< Mambo ya Walawi 7 >

1 “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya hatia, ambayo ni takatifu sana:
Dette er Loven om Skyldofferet. Det er højhelligt
2 Sadaka ya hatia itachinjiwa mahali pale ambapo sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, nayo damu yake itanyunyizwa pande zote za madhabahu.
Der, hvor Brændofferet slagtes, skal Skyldofferet slagtes. Dets Blod skal sprænges rundt om på Alteret,
3 Mafuta yake yote yatatolewa sadaka: mafuta ya mkia na mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani,
og alt dets Fedt skal frembæres. Fedthalen, Fedtet, der dækker Indvoldene, og alt Fedtet på Indvoldene,
4 figo zote mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo yataondolewa pamoja na hizo figo.
begge Nyrerne med det Fedt, som sidder på dem ved Lændemusklerne, og Leverlappen, som skal skilles fra ved Nyrerne.
5 Kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kuwa sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia.
Og Præsten skal bringe det som Røgoffer på Alteret, et Ildoffer for HERREN. Det er et Skyldoffer.
6 Mwanaume yeyote katika jamaa ya kuhani aweza kuila, lakini lazima iliwe mahali patakatifu; ni takatifu sana.
Alle af Mandkøn blandt Præsterne må spise det; på et helligt Sted skal det spises; det er højhelligt.
7 “‘Sheria hii ya sadaka ya hatia ni sawasawa na ile ya sadaka ya dhambi: Nyama ya yule mnyama aliyetolewa sadaka ni ya yule kuhani anayesimamia ibada ya upatanisho.
Det er med Skyldofferet som med Syndofferet, en og samme Lov gælder for dem: Det tilfalder den Præst, der skaffer Soning ved det.
8 Kuhani anayetoa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuichukua ngozi ya mnyama yule aliyetolewa iwe yake.
Den Præst, som frembærer nogens Brændoffer, ham skal Huden af det Brændoffer, han frembærer, tilfalde.
9 Kila sadaka ya nafaka iliyookwa jikoni au kupikwa katika sufuria au katika kikaangio itakuwa ya kuhani anayeitoa.
Ethvert Afgrødeoffer, der bages i Ovnen, eller som er tilberedt i Pande eller på Plade, tilfalder den Præst, der frembærer det;
10 Nayo kila sadaka ya nafaka, iwe imechanganywa na mafuta au iko kavu, itakuwa ya wana wa Aroni, nayo itagawanywa sawa kati yao.
men ethvert Afgrødeoffer, der er rørt i Olie eller tørt, tilfalder alle Arons Sønner, den ene lige så vel som den anden.
11 “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya amani ambayo mtu aweza kuileta kwa Bwana:
Dette er Loven om Takofferet, som bringes HERREN.
12 “‘Ikiwa mtu atatoa sadaka ya amani kwa ajili ya kuonyesha shukrani, pamoja na sadaka hii ya shukrani, atatoa maandazi yasiyotiwa chachu yaliyochanganywa na mafuta, mikate myembamba isiyotiwa chachu iliyopakwa mafuta, maandazi ya unga laini uliokandwa vizuri na kuchanganywa na mafuta.
Hvis det bringes som Lovprisningsoffer, skal han sammen med Slagtofferet, der hører til hans Lovprisningsoffer, frembære usyrede Kager, rørte i Olie, usyrede Fladbrød, smurte med Olie, og fint Hvedemel, æltet til Kager, rørte i Olie;
13 Pamoja na sadaka hii ya amani ya shukrani ataleta sadaka ya maandazi yaliyotengenezwa kwa chachu.
sammen med syrede Brødkager skal han frembære sin Offergave som sit Lovprisningstakoffer.
14 Ataleta moja ya kila aina ya andazi kama sadaka, matoleo kwa Bwana; hii ni ya kuhani anayenyunyiza damu ya sadaka ya amani.
Han skal deraf frembære een Kage af hver Offergave som en Offerydelse til HERREN; den tilfalder den Præst, der sprænger Blodet af Takofferet på Alteret.
15 Nyama ya sadaka ya amani kwa ajili ya shukrani lazima iliwe siku iyo hiyo inapotolewa; hutabakiza kitu chochote mpaka asubuhi.
Kødet af hans Lovprisningstakoffer skal spises på selve Offerdagen, intet de1af må gemmes til næste Morgen.
16 “‘Lakini kama sadaka yake ni kwa ajili ya nadhiri au ni sadaka ya hiari, sadaka hiyo italiwa siku hiyo inapotolewa, lakini chochote kinachobakia kinaweza kuliwa kesho yake.
Er hans Offergaver derimod et Løfteoffer eller et Frivilligoffer, skal det vel spises på selve Offerdagen, men hvad der levnes, må spises Dagen efter;
17 Nyama yoyote ya sadaka inayobaki mpaka siku ya tatu lazima iteketezwe kwa moto.
men hvad der så er tilbage af Offerkødet, skal opbrændes på den tredje Dag;
18 Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani italiwa siku ya tatu, Bwana hataikubali. Haitahesabiwa kwake huyo aliyeitoa, kwa kuwa ni najisi. Mtu atakayekula sehemu yake yoyote atahesabiwa hatia.
og hvis der spises noget af hans Takoffers Kød på den tredje Dag, så vil den, som bringer Offeret, ikke kunne finde Guds Velbehag, det skal ikke tilregnes ham, men regnes for urent Kød, og den, der spiser deraf, skal undgælde for sin Brøde.
19 “‘Nyama ile inayogusa chochote ambacho ni najisi kwa kawaida ya ibada kamwe haitaliwa, ni lazima iteketezwe kwa moto. Kuhusu nyama nyingine, mtu yeyote aliye safi kwa kawaida ya ibada anaweza kuila.
Det Kød, der kommer i Berøring med noget som helst urent, må ikke spises, det skal opbrændes. I øvrigt må enhver, der er ren, spise Kødet;
20 Lakini kama mtu yeyote najisi akila nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, huyo mtu lazima akatiliwe mbali na watu wake.
men enhver, som i uren Tilstand spiser Kød af HERRENs Takoffer, skal udryddes af sin Slægt;
21 Kama mtu yeyote akigusa kitu kilicho najisi, iwe ni uchafu wa mwanadamu, au mnyama najisi, au kitu chochote kilicho najisi, kitu cha kuchukiza, kisha akala nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
og når nogen rører ved noget urent, enten menneskelig Urenhed eller urent Kvæg eller nogen Slags urent Kryb, og så spiser Kød af HERRENs Takoffer, skal han udryddes af sin Slægt.
22 Bwana akamwambia Mose,
HERREN talede fremdeles til Moses og sagde:
23 “Waambie Waisraeli: ‘Msile mafuta yoyote ya ngʼombe, kondoo wala mbuzi.
Tal til Israeliterne og sig: I må ikke spise noget som helst Fedt af Okser, Får eller Geder.
24 Mafuta ya mnyama aliyekutwa amekufa au ameraruliwa na mnyama pori yanaweza kutumika kwa kazi nyingine yoyote, lakini kamwe msiyale.
Fedt af selvdøde og sønderrevne Dyr må bruges til alt, men I må under ingen Omstændigheder spise det.
25 Mtu yeyote alaye mafuta ya mnyama ambaye ametolewa sadaka kwa Bwana kwa moto ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
Thi enhver, der spiser Fedtet af det Kvæg, hvoraf der bringes HERREN Ildofre, den, der spiser noget deraf, skal udryddes af sit Folk.
26 Popote mtakapoishi, kamwe msinywe damu ya ndege yeyote wala ya mnyama.
Og I må heller ikke nyde noget som helst Blod af Fugle eller Kvæg, hvor I end opholder eder;
27 Ikiwa mtu yeyote atakunywa damu, mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.’”
enhver, der nyder noget som helst Blod, skal udryddes af sin Slægt.
28 Bwana akamwambia Mose,
HERREN talede fremdeles til Moses og sagde:
29 “Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote aletaye sadaka ya amani kwa Bwana ataleta sehemu ya sadaka hiyo kama dhabihu yake kwa Bwana.
Tal til Israeliterne og sig: Den, der bringer HERREN sit Takoffer, skal af sit Takoffer frembære for HERREN den ham tilkommende Offergave;
30 Ataleta sadaka kwa mikono yake mwenyewe iliyotolewa kwa Bwana kwa moto; ataleta mafuta ya huyo mnyama pamoja na kidari, naye atainua hicho kidari mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
med egne Hænder skal han frembære HERRENs Ildofre. Han skal frembære Fedtet tillige med Brystet; Brystet, for at Svingningen kan udføres dermed for HERRENs Åsyn;
31 Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe.
og Præsten skal bringe Fedtet som Røgoffer på Alteret, men Brystet skal tilfalde Aron og hans Sønner.
32 Paja la kulia la sadaka zako za amani utampa kuhani kama matoleo.
Desuden skal I give Præsten højre Kølle som Offerydelse af eders Takofre.
33 Mwana wa Aroni atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani ndiye atakayepewa paja hilo la kulia kuwa fungu lake.
Den af Arons Sønner, der frembærer Takofferets Blod og Fedtet, ham tilfalder højre Kølle som hans Del.
34 Kutoka kwenye sadaka za amani za Waisraeli, mimi Mungu nimepokea kidari kile kilichoinuliwa pamoja na lile paja lililotolewa, nami nimevitoa kwa kuhani Aroni na wanawe kuwa fungu lao la kawaida kutoka kwa Waisraeli.’”
Thi Svingningsbrystet og Offerydelseskøllen tager jeg fra Israeliterne af deres Takofre og giver dem til Præsten Aron og hans Sønner, en evig gyldig Rettighed, som de har Krav på hos Israeliterne.
35 Hii ndiyo sehemu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, ambazo zilitengwa kwa ajili ya Aroni na wanawe siku ile walipowekwa wakfu ili kumtumikia Bwana katika kazi ya ukuhani.
Det er Arons og hans Sønners Del af HERRENs Ildofre, den, som blev givet dem, den dag han lod dem træde frem for at gøre Præstetjeneste for HERREN,
36 Siku ile walipotiwa mafuta, Bwana aliagiza kwamba Waisraeli wawape hili kama fungu lao la kawaida kwa vizazi vijavyo.
den, som HERREN, den Dag han salvede dem, bød Israeliterne at give dem, en evig gyldig Rettighed, som de har Krav på fra Slægt til Slægt.
37 Basi haya ndiyo masharti kuhusu sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia, sadaka ya kuwekwa wakfu, na sadaka ya amani,
Det er Loven om Brændofferet, Afgrødeofferet, Syndofferet, Skyldofferet, Indsættelsesofferet og Takofferet,
38 ambayo Bwana alimpa Mose juu ya Mlima Sinai siku ile alipowaagiza Waisraeli walete sadaka zao kwa Bwana, katika Jangwa la Sinai.
som HERREN pålagde Moses på Sinaj Bjerg, den Dag han bød Israeliterne at bringe HERREN deres Offergaver i Sinaj Ørken.

< Mambo ya Walawi 7 >