< Mambo ya Walawi 1 >

1 Bwana akamwita Mose na kusema naye kutoka kwenye Hema la Kukutania, akamwambia,
and to call: call to to(wards) Moses and to speak: speak LORD to(wards) him from tent meeting to/for to say
2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Yeyote miongoni mwenu aletapo sadaka ya mnyama kwa Bwana, alete mnyama kama sadaka yake kutoka kundi lake la ngʼombe au la kondoo na mbuzi.
to speak: speak to(wards) son: descendant/people Israel and to say to(wards) them man for to present: bring from you offering to/for LORD from [the] animal from [the] cattle and from [the] flock to present: bring [obj] offering your
3 “‘Kama sadaka hiyo ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la ngʼombe, atamtoa ngʼombe dume asiye na dosari. Ni lazima amlete kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili aweze kukubalika kwa Bwana.
if burnt offering offering his from [the] cattle male unblemished to present: bring him to(wards) entrance tent meeting to present: bring [obj] him to/for acceptance his to/for face: before LORD
4 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya kuteketezwa, nayo itakubaliwa kwa niaba yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake.
and to support hand his upon head [the] burnt offering and to accept to/for him to/for to atone upon him
5 Atamchinja yule fahali mchanga mbele za Bwana, kisha wana wa Aroni walio makuhani wataleta damu na kuinyunyiza pande zote za madhabahu yaliyo penye ingilio la Hema la Kukutania.
and to slaughter [obj] son: young animal [the] cattle to/for face: before LORD and to present: bring son: child Aaron [the] priest [obj] [the] blood and to scatter [obj] [the] blood upon [the] altar around: side which entrance tent meeting
6 Ataichuna hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande vipande.
and to strip [obj] [the] burnt offering and to cut [obj] her to/for piece her
7 Wana wa Aroni kuhani wataweka moto juu ya madhabahu na kupanga kuni juu ya huo moto.
and to give: put son: child Aaron [the] priest fire upon [the] altar and to arrange tree: wood upon [the] fire
8 Kisha wana wa Aroni walio makuhani watapanga vile vipande vya nyama, pamoja na kichwa na mafuta ya huyo mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
and to arrange son: child Aaron [the] priest [obj] [the] piece [obj] [the] head and [obj] [the] suet upon [the] tree: wood which upon [the] fire which upon [the] altar
9 Ataziosha sehemu za ndani na miguu yake kwa maji, naye kuhani atavichoma vyote juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, yenye harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
and entrails: inner parts his and leg his to wash: wash in/on/with water and to offer: burn [the] priest [obj] [the] all [the] altar [to] burnt offering food offering aroma soothing to/for LORD
10 “‘Kama sadaka ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la kondoo au mbuzi, atamtoa mnyama dume asiye na dosari.
and if from [the] flock offering his from [the] sheep or from [the] goat to/for burnt offering male unblemished to present: bring him
11 Atamchinjia upande wa kaskazini wa madhabahu mbele za Bwana, nao wana wa Aroni walio makuhani watanyunyizia damu yake pande zote za madhabahu.
and to slaughter [obj] him upon thigh [the] altar north [to] to/for face: before LORD and to scatter son: child Aaron [the] priest [obj] blood his upon [the] altar around: side
12 Atamkata vipande vipande, naye kuhani atavipanga, pamoja na kichwa na mafuta ya mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
and to cut [obj] him to/for piece his and [obj] head his and [obj] suet his and to arrange [the] priest [obj] them upon [the] tree: wood which upon [the] fire which upon [the] altar
13 Ataosha sehemu za ndani na miguu kwa maji, naye kuhani atavileta vyote na kuvichoma juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
and [the] entrails: inner parts and [the] leg to wash: wash in/on/with water and to present: bring [the] priest [obj] [the] all and to offer: burn [the] altar [to] burnt offering he/she/it food offering aroma soothing to/for LORD
14 “‘Kama sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwa Bwana ni ndege, atamtoa hua au kinda la njiwa.
and if from [the] bird burnt offering offering his to/for LORD and to present: bring from [the] turtledove or from son: young animal [the] dove [obj] offering his
15 Kuhani atamleta kwenye madhabahu, naye atamvunja shingo na kumnyofoa kichwa na kumchoma juu ya madhabahu. Damu yake itachuruzishwa ubavuni mwa madhabahu.
and to present: bring him [the] priest to(wards) [the] altar and to nip [obj] head his and to offer: burn [the] altar [to] and to drain blood his upon wall [the] altar
16 Ataondoa kifuko cha chakula pamoja na uchafu wake na kuvitupa upande wa mashariki wa madhabahu, mahali pale penye majivu.
and to turn aside: remove [obj] crop his in/on/with plumage her and to throw [obj] her beside [the] altar east [to] to(wards) place [the] ashes
17 Atampasua na kumweka wazi katika mabawa yake, lakini asimwachanishe kabisa, kisha kuhani ataichoma juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
and to cleave [obj] him in/on/with wing his not to separate and to offer: burn [obj] him [the] priest [the] altar [to] upon [the] tree: wood which upon [the] fire burnt offering he/she/it food offering aroma soothing to/for LORD

< Mambo ya Walawi 1 >