< Mambo ya Walawi 9 >

1 Katika siku ya nane, Mose akawaita Aroni na wanawe, na wazee wa Israeli.
Or, le huitième jour venu. Moïse appela Aaron et ses fils, et les anciens d’Israël, et il dit à Aaron:
2 Akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka yako ya dhambi, na kondoo dume kwa sadaka yako ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, nao uwalete mbele za Bwana.
Prends d’un troupeau de gros bétail un veau pour le péché et un bélier pour un holocauste, l’un et l’autre sans tache, et offre-les devant le Seigneur.
3 Kisha waambie Waisraeli: ‘Chukueni mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na ndama na mwana-kondoo, wote wawili wawe wa umri wa mwaka mmoja, na wasio na dosari, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,
Et tu diras aux enfants d’Israël: Prenez un bouc pour le péché, un veau et un agneau d’un an et sans tache pour un holocauste,
4 na pia maksai na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya amani, ili kutoa dhabihu mbele za Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta. Kwa kuwa leo Bwana atawatokea.’”
Un bœuf et un bélier pour des sacrifices pacifiques, et immolez-les devant le Seigneur, offrant dans le sacrifice de chacun de ces animaux de la fleur de farine arrosée d’huile; car aujourd’hui le Seigneur vous apparaîtra.
5 Wakavileta vile vitu Mose alivyowaagiza mbele ya Hema la Kukutania, nalo kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Bwana.
Ils portèrent donc tout ce que leur avait ordonné Moïse, à la porte du tabernacle, où pendant que toute la multitude se tenait debout,
6 Ndipo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana alilowaagiza mlifanye, ili utukufu wa Bwana upate kuonekana kwenu.”
Moïse dit: Voici la parole qu’a ordonnée le Seigneur; accomplissez-la et sa gloire vous apparaîtra.
7 Mose akamwambia Aroni, “Njoo madhabahuni ili utoe dhabihu yako ya sadaka ya dhambi na sadaka yako ya kuteketezwa, ufanye upatanisho kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watu. Kisha utoe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya watu, kama vile Bwana alivyoagiza.”
Et il dit à Aaron: Approche-toi de l’autel, et immole pour ton péché; offre l’holocauste, et prie pour toi et pour le peuple, et lorsque tu auras sacrifié l’hostie du peuple, prie pour lui, comme a ordonné le Seigneur.
8 Hivyo Aroni akaja madhabahuni na kumchinja yule ndama kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe.
Et aussitôt Aaron s’approchant de l’autel immola pour son péché le veau,
9 Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika hiyo damu, akaitia kwenye pembe za madhabahu, nayo damu iliyobaki akaimwaga chini ya madhabahu.
Dont ses fils lui présentèrent le sang, dans lequel trempant le doigt, il toucha les cornes de l’autel, et il répandit le reste du sang au pied de l’autel.
10 Juu ya madhabahu akateketeza mafuta, figo na mafuta yanayofunika ini kutoka kwenye hiyo sadaka ya dhambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Quant à la graisse, aux reins, et à la membrane réticulaire du foie, qui sont pour le péché, il les brûla sur l’autel, comme avait ordonné le Seigneur à Moïse;
11 Akateketeza nyama na ngozi nje ya kambi.
Mais la chair et la peau, c’est hors du camp qu’il les brûla au feu.
12 Kisha Aroni akachinja sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyiza pande zote za madhabahu.
Il immola aussi la victime de l’holocauste; et ses fils lui en présentèrent le sang, qu’il répandit autour de l’autel.
13 Wakamletea sadaka ya kuteketezwa kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
Ils lui présentèrent aussi l’hostie elle-même coupée en morceaux avec la tête et chacun de ses membres; lesquelles choses il brûla toutes au feu sur l’autel,
14 Akasafisha sehemu za ndani na miguu, akaviteketeza juu ya sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
Les intestins et les pieds ayant été auparavant lavés dans l’eau.
15 Kisha Aroni akaleta sadaka ile iliyokuwa kwa ajili ya watu. Akachukua yule mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, akamchinja na kumtoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kama alivyofanya kwa ile ya kwanza.
Et offrant le sacrifice pour le péché du peuple, il immola le bouc; et, l’autel purifié,
16 Aroni akaleta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama ilivyoelekezwa.
Il fit l’holocauste,
17 Pia akaleta sadaka ya nafaka, akachukua konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi.
Ajoutant au sacrifice les libations, qui sont pareillement offertes, et les brûlant sur l’autel, outre les cérémonies de l’holocauste du matin.
18 Akachinja maksai na kondoo dume kama sadaka ya amani kwa ajili ya watu. Wanawe Aroni wakampa ile damu, naye akainyunyiza kwenye madhabahu pande zote.
Il immola aussi le bœuf et le bélier, hosties pacifiques du peuple; et ses fils lui présentèrent le sang, qu’il répandit sur l’autel tout autour.
19 Lakini sehemu zile za mafuta ya yule maksai na kondoo dume, yaani mafuta ya mkia, mafuta yaliyofunika tumbo, ya figo na yaliyofunika ini,
Mais la graisse du bœuf, la queue du bélier, les reins avec leurs graisses et la membrane réticulaire du foie,
20 hivi vyote wakaviweka juu ya vidari, kisha Aroni akayateketeza hayo mafuta ya wanyama juu ya madhabahu.
Ils les posèrent sur les poitrines; et lorsque les graisses eurent été brûlées sur l’autel,
21 Aroni akaviinua vile vidari na paja la kulia mbele za Bwana ili viwe sadaka ya kuinuliwa, kama Mose alivyoagiza.
Aaron sépara les poitrines des hosties et les épaules droites, les élevant devant le Seigneur, comme avait ordonné Moïse.
22 Kisha Aroni akainua mikono yake kuwaelekea watu na kuwabariki. Naye baada ya kutoa dhabihu ya sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani, akashuka chini.
Et étendant les mains vers le peuple, il le bénit. Or, les oblations des hosties pour le péché, des holocaustes et des sacrifices pacifiques ainsi achevées, il descendit.
23 Kisha Mose na Aroni wakaingia kwenye Hema la Kukutania. Walipotoka nje, wakawabariki watu. Nao utukufu wa Bwana ukawatokea watu wote.
Mais Moïse et Aaron étant entrés dans le tabernacle de témoignage, et ensuite étant sortis, ils bénirent le peuple. Alors la gloire du Seigneur apparut à toute la multitude;
24 Moto ukaja kutoka uwepo wa Bwana, ukairamba ile sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sehemu ya mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipoona jambo hili, wakapiga kelele kwa furaha na kusujudu.
Et voilà qu’un feu sorti du Seigneur dévora l’holocauste et les graisses qui étaient sur l’autel. Ce qu’ayant vu la multitude, ils louèrent le Seigneur, tombant sur leur face.

< Mambo ya Walawi 9 >