< Mambo ya Walawi 9 >

1 Katika siku ya nane, Mose akawaita Aroni na wanawe, na wazee wa Israeli.
Forsothe whanne the eiytithe dai was maad, Moises clepide Aaron, and hise sones, and the grettere men in birthe of Israel;
2 Akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka yako ya dhambi, na kondoo dume kwa sadaka yako ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, nao uwalete mbele za Bwana.
and he seide to Aaron, Take thou of the droue a calf for synne, and a ram `in to brent sacrifice, euer either with oute wem, and offre tho bifor the Lord.
3 Kisha waambie Waisraeli: ‘Chukueni mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na ndama na mwana-kondoo, wote wawili wawe wa umri wa mwaka mmoja, na wasio na dosari, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,
And thou schalt speke to the sones of Israel, Take ye a buk of geet for synne, and a calf, and a lomb of o yeer and with out wem,
4 na pia maksai na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya amani, ili kutoa dhabihu mbele za Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta. Kwa kuwa leo Bwana atawatokea.’”
in to brent sacrifice, an oxe and a ram for pesible thingis; and offre ye tho bifor the Lord, and offre ye whete flour spreynt with oile in the sacrifice of ech; for to dai the Lord schal appere to you.
5 Wakavileta vile vitu Mose alivyowaagiza mbele ya Hema la Kukutania, nalo kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Bwana.
Therfor thei token alle thingis, whiche Moises comaundide, to the dore of the tabernacle, where, whanne al the multitude stood,
6 Ndipo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana alilowaagiza mlifanye, ili utukufu wa Bwana upate kuonekana kwenu.”
Moises seide, This is the word, which the Lord comaundide, do ye, and his glorie schal appere to you.
7 Mose akamwambia Aroni, “Njoo madhabahuni ili utoe dhabihu yako ya sadaka ya dhambi na sadaka yako ya kuteketezwa, ufanye upatanisho kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watu. Kisha utoe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya watu, kama vile Bwana alivyoagiza.”
And Moises seide to Aaron, Neiye thou to the auter, and offre thou for thi synne; offre thou brent sacrifice, and preye for thee, and for the puple; and whanne thou hast slayn the sacrifice of the puple, preye thou for hem, as the Lord comaundide.
8 Hivyo Aroni akaja madhabahuni na kumchinja yule ndama kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe.
And anoon Aaron neiyede to the auter, and offride a calf for his synne;
9 Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika hiyo damu, akaitia kwenye pembe za madhabahu, nayo damu iliyobaki akaimwaga chini ya madhabahu.
whos blood hise sones offriden to him, in which blood he dippide the fyngur, and touchide the hornes of the auter, and schedde the residue at the foundement therof;
10 Juu ya madhabahu akateketeza mafuta, figo na mafuta yanayofunika ini kutoka kwenye hiyo sadaka ya dhambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
and he brente on the auter the ynnere fatnesse, and litle reynes, and the calle of the mawe, as the Lord comaundide to Moises.
11 Akateketeza nyama na ngozi nje ya kambi.
Forsothe he brente bi fier without the castels the fleischis and skyn therof.
12 Kisha Aroni akachinja sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyiza pande zote za madhabahu.
And he offride the beeste of brent sacrifice, and hise sones offriden to hym the blood therof, which he schedde bi the cumpas of the auter;
13 Wakamletea sadaka ya kuteketezwa kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
thei offriden also thilke sacrifice kit in to gobetis, with the heed, and alle membris; and he brente bi fier alle these thingis on the auter,
14 Akasafisha sehemu za ndani na miguu, akaviteketeza juu ya sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
whanne the entrailis and feet weren waischun bifor with watir.
15 Kisha Aroni akaleta sadaka ile iliyokuwa kwa ajili ya watu. Akachukua yule mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, akamchinja na kumtoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kama alivyofanya kwa ile ya kwanza.
And he offride and killide a buk of geet, for the synne of the puple; and whanne the auter was clensid,
16 Aroni akaleta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama ilivyoelekezwa.
he made brent sacrifice,
17 Pia akaleta sadaka ya nafaka, akachukua konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi.
and addide in to the sacrifice fletynge offryngis that ben offrid togidere; and he brente tho on the auter, without cerymonyes of brent sacrifice of the morewtid.
18 Akachinja maksai na kondoo dume kama sadaka ya amani kwa ajili ya watu. Wanawe Aroni wakampa ile damu, naye akainyunyiza kwenye madhabahu pande zote.
He offride also an oxe, and a ram, pesible sacrifices of the puple; and hise sones offriden to hym the blood, which he schedde bi the cumpas of the auter.
19 Lakini sehemu zile za mafuta ya yule maksai na kondoo dume, yaani mafuta ya mkia, mafuta yaliyofunika tumbo, ya figo na yaliyofunika ini,
Forsothe thei puttiden on the brestis the ynnere fatnesse of the oxe, and the tail of the ram, and the litle reynes with her fatnessis, and the calle of the mawe.
20 hivi vyote wakaviweka juu ya vidari, kisha Aroni akayateketeza hayo mafuta ya wanyama juu ya madhabahu.
And whanne the ynnere fatnessis weren brent in the auter,
21 Aroni akaviinua vile vidari na paja la kulia mbele za Bwana ili viwe sadaka ya kuinuliwa, kama Mose alivyoagiza.
Aaron departide the brestis, and the riyt schuldris of tho, and reiside bifor the Lord, as Moises comaundide.
22 Kisha Aroni akainua mikono yake kuwaelekea watu na kuwabariki. Naye baada ya kutoa dhabihu ya sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani, akashuka chini.
And he streiyte forth hondis to the puple, and blesside it; and so whanne the sacrifices for synne, and brent sacrifices, and pesible sacrifices, weren fillid, he cam doun.
23 Kisha Mose na Aroni wakaingia kwenye Hema la Kukutania. Walipotoka nje, wakawabariki watu. Nao utukufu wa Bwana ukawatokea watu wote.
Sotheli Moyses and Aaron entriden in to the tabernacle of witnessyng, and yeden out aftirward, and blessiden the puple; and the glorie of the Lord apperide to al the multitude.
24 Moto ukaja kutoka uwepo wa Bwana, ukairamba ile sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sehemu ya mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipoona jambo hili, wakapiga kelele kwa furaha na kusujudu.
And lo! fier yede out fro the Lord, and deuouride the brent sacrifice, and the ynnere fatnesses that weren on the auter; and whanne the cumpanyes hadden seyn this thing, thei preiseden the Lord, `and felden on her faces.

< Mambo ya Walawi 9 >