< Mambo ya Walawi 5 >

1 “‘Ikiwa mtu atakuwa ametenda dhambi kwa sababu hakusema alipotakiwa kutoa ushahidi hadharani kuhusu jambo aliloona au kujua habari zake, yeye anastahili adhabu.
And anyone if it will sin and it will hear [the] sound of an oath and he [was] a witness or he saw or he knew if not he will tell and he will bear iniquity his.
2 “‘Au kama mtu akigusa kitu chochote ambacho ni najisi, iwe ni mizoga ya wanyama pori walio najisi, au ya wanyama wafugwao walio najisi, au ya viumbe vitambaavyo ardhini, hata akiwa hana habari, amekuwa najisi na mwenye hatia.
Or anyone who it will touch every thing unclean or a carcass of an animal unclean or a carcass of livestock unclean or a carcass of a swarming thing unclean and it will be hidden from him and he [is] unclean and he will be guilty.
3 “‘Au kama akigusa kitu kilicho kichafu kinachotokana na binadamu, kitu chochote kile kinachoweza kumfanya awe najisi, hata akiwa hana habari, atakapofahamu atakuwa na hatia.
Or if he will touch [the] uncleanness of a human to all uncleanness his which he will be unclean by it and it will be hidden from him and he he knew and he will be guilty.
4 “‘Au kama mtu ameapa kufanya kitu chochote bila kufikiri, kiwe chema au kibaya, kwa vyovyote mtu aweza kuapa bila kujali, hata akiwa hana habari, atakapofahamu atakuwa na hatia.
Or anyone if it will swear an oath by speaking rashly with lips to do evil - or to do good to all that he will speak rashly humankind in an oath and it will be hidden from him and he he knew and he will be guilty to one of these [things].
5 “‘Wakati mtu yeyote atakapokuwa na hatia katika mojawapo ya haya, lazima akiri ni kwa njia gani ametenda dhambi,
And it will be that he will be guilty to one of these [things] and he will confess that he had sinned on it.
6 na kama adhabu ya dhambi aliyoitenda, lazima alete kwa Bwana kondoo jike au mbuzi jike kutoka kwenye kundi lake kama sadaka ya dhambi; naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi yake.
And he will bring guilt offering his to Yahweh on sin his which he has sinned a female from the flock a ewe lamb or a female goat of goats to a sin offering and he will make atonement on him the priest from sin his.
7 “‘Lakini huyo mtu kama hataweza kumtoa mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa Bwana kuwa adhabu kwa ajili ya dhambi yake, mmoja wa hao ndege kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na wa pili kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
And if not it will reach hand his sufficiency of a sheep and he will bring guilt offering his which he has sinned two turtle-doves or two young ones of a dove to Yahweh one to a sin offering and one to a burnt offering.
8 Atawaleta kwa kuhani, ambaye atamtoa kwanza ndege mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Atamvunja shingo na kuacha kichwa chake kikiningʼinia,
And he will bring them to the priest and he will present [the one] which [is] for the sin offering first and he will nip off head its from in front of neck its and not he will separate [it].
9 naye atanyunyiza sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi kwenye pembe za madhabahu. Damu iliyobaki lazima ichuruzwe chini ya madhabahu. Hii ni sadaka ya dhambi.
And he will spatter some of [the] blood of the sin offering on [the] side of the altar and the remainder in the blood it will be drained out to [the] base of the altar [is] a sin offering it.
10 Kisha kuhani atamtoa yule ndege wa pili kama sadaka ya kuteketezwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa, na hivyo kufanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.
And the second [bird] he will offer a burnt offering according to the ordinance and he will make atonement on him the priest from sin his which he has sinned and it will be forgiven to him.
11 “‘Ikiwa basi, hawezi kupata hua wawili au makinda mawili ya njiwa, ataleta sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kamwe asiweke mafuta wala uvumba juu yake, kwa sababu ni sadaka ya dhambi.
And if not it will reach hand his to two turtle-doves or to two young ones of a dove and he will bring present his which he has sinned tenth of ephah fine flour to a sin offering not he will place on it oil and not he will put on it frankincense for [is] a sin offering it.
12 Atauleta unga kwa kuhani, ambaye atachukua konzi moja kama sehemu ya kumbukumbu na atauteketeza kwenye madhabahu juu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya dhambi.
And he will bring it to the priest and he will take a handful the priest - from it [the] fullness of handful his memorial offering its and he will make [it] smoke the altar towards on [the] fire offerings of Yahweh [is] a sin offering it.
13 Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi yoyote ya hizo alizotenda, naye atasamehewa. Sadaka iliyobaki itakuwa ya kuhani, kama ilivyokuwa ile sadaka ya nafaka.’”
And he will make atonement on him the priest on sin his which he has sinned any one of these [things] and it will be forgiven to him and it will belong to the priest like the grain offering.
14 Bwana akamwambia Mose:
And he spoke Yahweh to Moses saying.
15 “Mtu anapokiuka na kutenda dhambi pasipo kukusudia kuhusu mojawapo ya mambo matakatifu ya Bwana, huyo mtu ataleta kwa Bwana kama adhabu kondoo dume mmoja kutoka kundi lake, asiye na dosari na mwenye thamani halisi kifedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. Hii ni sadaka ya hatia.
Anyone if it will act unfaithfully unfaithfulness and it will sin by inadvertence from [the] holy things of Yahweh and he will bring guilt offering his to Yahweh a ram unblemished from the flock by valuation your silver of shekels by [the] shekel of the holy place to a guilt offering.
16 Ni lazima alipe kwa yale aliyoshindwa kufanya kuhusu vitu vitakatifu, kwa kuongeza sehemu ya tano ya thamani ile na kuitoa yote kwa kuhani, ambaye atamfanyia upatanisho kwa huyo kondoo dume kama sadaka ya dhambi, naye atasamehewa.
And [that] which he sinned from the holy thing he will repay and fifth its let him add to it and he will give it to the priest and the priest he will make atonement on him by [the] ram of the guilt offering and it will be forgiven to him.
17 “Kama mtu akifanya dhambi na kufanya yale yaliyokatazwa katika mojawapo ya amri za Bwana, hata ikiwa hajui, yeye ana hatia na anastahili adhabu.
And if anyone that it will sin and it will do one of all [the] commandments of Yahweh which not they will be done and not he knew and he will be guilty and he will bear iniquity his.
18 Atamletea kuhani kama sadaka ya hatia kondoo dume kutoka kundi lake, kondoo asiye na dosari na mwenye thamani halisi kifedha. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa kosa alilotenda bila kukusudia, naye atasamehewa.
And he will bring a ram unblemished from the flock by valuation your to a guilt offering to the priest and he will make atonement on him the priest on inadvertence his which he has gone astray and he not he knew and it will be forgiven to him.
19 Hii ni sadaka ya hatia; amekuwa na hatia kwa kufanya kosa dhidi ya Bwana.”
[is] a guilt offering It certainly he was guilty to Yahweh.

< Mambo ya Walawi 5 >