< Luka 10 >
1 Baada ya hayo, Bwana akawachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawili wawili katika kila mji na kila sehemu aliyokusudia kwenda baadaye.
After that, the Lord Jesus appointed 72 other [people]. He [prepared to] send them out, two-by-two, to every town and village where he [SYN] intended to go.
2 Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini watendakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno.
He said to them, “The [people who are ready to receive my message] are like a field [of] [MET] [grain] that is ready for [people] to harvest {to be harvested}. But there are not many people [to bring them to God]. So pray and ask the Lord [God] to send [more] workers [who will gather people together and teach them my message, just like a landowner sends workers] into his fields [to gather the] harvest.
3 Haya! nendeni. Ninawatuma kama wana-kondoo katikati ya mbwa mwitu.
Start going; but [remember that] I am sending you [(pl)] out [to tell my message to people who will try to get rid of you. You will be] like lambs among wolves.
4 Msichukue mkoba, wala mfuko, wala viatu, na msimsalimu mtu yeyote njiani.
Do not take along [any money in] a purse. Do not take a traveler’s bag. Do not take [extra] sandals. Do not [spend a lot of time] greeting people along the way.
5 “Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza semeni, ‘Amani iwe kwenu.’
Whenever you enter a house [to lodge there], first say to those people, ‘May [God give inner] peace to [you people] [MTY] [in] this house!’
6 Kama kuna mtu wa amani humo, basi amani yenu itakuwa juu yake. La sivyo, itawarudia.
If people who [live] there [are (desiring to have]/worthy of receiving) [God’s] peace, they will experience the [inner] peace that you are [offering them]. If people who [live] there [are not desiring to have God’s] peace, you [will experience God’s inner] peace, [but they will not].
7 Kaeni katika nyumba hiyo, mkila na kunywa kile watakachowapa, kwa sababu kila mtendakazi anastahili malipo yake. Msihamehame kutoka nyumba hadi nyumba.
[If they welcome you], stay in that same house [until you leave that village]. Do not move around from one house to another. Eat and drink whatever they provide for you. A worker deserves to get pay [MET] [from the people for whom he works, so you deserve to receive food and a place to stay from the people to whom you go].
8 “Mkienda katika mji na watu wake wakawakaribisha, kuleni chochote kiwekwacho mbele yenu,
Whenever you enter a town and the people [there] welcome you, eat what is provided {what [they] provide} for you.
9 waponyeni wagonjwa waliomo na waambieni: ‘Ufalme wa Mungu umekaribia.’
Heal the people there who are sick. Tell them, ‘It is almost [time for] God to send his king to rule [MET] [your lives].’
10 Lakini mkiingia katika mji, nao hawakuwakaribisha, tokeni mwende katika barabara zake mkaseme:
But if you enter a town whose [people] do not welcome you, go into its [main] streets and say,
11 ‘Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu, tunayakungʼuta dhidi yenu. Lakini mjue kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.’
‘[Because you have refused to hear our message, we(exc) will not only leave], we will also shake off the dust of your town that clings to our sandals, to warn you [that God will reject/punish you]. But [we want you to know that] it is almost [the time when] God will start to rule!’
12 Ninawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ile kuliko mji ule.
I will tell you this: On the [MTY] [final] day when [God judges everyone], he will punish the wicked people [MTY] who long ago lived in Sodom, [the city that he destroyed because its people were so wicked]. But he will punish [even] more severely the people [MTY] of any town [whose people refused to hear your message]!”
13 “Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani, kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
“There will be terrible [punishment] for [you people who live in] [MTY] Chorazin and Bethsaida [cities]. I did great miracles in your cities [to show God’s power, but you did not turn from your sinful behavior]. If the miracles that I performed in your [cities] had been done in Tyre and Sidon [cities], the wicked people who lived there would have long ago [shown that they were sorry for their sins by] sitting on the ground wearing coarse cloth and putting ashes on their heads.
14 Lakini itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
[But they did not have the opportunity that you have, so when God punishes people, he will punish the wicked people who lived in] Tyre and Sidon, but he will punish you more severely [because you did not pay attention to my message].
15 Nawe, Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu.” (Hadēs )
[I also have something to say to] you [people who live in] Capernaum [city]. (Do not [think that you will be honored] {[that God] will honor you} in heaven!/Do you [think that you will be honored] {[that God] will honor you} in heaven?) [RHQ] [That will not happen! On the contrary], [after you die, God] will send you down to the place where [sinful people] will be punished [forever]!” (Hadēs )
16 “Yeye awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi; naye awakataaye ninyi amenikataa mimi. Lakini yeye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.”
[Jesus also said to the disciples, “God will consider that] those who listen to your [message] are listening to me, and that those who reject your [message] are rejecting me. And [he will consider that] those who reject me are rejecting [God], the one who sent me.”
17 Wale sabini na wawili wakarudi kwa furaha, na kusema, “Bwana, hata pepo wachafu wanatutii kwa jina lako.”
The 72 [people whom Jesus appointed went and did as he told them to]. When they returned, they were very joyful. They said, “Lord, [people did what we(exc) told them to do]! Demons also obeyed us when by your [(sg)] authority [MTY] [we commanded them to leave people]!”
18 Yesu akawaambia, “Nilimwona Shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme wa radi.
Jesus replied, “[When those demons were obeying you, because God had enabled you to defeat them, it was as though] [MET] I saw Satan fall from heaven [as suddenly and quickly] as lightning [strikes].
19 Tazama nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na juu ya nguvu zote za adui; wala hakuna kitu chochote kitakachowadhuru.
Listen! I have given you authority so that if you oppose evil spirits [MET] [they will not hurt you]. I have given you authority to defeat our enemy, [Satan]. Nothing shall hurt you.
20 Basi, msifurahi kwa kuwa pepo wachafu wanawatii, bali furahini kwa kuwa majina yenu yameandikwa mbinguni.”
But [although] you can rejoice that evil spirits obey you, you should rejoice [more] that your names have been written {that [God] has written your names} in heaven, [because you will be with God forever].”
21 Wakati huo Yesu akashangilia katika Roho Mtakatifu, akasema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo. Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
At that time the Holy Spirit caused [Jesus] to be very happy. He said, “Father, you [(sg)] rule over [everything in] heaven and [on] the earth! Some [people think that they are] wise [because] they are well-educated. But I thank you that you have prevented them from [knowing] these things. [Instead], you have revealed them to [people who accept your truth as readily] [MET] [as] little children [do]. Yes, Father, [you have done that] because it seemed good to you [to do] so.”
22 “Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu. Hakuna mtu amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ni nani ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.”
[Jesus also said to the 72 disciples], “[God], my Father, has revealed to me all [I need to know and the power I need for my work]. Only my Father knows who I [really] am. Furthermore, only I and those [people] to whom I wish to reveal him know what [God] my Father is [like].”
23 Basi Yesu akawageukia wanafunzi wake akanena nao faraghani, akawaambia, “Heri macho yanayoona yale mambo mnayoyaona.
Then when Jesus’ disciples were alone with him, he turned toward them and said, “[God] is pleased with you [SYN] who have seen [the things that I have done]!
24 Kwa maana nawaambia, manabii wengi na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.”
I want you to know that many prophets and kings [who lived long ago] desired to see the things that you are seeing [me do], but these things did not [happen] then. They longed to hear the things that you have been hearing [me say], but these things were not [revealed to them] then.”
25 Wakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Yesu, akamuuliza, “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios )
[One day as Jesus was teaching people], a man was there who had studied carefully the laws that [God gave Moses]. He wanted to ask Jesus a difficult question. So he stood up and asked, “Teacher, what shall I do in order to live [with God] forever?” (aiōnios )
26 Yesu akamjibu, “Imeandikwaje katika Sheria? Kwani unasoma nini humo?”
Jesus said to him, “You [(sg)] have read [RHQ] what [Moses] has written in the laws that [God gave him]. What did Moses write about living forever?”
27 Akajibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote’; tena, ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’”
The man replied, “[He wrote that] we [(inc)] must love the Lord our God. [We must show that] by what we feel and by what we do and by what we think. [He] also [wrote that we must love] people that we come in contact with as much as [we love] ourselves.”
28 Yesu akamwambia, “Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi.”
Jesus replied, “You [(sg)] have answered [your question] correctly. If you do all that [continually], you will live [with God forever].”
29 Lakini yule mtaalamu wa sheria, akitaka kujionyesha kuwa mwenye haki, akamuuliza Yesu, “Jirani yangu ni nani?”
But the man wanted to defend [the way] he [acted toward people that he came in contact with] (OR, to defend why he [had asked a question that Jesus answered so simply]). So he said to Jesus, “Which people that I come in contact with [should I love]?”
30 Yesu akamjibu akasema, “Mtu mmoja alikuwa akiteremka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko, naye akaangukia mikononi mwa wanyangʼanyi. Wakampiga, wakaondoka, wakamwacha akiwa karibu kufa.
Jesus replied [by telling him this illustration]: “A [Jewish] man was once going down along the road from Jerusalem to Jericho. Bandits attacked him. They took away [most of] the man’s clothes [and everything else that he had], and they beat him until he was almost dead. Then they left him.
31 Kuhani mmoja alikuwa akipitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani.
It happened that a [Jewish] priest was going along that road. When he saw that man, [instead of helping him], he passed by on the other side [of the road].
32 Vivyo hivyo, Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani
Similarly, a man who worked in the temple [in Jerusalem] came to that place and saw the man. But he also passed by on the other side [of the road].
33 Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri alipomwona, alimhurumia.
Then a man from Samaria [province] came along that road to where the man was lying. [People from Samaria despise Jews. But] when he saw that man, he pitied him.
34 Akaenda alipokuwa na akasafisha majeraha yake kwa divai na mafuta, kisha akayafunga. Ndipo akampandisha kwenye punda wake, akampeleka mpaka kwenye nyumba ya wageni na kumtunza.
He went over to him and put some [olive] oil and wine on his wounds [to help heal them]. He wound strips of cloth [around the wounds]. He placed the man on his own donkey and took him to an inn and took care of him.
35 Kesho yake, yule Msamaria akachukua dinari mbiliakampa yule mwenye nyumba ya wageni na kusema, ‘Mtunze, nami nirudipo nitakulipa gharama yoyote ya ziada uliyotumia kwa ajili yake.’
The next morning he gave two silver coins to the innkeeper and said, ‘Take care of this man. If you [(sg)] spend more than this amount [to care for him], I will pay you back when I return.’”
36 “Ni yupi basi miongoni mwa hawa watatu wewe unadhani ni jirani yake yule mtu aliyeangukia mikononi mwa wanyangʼanyi?”
Then Jesus said, “Three people [saw] the man whom bandits attacked. Which one of them [acted in a loving way toward] that man?”
37 Yule mtaalamu wa sheria akajibu, “Ni yule aliyemhurumia.” Ndipo Yesu akamwambia, “Nenda, ukafanye vivyo hivyo.”
The man who studied the Scriptures replied, “The one who acted mercifully toward him.” Jesus said to him, “You [(sg)] go and act like that [toward] everyone whom [you can help]!”
38 Ikawa Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakienda Yerusalemu, akaingia kwenye kijiji kimoja ambapo mwanamke mmoja aliyeitwa Martha alimkaribisha nyumbani kwake.
As Jesus and his disciples continued to travel, they entered a village [near Jerusalem]. A woman whose name was Martha invited them to come to her house.
39 Martha alikuwa na mdogo wake aliyeitwa Maria, ambaye aliketi chini miguuni mwa Bwana akisikiliza yale aliyokuwa akisema.
Her [younger] sister, whose name was Mary, sat near Jesus. She was listening to what he was teaching.
40 Lakini Martha alikuwa akihangaika na maandalizi yote yaliyokuwa yafanyike. Martha akaja kwa Yesu na kumuuliza, “Bwana, hujali kwamba ndugu yangu ameniachia kazi zote mwenyewe? Basi mwambie anisaidie.”
But Martha was very much concerned about preparing [a meal]. She went to Jesus and said, “Lord, (you do not seem to care that my sister has left me to prepare everything by myself!/do you not care that my sister has left me to prepare everything by myself?) [RHQ] Tell her that she should help me!”
41 Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, mbona unasumbuka na kuhangaika na mengi?
But the Lord replied, “Martha, Martha, you [(sg)] are very worried about many things.
42 Lakini kunahitajika kitu kimoja tu. Maria amechagua kile kilicho bora, wala hakuna mtu atakayemwondolea.”
But only one thing is truly necessary, and that is, [to listen to what I am teaching]. Mary has decided to [do that], and that is better [than worrying]. [The blessing that she is receiving from listening to me] will not be taken away from her {No one will take away from her [the blessing that she is receiving from listening to me]}.”