< Mambo ya Walawi 9 >

1 Katika siku ya nane, Mose akawaita Aroni na wanawe, na wazee wa Israeli.
در روز هشتم، موسی هارون و پسرانش را با مشایخ اسرائیل جمع کرد
2 Akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka yako ya dhambi, na kondoo dume kwa sadaka yako ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, nao uwalete mbele za Bwana.
و به هارون گفت: «یک گوسالهٔ نر سالم و بی‌عیب برای قربانی گناه و یک قوچ سالم و بی‌عیب برای قربانی سوختنی بگیر و آنها را به حضور خداوند تقدیم کن.
3 Kisha waambie Waisraeli: ‘Chukueni mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na ndama na mwana-kondoo, wote wawili wawe wa umri wa mwaka mmoja, na wasio na dosari, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,
بعد به قوم اسرائیل بگو که یک بزغالهٔ نر برای قربانی گناه خود و یک گوساله و یک بره که هر دو یک ساله و بی‌عیب باشند برای قربانی سوختنی بیاورند.
4 na pia maksai na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya amani, ili kutoa dhabihu mbele za Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta. Kwa kuwa leo Bwana atawatokea.’”
همچنین قوم اسرائیل باید یک گاو و یک قوچ برای قربانی سلامتی، و آرد مخلوط با روغن زیتون برای هدیهٔ آردی به خداوند تقدیم کنند زیرا امروز خداوند بر ایشان ظاهر خواهد شد.»
5 Wakavileta vile vitu Mose alivyowaagiza mbele ya Hema la Kukutania, nalo kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Bwana.
پس قوم آنچه را که موسی امر فرموده بود، جلوی خیمۀ ملاقات آوردند و تمام جماعت نزدیک شده، در حضور خداوند ایستادند.
6 Ndipo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana alilowaagiza mlifanye, ili utukufu wa Bwana upate kuonekana kwenu.”
موسی به ایشان گفت: «خداوند فرموده دستورهای او را انجام دهید تا حضور پرجلال خود را بر شما ظاهر کند.»
7 Mose akamwambia Aroni, “Njoo madhabahuni ili utoe dhabihu yako ya sadaka ya dhambi na sadaka yako ya kuteketezwa, ufanye upatanisho kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watu. Kisha utoe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya watu, kama vile Bwana alivyoagiza.”
آنگاه موسی به هارون گفت: «نزدیک مذبح بیا و همان‌طور که خداوند فرموده است قربانی گناه و قربانی سوختنی خود را تقدیم کرده، برای خود کفاره کن و سپس قربانیهای قوم را تقدیم نموده، برای آنها کفاره نما.»
8 Hivyo Aroni akaja madhabahuni na kumchinja yule ndama kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe.
بنابراین هارون به مذبح نزدیک شد و گوسالهٔ قربانی گناه خود را ذبح کرد.
9 Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika hiyo damu, akaitia kwenye pembe za madhabahu, nayo damu iliyobaki akaimwaga chini ya madhabahu.
پسرانش خون گوساله را پیش وی آوردند و او انگشت خود را در خون فرو برد و بر شاخهای مذبح مالید و باقیماندهٔ خون را به پای مذبح ریخت.
10 Juu ya madhabahu akateketeza mafuta, figo na mafuta yanayofunika ini kutoka kwenye hiyo sadaka ya dhambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
بعد همان‌طور که خداوند به موسی دستور داده بود، چربی، قلوه‌ها و سفیدی روی جگر قربانی گناه را بر مذبح،
11 Akateketeza nyama na ngozi nje ya kambi.
و گوشت و پوست آن را بیرون از اردوگاه سوزانید.
12 Kisha Aroni akachinja sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyiza pande zote za madhabahu.
پس از آن هارون قربانی سوختنی را ذبح کرد و پسرانش خون قربانی را آوردند و هارون آن را بر چهار طرف مذبح پاشید.
13 Wakamletea sadaka ya kuteketezwa kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
ایشان کله و قطعه‌های دیگر حیوان را نزد هارون آوردند و او آنها را بر مذبح سوزانید.
14 Akasafisha sehemu za ndani na miguu, akaviteketeza juu ya sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
دل و روده و پاچه‌ها را شست و اینها را نیز به عنوان قربانی سوختنی بر مذبح سوزانید.
15 Kisha Aroni akaleta sadaka ile iliyokuwa kwa ajili ya watu. Akachukua yule mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, akamchinja na kumtoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kama alivyofanya kwa ile ya kwanza.
سپس هارون قربانی قوم اسرائیل را تقدیم کرد. او بز قربانی گناه قوم را ذبح نموده، آن را مانند قربانی گناه خود برای گناه قوم تقدیم کرد.
16 Aroni akaleta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama ilivyoelekezwa.
آنگاه مطابق قوانین، قربانی سوختنی ایشان را به خداوند تقدیم نمود.
17 Pia akaleta sadaka ya nafaka, akachukua konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi.
بعد هدیهٔ آردی را آورد و مشتی از آن را گرفت و بر مذبح سوزانید. (این قربانی غیر از قربانی سوختنی‌ای بود که هر روز صبح تقدیم می‌شد.)
18 Akachinja maksai na kondoo dume kama sadaka ya amani kwa ajili ya watu. Wanawe Aroni wakampa ile damu, naye akainyunyiza kwenye madhabahu pande zote.
پس از آن هارون گاو و قوچ را به عنوان قربانی سلامتی قوم ذبح کرد. پسران هارون خون قربانی را نزد او آوردند و او آن را بر چهار طرف مذبح پاشید.
19 Lakini sehemu zile za mafuta ya yule maksai na kondoo dume, yaani mafuta ya mkia, mafuta yaliyofunika tumbo, ya figo na yaliyofunika ini,
سپس چربی گاو و قوچ را که شامل چربی داخل شکم و قلوه‌ها و سفیدی روی جگر گاو و قوچ می‌شد، گرفت
20 hivi vyote wakaviweka juu ya vidari, kisha Aroni akayateketeza hayo mafuta ya wanyama juu ya madhabahu.
و آنها را روی سینه‌های حیوان گذاشته، نزدیک مذبح آورد و تمام چربی را روی مذبح سوزانید.
21 Aroni akaviinua vile vidari na paja la kulia mbele za Bwana ili viwe sadaka ya kuinuliwa, kama Mose alivyoagiza.
همان‌طور که موسی دستور داده بود، هارون سینه‌ها، و رانهای راست حیوان را به عنوان هدیهٔ مخصوص در حضور خداوند تکان داد.
22 Kisha Aroni akainua mikono yake kuwaelekea watu na kuwabariki. Naye baada ya kutoa dhabihu ya sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani, akashuka chini.
پس از تقدیم قربانیها، هارون دستهای خود را به طرف قوم اسرائیل دراز کرده، ایشان را برکت داد و از مذبح به زیر آمد.
23 Kisha Mose na Aroni wakaingia kwenye Hema la Kukutania. Walipotoka nje, wakawabariki watu. Nao utukufu wa Bwana ukawatokea watu wote.
موسی و هارون به خیمۀ ملاقات رفتند. وقتی از آنجا بیرون آمدند قوم اسرائیل را برکت دادند. آنگاه حضور پرجلال خداوند بر تمام جماعت ظاهر شد
24 Moto ukaja kutoka uwepo wa Bwana, ukairamba ile sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sehemu ya mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipoona jambo hili, wakapiga kelele kwa furaha na kusujudu.
و از حضور خداوند آتش فرود آمده، قربانی سوختنی و چربی روی مذبح را بلعید. بنی‌اسرائیل وقتی این را دیدند، فریاد برآورده، در حضور خداوند به خاک افتادند.

< Mambo ya Walawi 9 >