< Luka 10 >

1 Baada ya hayo, Bwana akawachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawili wawili katika kila mji na kila sehemu aliyokusudia kwenda baadaye.
And after these things the Lord appointed also other seventy-two: and he sent them two and two before his face into every city and place whither he himself was to come.
2 Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini watendakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno.
And he said to them: The harvest indeed is great, but the labourers are few. Pray ye therefore the Lord of the harvest, that he send labourers into his harvest.
3 Haya! nendeni. Ninawatuma kama wana-kondoo katikati ya mbwa mwitu.
Go: Behold I send you as lambs among wolves.
4 Msichukue mkoba, wala mfuko, wala viatu, na msimsalimu mtu yeyote njiani.
Carry neither purse, nor scrip, nor shoes; and salute no man by the way.
5 “Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza semeni, ‘Amani iwe kwenu.’
Into whatsoever house you enter, first say: Peace be to this house.
6 Kama kuna mtu wa amani humo, basi amani yenu itakuwa juu yake. La sivyo, itawarudia.
And if the son of peace be there, your peace shall rest upon him; but if not, it shall return to you.
7 Kaeni katika nyumba hiyo, mkila na kunywa kile watakachowapa, kwa sababu kila mtendakazi anastahili malipo yake. Msihamehame kutoka nyumba hadi nyumba.
And in the same house, remain, eating and drinking such things as they have: for the labourer is worthy of his hire. Remove not from house to house.
8 “Mkienda katika mji na watu wake wakawakaribisha, kuleni chochote kiwekwacho mbele yenu,
And into what city soever you enter, and they receive you, eat such things as are set before you.
9 waponyeni wagonjwa waliomo na waambieni: ‘Ufalme wa Mungu umekaribia.’
And heal the sick that are therein, and say to them: The kingdom of God is come nigh unto you.
10 Lakini mkiingia katika mji, nao hawakuwakaribisha, tokeni mwende katika barabara zake mkaseme:
But into whatsoever city you enter, and they receive you not, going forth into the streets thereof, say:
11 ‘Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu, tunayakungʼuta dhidi yenu. Lakini mjue kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.’
Even the very dust of your city that cleaveth to us, we wipe off against you. Yet know this, that the kingdom of God is at hand.
12 Ninawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ile kuliko mji ule.
I say to you, it shall be more tolerable at that day for Sodom, than for that city.
13 “Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani, kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
Woe to thee, Corozain, woe to thee, Bethsaida. For if in Tyre and Sidon had been wrought the mighty works that have been wrought in you, they would have done penance long ago, sitting in sackcloth and ashes.
14 Lakini itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
But it shall be more tolerable for Tyre and Sidon at the judgement, than for you.
15 Nawe, Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu.” (Hadēs g86)
And thou, Capharnaum, which art exalted unto heaven, thou shalt be thrust down to hell. (Hadēs g86)
16 “Yeye awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi; naye awakataaye ninyi amenikataa mimi. Lakini yeye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.”
He that heareth you, heareth me; and he that despiseth you, despiseth me; and he that despiseth me, despiseth him that sent me.
17 Wale sabini na wawili wakarudi kwa furaha, na kusema, “Bwana, hata pepo wachafu wanatutii kwa jina lako.”
And the seventy-two returned with joy, saying: Lord, the devils also are subject to us in thy name.
18 Yesu akawaambia, “Nilimwona Shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme wa radi.
And he said to them: I saw Satan like lightening falling from heaven.
19 Tazama nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na juu ya nguvu zote za adui; wala hakuna kitu chochote kitakachowadhuru.
Behold, I have given you power to tread upon serpents and scorpions, and upon all the power of the enemy: and nothing shall hurt you.
20 Basi, msifurahi kwa kuwa pepo wachafu wanawatii, bali furahini kwa kuwa majina yenu yameandikwa mbinguni.”
But yet rejoice not in this, that spirits are subject unto you; but rejoice in this, that your names are written in heaven.
21 Wakati huo Yesu akashangilia katika Roho Mtakatifu, akasema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo. Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
In that same hour, he rejoiced in the Holy Ghost, and said: I confess to thee, O Father, Lord of heaven and earth, because thou hast hidden these things from the wise and prudent, and hast revealed them to little ones. Yea, Father, for so it hath seemed good in thy sight.
22 “Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu. Hakuna mtu amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ni nani ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.”
All things are delivered to me by my Father; and no one knoweth who the Son is, but the Father; and who the Father is, but the Son, and to whom the Son will reveal him.
23 Basi Yesu akawageukia wanafunzi wake akanena nao faraghani, akawaambia, “Heri macho yanayoona yale mambo mnayoyaona.
And turning to his disciples, he said: Blessed are the eyes that see the things which you see.
24 Kwa maana nawaambia, manabii wengi na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.”
For I say to you, that many prophets and kings have desired to see the things that you see, and have not seen them; and to hear the things that you hear, and have not heard them.
25 Wakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Yesu, akamuuliza, “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
And behold a certain lawyer stood up, tempting him, and saying, Master, what must I do to possess eternal life? (aiōnios g166)
26 Yesu akamjibu, “Imeandikwaje katika Sheria? Kwani unasoma nini humo?”
But he said to him: What is written in the law? how readest thou?
27 Akajibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote’; tena, ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’”
He answering, said: Thou shalt love the Lord thy God with thy whole heart, and with thy whole soul, and with all thy strength, and with all thy mind: and thy neighbour as thyself.
28 Yesu akamwambia, “Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi.”
And he said to him: Thou hast answered right: this do, and thou shalt live.
29 Lakini yule mtaalamu wa sheria, akitaka kujionyesha kuwa mwenye haki, akamuuliza Yesu, “Jirani yangu ni nani?”
But he willing to justify himself, said to Jesus: And who is my neighbour?
30 Yesu akamjibu akasema, “Mtu mmoja alikuwa akiteremka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko, naye akaangukia mikononi mwa wanyangʼanyi. Wakampiga, wakaondoka, wakamwacha akiwa karibu kufa.
And Jesus answering, said: A certain man went down from Jerusalem to Jericho, and fell among robbers, who also stripped him, and having wounded him went away, leaving him half dead.
31 Kuhani mmoja alikuwa akipitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani.
And it chanced, that a certain priest went down the same way: and seeing him, passed by.
32 Vivyo hivyo, Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani
In like manner also a Levite, when he was near the place and saw him, passed by.
33 Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri alipomwona, alimhurumia.
But a certain Samaritan being on his journey, came near him; and seeing him, was moved with compassion.
34 Akaenda alipokuwa na akasafisha majeraha yake kwa divai na mafuta, kisha akayafunga. Ndipo akampandisha kwenye punda wake, akampeleka mpaka kwenye nyumba ya wageni na kumtunza.
And going up to him, bound up his wounds, pouring in oil and wine: and setting him upon his own beast, brought him to an inn, and took care of him.
35 Kesho yake, yule Msamaria akachukua dinari mbiliakampa yule mwenye nyumba ya wageni na kusema, ‘Mtunze, nami nirudipo nitakulipa gharama yoyote ya ziada uliyotumia kwa ajili yake.’
And the next day he took out two pence, and gave to the host, and said: Take care of him; and whatsoever thou shalt spend over and above, I, at my return, will repay thee.
36 “Ni yupi basi miongoni mwa hawa watatu wewe unadhani ni jirani yake yule mtu aliyeangukia mikononi mwa wanyangʼanyi?”
Which of these three, in thy opinion, was neighbour to him that fell among the robbers?
37 Yule mtaalamu wa sheria akajibu, “Ni yule aliyemhurumia.” Ndipo Yesu akamwambia, “Nenda, ukafanye vivyo hivyo.”
But he said: He that shewed mercy to him. And Jesus said to him: Go, and do thou in like manner.
38 Ikawa Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakienda Yerusalemu, akaingia kwenye kijiji kimoja ambapo mwanamke mmoja aliyeitwa Martha alimkaribisha nyumbani kwake.
Now it came to pass as they went, that he entered into a certain town: and a certain woman named Martha, received him into her house.
39 Martha alikuwa na mdogo wake aliyeitwa Maria, ambaye aliketi chini miguuni mwa Bwana akisikiliza yale aliyokuwa akisema.
And she had a sister called Mary, who sitting also at the Lord’s feet, heard his word.
40 Lakini Martha alikuwa akihangaika na maandalizi yote yaliyokuwa yafanyike. Martha akaja kwa Yesu na kumuuliza, “Bwana, hujali kwamba ndugu yangu ameniachia kazi zote mwenyewe? Basi mwambie anisaidie.”
But Martha was busy about much serving. Who stood and said: Lord, hast thou no care that my sister hath left me alone to serve? speak to her therefore, that she help me.
41 Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, mbona unasumbuka na kuhangaika na mengi?
And the Lord answering, said to her: Martha, Martha, thou art careful, and art troubled about many things:
42 Lakini kunahitajika kitu kimoja tu. Maria amechagua kile kilicho bora, wala hakuna mtu atakayemwondolea.”
But one thing is necessary. Mary hath chosen the best part, which shall not be taken away from her.

< Luka 10 >