< Luka 10 >

1 Baada ya hayo, Bwana akawachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawili wawili katika kila mji na kila sehemu aliyokusudia kwenda baadaye.
After this the appointed seventy others, and sent them two by two before his face, into every city and place into which he himself intended to go.
2 Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini watendakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno.
And he thus addressed them. "The harvest is abundant, but the harvesters are few. do you therefore pray the lord of the harvest to send forth harvesters into his harvest.
3 Haya! nendeni. Ninawatuma kama wana-kondoo katikati ya mbwa mwitu.
"Go your way; behold, I am sending you forth like lambs among wolves.
4 Msichukue mkoba, wala mfuko, wala viatu, na msimsalimu mtu yeyote njiani.
"Carry no purse, no bag, no shoes; and do not salute any one on your journey.
5 “Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza semeni, ‘Amani iwe kwenu.’
"Into whatever you first enter, say, ‘Peace be to this house!’
6 Kama kuna mtu wa amani humo, basi amani yenu itakuwa juu yake. La sivyo, itawarudia.
"And if there be any son of peace there, your peace shall rest upon him; but if not it shall return to you.
7 Kaeni katika nyumba hiyo, mkila na kunywa kile watakachowapa, kwa sababu kila mtendakazi anastahili malipo yake. Msihamehame kutoka nyumba hadi nyumba.
"Stay in that same house, eating and drinking what they give. for the laborer is worthy of his hire. Do not go from house to house.
8 “Mkienda katika mji na watu wake wakawakaribisha, kuleni chochote kiwekwacho mbele yenu,
"And whatever town you come to, and they receive you, eat whatever they put before you.
9 waponyeni wagonjwa waliomo na waambieni: ‘Ufalme wa Mungu umekaribia.’
"Heal the sick in that town and tell them, The kingdom of God draws near to you.
10 Lakini mkiingia katika mji, nao hawakuwakaribisha, tokeni mwende katika barabara zake mkaseme:
"But whatever town you enter, and they do not receive you, Go out into the streets and cry,
11 ‘Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu, tunayakungʼuta dhidi yenu. Lakini mjue kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.’
"‘The very dust of your town which clings to your feet we wipe off as protest; but know this, that the kingdom of God is drawing near to you.’
12 Ninawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ile kuliko mji ule.
"For I tell you that it will be mare tolerable for Sodom in that day than for that town.
13 “Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani, kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
"Woe unto you, Chorazin! Woe unto you, Bethsaida! For had the mighty been done in Tyre and Sidon which were done in you, they would have repented long ago, sitting in sackcloth and ashes.
14 Lakini itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
"However, it will be more tolerable for Tyre and Sidon in the judgment than for you.
15 Nawe, Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu.” (Hadēs g86)
"And you Capernaum, shall you be exalted to heaven? No! you shall be brought down to Hades! (Hadēs g86)
16 “Yeye awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi; naye awakataaye ninyi amenikataa mimi. Lakini yeye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.”
"He who listens to you listens to me. and he who rejects you, rejects me; he who rejects me, rejects him who sent me."
17 Wale sabini na wawili wakarudi kwa furaha, na kusema, “Bwana, hata pepo wachafu wanatutii kwa jina lako.”
Then the Seventy returned with joy, saying, "Lord even the demons are subject to us in your name."
18 Yesu akawaambia, “Nilimwona Shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme wa radi.
And he said to them. "I watched Satan fall from heaven like a lightning flash.
19 Tazama nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na juu ya nguvu zote za adui; wala hakuna kitu chochote kitakachowadhuru.
"Behold, I give you the power to tread upon serpents and scorpions, and to trample on all the power of the enemy. In no case shall anything do you harm.
20 Basi, msifurahi kwa kuwa pepo wachafu wanawatii, bali furahini kwa kuwa majina yenu yameandikwa mbinguni.”
"Nevertheless, do not rejoice at this, that the spirits are subject to you; but rejoice that your names are written in Heaven."
21 Wakati huo Yesu akashangilia katika Roho Mtakatifu, akasema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo. Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
In the same hour he thrilled with joy in the Holy Ghost. "I praise thee, Father, Lord of Heaven and Earth," he said "for hiding these things from the wise and prudent, and for revealing them to babes. Yea, Father, for so it was well pleasing in thy sight!
22 “Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu. Hakuna mtu amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ni nani ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.”
"All things have been delivered to me by my Father, and no one knows who the Son is except the Father; and who the Father is except the Son, and he the Son wishes to reveal him."
23 Basi Yesu akawageukia wanafunzi wake akanena nao faraghani, akawaambia, “Heri macho yanayoona yale mambo mnayoyaona.
And turning to his disciples he said privately. "Blessed are the eyes that see what you see!
24 Kwa maana nawaambia, manabii wengi na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.”
"For I tell you that many prophets and kings have longed to see what you see, and have seen it; and to hear what you hear, and have heard it not.’
25 Wakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Yesu, akamuuliza, “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
Then a certain lawyer stood up and tempted him. "Master," he said "what shall I do to inherit eternal life?" (aiōnios g166)
26 Yesu akamjibu, “Imeandikwaje katika Sheria? Kwani unasoma nini humo?”
And he said to him. "What is written in the Law? What do you read there?"
27 Akajibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote’; tena, ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’”
"You must love the Lord your God," he answered, with all your heart, and with all your soul, and with all your strength, and with all your with all your mind; and your neighbor as yourself."
28 Yesu akamwambia, “Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi.”
"You have answered right," said Jesus "do that and you shall live."
29 Lakini yule mtaalamu wa sheria, akitaka kujionyesha kuwa mwenye haki, akamuuliza Yesu, “Jirani yangu ni nani?”
But he, determined to justify himself, said to Jesus, "But who is my neighbor?" Jesus answered.
30 Yesu akamjibu akasema, “Mtu mmoja alikuwa akiteremka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko, naye akaangukia mikononi mwa wanyangʼanyi. Wakampiga, wakaondoka, wakamwacha akiwa karibu kufa.
"A certain man was going down from Jerusalem to Jericho, when he fell among bandits who both stripped him and beat him, and went off leaving him half dead.
31 Kuhani mmoja alikuwa akipitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani.
"Now a certain priest chanced to be going down that way, but on seeing him he passed on the other side.
32 Vivyo hivyo, Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani
"In like manner also a Levite who came to the spot, came and looked at him, and passed on the other side.
33 Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri alipomwona, alimhurumia.
"But a certain Samaritan, as he journeyed, came where he was, and when he saw him was moved with compassion.
34 Akaenda alipokuwa na akasafisha majeraha yake kwa divai na mafuta, kisha akayafunga. Ndipo akampandisha kwenye punda wake, akampeleka mpaka kwenye nyumba ya wageni na kumtunza.
"He went to him bound up his wounds, pouring on them oil and wine. He set him on his own beast, and took him to an inn, and took care of him.
35 Kesho yake, yule Msamaria akachukua dinari mbiliakampa yule mwenye nyumba ya wageni na kusema, ‘Mtunze, nami nirudipo nitakulipa gharama yoyote ya ziada uliyotumia kwa ajili yake.’
"The next day he took two silver pieces and gave them to the landlord and said, "‘Take care of him, and whatever more you spend I will repay it to you on my way back.’
36 “Ni yupi basi miongoni mwa hawa watatu wewe unadhani ni jirani yake yule mtu aliyeangukia mikononi mwa wanyangʼanyi?”
"Which then of these three seems to you to have behaved like a neighbor to the man who fell among bandits?"
37 Yule mtaalamu wa sheria akajibu, “Ni yule aliyemhurumia.” Ndipo Yesu akamwambia, “Nenda, ukafanye vivyo hivyo.”
He replied, "The one who showed mercy on him." "Go, then," said Jesus, "and do likewise."
38 Ikawa Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakienda Yerusalemu, akaingia kwenye kijiji kimoja ambapo mwanamke mmoja aliyeitwa Martha alimkaribisha nyumbani kwake.
It happened as they went on their way that he entered into a certain village were a woman named Martha received him into her house.
39 Martha alikuwa na mdogo wake aliyeitwa Maria, ambaye aliketi chini miguuni mwa Bwana akisikiliza yale aliyokuwa akisema.
She had a sister named Mary, who after seating herself at the Lord’s feet was listening to his teaching.
40 Lakini Martha alikuwa akihangaika na maandalizi yote yaliyokuwa yafanyike. Martha akaja kwa Yesu na kumuuliza, “Bwana, hujali kwamba ndugu yangu ameniachia kazi zote mwenyewe? Basi mwambie anisaidie.”
But Martha meanwhile was growing distracted about much serving. She came up to him and said. "Lord do you not care that my sister has left me alone to do the serving? Come tell her to take hold of her end of the work along with me."
41 Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, mbona unasumbuka na kuhangaika na mengi?
"Martha, Martha," said Jesus, "you are anxious and worried about many things,
42 Lakini kunahitajika kitu kimoja tu. Maria amechagua kile kilicho bora, wala hakuna mtu atakayemwondolea.”
"only one thing is really necessary. Mary, moreover, has chosen that good part which shall not be taken away from her."

< Luka 10 >