< Mambo ya Walawi 5 >

1 “‘Ikiwa mtu atakuwa ametenda dhambi kwa sababu hakusema alipotakiwa kutoa ushahidi hadharani kuhusu jambo aliloona au kujua habari zake, yeye anastahili adhabu.
"'Si quelqu'un pèche, en entendant une adjuration publique pour témoigner, lui étant témoin, qu'il a vu ou connu, s'il ne le rapporte pas, il portera sa faute.
2 “‘Au kama mtu akigusa kitu chochote ambacho ni najisi, iwe ni mizoga ya wanyama pori walio najisi, au ya wanyama wafugwao walio najisi, au ya viumbe vitambaavyo ardhini, hata akiwa hana habari, amekuwa najisi na mwenye hatia.
"'Si quelqu'un touche une chose impure, qu'il s'agisse du cadavre d'un animal impur, du cadavre d'un animal de rente impur ou du cadavre d'un reptile impur, et que cela lui soit caché, et qu'il soit impur, il sera coupable.
3 “‘Au kama akigusa kitu kilicho kichafu kinachotokana na binadamu, kitu chochote kile kinachoweza kumfanya awe najisi, hata akiwa hana habari, atakapofahamu atakuwa na hatia.
"'Ou bien, s'il touche l'impureté de l'homme, quelle que soit l'impureté avec laquelle il est souillé, et qu'elle lui soit cachée, quand il en aura connaissance, il sera coupable.
4 “‘Au kama mtu ameapa kufanya kitu chochote bila kufikiri, kiwe chema au kibaya, kwa vyovyote mtu aweza kuapa bila kujali, hata akiwa hana habari, atakapofahamu atakuwa na hatia.
"'Si quelqu'un jure témérairement de ses lèvres de faire du mal ou de faire du bien - tout ce qu'un homme peut proférer témérairement par un serment, et que cela lui soit caché - lorsqu'il en aura connaissance, il sera coupable de l'une de ces choses.
5 “‘Wakati mtu yeyote atakapokuwa na hatia katika mojawapo ya haya, lazima akiri ni kwa njia gani ametenda dhambi,
S'il se rend coupable de l'une de ces choses, il confessera le péché qu'il a commis;
6 na kama adhabu ya dhambi aliyoitenda, lazima alete kwa Bwana kondoo jike au mbuzi jike kutoka kwenye kundi lake kama sadaka ya dhambi; naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi yake.
et il apportera à l'Éternel son sacrifice de culpabilité pour le péché qu'il a commis: une femelle du troupeau, un agneau ou une chèvre, en sacrifice pour le péché; et le prêtre fera pour lui l'expiation de son péché.
7 “‘Lakini huyo mtu kama hataweza kumtoa mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa Bwana kuwa adhabu kwa ajili ya dhambi yake, mmoja wa hao ndege kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na wa pili kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
"'S'il n'a pas les moyens de se procurer un agneau, il apportera à Yahvé son sacrifice pour le péché qu'il a commis, deux tourterelles ou deux jeunes pigeons, l'un pour le sacrifice pour le péché, l'autre pour l'holocauste.
8 Atawaleta kwa kuhani, ambaye atamtoa kwanza ndege mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Atamvunja shingo na kuacha kichwa chake kikiningʼinia,
Il les apportera au sacrificateur, qui offrira d'abord celle qui est pour le sacrifice pour le péché. Il lui arrachera la tête du cou, mais il ne la coupera pas complètement.
9 naye atanyunyiza sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi kwenye pembe za madhabahu. Damu iliyobaki lazima ichuruzwe chini ya madhabahu. Hii ni sadaka ya dhambi.
Il fera aspersion d'une partie du sang du sacrifice pour le péché sur le côté de l'autel, et le reste du sang sera versé au pied de l'autel. C'est un sacrifice pour le péché.
10 Kisha kuhani atamtoa yule ndege wa pili kama sadaka ya kuteketezwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa, na hivyo kufanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.
Il offrira le second en holocauste, selon les règles établies; le sacrificateur fera pour lui l'expiation du péché qu'il a commis, et il lui sera pardonné.
11 “‘Ikiwa basi, hawezi kupata hua wawili au makinda mawili ya njiwa, ataleta sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kamwe asiweke mafuta wala uvumba juu yake, kwa sababu ni sadaka ya dhambi.
"'Mais s'il n'a pas les moyens de se procurer deux tourterelles ou deux jeunes pigeons, il apportera en offrande pour le péché qu'il a commis, un dixième d'épha de fleur de farine en sacrifice pour le péché. Il n'y mettra pas d'huile et il n'y mettra pas d'encens, car c'est un sacrifice pour le péché.
12 Atauleta unga kwa kuhani, ambaye atachukua konzi moja kama sehemu ya kumbukumbu na atauteketeza kwenye madhabahu juu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya dhambi.
Il l'apportera au prêtre; le prêtre en prendra une poignée comme portion commémorative, et il la brûlera sur l'autel, sur les offrandes consumées par le feu de Yahvé. C'est un sacrifice pour le péché.
13 Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi yoyote ya hizo alizotenda, naye atasamehewa. Sadaka iliyobaki itakuwa ya kuhani, kama ilivyokuwa ile sadaka ya nafaka.’”
Le prêtre fera pour lui l'expiation du péché qu'il a commis à l'égard de l'une de ces choses, et il lui sera pardonné; le reste appartiendra au prêtre, comme l'offrande de repas.'"
14 Bwana akamwambia Mose:
L'Éternel parla à Moïse et dit:
15 “Mtu anapokiuka na kutenda dhambi pasipo kukusudia kuhusu mojawapo ya mambo matakatifu ya Bwana, huyo mtu ataleta kwa Bwana kama adhabu kondoo dume mmoja kutoka kundi lake, asiye na dosari na mwenye thamani halisi kifedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. Hii ni sadaka ya hatia.
« Si quelqu'un commet une faute et pèche involontairement à l'égard des choses saintes de l'Éternel, il apportera à l'Éternel son sacrifice de culpabilité: un bélier sans défaut du troupeau, selon votre estimation en sicles d'argent, selon le sicle du sanctuaire, pour le sacrifice de culpabilité.
16 Ni lazima alipe kwa yale aliyoshindwa kufanya kuhusu vitu vitakatifu, kwa kuongeza sehemu ya tano ya thamani ile na kuitoa yote kwa kuhani, ambaye atamfanyia upatanisho kwa huyo kondoo dume kama sadaka ya dhambi, naye atasamehewa.
Il restituera ce qu'il a fait de mal par rapport à la chose sainte, il y ajoutera un cinquième et le donnera au prêtre; le prêtre fera pour lui l'expiation avec le bélier du sacrifice de culpabilité, et il lui sera pardonné.
17 “Kama mtu akifanya dhambi na kufanya yale yaliyokatazwa katika mojawapo ya amri za Bwana, hata ikiwa hajui, yeye ana hatia na anastahili adhabu.
« Si quelqu'un commet un péché en faisant l'une des choses que l'Éternel a ordonné de ne pas faire, sans le savoir, il est néanmoins coupable, et il portera la peine de son iniquité.
18 Atamletea kuhani kama sadaka ya hatia kondoo dume kutoka kundi lake, kondoo asiye na dosari na mwenye thamani halisi kifedha. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa kosa alilotenda bila kukusudia, naye atasamehewa.
Il apportera au prêtre un bélier sans défaut du troupeau, selon votre estimation, en sacrifice de culpabilité; le prêtre fera pour lui l'expiation de la faute qu'il a commise sans le savoir, et il lui sera pardonné.
19 Hii ni sadaka ya hatia; amekuwa na hatia kwa kufanya kosa dhidi ya Bwana.”
C'est un sacrifice de culpabilité. Il est certainement coupable devant Yahvé. »

< Mambo ya Walawi 5 >