< Mambo ya Walawi 6 >
Yahweh spoke to Moses, saying,
2 “Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
“If anyone sins and acts unfaithfully against Yahweh by deceiving his neighbor regarding something held in trust, or was left in his care, or about something that was stolen, or if he has oppressed his neighbor,
3 au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
or he has found something that his neighbor lost and lies about it, or if he swears falsely, or in any matters like these by which people sin,
4 wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
and if he has sinned and is found to be guilty, he must restore whatever he took by robbery or oppression, or that which was entrusted to him, or that which was lost but that he had found.
5 au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
In addition, in any matter in which he swore falsely, he must restore it in full and he must add one-fifth of the value of it and pay it all to the owner on the day that he is found guilty.
6 Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
Then he must bring his guilt offering to Yahweh, a ram without blemish from the flock that is worth the current value, as a guilt offering to the priest.
7 Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
The priest will make atonement for him before Yahweh, and he will be forgiven concerning whatever he has become guilty of doing.”
Then Yahweh spoke to Moses, saying,
9 “Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
“Command Aaron and his sons, saying, 'This is the law of the burnt offering: The burnt offering must be on the hearth of the altar all night until morning, and the fire of the altar will be kept burning.
10 Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
The priest will put on his linen clothes, and he will also put on his linen underclothes. He will pick up the ashes that are left after the fire has consumed the burnt offering on the altar, and he will put the ashes beside the altar.
11 Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
He will take off his garments and put on other garments to carry the ashes outside the camp to a place that is clean.
12 Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
The fire on the altar will be kept burning. It must not go out, and the priest will burn wood on it every morning. He will arrange the burnt offering as required on it, and he will burn on it the fat of the peace offerings.
13 Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
Fire must be kept burning on the altar continually. It must not go out.
14 “‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
This is the law of the grain offering. The sons of Aaron will offer it before Yahweh before the altar.
15 Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
The priest will take up a handful of the fine flour of the grain offering and of the oil and the incense which is on the grain offering, and he will burn it on the altar to produce a sweet aroma as a representative offering.
16 Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
Aaron and his sons will eat whatever is left of the offering. It must be eaten without yeast in a holy place. They will eat it in the courtyard of the tent of meeting.
17 Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
It must not be baked with yeast. I have given it as their part of my offerings made by fire. It is most holy, as the sin offering and the guilt offering.
18 Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
For all time to come throughout your people's generations, any male descended from Aaron may eat it as his share, taken from the offerings of Yahweh made by fire. Whoever touches them will become holy.'”
19 Tena Bwana akamwambia Mose,
So Yahweh spoke to Moses again, saying,
20 “Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
“This is the offering of Aaron and of his sons, which they will offer to Yahweh on the day when each son is anointed: a tenth part of an ephah of fine flour as a regular grain offering, half of it in the morning and half of it in the evening.
21 Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
It will be made with oil in a baking pan. When it is soaked, you will bring it in. In baked pieces you will offer the grain offering to produce a sweet aroma for Yahweh.
22 Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
The son of the high priest who is becoming the new high priest from among his sons will offer it. As commanded forever, all of it shall be burned to Yahweh.
23 Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
Every grain offering of the priest will be completely burned up. It must not be eaten.”
24 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh spoke to Moses again, saying,
25 “Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
“Speak to Aaron and to his sons, saying, 'This is the law of the sin offering: The sin offering must be killed at the place where the burnt offering is killed before Yahweh. It is most holy.
26 Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
The priest who offers it for sin will eat it. It must be eaten in a holy place in the courtyard of the tent of meeting.
27 Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
Whatever touches its meat will become holy, and if the blood is sprinkled on any garment, you must wash it, the part that was sprinkled on, in a holy place.
28 Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
But the clay pot in which it is boiled must be broken. If it is boiled in a bronze pot, it must be scrubbed and rinsed clean in water.
29 Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
Any male among the priests may eat some of it because it is most holy.
30 Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.
But any sin offering whose blood is brought into the tent of meeting to make atonement in the holy place must not be eaten. It must be burned.