< Mambo ya Walawi 9 >
1 Katika siku ya nane, Mose akawaita Aroni na wanawe, na wazee wa Israeli.
Na osmi dan se je pripetilo, da je Mojzes poklical Arona, njegove sinove in Izraelove starešine.
2 Akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka yako ya dhambi, na kondoo dume kwa sadaka yako ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, nao uwalete mbele za Bwana.
Aronu je rekel: »Vzemi si mlado tele za daritev za greh in ovna za žgalno daritev, brez pomanjkljivosti in ju daruj pred Gospodom.
3 Kisha waambie Waisraeli: ‘Chukueni mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na ndama na mwana-kondoo, wote wawili wawe wa umri wa mwaka mmoja, na wasio na dosari, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,
Izraelovim otrokom boš govoril, rekoč: ›Vzemite kozlička od koz za daritev za greh ter tele in jagnje, oba enoletna, brez pomanjkljivosti, za žgalno daritev.
4 na pia maksai na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya amani, ili kutoa dhabihu mbele za Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta. Kwa kuwa leo Bwana atawatokea.’”
Tudi bikca in ovna za mirovno daritev, da žrtvujete pred Gospodom in jedilno daritev umešano z oljem, kajti danes se vam bo prikazal Gospod.‹«
5 Wakavileta vile vitu Mose alivyowaagiza mbele ya Hema la Kukutania, nalo kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Bwana.
Pred šotorsko svetišče skupnosti so privedli to, kar je Mojzes zapovedal, in vsa skupnost se je približala ter stala pred Gospodom.
6 Ndipo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana alilowaagiza mlifanye, ili utukufu wa Bwana upate kuonekana kwenu.”
Mojzes je rekel: »To je stvar, ki jo je Gospod zapovedal, da naj bi jo storili; in prikazala se vam bo Gospodova slava.«
7 Mose akamwambia Aroni, “Njoo madhabahuni ili utoe dhabihu yako ya sadaka ya dhambi na sadaka yako ya kuteketezwa, ufanye upatanisho kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watu. Kisha utoe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya watu, kama vile Bwana alivyoagiza.”
Mojzes je rekel Aronu: »Pojdi k oltarju in daruj svojo daritev za greh in svojo žgalno daritev in opravi spravo zase in za ljudstvo in daruj dar ljudstva in opravi spravo zanje; kakor je zapovedal Gospod.«
8 Hivyo Aroni akaja madhabahuni na kumchinja yule ndama kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe.
Aron je torej odšel k oltarju in zaklal tele za daritev za greh, ki je bilo zanj.
9 Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika hiyo damu, akaitia kwenye pembe za madhabahu, nayo damu iliyobaki akaimwaga chini ya madhabahu.
Aronovi sinovi so k njemu prinesli kri, in svoj prst je pomočil v kri in jo dal na rogove oltarja in kri izlil ob vznožju oltarja.
10 Juu ya madhabahu akateketeza mafuta, figo na mafuta yanayofunika ini kutoka kwenye hiyo sadaka ya dhambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Toda tolščo, ledvici in opno nad jetri daritve za greh je sežgal na oltarju, kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
11 Akateketeza nyama na ngozi nje ya kambi.
Meso in kožo pa je sežgal z ognjem zunaj tabora.
12 Kisha Aroni akachinja sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyiza pande zote za madhabahu.
Zaklal je žgalno daritev in Aronovi sinovi so mu podali kri, ki jo je poškropil naokoli nad oltarjem.
13 Wakamletea sadaka ya kuteketezwa kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
Podali so mu žgalno daritev, z njenimi kosi in glavo, in sežgal jih je na oltarju.
14 Akasafisha sehemu za ndani na miguu, akaviteketeza juu ya sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
Opral je drobovje in noge ter jih sežgal na žgalni daritvi, na oltarju.
15 Kisha Aroni akaleta sadaka ile iliyokuwa kwa ajili ya watu. Akachukua yule mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, akamchinja na kumtoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kama alivyofanya kwa ile ya kwanza.
Prinesel je dar ljudstva in vzel kozla, ki je bil daritev za greh za ljudstvo in ga zaklal ter ga daroval za greh kakor prvega.
16 Aroni akaleta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama ilivyoelekezwa.
Privedel je žgalno daritev in jo daroval glede na določen način.
17 Pia akaleta sadaka ya nafaka, akachukua konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi.
Prinesel je jedilno daritev in od nje vzel prgišče in to sežgal na oltarju poleg jutranje žgalne daritve.
18 Akachinja maksai na kondoo dume kama sadaka ya amani kwa ajili ya watu. Wanawe Aroni wakampa ile damu, naye akainyunyiza kwenye madhabahu pande zote.
Za ljudstvo je zaklal tudi bikca in ovna za žrtvovanje mirovnih daritev, Aronovi sinovi pa so mu podali kri, ki jo je poškropil naokoli po oltarju,
19 Lakini sehemu zile za mafuta ya yule maksai na kondoo dume, yaani mafuta ya mkia, mafuta yaliyofunika tumbo, ya figo na yaliyofunika ini,
in tolščo bikca in ovna, tolsti rep in to, kar pokriva drobovje, ledvici in opno nad jetri.
20 hivi vyote wakaviweka juu ya vidari, kisha Aroni akayateketeza hayo mafuta ya wanyama juu ya madhabahu.
Tolščo so položili na prsi in tolščo je sežgal na oltarju.
21 Aroni akaviinua vile vidari na paja la kulia mbele za Bwana ili viwe sadaka ya kuinuliwa, kama Mose alivyoagiza.
Prsi in desno pleče je Aron majal za majalno daritev pred Gospodom; kakor je zapovedal Mojzes.
22 Kisha Aroni akainua mikono yake kuwaelekea watu na kuwabariki. Naye baada ya kutoa dhabihu ya sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani, akashuka chini.
Aron je svojo roko vzdignil proti ljudstvu in jih blagoslovil in prišel dol od darovanja daritve za greh, žgalne daritve in mirovnih daritev.
23 Kisha Mose na Aroni wakaingia kwenye Hema la Kukutania. Walipotoka nje, wakawabariki watu. Nao utukufu wa Bwana ukawatokea watu wote.
Mojzes in Aron sta odšla v šotorsko svetišče skupnosti in prišla ven ter blagoslovila ljudstvo in Gospodova slava se je prikazala vsemu ljudstvu.
24 Moto ukaja kutoka uwepo wa Bwana, ukairamba ile sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sehemu ya mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipoona jambo hili, wakapiga kelele kwa furaha na kusujudu.
Tam je prišel ogenj izpred Gospoda in na oltarju použil žgalno daritev in tolščo. Ko je vse ljudstvo to videlo, so zavpili in padli na svoje obraze.