< Luka 1 >

1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
Inasmuch as many have undertaken to arrange a narrative of those things which are fully believed among us,
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
even as they were delivered to us by those who were eye-witnesses from the beginning and became ministers of the word,
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
it seemed good to me also, having accurately traced up all things from the first, to write to thee a connected account, most excellent Theophilus,
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
that thou mightst know the exact truth with regard to those things in which thou wast instructed.
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
There was in the days of Herod, king of Judaea, a certain priest named Zachariah, of the course of Abijah; and he had a wife of the daughters of Aaron, and her name was Elizabeth.
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
And they were both righteous in the sight of God, walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
And they had no child, because Elizabeth was barren, and they were both far advanced in years.
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
And it came to pass, that, while he was serving as priest before God in the order of his course,
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
according to the custom of the priesthood the lot fell to him to go into the temple of the Lord and burn the incense.
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
And the whole multitude of the people was praying without at the time of the incense.
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
And there appeared to him an angel of the Lord, standing on the right of the altar of incense.
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
And Zachariah was troubled at the sight, and fear fell upon him.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
But the angel said to him, Fear not, Zachariah; for thy prayer was heard, and thy wife Elizabeth shall bear thee a son; and thou shalt call his name John.
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
And thou wilt have joy and gladness, and many will rejoice for his birth.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
For he will be great in the sight of the Lord; and will drink neither wine nor strong drink; and he will be filled with the Holy Spirit from his very birth.
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
And many of the sons of Israel will he turn to the Lord their God.
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
And he will go before his face in the spirit and power of Elijah, to turn the hearts of fathers to children, and the disobedient to the wisdom of the righteous, to make ready for the Lord a prepared people.
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
And Zachariah said to the angel, Whereby shall I know this? for I am an old man, and my wife is far advanced in years.
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
And the angel answering said to him, I am Gabriel, who stand in the presence of God; and I was sent to speak to thee, and to tell thee these glad tidings.
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
And lo! thou shalt be silent, and not able to speak, until the day when these things shall come to pass, because thou didst not believe my words, which will be fulfilled in their season.
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
And the people were looking for Zachariah, and wondering that he remained so long in the temple.
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
And on coming out, he was not able to speak to them; and they perceived that he had seen a vision in the temple; and he was beckoning to them, and remained speechless.
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
And it came to pass, when the days of his ministration were completed, that he returned to his house.
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
And after those days his wife Elizabeth conceived, and hid herself five months, saying,
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
Thus hath the Lord dealt with me in the days wherein he looked on me to take away my reproach among men.
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
And in her sixth month the angel Gabriel was sent from God to a city of Galilee, called Nazareth,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
to a virgin betrothed to a man whose name was Joseph, of the house of David; and the virgin's name was Mary.
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
And the angel came in to her and said, Hail, thou that art highly favored! the Lord is with thee.
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
And she was troubled at the words, and was considering what this salutation could mean.
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
And the angel said to her, Fear not, Mary; for thou hast found favor with God.
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
And lo! thou shalt conceive in thy womb, and hear a son, and shalt call his name Jesus.
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
He shall be great, and shall be called the Son of the Most High; and the Lord God will give to him the throne of David his father;
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
and he shall reign over the house of Jacob for ever; and of his kingdom there shall be no end. (aiōn g165)
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
Then said Mary to the angel, How shall this be, since I know not a man?
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
And the angel answering said to her, The Holy Spirit will come upon thee, and the power of the Most High will overshadow thee; wherefore the holy one that is to be born will be called the Son of God.
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
And lo! Elizabeth, thy kinswoman, she also hath conceived a son in her old age; and this is the sixth month with her who is called barren.
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
For nothing will be impossible with God.
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
And Mary said, Lo, the handmaid of the Lord! May it be to me according to thy word. And the angel departed from her.
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
And Mary arose and went in those days into the hill-country with haste, into a city of Judah.
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
And she entered the house of Zachariah, and saluted Elizabeth.
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
And it came to pass, when Elizabeth heard the salutation of Mary, that the babe leaped in her womb; and Elizabeth was filled with the Holy Spirit,
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
and cried out with a loud voice, and said, Blessed art thou among women; and blessed is the fruit of thy womb!
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
And whence is this to me, that the mother of my Lord should come to me?
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
For lo! as soon as the voice of thy salutation came to my ears, the babe leaped in my womb in exultation.
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
And blessed is she who hath believed that there will be an accomplishment of those things which were told her from the Lord.
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
And Mary said, My soul magnifieth the Lord,
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
and my spirit hath exulted in God my Saviour;
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
for he hath looked upon the low estate of his handmaiden. For lo! from this time all generations will call me blessed;
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
for the Mighty One hath done great things for me; and holy is his name;
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
and his mercy is from generation to generation on them that fear him.
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
He hath wrought mightily with his arm; he hath scattered the proud in the device of their heart.
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
He hath cast down princes from thrones, and exalted men of low degree.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
The hungry he hath filled with good things, and the rich he hath sent away empty.
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
He hath given help to Israel his servant, in remembrance of his mercy
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
toward Abraham and his offspring for ever, as he spoke to our fathers. (aiōn g165)
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
And Mary abode with her about three months, and returned to her own house.
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
Now Elizabeth's full time came that she should be delivered; and she brought forth a son.
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
And her neighbors and her kinsfolk heard that the Lord had showed great mercy toward her; and they rejoiced with her.
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
And it came to pass that on the eighth day they came to circumcise the child; and they were about to call him Zachariah, after the name of his father.
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
And his mother answering said, Not so; but he shall be called John.
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
And they said to her, There is no one of thy kindred that is called by this name.
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
And they made signs to his father, how he would have him named.
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
And he asked for a writing-tablet, and wrote, saying, His name is John. And they all marveled.
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
And his mouth was opened immediately, and his tongue was loosed; and he spoke, blessing God.
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
And fear came on all that dwelt around them; and all these things were talked of throughout the whole of the hill-country of Judaea.
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
And all that heard them laid them up in their hearts, saying, What then will this child be? For the hand of the Lord was with him.
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
And Zachariah his father was filled with the Holy Spirit, and prophesied, saying,
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
Blessed be the Lord, the God of Israel! for he hath visited and redeemed his people,
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
and hath raised up a horn of salvation for us in the house of David his servant, —
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
as he spoke by the mouth of his holy prophets of old, (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
salvation from our enemies, and from the hand of all that hate us,
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
to accomplish his mercy toward our fathers, and to remember his holy covenant,
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
the oath which he swore to Abraham our father,
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
to grant to us, that being delivered from the hand of our enemies, we might worship him without fear,
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
in holiness and righteousness before him, all our days.
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
And thou, child, shalt be called a prophet of the Most High; for thou shalt go in advance before the face of the Lord to prepare his ways,
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
to give knowledge of salvation to his people in the remission of their sins
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
through the tender mercy of our God, whereby the day-spring from on high hath visited us,
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
to give light to those sitting in darkness and the shadow of death, to guide our feet into the way of peace.
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
And the child grew, and waxed strong in spirit; and was in the deserts till the day of his manifestation to Israel.

< Luka 1 >