< Mambo ya Walawi 6 >

1 Bwana akamwambia Mose:
And the Lord spake vnto Moses, saying,
2 “Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
If any sinne and commit a trespasse against the Lord, and denie vnto his neighbour that, which was take him to keepe, or that which was put to him of trust, or doth by robberie, or by violence oppresse his neighbour,
3 au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
Or hath found that which was lost, and denieth it, and sweareth falsely, for any of these things that a man doeth, wherein he sinneth:
4 wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
When, I say, he thus sinneth and trespasseth, he shall then restore the robbery that he robbed, or the thing taken by violence which hee tooke by force, or the thing which was deliuered him to keepe, or the lost thing which he founde,
5 au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
Or for whatsoeuer he hath sworne falsely, he shall both restore it in the whole summe, and shall adde the fift parte more thereto, and giue it vnto him to whome perteyneth, the same day that he offreth for trespasse.
6 Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
Also he shall bring for his trespasse vnto the Lord, a ramme without blemish out of the flocke in thy estimation worth two shekels for a trespasse offring vnto the Priest.
7 Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
And the Priest shall make an atonement for him before the Lord, and it shall be forgiuen him, whatsoeuer thing he hath done, and trespassed therein.
8 Bwana akamwambia Mose:
Then the Lord spake vnto Moses, saying,
9 “Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
Commaund Aaron and his sonnes, saying, This is the lawe of the burnt offring, (it is the burnt offring because it burneth vpon the altar al the night vnto the morning, and the fire burneth on the altar)
10 Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
And the Priest shall put on his linen garment, and shall put on his linen breeches vpon his flesh, and take away the ashes when the fire hath consumed the burnt offring vpon the altar, and he shall put them beside the altar.
11 Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
After, he shall put off his garments, and put on other raiment, and cary the ashes foorth without the hoste vnto a cleane place.
12 Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
But the fire vpon the altar shall burne thereon and neuer be put out: wherefore the Priest shall burne wood on it euery morning, and lay the burnt offering in order vpon it, and he shall burne thereon the fat of the peace offrings.
13 Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
The fire shall euer burne vpon the altar, and neuer go out.
14 “‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
Also this is the lawe of the meate offring, which Aarons sonnes shall offer in the presence of the Lord, before the altar.
15 Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
He shall euen take thence his handfull of fine flowre of the meate offring and of the oyle, and all the incense which is vpon the meat offring, and shall burne it vpon the altar for a sweete sauour, as a memoriall therefore vnto the Lord:
16 Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
But the rest thereof shall Aaron and his sonnes eate: it shalbe eaten without leauen in the holy place: in the court of the Tabernacle of the Congregation they shall eate it.
17 Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
It shall not be baken with leauen: I haue giuen it for their portion of mine offrings made by fire: for it is as the sinne offering and as the trespasse offring.
18 Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
All the males among the children of Aaron shall eate of it: It shalbe a statute for euer in your generations concerning the offrings of the Lord, made by fire: whatsoeuer toucheth them shall be holy.
19 Tena Bwana akamwambia Mose,
Agayne the Lord spake vnto Moses, saying,
20 “Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
This is the offering of Aaron and his sonnes, which they shall offer vnto the Lord in the day when he is anointed: the tenth part of an Ephah of fine floure, for a meate offering perpetuall: halfe of it in ye morning, and halfe thereof at night.
21 Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
In the frying panne it shalbe made with oyle: thou shalt bring it fryed, and shalt offer the baken pieces of the meate offering for a sweete sauour vnto the Lord.
22 Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
And the Priest that is anointed in his steade, among his sonnes shall offer it: It is the Lordes ordinance for euer, it shall be burnt altogether.
23 Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
For euery meate offring of the Priest shall be burnt altogether, it shall not be eaten.
24 Bwana akamwambia Mose,
Furthermore, the Lord spake vnto Moses, saying,
25 “Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
Speake vnto Aaron, and vnto his sonnes, and say, This is the Lawe of the sinne offering, In the place where the burnt offring is killed, shall the sinne offring be killed before the Lord, for it is most holy.
26 Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
The Priest that offreth this sinne offring, shall eate it: in the holy place shall it be eaten, in the court of ye Tabernacle of the Congregation.
27 Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
Whatsoeuer shall touch the flesh thereof shalbe holy: and when there droppeth of the blood thereof vpon a garment, thou shalt wash that whereon it droppeth in the holy place.
28 Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
Also the earthen pot that it is sodden in, shalbe broken, but if it be sodden in a brasen pot, it shall both be scoured and washed with water.
29 Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
All the males among the Priestes shall eate thereof, for it is most holy.
30 Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.
But no sinne offering, whose blood is brought into the Tabernacle of the Congregation to make reconciliation in the holy place, shalbe eaten, but shalbe burnt in the fire.

< Mambo ya Walawi 6 >