< Mambo ya Walawi 9 >

1 Katika siku ya nane, Mose akawaita Aroni na wanawe, na wazee wa Israeli.
And it came to pass on the eighth day, that Moses called Aaron and his sons, and the elders of Israel;
2 Akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka yako ya dhambi, na kondoo dume kwa sadaka yako ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, nao uwalete mbele za Bwana.
and he said unto Aaron: 'Take thee a bull-calf for a sin-offering, and a ram for a burnt-offering, without blemish, and offer them before the LORD.
3 Kisha waambie Waisraeli: ‘Chukueni mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na ndama na mwana-kondoo, wote wawili wawe wa umri wa mwaka mmoja, na wasio na dosari, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,
And unto the children of Israel thou shalt speak, saying: Take ye a he-goat for a sin-offering; and a calf and a lamb, both of the first year, without blemish, for a burnt-offering;
4 na pia maksai na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya amani, ili kutoa dhabihu mbele za Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta. Kwa kuwa leo Bwana atawatokea.’”
and an ox and a ram for peace-offerings, to sacrifice before the LORD; and a meal-offering mingled with oil; for to-day the LORD appeareth unto you.'
5 Wakavileta vile vitu Mose alivyowaagiza mbele ya Hema la Kukutania, nalo kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Bwana.
And they brought that which Moses commanded before the tent of meeting; and all the congregation drew near and stood before the LORD.
6 Ndipo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana alilowaagiza mlifanye, ili utukufu wa Bwana upate kuonekana kwenu.”
And Moses said: 'This is the thing which the LORD commanded that ye should do; that the glory of the LORD may appear unto you.'
7 Mose akamwambia Aroni, “Njoo madhabahuni ili utoe dhabihu yako ya sadaka ya dhambi na sadaka yako ya kuteketezwa, ufanye upatanisho kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watu. Kisha utoe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya watu, kama vile Bwana alivyoagiza.”
And Moses said unto Aaron: 'Draw near unto the altar, and offer thy sin-offering, and thy burnt-offering, and make atonement for thyself, and for the people; and present the offering of the people, and make atonement for them; as the LORD commanded.'
8 Hivyo Aroni akaja madhabahuni na kumchinja yule ndama kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe.
So Aaron drew near unto the altar, and slew the calf of the sin-offering, which was for himself.
9 Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika hiyo damu, akaitia kwenye pembe za madhabahu, nayo damu iliyobaki akaimwaga chini ya madhabahu.
And the sons of Aaron presented the blood unto him; and he dipped his finger in the blood, and put it upon the horns of the altar, and poured out the blood at the base of the altar.
10 Juu ya madhabahu akateketeza mafuta, figo na mafuta yanayofunika ini kutoka kwenye hiyo sadaka ya dhambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
But the fat, and the kidneys, and the lobe of the liver of the sin-offering, he made smoke upon the altar; as the LORD commanded Moses.
11 Akateketeza nyama na ngozi nje ya kambi.
And the flesh and the skin were burnt with fire without the camp.
12 Kisha Aroni akachinja sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyiza pande zote za madhabahu.
And he slew the burnt-offering; and Aaron's sons delivered unto him the blood, and he dashed it against the altar round about.
13 Wakamletea sadaka ya kuteketezwa kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
And they delivered the burnt-offering unto him, piece by piece, and the head; and he made them smoke upon the altar.
14 Akasafisha sehemu za ndani na miguu, akaviteketeza juu ya sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
And he washed the inwards and the legs, and made them smoke upon the burnt-offering on the altar.
15 Kisha Aroni akaleta sadaka ile iliyokuwa kwa ajili ya watu. Akachukua yule mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, akamchinja na kumtoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kama alivyofanya kwa ile ya kwanza.
And the people's offering was presented; and he took the goat of the sin-offering which was for the people, and slew it, and offered it for sin, as the first.
16 Aroni akaleta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama ilivyoelekezwa.
And the burnt-offering was presented; and he offered it according to the ordinance.
17 Pia akaleta sadaka ya nafaka, akachukua konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi.
And the meal-offering was presented; and he filled his hand therefrom, and made it smoke upon the altar, besides the burnt-offering of the morning.
18 Akachinja maksai na kondoo dume kama sadaka ya amani kwa ajili ya watu. Wanawe Aroni wakampa ile damu, naye akainyunyiza kwenye madhabahu pande zote.
He slew also the ox and the ram, the sacrifice of peace-offerings, which was for the people; and Aaron's sons delivered unto him the blood, and he dashed it against the altar round about,
19 Lakini sehemu zile za mafuta ya yule maksai na kondoo dume, yaani mafuta ya mkia, mafuta yaliyofunika tumbo, ya figo na yaliyofunika ini,
and the fat of the ox, and of the ram, the fat tail, and that which covereth the inwards, and the kidneys, and the lobe of the liver.
20 hivi vyote wakaviweka juu ya vidari, kisha Aroni akayateketeza hayo mafuta ya wanyama juu ya madhabahu.
And they put the fat upon the breasts, and he made the fat smoke upon the altar.
21 Aroni akaviinua vile vidari na paja la kulia mbele za Bwana ili viwe sadaka ya kuinuliwa, kama Mose alivyoagiza.
And the breasts and the right thigh Aaron waved for a wave-offering before the LORD; as Moses commanded.
22 Kisha Aroni akainua mikono yake kuwaelekea watu na kuwabariki. Naye baada ya kutoa dhabihu ya sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani, akashuka chini.
And Aaron lifted up his hands toward the people, and blessed them; and he came down from offering the sin-offering, and the burnt-offering, and the peace-offerings.
23 Kisha Mose na Aroni wakaingia kwenye Hema la Kukutania. Walipotoka nje, wakawabariki watu. Nao utukufu wa Bwana ukawatokea watu wote.
And Moses and Aaron went into the tent of meeting, and came out, and blessed the people; and the glory of the LORD appeared unto all the people.
24 Moto ukaja kutoka uwepo wa Bwana, ukairamba ile sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sehemu ya mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipoona jambo hili, wakapiga kelele kwa furaha na kusujudu.
And there came forth fire from before the LORD, and consumed upon the altar the burnt-offering and the fat; and when all the people saw it, they shouted, and fell on their faces.

< Mambo ya Walawi 9 >