< Mambo ya Walawi 1 >

1 Bwana akamwita Mose na kusema naye kutoka kwenye Hema la Kukutania, akamwambia,
Et l'Éternel appela Moïse, et de la Tente du Rendez-vous Il lui parla en ces termes:
2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Yeyote miongoni mwenu aletapo sadaka ya mnyama kwa Bwana, alete mnyama kama sadaka yake kutoka kundi lake la ngʼombe au la kondoo na mbuzi.
Parle aux enfants d'Israël et dis-leur: Si quelqu'un de vous veut offrir une oblation à l'Éternel, l'oblation que vous offrirez sera prise parmi vos bestiaux, parmi vos bœufs et vos brebis.
3 “‘Kama sadaka hiyo ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la ngʼombe, atamtoa ngʼombe dume asiye na dosari. Ni lazima amlete kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili aweze kukubalika kwa Bwana.
Si l'oblation consiste dans l'Holocauste d'une pièce de gros bétail, il offrira un mâle sans défaut, et l'amènera à l'entrée de la Tente du Rendez-vous, afin qu'il soit agréé devant l'Éternel.
4 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya kuteketezwa, nayo itakubaliwa kwa niaba yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake.
Et il posera sa main sur la tête de l'holocauste pour se faire agréer de Lui pour sa réconciliation.
5 Atamchinja yule fahali mchanga mbele za Bwana, kisha wana wa Aroni walio makuhani wataleta damu na kuinyunyiza pande zote za madhabahu yaliyo penye ingilio la Hema la Kukutania.
Alors il égorgera le jeune taureau devant l'Éternel, et les Prêtres, fils d'Aaron, apporteront le sang qu'ils répandront à l'Autel qui est à l'entrée de la Tente du Rendez-vous.
6 Ataichuna hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande vipande.
Et il dépouillera l'holocauste et le détaillera en sept quartiers.
7 Wana wa Aroni kuhani wataweka moto juu ya madhabahu na kupanga kuni juu ya huo moto.
Et les fils du Prêtre Aaron mettront du feu sur l'Autel et disposeront le bois sur le feu.
8 Kisha wana wa Aroni walio makuhani watapanga vile vipande vya nyama, pamoja na kichwa na mafuta ya huyo mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
Et les Prêtres, fils d'Aaron, rangeront les pièces, la tête et la graisse sur le bois placé sur le feu mis sur l'Autel.
9 Ataziosha sehemu za ndani na miguu yake kwa maji, naye kuhani atavichoma vyote juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, yenye harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Et il lavera dans l'eau la fressure et les jambes, et le Prêtre fera fumer le tout sur l'Autel en holocauste, en victime brûlée, d'un parfum agréable à l'Éternel.
10 “‘Kama sadaka ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la kondoo au mbuzi, atamtoa mnyama dume asiye na dosari.
Et si son oblation est de menu bétail, chèvres ou brebis, pour holocauste, il offrira un mâle sans défaut.
11 Atamchinjia upande wa kaskazini wa madhabahu mbele za Bwana, nao wana wa Aroni walio makuhani watanyunyizia damu yake pande zote za madhabahu.
Et il l'égorgera à côté de l'Autel au nord devant l'Éternel, et les Prêtres, fils d'Aaron, en répandront le sang autour de l'Autel.
12 Atamkata vipande vipande, naye kuhani atavipanga, pamoja na kichwa na mafuta ya mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
Et il le détaillera en ses quartiers, outre la tête et la graisse, et le Prêtre les rangera sur le bois placé sur le feu mis sur l'Autel.
13 Ataosha sehemu za ndani na miguu kwa maji, naye kuhani atavileta vyote na kuvichoma juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Et il lavera dans l'eau la fressure et les jambes, et le Prêtre offrira le tout et le fera fumer sur l'Autel: c'est un holocauste, une victime brûlée, d'un parfum agréable à l'Éternel.
14 “‘Kama sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwa Bwana ni ndege, atamtoa hua au kinda la njiwa.
Et si l'oblation destinée à l'Éternel consiste dans un holocauste d'oiseaux, il offrira pour son oblation ou des tourterelles, ou de jeunes pigeons.
15 Kuhani atamleta kwenye madhabahu, naye atamvunja shingo na kumnyofoa kichwa na kumchoma juu ya madhabahu. Damu yake itachuruzishwa ubavuni mwa madhabahu.
Et le Prêtre les approchera de l'Autel, il leur fendra la tête avec l'ongle et les fera fumer sur l'Autel, et leur sang dégouttera sur les parois de l'Autel,
16 Ataondoa kifuko cha chakula pamoja na uchafu wake na kuvitupa upande wa mashariki wa madhabahu, mahali pale penye majivu.
et il enlèvera le gésier avec ses immondices et le jettera à côté de l'Autel vers l'orient dans le cendrier.
17 Atampasua na kumweka wazi katika mabawa yake, lakini asimwachanishe kabisa, kisha kuhani ataichoma juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Et il rompra l'oiseau aux ailes, mais sans les détacher, et le prêtre le fera fumer sur l'Autel, sur le bois placé sur le feu: c'est un holocauste, une victime brûlée, d'un parfum agréable à l'Éternel.

< Mambo ya Walawi 1 >