< Mambo ya Walawi 7 >

1 “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya hatia, ambayo ni takatifu sana:
And this is the law of the guilt-offering: it is most holy.
2 Sadaka ya hatia itachinjiwa mahali pale ambapo sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, nayo damu yake itanyunyizwa pande zote za madhabahu.
In the place where they kill the burnt-offering shall they kill the guilt-offering: and the blood thereof shall be dashed against the altar round about.
3 Mafuta yake yote yatatolewa sadaka: mafuta ya mkia na mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani,
And he shall offer of it all the fat thereof: the fat tail, and the fat that covereth the inwards,
4 figo zote mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo yataondolewa pamoja na hizo figo.
and the two kidneys, and the fat that is on them, which is by the loins, and the lobe above the liver, which he shall take away by the kidneys.
5 Kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kuwa sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia.
And the priest shall make them smoke upon the altar for an offering made by fire unto the LORD; it is a guilt-offering.
6 Mwanaume yeyote katika jamaa ya kuhani aweza kuila, lakini lazima iliwe mahali patakatifu; ni takatifu sana.
Every male among the priests may eat thereof; it shall be eaten in a holy place; it is most holy.
7 “‘Sheria hii ya sadaka ya hatia ni sawasawa na ile ya sadaka ya dhambi: Nyama ya yule mnyama aliyetolewa sadaka ni ya yule kuhani anayesimamia ibada ya upatanisho.
As is the sin-offering, so is the guilt-offering; there is one law for them; the priest that maketh atonement therewith, he shall have it.
8 Kuhani anayetoa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuichukua ngozi ya mnyama yule aliyetolewa iwe yake.
And the priest that offereth any man's burnt-offering, even the priest shall have to himself the skin of the burnt-offering which he hath offered.
9 Kila sadaka ya nafaka iliyookwa jikoni au kupikwa katika sufuria au katika kikaangio itakuwa ya kuhani anayeitoa.
And every meal-offering that is baked in the oven, and all that is dressed in the stewing-pan, and on the griddle, shall be the priest's that offereth it.
10 Nayo kila sadaka ya nafaka, iwe imechanganywa na mafuta au iko kavu, itakuwa ya wana wa Aroni, nayo itagawanywa sawa kati yao.
And every meal-offering, mingled with oil, or dry, shall all the sons of Aaron have, one as well as another.
11 “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya amani ambayo mtu aweza kuileta kwa Bwana:
And this is the law of the sacrifice of peace-offerings, which one may offer unto the LORD.
12 “‘Ikiwa mtu atatoa sadaka ya amani kwa ajili ya kuonyesha shukrani, pamoja na sadaka hii ya shukrani, atatoa maandazi yasiyotiwa chachu yaliyochanganywa na mafuta, mikate myembamba isiyotiwa chachu iliyopakwa mafuta, maandazi ya unga laini uliokandwa vizuri na kuchanganywa na mafuta.
If he offer it for a thanksgiving, then he shall offer with the sacrifice of thanksgiving unleavened cakes mingled with oil, and unleavened wafers spread with oil, and cakes mingled with oil, of fine flour soaked.
13 Pamoja na sadaka hii ya amani ya shukrani ataleta sadaka ya maandazi yaliyotengenezwa kwa chachu.
With cakes of leavened bread he shall present his offering with the sacrifice of his peace-offerings for thanksgiving.
14 Ataleta moja ya kila aina ya andazi kama sadaka, matoleo kwa Bwana; hii ni ya kuhani anayenyunyiza damu ya sadaka ya amani.
And of it he shall present one out of each offering for a gift unto the LORD; it shall be the priest's that dasheth the blood of the peace-offerings against the altar.
15 Nyama ya sadaka ya amani kwa ajili ya shukrani lazima iliwe siku iyo hiyo inapotolewa; hutabakiza kitu chochote mpaka asubuhi.
And the flesh of the sacrifice of his peace-offerings for thanksgiving shall be eaten on the day of his offering; he shall not leave any of it until the morning.
16 “‘Lakini kama sadaka yake ni kwa ajili ya nadhiri au ni sadaka ya hiari, sadaka hiyo italiwa siku hiyo inapotolewa, lakini chochote kinachobakia kinaweza kuliwa kesho yake.
But if the sacrifice of his offering be a vow, or a freewill-offering, it shall be eaten on the day that he offereth his sacrifice; and on the morrow that which remaineth of it may be eaten.
17 Nyama yoyote ya sadaka inayobaki mpaka siku ya tatu lazima iteketezwe kwa moto.
But that which remaineth of the flesh of the sacrifice on the third day shall be burnt with fire.
18 Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani italiwa siku ya tatu, Bwana hataikubali. Haitahesabiwa kwake huyo aliyeitoa, kwa kuwa ni najisi. Mtu atakayekula sehemu yake yoyote atahesabiwa hatia.
And if any of the flesh of the sacrifice of his peace-offerings be at all eaten on the third day, it shall not be accepted, neither shall it be imputed unto him that offereth it; it shall be an abhorred thing, and the soul that eateth of it shall bear his iniquity.
19 “‘Nyama ile inayogusa chochote ambacho ni najisi kwa kawaida ya ibada kamwe haitaliwa, ni lazima iteketezwe kwa moto. Kuhusu nyama nyingine, mtu yeyote aliye safi kwa kawaida ya ibada anaweza kuila.
And the flesh that toucheth any unclean thing shall not be eaten; it shall be burnt with fire. And as for the flesh, every one that is clean may eat thereof.
20 Lakini kama mtu yeyote najisi akila nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, huyo mtu lazima akatiliwe mbali na watu wake.
But the soul that eateth of the flesh of the sacrifice of peace-offerings, that pertain unto the LORD, having his uncleanness upon him, that soul shall be cut off from his people.
21 Kama mtu yeyote akigusa kitu kilicho najisi, iwe ni uchafu wa mwanadamu, au mnyama najisi, au kitu chochote kilicho najisi, kitu cha kuchukiza, kisha akala nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
And when any one shall touch any unclean thing, whether it be the uncleanness of man, or an unclean beast, or any unclean detestable thing, and eat of the flesh of the sacrifice of peace-offerings, which pertain unto the LORD, that soul shall be cut off from his people.
22 Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
23 “Waambie Waisraeli: ‘Msile mafuta yoyote ya ngʼombe, kondoo wala mbuzi.
Speak unto the children of Israel, saying: Ye shall eat no fat, of ox, or sheep, or goat.
24 Mafuta ya mnyama aliyekutwa amekufa au ameraruliwa na mnyama pori yanaweza kutumika kwa kazi nyingine yoyote, lakini kamwe msiyale.
And the fat of that which dieth of itself, and the fat of that which is torn of beasts, may be used for any other service; but ye shall in no wise eat of it.
25 Mtu yeyote alaye mafuta ya mnyama ambaye ametolewa sadaka kwa Bwana kwa moto ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
For whosoever eateth the fat of the beast, of which men present an offering made by fire unto the LORD, even the soul that eateth it shall be cut off from his people.
26 Popote mtakapoishi, kamwe msinywe damu ya ndege yeyote wala ya mnyama.
And ye shall eat no manner of blood, whether it be of fowl or of beast, in any of your dwellings.
27 Ikiwa mtu yeyote atakunywa damu, mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
Whosoever it be that eateth any blood, that soul shall be cut off from his people.
28 Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
29 “Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote aletaye sadaka ya amani kwa Bwana ataleta sehemu ya sadaka hiyo kama dhabihu yake kwa Bwana.
Speak unto the children of Israel, saying: He that offereth his sacrifice of peace-offerings unto the LORD shall bring his offering unto the LORD out of his sacrifice of peace-offerings.
30 Ataleta sadaka kwa mikono yake mwenyewe iliyotolewa kwa Bwana kwa moto; ataleta mafuta ya huyo mnyama pamoja na kidari, naye atainua hicho kidari mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
His own hands shall bring the offerings of the LORD made by fire: the fat with the breast shall he bring, that the breast may be waved for a wave-offering before the LORD.
31 Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe.
And the priest shall make the fat smoke upon the altar; but the breast shall be Aaron's and his sons'.
32 Paja la kulia la sadaka zako za amani utampa kuhani kama matoleo.
And the right thigh shall ye give unto the priest for a heave-offering out of your sacrifices of peace-offerings.
33 Mwana wa Aroni atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani ndiye atakayepewa paja hilo la kulia kuwa fungu lake.
He among the sons of Aaron, that offereth the blood of the peace-offerings, and the fat, shall have the right thigh for a portion.
34 Kutoka kwenye sadaka za amani za Waisraeli, mimi Mungu nimepokea kidari kile kilichoinuliwa pamoja na lile paja lililotolewa, nami nimevitoa kwa kuhani Aroni na wanawe kuwa fungu lao la kawaida kutoka kwa Waisraeli.’”
For the breast of waving and the thigh of heaving have I taken of the children of Israel out of their sacrifices of peace-offerings, and have given them unto Aaron the priest and unto his sons as a due for ever from the children of Israel.
35 Hii ndiyo sehemu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, ambazo zilitengwa kwa ajili ya Aroni na wanawe siku ile walipowekwa wakfu ili kumtumikia Bwana katika kazi ya ukuhani.
This is the consecrated portion of Aaron, and the consecrated portion of his sons, out of the offerings of the LORD made by fire, in the day when they were presented to minister unto the LORD in the priest's office;
36 Siku ile walipotiwa mafuta, Bwana aliagiza kwamba Waisraeli wawape hili kama fungu lao la kawaida kwa vizazi vijavyo.
which the LORD commanded to be given them of the children of Israel, in the day that they were anointed. It is a due for ever throughout their generations.
37 Basi haya ndiyo masharti kuhusu sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia, sadaka ya kuwekwa wakfu, na sadaka ya amani,
This is the law of the burnt-offering, of the meal-offering, and of the sin-offering, and of the guilt-offering, and of the consecration-offering, and of the sacrifice of peace-offerings;
38 ambayo Bwana alimpa Mose juu ya Mlima Sinai siku ile alipowaagiza Waisraeli walete sadaka zao kwa Bwana, katika Jangwa la Sinai.
which the LORD commanded Moses in mount Sinai, in the day that he commanded the children of Israel to present their offerings unto the LORD, in the wilderness of Sinai.

< Mambo ya Walawi 7 >