< Mambo ya Walawi 9 >

1 Katika siku ya nane, Mose akawaita Aroni na wanawe, na wazee wa Israeli.
На осмия ден Моисей повика Аарона и синовете му и Израилевите старейшини;
2 Akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka yako ya dhambi, na kondoo dume kwa sadaka yako ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, nao uwalete mbele za Bwana.
и рече на Аарона: Вземи си мъжко теле в принос за грях, и овен за всеизгаряне, без недостатък, та ги принеси пред Господа.
3 Kisha waambie Waisraeli: ‘Chukueni mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na ndama na mwana-kondoo, wote wawili wawe wa umri wa mwaka mmoja, na wasio na dosari, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,
И да говориш на израилтяните, казвайки: Вземете козел в принос за грях, и за всеизгаряне теле и агне, едногодишни, без недостатък,
4 na pia maksai na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya amani, ili kutoa dhabihu mbele za Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta. Kwa kuwa leo Bwana atawatokea.’”
и за примирителен принос юнец и овен, за да ги пожертвувате пред Господа, и хлебен принос омесен с дървено масло; защото днес ще ви се яви Господ.
5 Wakavileta vile vitu Mose alivyowaagiza mbele ya Hema la Kukutania, nalo kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Bwana.
И тъй, донесоха пред шатъра за срещане онова, което заповяда Моисей; и цялото общество се приближи и застана пред Господа.
6 Ndipo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana alilowaagiza mlifanye, ili utukufu wa Bwana upate kuonekana kwenu.”
И Моисей каза: Това е, което Господ заповяда да направите; и Господната слава ще ви се яви.
7 Mose akamwambia Aroni, “Njoo madhabahuni ili utoe dhabihu yako ya sadaka ya dhambi na sadaka yako ya kuteketezwa, ufanye upatanisho kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watu. Kisha utoe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya watu, kama vile Bwana alivyoagiza.”
Тогава рече Моисей на Аарона: Пристъпи при олтара та принеси приноса си за грях и всеизгарянето си, и направи умилостивение за себе си и за людете; принеси и приноса за людете и направи умилостивение за тях, според както заповяда Господ.
8 Hivyo Aroni akaja madhabahuni na kumchinja yule ndama kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe.
Аарон, прочее, пристъпи при олтара та закла телето на приноса за грях, което беше за него.
9 Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika hiyo damu, akaitia kwenye pembe za madhabahu, nayo damu iliyobaki akaimwaga chini ya madhabahu.
А синовете на Аарона му донесоха кръвта; и той след като натопи пръста си в кръвта и я тури върху роговете на олтара, изля кръвта в подножието на олтара;
10 Juu ya madhabahu akateketeza mafuta, figo na mafuta yanayofunika ini kutoka kwenye hiyo sadaka ya dhambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
а тлъстината, бъбреците, и булото на дроба от приноса за грях изгори на олтара, според както Господ беше заповядал на Моисея.
11 Akateketeza nyama na ngozi nje ya kambi.
А месото и кожата изгори на огън вън от стана.
12 Kisha Aroni akachinja sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyiza pande zote za madhabahu.
Закла и всеизгарянето; и синовете на Аарона му представиха кръвта, с която поръси олтарът наоколо.
13 Wakamletea sadaka ya kuteketezwa kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu.
Тогава му донесоха всеизгарянето, къс по къс, с главата; и ги изгори на олтара;
14 Akasafisha sehemu za ndani na miguu, akaviteketeza juu ya sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
и изми вътрешностите и нозете, и изгори ги на олтара, върху всеизгарянето.
15 Kisha Aroni akaleta sadaka ile iliyokuwa kwa ajili ya watu. Akachukua yule mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, akamchinja na kumtoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kama alivyofanya kwa ile ya kwanza.
Тогава принесе приноса за людете, като взе козела на приноса за грях, който беше за людете, закла го, и го принесе за грях, както и първото.
16 Aroni akaleta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama ilivyoelekezwa.
И представи всеизгарянето и го принесе според наредбата.
17 Pia akaleta sadaka ya nafaka, akachukua konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi.
Принесе и хлебния принос, напълни ръката си от него, и го изгори на олтара, освен утринното всеизгаряне.
18 Akachinja maksai na kondoo dume kama sadaka ya amani kwa ajili ya watu. Wanawe Aroni wakampa ile damu, naye akainyunyiza kwenye madhabahu pande zote.
Закла още юнеца и овена на примирителната жертва, която беше за людете; и синовете на Аарона му представиха кръвта, (с която поръси олтарът наоколо),
19 Lakini sehemu zile za mafuta ya yule maksai na kondoo dume, yaani mafuta ya mkia, mafuta yaliyofunika tumbo, ya figo na yaliyofunika ini,
и тлъстините от юнеца, а от овена - опашката, тлъстината, която покрива вътрешностите, бъбреците и булото на дроба;
20 hivi vyote wakaviweka juu ya vidari, kisha Aroni akayateketeza hayo mafuta ya wanyama juu ya madhabahu.
и като туриха тлъстините върху гърдите, той изгори тлъстините върху олтара.
21 Aroni akaviinua vile vidari na paja la kulia mbele za Bwana ili viwe sadaka ya kuinuliwa, kama Mose alivyoagiza.
А гърдите и дясното бедро подвижи Аарон за движим принос пред Господа, според както Моисей беше заповядал.
22 Kisha Aroni akainua mikono yake kuwaelekea watu na kuwabariki. Naye baada ya kutoa dhabihu ya sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani, akashuka chini.
Тогава Аарон подигна ръцете си към людете и ги благослови; и, както беше вече принесъл приноса за грях, всеизгарянето, и примирителните приноси, слезе.
23 Kisha Mose na Aroni wakaingia kwenye Hema la Kukutania. Walipotoka nje, wakawabariki watu. Nao utukufu wa Bwana ukawatokea watu wote.
И Моисей и Аарон, като влязоха в шатъра за срещане, при излизането си благословиха людете; и Господната слава се яви на всичките люде.
24 Moto ukaja kutoka uwepo wa Bwana, ukairamba ile sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sehemu ya mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipoona jambo hili, wakapiga kelele kwa furaha na kusujudu.
И огън излезе от пред Господа и пояде всеизгарянето и тлъстините върху олтара; и като видяха това, всичките люде издадоха силен вик и паднаха на лице.

< Mambo ya Walawi 9 >