< Mambo ya Walawi 6 >

1 Bwana akamwambia Mose:
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 “Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
Anyone if it will sin and it will act unfaithfully unfaithfulness against Yahweh and he will deny fellow citizen his an item entrusted or deposited property of a hand or a robbery or he has oppressed fellow citizen his.
3 au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
Or he has found a thing lost and he will deny it and he will swear an oath on falsehood on one of all that he will do humankind to sin by them.
4 wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
And it will be that he will sin and he will be guilty and he will restore the thing robbed which he robbed or the oppression which he oppressed or the item entrusted which it was entrusted with him or the thing lost which he found.
5 au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
Or any of all that he will swear an oath on it to falsehood and he will repay it in sum its and fifth its let him add to it to [the one] whom it [belonged] to him he will give it on [the] day of guilt his.
6 Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
And guilt offering his he will bring to Yahweh a ram unblemished from the flock by valuation your to a guilt offering to the priest.
7 Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
And he will make atonement on him the priest before Yahweh and it will be forgiven to him on one of all that someone will do to guilt by it.
8 Bwana akamwambia Mose:
And he spoke Yahweh to Moses saying.
9 “Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
Command Aaron and sons his saying this [is] [the] legal [procedure] of the burnt offering it the burnt offering [will be] on [the] hearth on the altar all the night until the morning and [the] fire of the altar it will burn on it.
10 Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
And he will put on the priest garment his linen and undergarments of linen he will put on on body his and he will lift up the fatty ash which it will consume the fire the burnt offering on the altar and he will place it beside the altar.
11 Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
And he will strip off garments his and he will put on garments other and he will take out the fatty ash to from [the] outside of the camp to a place pure.
12 Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
And the fire on the altar it will burn on it not it will be extinguished and he will kindle on it the priest wood in the morning in the morning and he will arrange on it the burnt offering and he will make smoke on it [the] fat of the peace offerings.
13 Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
A fire continually it will burn on the altar not it will be extinguished.
14 “‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
And this [is] [the] legal [procedure] of the grain offering they will present it [the] sons of Aaron before Yahweh to [the] face of the altar.
15 Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
And he will lift up from it in handful his some of [the] fine flour of the grain offering and some of oil its and all the frankincense which [is] on the grain offering and he will make smoke the altar an odor of soothing memorial offering its to Yahweh.
16 Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
And the remainder of it they will eat Aaron and sons his unleavened bread it will be eaten in a place holy in [the] courtyard of [the] tent of meeting they will eat it.
17 Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
Not it will be baked leaven share their I have given it from fire offerings my [is] a holy thing of holy things it like the sin offering and like the guilt offering.
18 Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
Every male among [the] sons of Aaron he will eat it a prescribed portion of perpetuity to generations your from [the] fire offerings of Yahweh every [one] who he will touch them he will be holy.
19 Tena Bwana akamwambia Mose,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
20 “Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
This [is] [the] present of Aaron and sons his which they will present to Yahweh on [the] day is anointed him tenth of ephah fine flour grain offering continually half its in the morning and half its in the evening.
21 Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
On a baking tray with oil it will be made mixed [dough] you will bring it broken pieces of a grain offering of crumbs you will present an odor of soothing to Yahweh.
22 Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
And the priest anointed in place of him one of sons his he will offer it a prescribed portion of perpetuity to Yahweh a whole offering it will be made to smoke.
23 Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
And every grain offering of a priest a whole offering it will be not it will be eaten.
24 Bwana akamwambia Mose,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
25 “Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
Speak to Aaron and to sons his saying this [is] [the] legal [procedure] of the sin offering in [the] place where it has its throat cut the burnt offering it will have its throat cut the sin offering before Yahweh [is] a holy thing of holy things it.
26 Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
The priest who makes a sin offering it he will eat it in a place holy it will be eaten in [the] courtyard of [the] tent of meeting.
27 Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
All that it will touch meat its it will be holy and [one] who he will spatter any of blood its on the garment [that] which he will spatter on it you will wash in a place holy.
28 Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
And a vessel of earthenware which it will be boiled in it it will be broken and if in a vessel of bronze it was boiled and it will be scoured and it will be rinsed with water.
29 Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
Every male among the priests he will eat it [is] a holy thing of holy things it.
30 Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.
And any sin offering which it will be brought in any of blood its into [the] tent of meeting to make atonement in the holy place not it will be eaten with fire it will be burned.

< Mambo ya Walawi 6 >