< Mambo ya Walawi 8 >

1 Bwana akamwambia Mose,
RAB Musa'ya şöyle dedi:
2 “Waletee Aroni na wanawe mavazi yao, mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili na kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu.
“Harun'la oğullarını, kâhin giysilerini, mesh yağını, günah sunusu olarak sunulacak boğayı, iki koçu ve mayasız ekmek sepetini Buluşma Çadırı'nın giriş bölümüne getir. Bütün topluluğu da oraya çağır.”
3 Kisha kusanya mkutano wote kwenye ingilio la Hema la Kukutania.”
4 Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza, na mkutano ukakusanyika kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
Musa RAB'bin buyruğunu yerine getirdi. Herkes Buluşma Çadırı'nın önünde toplandı.
5 Mose akaliambia kusanyiko, “Hili ndilo Bwana ameagiza lifanyike.”
Musa topluluğa, “Şimdi RAB'bin buyruğunu yerine getireceğim” dedi.
6 Kisha Mose akamleta Aroni na wanawe mbele, akawaosha kwa maji.
Harun'la oğullarını öne çıkarıp yıkadı.
7 Akamvika Aroni koti, akamfunga mshipi, akamvika joho na kumvalisha kisibau. Pia akafunga kisibau juu yake na kukifunga kiunoni mwake kwa mshipi wake uliosokotwa kwa ustadi.
Harun'a mintanı giydirdi, beline kuşağı bağladı, üzerine kaftanı, onun üzerine de efodu giydirdi. Ustaca dokunmuş şeridiyle efodu bağladı.
8 Akaweka kifuko cha kifuani juu yake, na kuweka Urimu na Thumimu kwenye hicho kifuko.
Üzerine göğüslüğü taktı, göğüslüğün içine Urim ile Tummim'i koydu.
9 Kisha akamvika Aroni kilemba kichwani pake, akaweka lile bamba la dhahabu, yaani ile taji takatifu, upande wa mbele wa kilemba, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Başına sarığı sardı, ön kısmına kutsal tacı, altın levhayı koydu. Musa her şeyi RAB'bin buyurduğu gibi yaptı.
10 Ndipo Mose akachukua mafuta ya upako na kuipaka maskani na kila kitu kilichokuwamo ndani yake, kisha akaviweka wakfu.
Sonra mesh yağını aldı, Tanrı'nın Konutu'nu ve içindeki her şeyi meshederek kutsal kıldı.
11 Akanyunyiza baadhi ya mafuta juu ya madhabahu mara saba, akaipaka madhabahu mafuta na vyombo vyake vyote pamoja na sinia na kinara chake, ili kuviweka wakfu.
Yağı yedi kez sunağın üzerine serpti; sunağı, sunağın bütün aletlerini, kazanı ve ayaklıklarını kutsal kılmak için meshetti.
12 Akamimina sehemu ya hayo mafuta ya upako kichwani mwa Aroni, akamtia mafuta ili kumweka wakfu.
Harun'u kutsal kılmak için başına yağ dökerek meshetti.
13 Kisha akawaleta wana wa Aroni mbele, akawavika makoti, akawafunga mishipi na kuwavika vilemba, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Harun'un oğullarını öne çıkardı, onlara mintan giydirdi, bellerine kuşak bağladı, başlarına başlık koydu. Musa her şeyi RAB'bin buyurduğu gibi yaptı.
14 Kisha akamtoa fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nao Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa chake.
Sonra günah sunusu olarak sunulacak boğayı getirdi. Harun'la oğulları ellerini boğanın başına koydular.
15 Mose akamchinja yule fahali na akachukua sehemu ya hiyo damu, kisha kwa kidole chake akaitia kwenye pembe zote za madhabahu ili kutakasa madhabahu. Akaimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu. Kwa hiyo akayaweka wakfu ili kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu.
Musa boğayı kesti. Sunağı pak kılmak için kanını parmağıyla sunağın boynuzlarına çepeçevre sürdü. Artan kanı sunağın dibine döktü. Böylece sunağı arındırıp kutsal kıldı.
16 Pia Mose akachukua mafuta yote yanayozunguka sehemu za ndani, mafuta yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, akayateketeza juu ya madhabahu.
Musa hayvanın bağırsak ve işkembe yağlarını, karaciğer perdesini, böbreklerini ve böbrek yağlarını sunağın üzerinde yaktı.
17 Lakini fahali, ikiwa pamoja na ngozi yake na nyama yake na sehemu zake za ndani na matumbo, akaiteketeza nje ya kambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Boğanın geri kalan kısmını da –derisini, etini, gübresini– ordugahın dışında yaktı. Musa her şeyi RAB'bin buyurduğu gibi yaptı.
18 Kisha Mose akamleta kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa chake.
Sonra yakmalık sunu olarak sunulacak koçu getirdi. Harun'la oğulları ellerini koçun başına koydular.
19 Ndipo Mose akamchinja yule kondoo dume na kunyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
Musa koçu kesti, kanını sunağın her yanına döktü.
20 Mose akamkata yule kondoo dume vipande vipande na kukiteketeza kichwa, vile vipande na yale mafuta.
Koçu parçalara ayırıp parçaları, başını ve iç yağını yaktı.
21 Kisha akamsafisha sehemu za ndani na miguu kwa maji, na kumteketeza yule kondoo dume mzima juu ya madhabahu kuwa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Bağırsaklarını, işkembesini, ayaklarını yıkadı ve koçun tümünü sunağın üzerinde yaktı. Bu bir yakmalık sunu, RAB'bi hoşnut eden koku, yakılan sunuydu. Musa her şeyi RAB'bin buyurduğu gibi yaptı.
22 Kisha akaleta kondoo dume mwingine, ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa chake.
Sonra öteki koçu, atanma sunusu olarak sunulacak koçu getirdi. Harun'la oğulları ellerini koçun başına koydular.
23 Mose akamchinja yule kondoo dume, akaichukua sehemu ya damu yake na kuipaka juu ya ncha ya sikio la kuume la Aroni, na juu ya kidole gumba cha mkono wake wa kuume na juu ya kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
Musa koçu kesti. Kanını Harun'un sağ kulak memesine, sağ elinin ve sağ ayağının baş parmaklarına sürdü.
24 Pia Mose akawaleta hao wana wa Aroni mbele, akaipaka sehemu ya hiyo damu kwenye ncha za masikio yao ya kuume, juu ya vidole gumba vya mikono yao ya kuume, na juu ya vidole vikubwa vya miguu yao ya kuume. Kisha akanyunyiza damu pande zote za madhabahu.
Sonra Harun'un oğullarını öne çıkardı. Onların da sağ kulak memelerine, sağ ellerinin ve ayaklarının baş parmaklarına kan sürdü. Artan kanı sunağın her yanına döktü.
25 Akachukua mafuta ya mnyama, mafuta ya mkia, mafuta yote yanayozunguka sehemu za ndani, mafuta yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, na paja la kulia.
Hayvanın yağını, kuyruk yağını, bağırsak ve işkembe yağlarını, karaciğer perdesini, böbreklerini, böbrek yağlarını ve sağ budunu aldı.
26 Kisha kutoka kwenye kikapu cha mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichokuwa mbele za Bwana, akachukua andazi moja, na jingine lililotengenezwa kwa mafuta, na mkate mwembamba; akaviweka hivi vyote juu ya mafungu ya mafuta ya mnyama, na juu ya lile paja la kulia.
Sonra RAB'bin huzurunda bulunan mayasız ekmek sepetinden bir ekmek, yağlı pide ve yufka alıp hayvanın yağlarının ve sağ budunun üzerine koydu.
27 Akaviweka hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe, na kuviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
Hepsini Harun'la oğullarının eline verdi. Bunları RAB'bin huzurunda sallamalık sunu olarak salladı.
28 Kisha Mose akavichukua kutoka mikononi mwao na kuviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kuwa sadaka ya kuwekwa wakfu, harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
Sonra ellerinden alıp sunakta yakmalık sununun üzerinde yaktı. Bunlar atanma sunusu, RAB'bi hoşnut eden koku ve RAB için yakılan sunuydu.
29 Kisha akachukua kidari, kilicho fungu la Mose la kondoo dume kwa ajili ya kuwekwa wakfu, na kukiinua mbele za Bwana kama sadaka ya kuinuliwa, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Bundan sonra Musa döşü aldı ve sallamalık sunu olarak RAB'bin huzurunda salladı. Atanma sunusu olarak sunulan koçtan Musa'nın payına düşen buydu. Musa her şeyi RAB'bin buyurduğu gibi yaptı.
30 Kisha Mose akachukua sehemu ya mafuta ya upako, na sehemu ya damu kutoka kwenye madhabahu, na kuvinyunyiza juu ya Aroni na mavazi yake, na juu ya wanawe na mavazi yao. Kwa hiyo akamweka Aroni na mavazi yake wakfu, pamoja na wanawe na mavazi yao.
Musa mesh yağını ve sunağın üzerindeki kanı alıp Harun'la oğullarının ve giysilerinin üzerine serpti. Böylece Harun'u, oğullarını ve giysilerini kutsal kılmış oldu.
31 Kisha Mose akamwambia Aroni na wanawe, “Pika hiyo nyama kwenye ingilio la Hema la Kukutania, na uile hapo pamoja na mkate kutoka kwenye kikapu cha sadaka ya kuweka wakfu, kama nilivyoagiza, nikisema, ‘Aroni na wanawe wataila.’
Sonra Harun'la oğullarına, “Eti Buluşma Çadırı'nın giriş bölümünde haşlayın” dedi, “‘Eti Harun'la oğulları yiyecek’ diye buyurmuştum. Atanma sunularının bulunduğu sepetteki ekmekle birlikte onu orada yiyin.
32 Kisha teketeza nyama na mikate iliyobaki.
Etten ve ekmekten artanı yakın.
33 Msitoke kwenye ingilio la Hema la Kukutania kwa muda wa siku saba, mpaka siku zenu za kuwekwa wakfu ziwe zimetimia, kwa kuwa muda wenu wa kuwekwa wakfu utakuwa siku saba.
Atanma günleriniz doluncaya kadar, yedi gün boyunca Buluşma Çadırı'nın giriş bölümünden ayrılmayın. Çünkü atanmanız yedi gün sürecek.
34 Lile lililofanyika leo liliagizwa na Bwana ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
Bugün yapılan her şeyi günahlarınızı bağışlatmak için RAB buyurdu.
35 Lazima mkae kwenye ingilio la Hema la Kukutania usiku na mchana kwa siku saba, na kufanya lile Bwana analolitaka, ili kwamba msife; kwa kuwa hilo ndilo nililoamriwa.”
Yedi gün boyunca gece gündüz Buluşma Çadırı'nın giriş bölümünde bekleyecek, RAB'bin buyruğunu yerine getireceksiniz. Öyle ki, ölmeyesiniz. Bana böyle buyruk verildi.”
36 Kwa hiyo Aroni na wanawe wakafanya kila kitu Bwana alichoamuru kupitia kwa Mose.
Böylece Harun'la oğulları RAB'bin Musa aracılığıyla verdiği bütün buyrukları yerine getirdiler.

< Mambo ya Walawi 8 >