalme wa Mungu.
And they will arrive from the east and west, and from the north and south, and will sit down in the kingdom of God.
30 Tazama, kunao walio wa mwisho watakaokuwa wa kwanza, nao wa kwanza watakaokuwa wa mwisho.”
And behold, there are last who will be first, and there are first who will be last.
31 Wakati huo huo baadhi ya Mafarisayo wakamwendea Yesu na kumwambia, “Ondoka hapa uende mahali pengine kwa maana Herode anataka kukuua.”
In the same day some Pharisees came, saying to him, Get thee out and depart from here, because Herod wants to kill thee.
32 Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie yule mbweha, ‘Ninafukuza pepo wachafu na kuponya wagonjwa leo na kesho, nami siku ya tatu nitaikamilisha kazi yangu.’
And he said to them, Having gone, say to this fox, Behold, I cast out demons and finish cures today and tomorrow, and the third day I am fully perfected.
33 Sina budi kuendelea na safari yangu leo, kesho na kesho kutwa: kwa maana haiwezekani nabii kufa mahali pengine isipokuwa Yerusalemu.
Nevertheless it is necessary for me to go today and tomorrow and the following, because it is not possible for a prophet to perish outside of Jerusalem.
34 “Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka!
O Jerusalem, Jerusalem, that kills the prophets, and stones those who are sent to her. How often I wanted to gather thy children together as a hen does her brood under her wings, and ye would not.
35 Tazama nyumba yenu imeachwa ukiwa. Ninawaambia, hamtaniona tena mpaka wakati ule mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana.’”
Behold, your house is left to you desolate. And I say to you, that ye will, no, not see me, until it will come when ye say, Blessed is he who comes in the name of the Lord.

< Luka 13 >