< Mambo ya Walawi 7 >

1 “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya hatia, ambayo ni takatifu sana:
“These are the regulations concerning the offerings to be made by people who are guilty of not giving to me the things that are required to be given to me. Those are very sacred offerings.
2 Sadaka ya hatia itachinjiwa mahali pale ambapo sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, nayo damu yake itanyunyizwa pande zote za madhabahu.
Each animal that is to be offered by such people must be slaughtered in the same place where the animals that will be completely burned [on the altar] are slaughtered, and their blood must be sprinkled against all sides of the altar.
3 Mafuta yake yote yatatolewa sadaka: mafuta ya mkia na mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani,
All their fat, the fat tails that are cut close to the backbone, and all the fat that covers the inner parts of the animals or which is attached to them, must be burned [on the altar].
4 figo zote mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo yataondolewa pamoja na hizo figo.
That includes the kidneys with their fat near the lower back muscle, and the protruding lobe that is attached to the liver.
5 Kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kuwa sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia.
The priest must burn them on the altar to be offerings to me, Yahweh. They are an offering for the people to be forgiven for not doing what they were required to do.
6 Mwanaume yeyote katika jamaa ya kuhani aweza kuila, lakini lazima iliwe mahali patakatifu; ni takatifu sana.
All the males in the priest’s family are permitted to eat its meat, but it must be eaten in a sacred place, because it is very sacred.
7 “‘Sheria hii ya sadaka ya hatia ni sawasawa na ile ya sadaka ya dhambi: Nyama ya yule mnyama aliyetolewa sadaka ni ya yule kuhani anayesimamia ibada ya upatanisho.
“The regulation is the same for the offerings [to enable people to be forgiven for the sins they have committed] and the offerings for when they are guilty of not giving to me the things that are required to be given to me. The meat of those offerings belongs to the priest who offers them in order that the people will be forgiven.
8 Kuhani anayetoa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuichukua ngozi ya mnyama yule aliyetolewa iwe yake.
The priest who slaughters an animal that will be completely burned on the altar is permitted to keep the animal’s hide for himself.
9 Kila sadaka ya nafaka iliyookwa jikoni au kupikwa katika sufuria au katika kikaangio itakuwa ya kuhani anayeitoa.
Offerings of things made from grain that are baked in an oven or cooked in a pan or (in a shallow pan/on a griddle) belong to the priest who makes those offerings [for another person].
10 Nayo kila sadaka ya nafaka, iwe imechanganywa na mafuta au iko kavu, itakuwa ya wana wa Aroni, nayo itagawanywa sawa kati yao.
And offerings of things made from grain, whether they were mixed with olive oil or not, also belong to the sons of Aaron.”
11 “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya amani ambayo mtu aweza kuileta kwa Bwana:
These are the regulations concerning the offerings that people make to maintain fellowship [with Yahweh]:
12 “‘Ikiwa mtu atatoa sadaka ya amani kwa ajili ya kuonyesha shukrani, pamoja na sadaka hii ya shukrani, atatoa maandazi yasiyotiwa chachu yaliyochanganywa na mafuta, mikate myembamba isiyotiwa chachu iliyopakwa mafuta, maandazi ya unga laini uliokandwa vizuri na kuchanganywa na mafuta.
“If you bring an offering to thank [Yahweh], along with [the animal that you slaughter] you must offer loaves of bread made with olive oil mixed [with the flour] but without yeast, and wafers that are made without yeast but with olive oil smeared on them, and loaves made from fine flour with olive oil well mixed with the flour.
13 Pamoja na sadaka hii ya amani ya shukrani ataleta sadaka ya maandazi yaliyotengenezwa kwa chachu.
Along with that offering to thank Yahweh, you must bring an offering of loaves made with yeast.
14 Ataleta moja ya kila aina ya andazi kama sadaka, matoleo kwa Bwana; hii ni ya kuhani anayenyunyiza damu ya sadaka ya amani.
You must bring one of each kind for an offering to Yahweh, but they belong to the priest who sprinkles against the altar the blood of the animal that is [slaughtered as an offering] to maintain fellowship with Yahweh.
15 Nyama ya sadaka ya amani kwa ajili ya shukrani lazima iliwe siku iyo hiyo inapotolewa; hutabakiza kitu chochote mpaka asubuhi.
The meat of that offering must be eaten on the day that it is offered; none of it should be left to [be eaten on] the next day.
16 “‘Lakini kama sadaka yake ni kwa ajili ya nadhiri au ni sadaka ya hiari, sadaka hiyo italiwa siku hiyo inapotolewa, lakini chochote kinachobakia kinaweza kuliwa kesho yake.
“However, if your offering is the result of a solemn promise that you made to Yahweh, or if it is an offering that you make (voluntarily/without being required to), you are permitted to eat some of the meat on the day it is offered, but anything that is left may be eaten on the next day.
17 Nyama yoyote ya sadaka inayobaki mpaka siku ya tatu lazima iteketezwe kwa moto.
But any meat that is left until the third day must be completely burned.
18 Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani italiwa siku ya tatu, Bwana hataikubali. Haitahesabiwa kwake huyo aliyeitoa, kwa kuwa ni najisi. Mtu atakayekula sehemu yake yoyote atahesabiwa hatia.
If any meat from the offering to maintain fellowship with Yahweh is eaten on the third day, Yahweh will not accept that offering; it will be useless to offer it, because Yahweh will consider that it is worthless. Anyone who eats some of it will have to pay a penalty [to Yahweh].
19 “‘Nyama ile inayogusa chochote ambacho ni najisi kwa kawaida ya ibada kamwe haitaliwa, ni lazima iteketezwe kwa moto. Kuhusu nyama nyingine, mtu yeyote aliye safi kwa kawaida ya ibada anaweza kuila.
“Meat that touches something [that God considers to be] impure must not be eaten; it must be completely burned. Anyone who has performed the rituals to become acceptable to God is allowed to eat other meat [which has been offered as a sacrifice].
20 Lakini kama mtu yeyote najisi akila nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, huyo mtu lazima akatiliwe mbali na watu wake.
But if anyone who has not performed those rituals eats some of the meat of the offering to maintain fellowship with Yahweh, meat that belongs to Yahweh, he must no longer be allowed to associate with God’s people.
21 Kama mtu yeyote akigusa kitu kilicho najisi, iwe ni uchafu wa mwanadamu, au mnyama najisi, au kitu chochote kilicho najisi, kitu cha kuchukiza, kisha akala nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
If anyone touches something that God considers to be impure and very displeasing to him, whether it is from a human or from an animal, and then he eats any of the meat of the offering to maintain fellowship with Yahweh, meat that belongs to Yahweh, he must no longer be allowed to associate with God’s people.”
22 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh also said to Moses/me:
23 “Waambie Waisraeli: ‘Msile mafuta yoyote ya ngʼombe, kondoo wala mbuzi.
“Say this to the Israeli people: ‘Do not eat any of the fat of cattle or sheep or goats.
24 Mafuta ya mnyama aliyekutwa amekufa au ameraruliwa na mnyama pori yanaweza kutumika kwa kazi nyingine yoyote, lakini kamwe msiyale.
The fat of an animal that is found dead or that has been killed by a wild animal may be used for other purposes, but you must not eat it.
25 Mtu yeyote alaye mafuta ya mnyama ambaye ametolewa sadaka kwa Bwana kwa moto ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
Anyone who eats the fat of an animal from which an offering has been made to Yahweh must no longer be allowed to associate with God’s people.
26 Popote mtakapoishi, kamwe msinywe damu ya ndege yeyote wala ya mnyama.
And wherever you live, you must not eat the blood of any bird or animal.
27 Ikiwa mtu yeyote atakunywa damu, mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
If anyone eats blood, he must no longer be allowed to associate with God’s people.’”
28 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh also said to Moses/me,
29 “Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote aletaye sadaka ya amani kwa Bwana ataleta sehemu ya sadaka hiyo kama dhabihu yake kwa Bwana.
“Tell the Israeli people this: ‘Anyone who brings an offering to maintain fellowship with Yahweh must bring part of it to be a sacrifice to Yahweh.
30 Ataleta sadaka kwa mikono yake mwenyewe iliyotolewa kwa Bwana kwa moto; ataleta mafuta ya huyo mnyama pamoja na kidari, naye atainua hicho kidari mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
He himself must bring the offering that will be burned in the fire. He must bring the fat along with the breast of the animal and lift it up in front of Yahweh to indicate that it is an offering to him.
31 Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe.
The Supreme Priest must burn the fat on the altar, but the breast belongs to Aaron and all his sons.
32 Paja la kulia la sadaka zako za amani utampa kuhani kama matoleo.
You must give to the Supreme Priest the right thigh of the animal that is sacrificed to maintain fellowship with Yahweh.
33 Mwana wa Aroni atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani ndiye atakayepewa paja hilo la kulia kuwa fungu lake.
The son of Aaron who offers the blood and the fat of that sacrifice must be given the right thigh of the animal as his share.
34 Kutoka kwenye sadaka za amani za Waisraeli, mimi Mungu nimepokea kidari kile kilichoinuliwa pamoja na lile paja lililotolewa, nami nimevitoa kwa kuhani Aroni na wanawe kuwa fungu lao la kawaida kutoka kwa Waisraeli.’”
From the offerings that the Israeli people give to maintain fellowship with Yahweh, he has declared that he has given to Aaron and his sons the breast that is lifted up and the right thigh that is offered; those portions must always be their regular share from the Israeli people.’”
35 Hii ndiyo sehemu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, ambazo zilitengwa kwa ajili ya Aroni na wanawe siku ile walipowekwa wakfu ili kumtumikia Bwana katika kazi ya ukuhani.
Those are the portions of the offerings brought/given to Yahweh and burned in fire that are allotted to Aaron and his sons on the day that they are set apart to serve Yahweh as priests.
36 Siku ile walipotiwa mafuta, Bwana aliagiza kwamba Waisraeli wawape hili kama fungu lao la kawaida kwa vizazi vijavyo.
Yahweh commands that on the day that the priests are appointed [MTY], the Israeli people must always give those portions to the priests.
37 Basi haya ndiyo masharti kuhusu sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia, sadaka ya kuwekwa wakfu, na sadaka ya amani,
Those are the regulations for the offerings that are to be completely burned on the altar, the offerings made from grain, the offerings to enable people to become acceptable to God again, the offerings for when people are guilty of not giving to Yahweh the things that are required to be given to him, the offerings given when the priests are appointed, and the offerings to maintain fellowship with Yahweh.
38 ambayo Bwana alimpa Mose juu ya Mlima Sinai siku ile alipowaagiza Waisraeli walete sadaka zao kwa Bwana, katika Jangwa la Sinai.
They are regulations that Yahweh gave to Moses/me on Sinai Mountain in the Sinai Desert, on the day that he commanded the Israeli people to start bringing their offerings to him.

< Mambo ya Walawi 7 >