< Mambo ya Walawi 1 >

1 Bwana akamwita Mose na kusema naye kutoka kwenye Hema la Kukutania, akamwambia,
And the LORD called to Moses, and spoke to him out of the tabernacle of the congregation, saying,
2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Yeyote miongoni mwenu aletapo sadaka ya mnyama kwa Bwana, alete mnyama kama sadaka yake kutoka kundi lake la ngʼombe au la kondoo na mbuzi.
Speak to the children of Israel, and say to them, If any man of you bring an offering to the LORD, you shall bring your offering of the cattle, even of the herd, and of the flock.
3 “‘Kama sadaka hiyo ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la ngʼombe, atamtoa ngʼombe dume asiye na dosari. Ni lazima amlete kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili aweze kukubalika kwa Bwana.
If his offering be a burnt sacrifice of the herd, let him offer a male without blemish: he shall offer it of his own voluntary will at the door of the tabernacle of the congregation before the LORD.
4 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya kuteketezwa, nayo itakubaliwa kwa niaba yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake.
And he shall put his hand on the head of the burnt offering; and it shall be accepted for him to make atonement for him.
5 Atamchinja yule fahali mchanga mbele za Bwana, kisha wana wa Aroni walio makuhani wataleta damu na kuinyunyiza pande zote za madhabahu yaliyo penye ingilio la Hema la Kukutania.
And he shall kill the bullock before the LORD: and the priests, Aaron’s sons, shall bring the blood, and sprinkle the blood round about on the altar that is by the door of the tabernacle of the congregation.
6 Ataichuna hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande vipande.
And he shall flay the burnt offering, and cut it into his pieces.
7 Wana wa Aroni kuhani wataweka moto juu ya madhabahu na kupanga kuni juu ya huo moto.
And the sons of Aaron the priest shall put fire on the altar, and lay the wood in order on the fire:
8 Kisha wana wa Aroni walio makuhani watapanga vile vipande vya nyama, pamoja na kichwa na mafuta ya huyo mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
And the priests, Aaron’s sons, shall lay the parts, the head, and the fat, in order on the wood that is on the fire which is on the altar:
9 Ataziosha sehemu za ndani na miguu yake kwa maji, naye kuhani atavichoma vyote juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, yenye harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
But his inwards and his legs shall he wash in water: and the priest shall burn all on the altar, to be a burnt sacrifice, an offering made by fire, of a sweet smell to the LORD.
10 “‘Kama sadaka ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la kondoo au mbuzi, atamtoa mnyama dume asiye na dosari.
And if his offering be of the flocks, namely, of the sheep, or of the goats, for a burnt sacrifice; he shall bring it a male without blemish.
11 Atamchinjia upande wa kaskazini wa madhabahu mbele za Bwana, nao wana wa Aroni walio makuhani watanyunyizia damu yake pande zote za madhabahu.
And he shall kill it on the side of the altar northward before the LORD: and the priests, Aaron’s sons, shall sprinkle his blood round about on the altar.
12 Atamkata vipande vipande, naye kuhani atavipanga, pamoja na kichwa na mafuta ya mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
And he shall cut it into his pieces, with his head and his fat: and the priest shall lay them in order on the wood that is on the fire which is on the altar:
13 Ataosha sehemu za ndani na miguu kwa maji, naye kuhani atavileta vyote na kuvichoma juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
But he shall wash the inwards and the legs with water: and the priest shall bring it all, and burn it on the altar: it is a burnt sacrifice, an offering made by fire, of a sweet smell to the LORD.
14 “‘Kama sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwa Bwana ni ndege, atamtoa hua au kinda la njiwa.
And if the burnt sacrifice for his offering to the LORD be of fowls, then he shall bring his offering of turtledoves, or of young pigeons.
15 Kuhani atamleta kwenye madhabahu, naye atamvunja shingo na kumnyofoa kichwa na kumchoma juu ya madhabahu. Damu yake itachuruzishwa ubavuni mwa madhabahu.
And the priest shall bring it to the altar, and wring off his head, and burn it on the altar; and the blood thereof shall be wrung out at the side of the altar:
16 Ataondoa kifuko cha chakula pamoja na uchafu wake na kuvitupa upande wa mashariki wa madhabahu, mahali pale penye majivu.
And he shall pluck away his crop with his feathers, and cast it beside the altar on the east part, by the place of the ashes:
17 Atampasua na kumweka wazi katika mabawa yake, lakini asimwachanishe kabisa, kisha kuhani ataichoma juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
And he shall split it with the wings thereof, but shall not divide it asunder: and the priest shall burn it on the altar, on the wood that is on the fire: it is a burnt sacrifice, an offering made by fire, of a sweet smell to the LORD.

< Mambo ya Walawi 1 >