< Luka 12 >
1 Wakati huo, umati mkubwa wa watu maelfu, walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu akaanza kuzungumza kwanza na wanafunzi wake, akawaambia: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani, unafiki wao.
At which time the myriads of the multitude having been gathered together, so as to tread upon one another, he began to say unto his disciples, first, 'Take heed to yourselves of the leaven of the Pharisees, which is hypocrisy;
2 Hakuna jambo lolote lililositirika ambalo halitafunuliwa, au lililofichwa ambalo halitajulikana.
and there is nothing covered, that shall not be revealed; and hid, that shall not be known;
3 Kwa hiyo, lolote mlilosema gizani litasikiwa nuruni. Na kile mlichonongʼona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa.
because whatever in the darkness ye said, in the light shall be heard: and what to the ear ye spake in the inner-chambers, shall be proclaimed upon the house-tops.
4 “Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, lakini baada ya hilo hawawezi kufanya lolote zaidi.
'And I say to you, my friends, be not afraid of those killing the body, and after these things are not having anything over to do;
5 Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! (Geenna )
but I will show to you, whom ye may fear; Fear him who, after the killing, is having authority to cast to the gehenna; yes, I say to you, Fear ye Him. (Geenna )
6 Mnajua kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti mbili? Lakini Mungu hamsahau hata mmoja wao.
'Are not five sparrows sold for two assars? and one of them is not forgotten before God,
7 Naam, hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
but even the hairs of your head have been all numbered; therefore fear ye not, than many sparrows ye are of more value.
8 “Ninawaambia kwamba yeyote atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri mbele za malaika wa Mungu.
'And I say to you, Every one — whoever may confess with me before men, the Son of Man also shall confess with him before the messengers of God,
9 Lakini yeye atakayenikana mimi mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkana mbele ya malaika wa Mungu.
and he who hath denied me before men, shall be denied before the messengers of God,
10 Naye kila atakayenena neno baya dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
and every one whoever shall say a word to the Son of Man, it shall be forgiven to him, but to him who to the Holy Spirit did speak evil, it shall not be forgiven.
11 “Watakapowapeleka katika masinagogi, na mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema.
'And when they bring you before the synagogues, and the rulers, and the authorities, be not anxious how or what ye may reply, or what ye may say,
12 Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati huo huo mnachopaswa kusema.”
for the Holy Spirit shall teach you in that hour what it behoveth [you] to say.'
13 Mtu mmoja katika umati wa watu akamwambia Yesu, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane naye urithi wetu.”
And a certain one said to him, out of the multitude, 'Teacher, say to my brother to divide with me the inheritance.'
14 Lakini Yesu akamwambia, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa hakimu wenu au msuluhishi juu yenu?”
And he said to him, 'Man, who set me a judge or a divider over you?'
15 Ndipo Yesu akawaambia, “Jihadharini! Jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana maisha ya mtu hayatokani na wingi wa mali alizo nazo.”
And he said unto them, 'Observe, and beware of the covetousness, because not in the abundance of one's goods is his life.'
16 Kisha akawaambia mfano huu: “Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana.
And he spake a simile unto them, saying, 'Of a certain rich man the field brought forth well;
17 Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’
and he was reasoning within himself, saying, What shall I do, because I have not where I shall gather together my fruits?
18 “Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa ghala zangu za nafaka na kujenga nyingine kubwa zaidi na huko nitayahifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu.
and he said, This I will do, I will take down my storehouses, and greater ones I will build, and I will gather together there all my products and my good things,
19 Nami nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, unywe, ufurahi.”’
and I will say to my soul, Soul, thou hast many good things laid up for many years, be resting, eat, drink, be merry.
20 “Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
'And God said to him, Unthinking one! this night thy soul they shall require from thee, and what things thou didst prepare — to whom shall they be?
21 “Hivyo ndivyo ilivyo kwa wale wanaojiwekea mali lakini hawajitajirishi kwa Mungu.”
so [is] he who is treasuring up to himself, and is not rich toward God.'
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini.
And he said unto his disciples, 'Because of this, to you I say, Be not anxious for your life, what ye may eat; nor for the body, what ye may put on;
23 Maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
the life is more than the nourishment, and the body than the clothing.
24 Fikirini ndege! Wao hawapandi wala hawavuni, hawana ghala wala popote pa kuhifadhi nafaka; lakini Mungu huwalisha. Ninyi ni wa thamani zaidi kuliko ndege!
'Consider the ravens, that they sow not, nor reap, to which there is no barn nor storehouse, and God doth nourish them; how much better are ye than the fowls?
25 Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
and who of you, being anxious, is able to add to his age one cubit?
26 Kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini basi kuyasumbukia hayo mengine?
If, then, ye are not able for the least — why for the rest are ye anxious?
27 “Angalieni maua jinsi yameavyo: Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
'Consider the lilies, how do they grow? they labour not, nor do they spin, and I say to you, not even Solomon in all his glory was arrayed as one of these;
28 Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo, na kesho yanatupwa motoni, si atawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba!
and if the herbage in the field, that to-day is, and to-morrow into an oven is cast, God doth so clothe, how much more you — ye of little faith?
29 Wala msisumbuke mioyoni mwenu mtakula nini au mtakunywa nini. Msiwe na wasiwasi juu ya haya.
'And ye — seek not what ye may eat, or what ye may drink, and be not in suspense,
30 Watu wa mataifa ya duniani husumbuka sana kuhusu vitu hivi vyote, lakini Baba yenu anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
for all these things do the nations of the world seek after, and your Father hath known that ye have need of these things;
31 Bali utafuteni Ufalme wa Mungu, na haya yote atawapa pia.
but, seek ye the reign of God, and all these things shall be added to you.
32 “Msiogope enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi Ufalme.
'Fear not, little flock, because your Father did delight to give you the reign;
33 Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, mkajiwekee hazina mbinguni isiyokwisha, mahali ambapo mwizi hakaribii wala nondo haharibu.
sell your goods, and give alms, make to yourselves bags that become not old, a treasure unfailing in the heavens, where thief doth not come near, nor moth destroy;
34 Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo moyo wako utakapokuwa pia.
for where your treasure is, there also your heart will be.
35 “Kuweni tayari mkiwa mmevikwa kwa ajili ya huduma na taa zenu zikiwa zinawaka,
'Let your loins be girded, and the lamps burning,
36 kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka kwenye karamu ya arusi, ili ajapo na kubisha mlango waweze kumfungulia mara.
and ye like to men waiting for their lord, when he shall return out of the wedding feasts, that he having come and knocked, immediately they may open to him.
37 Heri wale watumishi ambao bwana wao atakapokuja atawakuta wakiwa wanakesha. Amin, nawaambia, atajifunga mkanda wake na kuwaketisha ili wale, naye atakuja na kuwahudumia.
'Happy those servants, whom the lord, having come, shall find watching; verily I say to you, that he will gird himself, and will cause them to recline (at meat), and having come near, will minister to them;
38 Itakuwa heri kwa watumwa hao ikiwa bwana wao atakapokuja atawakuta wamekesha hata kama atakuja mnamo usiku wa manane, au karibu na mapambazuko.
and if he may come in the second watch, and in the third watch he may come, and may find [it] so, happy are those servants.
39 Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angalijua saa mwizi atakuja, asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
'And this know, that if the master of the house had known what hour the thief doth come, he would have watched, and would not have suffered his house to be broken through;
40 Ninyi nanyi hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.”
and ye, then, become ye ready, because at the hour ye think not, the Son of Man doth come.'
41 Ndipo Petro akamuuliza, “Bwana, mfano huu unatuambia sisi peke yetu au watu wote?”
And Peter said to him, 'Sir, unto us this simile dost thou speak, or also unto all?'
42 Yesu akamjibu, “Ni yupi basi wakili mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamfanya msimamizi juu ya watumishi wake wote, ili awape watumishi wengine chakula chao wakati unaofaa?
And the Lord said, 'Who, then, is the faithful and prudent steward whom the lord shall set over his household, to give in season the wheat measure?
43 Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
Happy that servant, whom his lord, having come, shall find doing so;
44 Amin nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote.
truly I say to you, that over all his goods he will set him.
45 Lakini kama yule mtumishi atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kurudi,’ kisha akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, na kula na kunywa na kulewa.
'And if that servant may say in his heart, My lord doth delay to come, and may begin to beat the men-servants and the maid-servants, to eat also, and to drink, and to be drunken;
46 Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wale wasioamini.
the lord of that servant will come in a day in which he doth not look for [him], and in an hour that he doth not know, and will cut him off, and his portion with the unfaithful he will appoint.
47 “Yule mtumishi anayefahamu vyema mapenzi ya bwana wake na asijiandae wala kufanya kama apendavyo bwana wake, atapigwa kwa mapigo mengi.
'And that servant, who having known his lord's will, and not having prepared, nor having gone according to his will, shall be beaten with many stripes,
48 Lakini yeyote ambaye hakujua naye akafanya yale yastahiliyo kupigwa, atapigwa kidogo. Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi; na yeyote aliyekabidhiwa vingi, kwake vitatakiwa vingi.
and he who, not having known, and having done things worthy of stripes, shall be beaten with few; and to every one to whom much was given, much shall be required from him; and to whom they did commit much, more abundantly they will ask of him.
49 “Nimekuja kuleta moto duniani; laiti kama ungekuwa tayari umewashwa!
'Fire I came to cast to the earth, and what will I if already it was kindled?
50 Lakini ninao ubatizo ambao lazima nibatizwe, nayo dhiki yangu ni kuu mpaka ubatizo huo ukamilike!
but I have a baptism to be baptized with, and how am I pressed till it may be completed!
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? La, nawaambia sivyo, nimekuja kuleta mafarakano.
'Think ye that peace I came to give in the earth? no, I say to you, but rather division;
52 Kuanzia sasa, kutakuwa na watu watano katika nyumba moja, watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
for there shall be henceforth five in one house divided — three against two, and two against three;
53 Watafarakana baba dhidi ya mwanawe na mwana dhidi ya babaye, mama dhidi ya bintiye na binti dhidi ya mamaye, naye mama mkwe dhidi ya mkwewe na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.”
a father shall be divided against a son, and a son against a father, a mother against a daughter, and a daughter against a mother, a mother-in-law against her daughter-in-law, and a daughter-in-law against her mother-in-law.'
54 Pia Yesu akauambia ule umati wa watu, “Mwonapo wingu likitokea magharibi, mara mwasema, ‘Mvua itanyesha,’ nayo hunyesha.
And he said also to the multitudes, 'When ye may see the cloud rising from the west, immediately ye say, A shower doth come, and it is so;
55 Nanyi mwonapo upepo wa kusini ukivuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na joto,’ na huwa hivyo.
and when — a south wind blowing, ye say, that there will be heat, and it is;
56 Enyi wanafiki! Mnajua jinsi ya kutambua kuonekana kwa dunia na anga. Inakuwaje basi kwamba mnashindwa kutambua wakati huu wa sasa?
hypocrites! the face of the earth and of the heaven ye have known to make proof of, but this time — how do ye not make proof of [it]?
57 “Kwa nini hamwamui wenyewe lililo haki?
'And why, also, of yourselves, judge ye not what is righteous?
58 Uwapo njiani na mshtaki wako kwenda kwa hakimu, jitahidi kupatana naye mkiwa njiani. La sivyo, atakupeleka kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa afisa, naye afisa atakutupa gerezani.
for, as thou art going away with thy opponent to the ruler, in the way give diligence to be released from him, lest he may drag thee unto the judge, and the judge may deliver thee to the officer, and the officer may cast thee into prison;
59 Nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.”
I say to thee, thou mayest not come forth thence till even the last mite thou mayest give back.'