< Mambo ya Walawi 9 >

1 Katika siku ya nane, Mose akawaita Aroni na wanawe, na wazee wa Israeli.
Le huitième jour, Moïse appela Aaron et ses fils, et les anciens d'Israël.
2 Akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka yako ya dhambi, na kondoo dume kwa sadaka yako ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, nao uwalete mbele za Bwana.
Il dit à Aaron: " Prends un jeune veau pour le sacrifice pour le péché et un bélier pour l'holocauste, tous deux sans défaut, et offre-les devant Yahweh.
3 Kisha waambie Waisraeli: ‘Chukueni mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na ndama na mwana-kondoo, wote wawili wawe wa umri wa mwaka mmoja, na wasio na dosari, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,
Tu parleras aux enfants d'Israël, en disant: Prenez un bouc pour le sacrifice pour le péché; un veau et un agneau âgés d'un an et sans défaut pour l'holocauste;
4 na pia maksai na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya amani, ili kutoa dhabihu mbele za Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta. Kwa kuwa leo Bwana atawatokea.’”
un bœuf et un bélier pour le sacrifice pacifique, afin de les immoler devant Yahweh; et une oblation pétrie à l'huile. Car aujourd'hui Yahweh vous apparaîtra. "
5 Wakavileta vile vitu Mose alivyowaagiza mbele ya Hema la Kukutania, nalo kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Bwana.
Ils amenèrent devant la tente de réunion ce que Moïse avait commandé, et toute l'assemblée s'approcha et se tint devant Yahweh.
6 Ndipo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana alilowaagiza mlifanye, ili utukufu wa Bwana upate kuonekana kwenu.”
Alors Moïse dit: " Faites ce que Yahweh vous ordonne, et la gloire de Yahweh vous apparaîtra. "
7 Mose akamwambia Aroni, “Njoo madhabahuni ili utoe dhabihu yako ya sadaka ya dhambi na sadaka yako ya kuteketezwa, ufanye upatanisho kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watu. Kisha utoe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya watu, kama vile Bwana alivyoagiza.”
Moïse dit à Aaron: " Approche-toi de l'autel; offre ton sacrifice pour le péché et ton holocauste, et fais l'expiation pour toi et pour le peuple; présente aussi l'offrande du peuple et fais l'expiation pour lui, comme Yahweh l'a ordonné. "
8 Hivyo Aroni akaja madhabahuni na kumchinja yule ndama kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe.
Aaron s'approcha de l'autel et égorgea le veau du sacrifice pour le péché offert pour lui.
9 Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika hiyo damu, akaitia kwenye pembe za madhabahu, nayo damu iliyobaki akaimwaga chini ya madhabahu.
Les fils d'Aaron lui ayant présenté le sang, il y trempa son doigt, en mit sur les cornes de l'autel et répandit le sang au pied de l'autel.
10 Juu ya madhabahu akateketeza mafuta, figo na mafuta yanayofunika ini kutoka kwenye hiyo sadaka ya dhambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Il fit fumer sur l'autel la graisse, les rognons et la taie du foie de la victime pour le péché, comme Yahweh l'avait ordonné à Moïse;
11 Akateketeza nyama na ngozi nje ya kambi.
mais la chair et la peau, il les brûla par le feu hors du camp.
12 Kisha Aroni akachinja sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyiza pande zote za madhabahu.
Il égorgea l'holocauste, et les fils d'Aaron lui ayant présenté le sang, il le répandit sur l'autel, tout autour.
13 Wakamletea sadaka ya kuteketezwa kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
Ils lui présentèrent l'holocauste coupé en morceaux, avec la tête, et il les fit fumer sur l'autel.
14 Akasafisha sehemu za ndani na miguu, akaviteketeza juu ya sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
Il lava les entrailles et les jambes, et les fit fumer sur l'autel par-dessus l'holocauste.
15 Kisha Aroni akaleta sadaka ile iliyokuwa kwa ajili ya watu. Akachukua yule mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, akamchinja na kumtoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kama alivyofanya kwa ile ya kwanza.
Il présenta ensuite l'offrande du peuple. Il prit le bouc du sacrifice pour le péché offert pour le peuple, et l'ayant égorgé, il l'offrit en expiation, comme il avait fait pour la première victime.
16 Aroni akaleta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama ilivyoelekezwa.
il offrit de même l'holocauste et le sacrifia suivant le rite.
17 Pia akaleta sadaka ya nafaka, akachukua konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi.
Il présenta l'oblation, en prit une poignée et la consuma sur l'autel, en sus de l'holocauste du matin.
18 Akachinja maksai na kondoo dume kama sadaka ya amani kwa ajili ya watu. Wanawe Aroni wakampa ile damu, naye akainyunyiza kwenye madhabahu pande zote.
Enfin il égorgea le taureau et le bélier en sacrifice pacifique pour le peuple. Les fils d'Aaron lui présentèrent le sang, qu'il répandit sur l'autel tout autour;
19 Lakini sehemu zile za mafuta ya yule maksai na kondoo dume, yaani mafuta ya mkia, mafuta yaliyofunika tumbo, ya figo na yaliyofunika ini,
ainsi que les parties grasses du taureau et du bélier, la queue, la graisse qui enveloppe les entrailles, les rognons et la taie du foie;
20 hivi vyote wakaviweka juu ya vidari, kisha Aroni akayateketeza hayo mafuta ya wanyama juu ya madhabahu.
et ils placèrent les graisses sur les poitrines, et il fit fumer les graisses sur l'autel.
21 Aroni akaviinua vile vidari na paja la kulia mbele za Bwana ili viwe sadaka ya kuinuliwa, kama Mose alivyoagiza.
Puis Aaron balança devant Yahweh les poitrines et la cuisse droite en offrande balancée, comme Moïse l'avait ordonné.
22 Kisha Aroni akainua mikono yake kuwaelekea watu na kuwabariki. Naye baada ya kutoa dhabihu ya sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani, akashuka chini.
Alors Aaron, élevant ses mains vers le peuple, le bénit; et il descendit, après avoir offert le sacrifice pour le péché, l'holocauste et le sacrifice pacifique.
23 Kisha Mose na Aroni wakaingia kwenye Hema la Kukutania. Walipotoka nje, wakawabariki watu. Nao utukufu wa Bwana ukawatokea watu wote.
Moïse et Aaron entrèrent dans la tente de réunion; lorsqu'ils en sortirent, ils bénirent le peuple. Et la gloire de Yahweh apparut à tout le peuple,
24 Moto ukaja kutoka uwepo wa Bwana, ukairamba ile sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sehemu ya mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipoona jambo hili, wakapiga kelele kwa furaha na kusujudu.
et le feu, sortant de devant Yahweh, dévora sur l'autel l'holocauste et les graisses. Et tout le peuple le vit; et ils poussèrent des cris de joie, et ils tombèrent sur leur face.

< Mambo ya Walawi 9 >