< Mambo ya Walawi 7 >

1 “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya hatia, ambayo ni takatifu sana:
Likewise, this is the law of the sacrifice for a transgression. It is the Holy of holies.
2 Sadaka ya hatia itachinjiwa mahali pale ambapo sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, nayo damu yake itanyunyizwa pande zote za madhabahu.
Therefore, where the holocaust is immolated, the victim for a transgression shall also be slain. Its blood shall be poured out all around the altar.
3 Mafuta yake yote yatatolewa sadaka: mafuta ya mkia na mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani,
They shall offer from it: the rump, and the fat that covers the vital organs,
4 figo zote mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo yataondolewa pamoja na hizo figo.
the two little kidneys, and the fat that is near the sides, and the mesh of the liver with the little kidneys.
5 Kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kuwa sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia.
And the priest shall burn them upon the altar. It is the incense of the Lord on behalf of a transgression.
6 Mwanaume yeyote katika jamaa ya kuhani aweza kuila, lakini lazima iliwe mahali patakatifu; ni takatifu sana.
Every male of priestly descent shall feed on this flesh in a holy place, because it is the Holy of holies.
7 “‘Sheria hii ya sadaka ya hatia ni sawasawa na ile ya sadaka ya dhambi: Nyama ya yule mnyama aliyetolewa sadaka ni ya yule kuhani anayesimamia ibada ya upatanisho.
Just as the sacrifice for sin is offered, so also for a transgression; one law shall be for both sacrifices. It shall belong to the priest who offers it.
8 Kuhani anayetoa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuichukua ngozi ya mnyama yule aliyetolewa iwe yake.
The priest who offers the victim of holocaust shall have its skin.
9 Kila sadaka ya nafaka iliyookwa jikoni au kupikwa katika sufuria au katika kikaangio itakuwa ya kuhani anayeitoa.
And every sacrifice of fine wheat flour which is baked in the oven, and whatever is prepared on the oven grating or in the frying pan, shall be for the priest who offers it.
10 Nayo kila sadaka ya nafaka, iwe imechanganywa na mafuta au iko kavu, itakuwa ya wana wa Aroni, nayo itagawanywa sawa kati yao.
Whether these will be sprinkled with oil, or left dry, an equal measure shall be divided to each one of the sons of Aaron.
11 “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya amani ambayo mtu aweza kuileta kwa Bwana:
This is the law of the victim of peace offerings, which is offered to the Lord.
12 “‘Ikiwa mtu atatoa sadaka ya amani kwa ajili ya kuonyesha shukrani, pamoja na sadaka hii ya shukrani, atatoa maandazi yasiyotiwa chachu yaliyochanganywa na mafuta, mikate myembamba isiyotiwa chachu iliyopakwa mafuta, maandazi ya unga laini uliokandwa vizuri na kuchanganywa na mafuta.
If the oblation will be an act for giving thanks, they shall offer bread without leaven sprinkled with oil, and unleavened wafers anointed with oil, and fine wheat flour fried, and cakes sprinkled and mixed with oil,
13 Pamoja na sadaka hii ya amani ya shukrani ataleta sadaka ya maandazi yaliyotengenezwa kwa chachu.
and also, leavened bread with the sacrifice of thanksgiving, which is immolated for peace offerings.
14 Ataleta moja ya kila aina ya andazi kama sadaka, matoleo kwa Bwana; hii ni ya kuhani anayenyunyiza damu ya sadaka ya amani.
Of these, one shall be offered to the Lord as the first-fruits, and one shall be for the priest who will pour out the blood of the victim.
15 Nyama ya sadaka ya amani kwa ajili ya shukrani lazima iliwe siku iyo hiyo inapotolewa; hutabakiza kitu chochote mpaka asubuhi.
The flesh of it shall be eaten on the same day; neither shall any of it remain until morning.
16 “‘Lakini kama sadaka yake ni kwa ajili ya nadhiri au ni sadaka ya hiari, sadaka hiyo italiwa siku hiyo inapotolewa, lakini chochote kinachobakia kinaweza kuliwa kesho yake.
If anyone, by a vow or of his own accord, will have offered a sacrifice, it shall be eaten in a similar manner on the same day. But then if any of it will have remained until tomorrow, it is lawful to eat it.
17 Nyama yoyote ya sadaka inayobaki mpaka siku ya tatu lazima iteketezwe kwa moto.
Then whatever will be found on the third day shall be consumed with fire.
18 Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani italiwa siku ya tatu, Bwana hataikubali. Haitahesabiwa kwake huyo aliyeitoa, kwa kuwa ni najisi. Mtu atakayekula sehemu yake yoyote atahesabiwa hatia.
If anyone will have eaten from the flesh of the victim of peace offerings on the third day, the oblation will be nullified; neither will it benefit the one who offered it. But instead, whatever soul will contaminate itself with such foods will be guilty of a betrayal.
19 “‘Nyama ile inayogusa chochote ambacho ni najisi kwa kawaida ya ibada kamwe haitaliwa, ni lazima iteketezwe kwa moto. Kuhusu nyama nyingine, mtu yeyote aliye safi kwa kawaida ya ibada anaweza kuila.
The flesh that has touched anything unclean shall not be eaten, but it shall be burnt with fire. He that is clean will feed on it.
20 Lakini kama mtu yeyote najisi akila nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, huyo mtu lazima akatiliwe mbali na watu wake.
If a soul which is polluted will have eaten from the flesh of the sacrifice of peace offerings, which is offered to the Lord, he shall perish from his people.
21 Kama mtu yeyote akigusa kitu kilicho najisi, iwe ni uchafu wa mwanadamu, au mnyama najisi, au kitu chochote kilicho najisi, kitu cha kuchukiza, kisha akala nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
And whoever will have touched the uncleanness of man, or of beast, or of anything which is able to defile, and who will have eaten from this kind of flesh, shall be cut off from his people.
22 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke to Moses, saying:
23 “Waambie Waisraeli: ‘Msile mafuta yoyote ya ngʼombe, kondoo wala mbuzi.
Say to the sons of Israel: The fat of a sheep, and of an ox, and of a goat you shall not eat.
24 Mafuta ya mnyama aliyekutwa amekufa au ameraruliwa na mnyama pori yanaweza kutumika kwa kazi nyingine yoyote, lakini kamwe msiyale.
The fat of a carcass that has died on its own, or of an animal that has been seized by a wild beast, you shall have for various uses.
25 Mtu yeyote alaye mafuta ya mnyama ambaye ametolewa sadaka kwa Bwana kwa moto ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
If anyone will have eaten the fat which ought to be offered as a burnt sacrifice of the Lord, he shall perish from his people.
26 Popote mtakapoishi, kamwe msinywe damu ya ndege yeyote wala ya mnyama.
Likewise, you shall not take as food the blood of any animals at all, whether of birds or beasts.
27 Ikiwa mtu yeyote atakunywa damu, mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
Every soul that will have eaten blood shall perish from his people.
28 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke to Moses, saying:
29 “Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote aletaye sadaka ya amani kwa Bwana ataleta sehemu ya sadaka hiyo kama dhabihu yake kwa Bwana.
Speak to the sons of Israel, saying: Whoever offers a victim of peace offerings to the Lord, let him also offer at the same time a sacrifice, that is, its libations.
30 Ataleta sadaka kwa mikono yake mwenyewe iliyotolewa kwa Bwana kwa moto; ataleta mafuta ya huyo mnyama pamoja na kidari, naye atainua hicho kidari mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
He shall hold in his hands the fat of the victim, and the breast. And when he will have offered and consecrated both to the Lord, he shall deliver them to the priest,
31 Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe.
who shall burn the fat upon the altar. But the breast shall be for Aaron and his sons.
32 Paja la kulia la sadaka zako za amani utampa kuhani kama matoleo.
Likewise also, the right shoulder of the victim of peace offerings shall fall to the priest as first-fruits.
33 Mwana wa Aroni atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani ndiye atakayepewa paja hilo la kulia kuwa fungu lake.
Among the sons of Aaron, whoever will have offered the blood and the fat, the same one shall also have the right shoulder for his portion.
34 Kutoka kwenye sadaka za amani za Waisraeli, mimi Mungu nimepokea kidari kile kilichoinuliwa pamoja na lile paja lililotolewa, nami nimevitoa kwa kuhani Aroni na wanawe kuwa fungu lao la kawaida kutoka kwa Waisraeli.’”
So then, the breast that is lifted up, and the shoulder that is separated, I have taken from the sons of Israel, from their victims of peace offerings, and I have given these to Aaron the priest and to his sons, as a law in perpetuity, from all the people of Israel.
35 Hii ndiyo sehemu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, ambazo zilitengwa kwa ajili ya Aroni na wanawe siku ile walipowekwa wakfu ili kumtumikia Bwana katika kazi ya ukuhani.
This is the anointing of Aaron and his sons, by the ceremonies of the Lord, in the day when Moses offered them, so that they may fulfill the priesthood,
36 Siku ile walipotiwa mafuta, Bwana aliagiza kwamba Waisraeli wawape hili kama fungu lao la kawaida kwa vizazi vijavyo.
and this is what the Lord instructed to be given to them by the sons of Israel, as a perpetual observance in their generations.
37 Basi haya ndiyo masharti kuhusu sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia, sadaka ya kuwekwa wakfu, na sadaka ya amani,
This is the law of the holocaust, and of the sacrifice for sin, and for transgression, and for consecration, and for the victims of peace offerings,
38 ambayo Bwana alimpa Mose juu ya Mlima Sinai siku ile alipowaagiza Waisraeli walete sadaka zao kwa Bwana, katika Jangwa la Sinai.
which the Lord appointed to Moses on mount Sinai, when he commanded the sons of Israel to offer their oblations to the Lord in the desert of Sinai.

< Mambo ya Walawi 7 >