< Luka 12 >
1 Wakati huo, umati mkubwa wa watu maelfu, walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu akaanza kuzungumza kwanza na wanafunzi wake, akawaambia: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani, unafiki wao.
In the mean time, when the multitude was gathered together in myriads, so that they trod one upon another, he began to say to his disciples first, Beware of the leaven of the Pharisees, which is hypocrisy.
2 Hakuna jambo lolote lililositirika ambalo halitafunuliwa, au lililofichwa ambalo halitajulikana.
But there is nothing covered, that will not be revealed; and hid, that will not be known.
3 Kwa hiyo, lolote mlilosema gizani litasikiwa nuruni. Na kile mlichonongʼona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa.
Therefore, whatever ye have said in darkness, will be heard in the light; and what ye have spoken in the ear in closets, will be proclaimed upon the house-tops.
4 “Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, lakini baada ya hilo hawawezi kufanya lolote zaidi.
And I say to you my friends, Fear not those who kill the body, and after this can do nothing more.
5 Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! (Geenna )
But I will warn you whom to fear; fear him who after he hath killed hath power to cast into hell; yea, I say to you, fear him. (Geenna )
6 Mnajua kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti mbili? Lakini Mungu hamsahau hata mmoja wao.
Are not five sparrows sold for two pennies? and not one of them is forgotten before God.
7 Naam, hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
But even the hairs of your head are all numbered. Fear not: ye are of more value than many sparrows.
8 “Ninawaambia kwamba yeyote atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri mbele za malaika wa Mungu.
And I say to you, Every one that acknowledgeth me before men, him will the Son of man also acknowledge before the angels of God.
9 Lakini yeye atakayenikana mimi mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkana mbele ya malaika wa Mungu.
But he that hath denied me before men, shall be denied before the angels of God.
10 Naye kila atakayenena neno baya dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
And every one that shall speak a word against the Son of man, it will be forgiven him; but to him that hath blasphemed against the Holy Spirit, it will not be forgiven.
11 “Watakapowapeleka katika masinagogi, na mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema.
And when they bring you to the synagogues and the magistrates and the authorities, be not anxious as to how or what ye shall answer, or what ye shall say;
12 Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati huo huo mnachopaswa kusema.”
for the Holy Spirit will teach you in that very hour what ye ought to say.
13 Mtu mmoja katika umati wa watu akamwambia Yesu, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane naye urithi wetu.”
And one from the multitude said to him, Teacher, bid my brother divide the inheritance with me.
14 Lakini Yesu akamwambia, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa hakimu wenu au msuluhishi juu yenu?”
But he said to him, Man, who made me a judge or a divider over you?
15 Ndipo Yesu akawaambia, “Jihadharini! Jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana maisha ya mtu hayatokani na wingi wa mali alizo nazo.”
And he said to them, Take heed and beware of all covetousness; for even when one hath great abundance, his life doth not depend upon his possessions.
16 Kisha akawaambia mfano huu: “Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana.
And he spoke a parable to them, saying, The ground of a certain rich man brought forth plentifully.
17 Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’
And he thought within himself, saying, What shall I do? for I have not where to store my crops.
18 “Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa ghala zangu za nafaka na kujenga nyingine kubwa zaidi na huko nitayahifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu.
And he said, This will I do; I will pull down my barns, and build greater; and there will I store all my crops and my goods;
19 Nami nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, unywe, ufurahi.”’
and I will say to my soul, Soul, thou hast many goods laid up for many years; take thine ease, eat, drink, be merry.
20 “Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
But God said to him, Fool! this night will thy soul he required of thee; and whose will those things be which thou hast laid up?
21 “Hivyo ndivyo ilivyo kwa wale wanaojiwekea mali lakini hawajitajirishi kwa Mungu.”
So is he that layeth up treasure for himself, and is not rich towards God.
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini.
And he said to his disciples, Therefore I say to you, Be not anxious for the life, what ye shall eat; nor for the body, what ye shall put on.
23 Maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
The life is more than its food, and the body than its raiment.
24 Fikirini ndege! Wao hawapandi wala hawavuni, hawana ghala wala popote pa kuhifadhi nafaka; lakini Mungu huwalisha. Ninyi ni wa thamani zaidi kuliko ndege!
Consider the ravens, that they neither sow nor reap; which have neither store-house, nor barn; and God feedeth them. Of how much greater value are ye than the birds!
25 Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
And who of you can by anxious thought add a cubit to his life?
26 Kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini basi kuyasumbukia hayo mengine?
If then ye cannot do even that which is least, why are ye anxious about the rest?
27 “Angalieni maua jinsi yameavyo: Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
Consider the lilies, that they neither spin nor weave; and yet I say to you, Not even Solomon in all his glory was arrayed like one of these.
28 Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo, na kesho yanatupwa motoni, si atawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba!
But if God so clothes the herbage in the field, which is to-day, and tomorrow is cast into an oven, how much more will he clothe you, O ye of little faith!
29 Wala msisumbuke mioyoni mwenu mtakula nini au mtakunywa nini. Msiwe na wasiwasi juu ya haya.
And seek not ye what ye shall eat, and what ye shall drink; and be not of a doubtful mind.
30 Watu wa mataifa ya duniani husumbuka sana kuhusu vitu hivi vyote, lakini Baba yenu anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
For all these things do the nations of the world seek after; and your Father knoweth that ye have need of these things.
31 Bali utafuteni Ufalme wa Mungu, na haya yote atawapa pia.
But rather seek his kingdom, and these things will also be given you.
32 “Msiogope enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi Ufalme.
Fear not, little flock! for it is your Father's good pleasure to give you the kingdom.
33 Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, mkajiwekee hazina mbinguni isiyokwisha, mahali ambapo mwizi hakaribii wala nondo haharibu.
Sell what ye have, and give alms. Make for yourselves purses which wax not old, treasure in the heavens that faileth not, where no thief approacheth, nor moth destroyeth.
34 Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo moyo wako utakapokuwa pia.
For where your treasure is, there will your heart be also.
35 “Kuweni tayari mkiwa mmevikwa kwa ajili ya huduma na taa zenu zikiwa zinawaka,
Let your loins be girded about, and your lamps burning;
36 kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka kwenye karamu ya arusi, ili ajapo na kubisha mlango waweze kumfungulia mara.
and be yourselves like men waiting for the return of their lord from the wedding; that when he cometh and knocketh, they may open to him immediately.
37 Heri wale watumishi ambao bwana wao atakapokuja atawakuta wakiwa wanakesha. Amin, nawaambia, atajifunga mkanda wake na kuwaketisha ili wale, naye atakuja na kuwahudumia.
Happy are those servants, whom their lord when he cometh shall find watching; truly do I say to you, that he will gird himself, and place them at table, and will come and wait on them.
38 Itakuwa heri kwa watumwa hao ikiwa bwana wao atakapokuja atawakuta wamekesha hata kama atakuja mnamo usiku wa manane, au karibu na mapambazuko.
And if in the second, or if in the third watch, he cometh and findeth them thus, happy are they.
39 Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angalijua saa mwizi atakuja, asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
And be sure of this, that if the master of the house had known at what hour the thief was coming, he would not have suffered his house to be broken through.
40 Ninyi nanyi hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.”
Be ye also ready; for at an hour when ye think not the Son of man cometh.
41 Ndipo Petro akamuuliza, “Bwana, mfano huu unatuambia sisi peke yetu au watu wote?”
And Peter said to him, Lord, dost thou speak this parable to us, or also to all?
42 Yesu akamjibu, “Ni yupi basi wakili mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamfanya msimamizi juu ya watumishi wake wote, ili awape watumishi wengine chakula chao wakati unaofaa?
And the Lord said, Who then is the faithful, the wise steward, whom his lord will place over his household, to give the portion of food in due season?
43 Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
Happy is that servant whom his lord, when he cometh, shall find so doing.
44 Amin nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote.
I say to you in truth, that he will place him in charge of all his substance.
45 Lakini kama yule mtumishi atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kurudi,’ kisha akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, na kula na kunywa na kulewa.
But if that servant say in his heart, My lord is long in coming; and begin to beat the men-servants and maid-servants, and to eat and drink and be drunken,
46 Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wale wasioamini.
the lord of that servant will come in a day when he looketh not for him, and at an hour when he is not aware, and will cut him asunder, and appoint him his portion with the unfaithful.
47 “Yule mtumishi anayefahamu vyema mapenzi ya bwana wake na asijiandae wala kufanya kama apendavyo bwana wake, atapigwa kwa mapigo mengi.
And that servant who knew his lord's will, and did not make ready, nor do according to his will, will be beaten with many stripes;
48 Lakini yeyote ambaye hakujua naye akafanya yale yastahiliyo kupigwa, atapigwa kidogo. Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi; na yeyote aliyekabidhiwa vingi, kwake vitatakiwa vingi.
but he that knew not and did things worthy of stripes, will be beaten with few. And from every one to whom much hath been given, will much be required; and to whom much hath been entrusted, of him will the more be demanded.
49 “Nimekuja kuleta moto duniani; laiti kama ungekuwa tayari umewashwa!
I came to cast fire upon the earth; and what do I wish, if it hath been already kindled?
50 Lakini ninao ubatizo ambao lazima nibatizwe, nayo dhiki yangu ni kuu mpaka ubatizo huo ukamilike!
But I have a baptism to be baptized with; and how is my soul troubled, till it be accomplished!
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? La, nawaambia sivyo, nimekuja kuleta mafarakano.
Think ye that I came to give peace in the earth? I tell you, nay, but rather division.
52 Kuanzia sasa, kutakuwa na watu watano katika nyumba moja, watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
For from this time forth five in one house will be divided, three against two, and two against three.
53 Watafarakana baba dhidi ya mwanawe na mwana dhidi ya babaye, mama dhidi ya bintiye na binti dhidi ya mamaye, naye mama mkwe dhidi ya mkwewe na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.”
They will be divided, father against son, and son against father; mother against daughter, and daughter against mother; the mother-in-law against her daughter-in-law, and the daughter-in-law against her mother-in-law.
54 Pia Yesu akauambia ule umati wa watu, “Mwonapo wingu likitokea magharibi, mara mwasema, ‘Mvua itanyesha,’ nayo hunyesha.
And he said also to the multitudes, When ye see a cloud rising in the west, ye say at once, A shower is coming; and it is so;
55 Nanyi mwonapo upepo wa kusini ukivuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na joto,’ na huwa hivyo.
and when ye perceive the south wind blowing, ye say, It will be hot; and it cometh to pass.
56 Enyi wanafiki! Mnajua jinsi ya kutambua kuonekana kwa dunia na anga. Inakuwaje basi kwamba mnashindwa kutambua wakati huu wa sasa?
Hypocrites! ye know how to judge of the face of the earth and the sky; but how is it that ye know not how to judge of this time
57 “Kwa nini hamwamui wenyewe lililo haki?
And why even of yourselves do ye not judge what is right?
58 Uwapo njiani na mshtaki wako kwenda kwa hakimu, jitahidi kupatana naye mkiwa njiani. La sivyo, atakupeleka kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa afisa, naye afisa atakutupa gerezani.
When thou art going with thine adversary at law to the magistrate, take pains, while on the way, to be released by him; lest he drag thee to the judge, and the judge deliver thee to the officer, and the officer cast thee into prison.
59 Nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.”
I tell thee, Thou wilt not come out thence, till thou hast paid the very last mite.