< Luka 1 >
1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
提阿非羅大人哪,有好些人提筆作書,述說在我們中間所成就的事,是照傳道的人從起初親眼看見又傳給我們的。
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
這些事我既從起頭都詳細考察了,就定意要按着次序寫給你,
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
使你知道所學之道都是確實的。
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
當猶太王希律的時候,亞比雅班裏有一個祭司,名叫撒迦利亞;他妻子是亞倫的後人,名叫伊利莎白。
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
他們二人在上帝面前都是義人,遵行主的一切誡命禮儀,沒有可指摘的,
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
只是沒有孩子;因為伊利莎白不生育,兩個人又年紀老邁了。
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
撒迦利亞按班次在上帝面前供祭司的職分,
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
照祭司的規矩掣籤,得進主殿燒香。
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
燒香的時候,眾百姓在外面禱告。
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
有主的使者站在香壇的右邊,向他顯現。
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
撒迦利亞看見,就驚慌害怕。
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
天使對他說:「撒迦利亞,不要害怕,因為你的祈禱已經被聽見了。你的妻子伊利莎白要給你生一個兒子,你要給他起名叫約翰。
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
你必歡喜快樂;有許多人因他出世,也必喜樂。
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
他在主面前將要為大,淡酒濃酒都不喝,從母腹裏就被聖靈充滿了。
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
他要使許多以色列人回轉,歸於主-他們的上帝。
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
他必有以利亞的心志能力,行在主的前面,叫為父的心轉向兒女,叫悖逆的人轉從義人的智慧,又為主預備合用的百姓。」
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
撒迦利亞對天使說:「我憑着甚麼可知道這事呢?我已經老了,我的妻子也年紀老邁了。」
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
天使回答說:「我是站在上帝面前的加百列,奉差而來對你說話,將這好信息報給你。
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
到了時候,這話必然應驗;只因你不信,你必啞巴,不能說話,直到這事成就的日子。」
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
百姓等候撒迦利亞,詫異他許久在殿裏。
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
及至他出來,不能和他們說話,他們就知道他在殿裏見了異象;因為他直向他們打手式,竟成了啞巴。
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
他供職的日子已滿,就回家去了。
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
這些日子以後,他的妻子伊利莎白懷了孕,就隱藏了五個月,
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
說:「主在眷顧我的日子,這樣看待我,要把我在人間的羞恥除掉。」
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
到了第六個月,天使加百列奉上帝的差遣往加利利的一座城去(這城名叫拿撒勒),
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
到一個童女那裏,是已經許配大衛家的一個人,名叫約瑟。童女的名字叫馬利亞;
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
天使進去,對她說:「蒙大恩的女子,我問你安,主和你同在了!」
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
馬利亞因這話就很驚慌,又反覆思想這樣問安是甚麼意思。
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
天使對她說:「馬利亞,不要怕!你在上帝面前已經蒙恩了。
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
你要懷孕生子,可以給他起名叫耶穌。
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
他要為大,稱為至高者的兒子;主上帝要把他祖大衛的位給他。
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
他要作雅各家的王,直到永遠;他的國也沒有窮盡。」 (aiōn )
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
馬利亞對天使說:「我沒有出嫁,怎麼有這事呢?」
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
天使回答說:「聖靈要臨到你身上,至高者的能力要蔭庇你,因此所要生的聖者必稱為上帝的兒子 。
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
況且你的親戚伊利莎白,在年老的時候也懷了男胎,就是那素來稱為不生育的,現在有孕六個月了。
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
因為,出於上帝的話,沒有一句不帶能力的。」
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
馬利亞說:「我是主的使女,情願照你的話成就在我身上。」天使就離開她去了。
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
那時候,馬利亞起身,急忙往山地裏去,來到猶大的一座城;
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
進了撒迦利亞的家,問伊利莎白安。
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
伊利莎白一聽馬利亞問安,所懷的胎就在腹裏跳動。伊利莎白且被聖靈充滿,
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
高聲喊着說:「你在婦女中是有福的!你所懷的胎也是有福的!
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
我主的母到我這裏來,這是從哪裏得的呢?
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
因為你問安的聲音一入我耳,我腹裏的胎就歡喜跳動。
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
這相信的女子是有福的!因為主對她所說的話都要應驗。」
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
馬利亞說: 我心尊主為大;
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
我靈以上帝我的救主為樂;
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
因為他顧念他使女的卑微; 從今以後, 萬代要稱我有福。
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
那有權能的,為我成就了大事; 他的名為聖。
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
他憐憫敬畏他的人, 直到世世代代。
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
他用膀臂施展大能; 那狂傲的人正心裏妄想就被他趕散了。
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
他叫有權柄的失位, 叫卑賤的升高;
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
叫飢餓的得飽美食, 叫富足的空手回去。
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
他扶助了他的僕人以色列,
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn )
為要記念亞伯拉罕和他的後裔, 施憐憫直到永遠, 正如從前對我們列祖所說的話。 (aiōn )
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
馬利亞和伊利莎白同住,約有三個月,就回家去了。
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
伊利莎白的產期到了,就生了一個兒子。
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
鄰里親族聽見主向她大施憐憫,就和她一同歡樂。
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
到了第八日,他們來要給孩子行割禮,並要照他父親的名字叫他撒迦利亞。
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
他母親說:「不可!要叫他約翰。」
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
他們說:「你親族中沒有叫這名字的。」
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
他們就向他父親打手式,問他要叫這孩子甚麼名字。
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
他要了一塊寫字的板,就寫上,說:「他的名字是約翰。」他們便都希奇。
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
撒迦利亞的口立時開了,舌頭也舒展了,就說出話來,稱頌上帝。
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
周圍居住的人都懼怕;這一切的事就傳遍了猶太的山地。
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
凡聽見的人都將這事放在心裏,說:「這個孩子將來怎麼樣呢?因為有主與他同在。」
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
他父親撒迦利亞被聖靈充滿了,就預言說:
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
主-以色列的上帝是應當稱頌的! 因他眷顧他的百姓,為他們施行救贖,
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
在他僕人大衛家中, 為我們興起了拯救的角,
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn )
正如主藉着從創世以來聖先知的口所說的話, (aiōn )
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
拯救我們脫離仇敵 和一切恨我們之人的手,
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
向我們列祖施憐憫, 記念他的聖約-
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
就是他對我們祖宗亞伯拉罕所起的誓-
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
叫我們既從仇敵手中被救出來,
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
就可以終身在他面前, 坦然無懼地用聖潔、公義事奉他。
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
孩子啊!你要稱為至高者的先知; 因為你要行在主的前面, 預備他的道路,
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
叫他的百姓因罪得赦, 就知道救恩。
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
因我們上帝憐憫的心腸, 叫清晨的日光從高天臨到我們,
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
要照亮坐在黑暗中死蔭裏的人, 把我們的腳引到平安的路上。
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
那孩子漸漸長大,心靈強健,住在曠野,直到他顯明在以色列人面前的日子。