< Luka 12 >
1 Wakati huo, umati mkubwa wa watu maelfu, walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu akaanza kuzungumza kwanza na wanafunzi wake, akawaambia: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani, unafiki wao.
I kad čedinde pe nekobor hiljade manuša, edobor džene inele da jekh avere gazinde, o Isus prvo lelja te vaćeri ple učenikonenđe: “Arakhen tumen taro kvasco e farisejengoro, te na oven dujemujengere sar soi on.
2 Hakuna jambo lolote lililositirika ambalo halitafunuliwa, au lililofichwa ambalo halitajulikana.
Sa soi garavdo, ka otkrijini pe; sa soi tajno, ka šunđol.
3 Kwa hiyo, lolote mlilosema gizani litasikiwa nuruni. Na kile mlichonongʼona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa.
Adalese, sa so vaćerđen ani tomina, ka šunđol ano svetlost; hem so pohari vaćerđen ko kan ano sobe, ka vaćeri pe taro krovija sare te šunen.”
4 “Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, lakini baada ya hilo hawawezi kufanya lolote zaidi.
“Ali phenava tumenđe, amalalen: ma daran okolendar kola šaj te mudaren samo o telo, adalese so više adalestar naka šaj te ćeren tumenđe.
5 Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! (Geenna )
A ka phenav tumenđe kastar te daran: te daran taro Devel kas palo mudariba isi zoralipe te frdel ano pakao. Oja, vaćerava tumenđe, olestar te daran! (Geenna )
6 Mnajua kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti mbili? Lakini Mungu hamsahau hata mmoja wao.
Na biknena pe li pandž čiriklja zako samo duj najtikore kovanice? A palem nijekh olendar nane bisterdi anglo Devel.
7 Naam, hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
A tumenđei hem svako bal ko šero džendo. Adalese, ma daran! E Devlese injen po dragocena negoli but čiriklja!”
8 “Ninawaambia kwamba yeyote atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri mbele za malaika wa Mungu.
“A vaćerava tumenđe: Svako kova anglo manuša ka priznajini dai mlo, me, o Čhavo e manušesoro, anglo anđelja e Devlesere ka priznajinav dai ov mlo.
9 Lakini yeye atakayenikana mimi mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkana mbele ya malaika wa Mungu.
A te odrekninđa pe neko mandar anglo manuša, hem me ka odrekninav man olestar anglo anđelja e Devlesere.
10 Naye kila atakayenena neno baya dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
I te vaćerđa neko lafi protiv o Čhavo e manušesoro, ka ovel lese oprostime; ali naka ovel oprostime okolese kova hulini upro Sveto Duho.
11 “Watakapowapeleka katika masinagogi, na mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema.
A kad ka anen tumen anglo sudo ko sinagoge, anglo vladarija hem o vlastija, ma oven zabrinuta sar hem soja te braninen tumen, so te vaćeren!
12 Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati huo huo mnachopaswa kusema.”
Adalese so tegani o Sveto Duho ka sikaj tumen so te vaćeren.”
13 Mtu mmoja katika umati wa watu akamwambia Yesu, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane naye urithi wetu.”
Tegani neko oto narodo phenđa e Isusese: “Učitelju, vaćer mle phralese te podelini mancar o nasledstvo.”
14 Lakini Yesu akamwambia, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa hakimu wenu au msuluhishi juu yenu?”
A o Isus phenđa lese: “Manušeja, ko čhivđa man te ovav sudija ili delioco upra tumende?”
15 Ndipo Yesu akawaambia, “Jihadharini! Jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana maisha ya mtu hayatokani na wingi wa mali alizo nazo.”
Tegani phenđa sarijenđe: “Arakhen tumen hem ciden tumen tari pohlepa. I sa edobor barvalipe te ovel e manuše, lesoro dživdipe na avela oto adava so isi le.”
16 Kisha akawaambia mfano huu: “Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana.
Tegani o Isus phenđa lenđe akaja priča: “Nesave barvale manušesiri phuv bijanđa but.
17 Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’
I ov mislinđa pe ana peste: ‘So te ćerav? Nane man edobor baro than kote te čhivav mli žetva.’
18 “Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa ghala zangu za nafaka na kujenga nyingine kubwa zaidi na huko nitayahifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu.
I phenđa: ‘Akava ka ćerav! Ka peravav mle purane šupe hem ka vazdav po bare, i adathe ka čhivav sa o điv hem avera šukaripa.
19 Nami nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, unywe, ufurahi.”’
Tegani ka vaćerav mla dušaće: Isi tut baro barvalipe bute beršenđe. Odmorin, ha, pi hem uživin!’
20 “Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
Ali o Devel phenđa lese: ‘Hulavona! Akaja rat ka mere! A sa adava so spreminđan, kasoro ka ovel?’
21 “Hivyo ndivyo ilivyo kwa wale wanaojiwekea mali lakini hawajitajirishi kwa Mungu.”
Ađahari okolese kova pese čedela barvalipe, a čororoi anglo Devel.”
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini.
Tegani o Isus phenđa ple učenikonenđe: “Adalese vaćerava tumenđe: ma oven zabrinuta zako tumaro dživdipe: ka ovel tumen li so te han; ni zako tumaro telo: ka ovel tumen li so te urjaven.
23 Maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
Adalese soi o dživdipe po bitno e hajbnastar hem tumaroi telo po bitno e šejendar.
24 Fikirini ndege! Wao hawapandi wala hawavuni, hawana ghala wala popote pa kuhifadhi nafaka; lakini Mungu huwalisha. Ninyi ni wa thamani zaidi kuliko ndege!
Dikhen e gavranen! Ni sejinena ni čedena, nane len ni šupa kote te čhiven o điv, a palem o Devel parvari len. A tumen injen e Devlese po vredna e čirikljendar!
25 Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
A kova tumendar šaj adaleja so brinini pe te produžini hari plo dživdipe?
26 Kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini basi kuyasumbukia hayo mengine?
Znači te našti ni adava najhari te ćeren, sose onda brininena tumen zako bilo so aver?
27 “Angalieni maua jinsi yameavyo: Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
Dikhen o divlja luluđa sar barjona. Na ćerena buti, niti sivenafse šeja, a vaćerava tumenđe da ni o caro o Solomon, kova inele but barvalo, na inole edobor šuže šeja sar jekha olendar.
28 Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo, na kesho yanatupwa motoni, si atawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba!
Te o Devel ađahar šukar urjavela o biljke ko polje savei avdive adathe, a već tejsa frdena pe ani jag, kobor li više tumenđe ka del šeja, tikora verakere manušalen!
29 Wala msisumbuke mioyoni mwenu mtakula nini au mtakunywa nini. Msiwe na wasiwasi juu ya haya.
Tumen ma oven zabrinuta zako adava so ka han hem so ka pijen,
30 Watu wa mataifa ya duniani husumbuka sana kuhusu vitu hivi vyote, lakini Baba yenu anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
adalese so adava rodena okola kola na džanen e Devlese. Tumaro Dad, o Devel, džanel da valjani tumenđe sa adava.
31 Bali utafuteni Ufalme wa Mungu, na haya yote atawapa pia.
Nego roden o carstvo e Devlesoro, a ov ka del tumen sa adava so valjani tumenđe!
32 “Msiogope enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi Ufalme.
Ma daran, mlo tikoro stado! Tumare Dadesiri volja inele te del tumen o carstvo.
33 Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, mkajiwekee hazina mbinguni isiyokwisha, mahali ambapo mwizi hakaribii wala nondo haharibu.
Bikninen so isi tumen hem o pare den e čororenđe! Ćeren tumenđe kese zako pare save na properena hem barvalipe ko nebo savo nikad na tikorini. Niko naka šaj te avel adari te čorel tumaro barvalipe hem nijekh moljco naka uništini le.
34 Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo moyo wako utakapokuwa pia.
Adalese so tumaro vilo ka ovel adari kaj tumaro barvalipe.”
35 “Kuweni tayari mkiwa mmevikwa kwa ajili ya huduma na taa zenu zikiwa zinawaka,
O Isus ple učenikonenđe phenđa hem akava: “Oven spremna, urjavde zaki buti hem tumare svetiljke te oven tharde,
36 kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka kwenye karamu ya arusi, ili ajapo na kubisha mlango waweze kumfungulia mara.
sar sluge kola adžićerena ple gospodare te irini pe čhere taro bijav. Kad irini pe o gospodari hem kad khuvela ko udar, o slugei spremna te phraven lese.
37 Heri wale watumishi ambao bwana wao atakapokuja atawakuta wakiwa wanakesha. Amin, nawaambia, atajifunga mkanda wake na kuwaketisha ili wale, naye atakuja na kuwahudumia.
Blago okole slugenđe kolen o gospodari, kad ka avel, ka arakhi len sar adžićerena le džangale! Čače, vaćerava tumenđe, ov, o gospodari, ka phandel pe i kecelja, ka bešljaćeri len te han hem ka kandel len.
38 Itakuwa heri kwa watumwa hao ikiwa bwana wao atakapokuja atawakuta wamekesha hata kama atakuja mnamo usiku wa manane, au karibu na mapambazuko.
Blago e slugenđe kolen o gospodari ka arakhi džangalen čak hem te alo ki ekvaš i rat ili anglo disljojba.
39 Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angalijua saa mwizi atakuja, asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
Ali akava te džanen: te džanel ine o domaćini ko savo sati avela o čor, naka mukel lese ine te đerdini ko čher te čorel.
40 Ninyi nanyi hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.”
Hem tumen oven spremna, adalese so o Čhavo e manušesoro ka avel tegani kad na nadinena tumen!”
41 Ndipo Petro akamuuliza, “Bwana, mfano huu unatuambia sisi peke yetu au watu wote?”
Tegani o Petar pučlja e Isuse: “Gospode, vaćereja li akaja priča samo amenđe e učenikonenđe ili sarijenđe?”
42 Yesu akamjibu, “Ni yupi basi wakili mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamfanya msimamizi juu ya watumishi wake wote, ili awape watumishi wengine chakula chao wakati unaofaa?
O Gospod Isus phenđa: “Kovai, onda, verno hem mudro upravniko kas o gospodari ka čhivel upreder ple sluge te del len hajba ko vreme?
43 Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
Blago okole slugase kas lesoro gospodari, kad ka avel, ka arakhi sar ćerela ađahar.
44 Amin nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote.
Čače vaćerava tumenđe, upreder sa o barvalipe plo ka čhivel le sar upravniko.
45 Lakini kama yule mtumishi atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kurudi,’ kisha akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, na kula na kunywa na kulewa.
A te vaćerđa adava sluga ana peste: ‘Naka avel pana mlo gospodari’ i lela te marel avere slugen, hem te hal, te pijel hem te mačol,
46 Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wale wasioamini.
lesoro gospodari ka avel ano okova dive hem okova sati kad naka adžićeri le, ka čhinel le ko ekvaš hem ka čhivel le maškaro nevernici.
47 “Yule mtumishi anayefahamu vyema mapenzi ya bwana wake na asijiandae wala kufanya kama apendavyo bwana wake, atapigwa kwa mapigo mengi.
A okova sluga kova džanđa i volja ple gospodaresiri, a na inele spremno ili na ćerđa pali e gospodaresiri volja, but mariba ka hal.
48 Lakini yeyote ambaye hakujua naye akafanya yale yastahiliyo kupigwa, atapigwa kidogo. Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi; na yeyote aliyekabidhiwa vingi, kwake vitatakiwa vingi.
A okova kova na džanđa e gospodaresiri volja, a ćerđa nešto zako so zaslužini kazna, hari mariba ka hal. Kasei dindo but, but ka rodel pe lestar. Kasei poverime but, više ka rodel pe lestar.”
49 “Nimekuja kuleta moto duniani; laiti kama ungekuwa tayari umewashwa!
Tegani o Isus phenđa: “Aljum te frdav jag e sudosiri ki phuv. So bi mangava ine već te ovel thardi!
50 Lakini ninao ubatizo ambao lazima nibatizwe, nayo dhiki yangu ni kuu mpaka ubatizo huo ukamilike!
A valjani te nakhavav e patibnasoro krstiba. But maje pharo đikote adava na završini pe!
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? La, nawaambia sivyo, nimekuja kuleta mafarakano.
Mislinena da aljum te anav mir ki phuv? Na. Aljum te ćerav o manuša te ciden pe jekh averestar.
52 Kuanzia sasa, kutakuwa na watu watano katika nyumba moja, watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
Adalese od akana, oto pandž čherutne, trin ka oven ki mli strana, a duj ki aver ili duj ki mli strana, a trin ki aver.
53 Watafarakana baba dhidi ya mwanawe na mwana dhidi ya babaye, mama dhidi ya bintiye na binti dhidi ya mamaye, naye mama mkwe dhidi ya mkwewe na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.”
Ka uštel o dad upro čhavo hem o čhavo upro dad, i daj upri čhaj hem i čhaj upri daj, i sasuj upri bori hem i bori upri sasuj.”
54 Pia Yesu akauambia ule umati wa watu, “Mwonapo wingu likitokea magharibi, mara mwasema, ‘Mvua itanyesha,’ nayo hunyesha.
Tegani o Isus vaćerđa e narodose: “Kad dikhena da o oblaci avena taro zapad, tegani phenena da ka perel bršin, i čače perela.
55 Nanyi mwonapo upepo wa kusini ukivuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na joto,’ na huwa hivyo.
Kad phudela i barval taro jug, phenena da ka ovel tatipe, i ovela.
56 Enyi wanafiki! Mnajua jinsi ya kutambua kuonekana kwa dunia na anga. Inakuwaje basi kwamba mnashindwa kutambua wakati huu wa sasa?
Dujemujengere manušalen! Džanen te pendžaren o izgled e phuvjakoro hem e nebosoro; sar onda na džanen te pendžaren o znakija akale vremesere?
57 “Kwa nini hamwamui wenyewe lililo haki?
Tumen korkore valjani te pendžaren okova soi ispravno.
58 Uwapo njiani na mshtaki wako kwenda kwa hakimu, jitahidi kupatana naye mkiwa njiani. La sivyo, atakupeleka kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa afisa, naye afisa atakutupa gerezani.
Te neko legari tut ko sudo te tužini tut adalese so na irinđan lese o pare, odrumal de sa tutar te mirine tut oleja angleder nego so resena adari. Te na ćerđan ađahar, ov šaj te vucini tut anglo sudija, a o sudija ka del tut ko manuš kova ka čhivel tut ano phandlipe.
59 Nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.”
Vaćerava će da čače naka ikljove adathar sa đikote na irineja đi i zadnjo para.”