< Mambo ya Walawi 6 >

1 Bwana akamwambia Mose:
The Lord spoke to Moses, saying:
2 “Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
The soul who will have sinned, and, despising the Lord, will have denied to his neighbor the deposit which he had entrusted to his safekeeping, or who will have extorted anything by force, or who will have made a false accusation,
3 au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
or who will have found a lost thing and then also withheld it by swearing falsely, or who will have done any other of the many things by which men usually sin:
4 wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
being convicted of the offense, he shall restore
5 au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
all that he wanted to obtain by fraud, the whole plus an additional fifth part, to the owner against whom he brought the damage.
6 Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
Then, on behalf of his sin, he shall offer an immaculate ram from the flock, and he shall give it to the priest, according to the estimation and measure of the offense.
7 Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
And he shall pray for him in the sight of the Lord, and he shall be released from any one of those things that he did when he sinned.
8 Bwana akamwambia Mose:
And the Lord spoke to Moses, saying:
9 “Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
Instruct Aaron and his sons: This is the law of a holocaust. It shall be burned upon the altar, all night until morning. The fire shall be from the same altar.
10 Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
The priest shall be vested with the tunic and the linen undergarments. And he shall take up the ashes of that which the devouring fire has consumed, and, placing them next to the altar,
11 Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
he shall strip off his former vestments, and being clothed with others, he shall carry them beyond the camp, and he shall cause them to be consumed, even to glowing embers, in a very clean place.
12 Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
But the fire on the altar shall burn always, for the priest shall nourish it by placing wood under it each day in the morning. And, laying down the holocaust, he shall burn the fat of the peace offerings upon it.
13 Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
This is the perpetual fire which shall never fail upon the altar.
14 “‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
This is the law of the sacrifice and the libations, which the sons of Aaron shall offer in the sight of the Lord, and before the altar.
15 Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
The priest shall take a handful of fine wheat flour, which has been sprinkled with oil, and all the frankincense, which has been placed upon the flour, and he shall burn it upon the altar as a memorial of most sweet odor to the Lord.
16 Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
And the remaining portion of the flour, Aaron shall eat with his sons, without leaven. And he shall eat it in the holy place, in the atrium of the tabernacle.
17 Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
Yet for this reason, it shall not be leavened, because part of it is offered as an incense of the Lord. The Holy of holies shall it be, just as what is offered on behalf of sin and of transgression.
18 Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
Only the males of the stock of Aaron shall eat it. This shall be an everlasting ordinance in your generations concerning the sacrifices of the Lord. All who will touch these shall be sanctified.
19 Tena Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke to Moses, saying:
20 “Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
This is the oblation of Aaron and of his sons, which they must offer to the Lord in the day of their anointing. They shall offer a tenth part of an ephah of fine wheat flour as a perpetual sacrifice, half of it in the morning, and half of it in the evening.
21 Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
It shall be sprinkled with oil and fried in a frying pan. Then it shall be offered hot, as a most sweet odor to the Lord,
22 Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
by the priest who by law succeeds his father. And it shall be entirely burned on the altar.
23 Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
For every sacrifice of the priest shall be consumed by fire; neither shall anyone eat from it.
24 Bwana akamwambia Mose,
Then the Lord spoke to Moses, saying:
25 “Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
Say to Aaron and his sons: This is the law of the victim for sin. In the place where the holocaust is offered, it shall be immolated in the sight of the Lord. It is the Holy of holies.
26 Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
The priest who offers it shall eat it in the holy place, in the atrium of the tabernacle.
27 Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
Whatever will touch its flesh shall be sanctified. If a garment will be sprinkled with its blood, it shall be washed in a holy place.
28 Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
Then the earthen vessel, in which it was soaked, shall be broken. But if the vessel will be of brass, it shall be scoured and washed with water.
29 Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
Every male of priestly descent shall feed on its flesh, because it is the Holy of holies.
30 Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.
For the victim that is slain for sin, whose blood is carried into the tabernacle of the testimony, for expiation in the Sanctuary, shall not be eaten, but it shall be consumed by fire.

< Mambo ya Walawi 6 >