< Mambo ya Walawi 6 >

1 Bwana akamwambia Mose:
Un Tas Kungs runāja uz Mozu un sacīja:
2 “Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
Ja kas laban apgrēkotos un pret To Kungu noziegtos un noliegtu savam tuvākam to, kas pie viņa nolikts, vai viņa rokā iedots, vai laupīts, vai ar ko viņš savu tuvāko piekrāpis,
3 au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
Vai kad viņš ko pazudušu atradis un to noliedzis, vai nepatiesi zvērējis kādas lietas dēļ, ko cilvēks dara apgrēkodamies,
4 wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
Kad tas tā apgrēkojies un noziedzies, tad tam būs atdot to laupījumu, ko viņš laupījis vai to, ar ko viņš piekrāpis, vai to nolikto, kas pie viņa nolikts, vai to pazudušo, ko viņš atradis,
5 au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
Vai visu to, par ko viņš nepatiesi zvērējis, to visu viņam būs atdot un piekto daļu pielikt klāt; tam, kam tas pieder, to būs viņam dot sava nozieguma upura dienā.
6 Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
Un par savu noziegumu tam būs nest Tam Kungam pie priestera no sava ganāmā pulka aunu, kas bez vainas pēc tava sprieduma par nozieguma upuri.
7 Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
Un priesterim to būs salīdzināt Tā Kunga priekšā, tad viņam taps piedots viss, ko viņš darījis noziegdamies.
8 Bwana akamwambia Mose:
Un Tas Kungs runāja uz Mozu un sacīja:
9 “Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
Pavēli Āronam un viņa dēliem un saki: šis ir tas dedzināmā upura likums. Šim dedzināmam upurim uz altāra būs degt visu nakti līdz rītam, un ar to altāra uguns paliks degošs.
10 Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
Un priesterim būs apvilkt savas nātnu(linu) drēbes un tās linu ūzas uz savu miesu un saņemt tos pelnus, kad uguns uz altāra sadedzinājis dedzināmo upuri un nobērt tos altārim sānis.
11 Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
Tad viņam būs novilkt savas drēbes un citas drēbes apvilkt, un tos pelnus iznest ārā no lēģera kādā šķīstā vietā.
12 Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
Un ugunij uz altāra tā būs palikt degošam un nebūs izdzist. Tur virsū priesterim ik rītu malku būs iededzināt, un uz to būs likt dedzināmo upuri un uz tā iededzināt pateicības upura taukus.
13 Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
Ugunij uz altāra vienmēr būs degt un nebūs izdzist.
14 “‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
Šis nu ir tas ēdamā upura likums: Ārona dēliem to būs upurēt priekš Tā Kunga, altāra priekšā.
15 Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Un būs ņemt pilnu sauju no tā, no ēdamā upura kviešu miltiem un no viņa eļļas, un visu to vīraku, kas uz tā ēdamā upura, un to iededzināt uz altāra, par saldu smaržu, par piemiņu Tam Kungam.
16 Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
Un kas no tā atlicies, to būs ēst Āronam un viņa dēliem; neraudzētu to būs ēst svētā vietā, saiešanas telts pagalmā tiem to būs ēst.
17 Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
To nebūs cept ar raugu. Šī ir viņu daļa, ko Es tiem esmu devis no Saviem uguns upuriem; tas ir augsti svēts, itin kā grēku upuris un kā nozieguma upuris.
18 Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
Visiem vīriešiem starp Ārona dēliem to būs ēst; tas lai ir par likumu uz jūsu pēcnākamiem mūžam, no Tā Kunga uguns upuriem: ikviens, kas tos aizskars, lai ir svēts.
19 Tena Bwana akamwambia Mose,
Un Tas Kungs runāja uz Mozu un sacīja:
20 “Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
Šis ir Ārona un viņa dēlu upuris, ko tiem būs upurēt Tam Kungam savā svaidāmā dienā: vienas ēfas desmitā tiesa kviešu miltu dienišķam ēdamam upurim, viena puse rītā un otra puse vakarā.
21 Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
To būs sataisīt pannā ar eļļu, iejauktu tev to būs nest, un tā ēdamā upura ceptos gabalus tev būs upurēt Tam Kungam par saldu smaržu.
22 Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
Un tam priesterim, kas no viņa dēliem viņa vietā top svaidīts, to būs darīt; tas lai ir likums mūžam; - to būs veselu sadedzināt Tam Kungam.
23 Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
Jo ikkatra priestera ēdamo upuri būs veselu sadedzināt, to nebūs ēst.
24 Bwana akamwambia Mose,
Un Tas Kungs runāja uz Mozu un sacīja:
25 “Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
Runā uz Āronu un uz viņa dēliem un saki: šis ir tas grēku upura likums. Tai vietā, kur dedzināmais upuris top nokauts, būs arī nokaut grēku upuri Tā Kunga priekšā; tas ir augsti svēts.
26 Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
Tam priesterim, kas grēku upuri upurē, to būs ēst, svētā vietā to būs ēst, saiešanas telts pagalmā.
27 Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
Ikviens kas viņa gaļu aizskar, būs svēts un ja kas no viņa asinīm slacīs uz kādām drēbēm, tad to, ko viņš ir apslacījis, būs mazgāt svētā vietā.
28 Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
Un to podu, kur tas vārīts, būs sasist; bet ja tas ir vara traukā vārīts, tad to būs berzt un ar ūdeni skalot.
29 Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
Visiem, kas no vīriešu kārtas starp priesteriem, to būs ēst; tas ir augsti svēts.
30 Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.
Bet visus tos grēku upurus, no kuru asinīm ienes saiešanas teltī par salīdzināšanu svētā vietā, tos nebūs ēst, bet sadedzināt ar uguni.

< Mambo ya Walawi 6 >