< Mambo ya Walawi 4 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
2 “Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote afanyapo dhambi bila kukusudia na akatenda lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana:
'Speak unto the sons of Israel, saying, When a person doth sin through ignorance against any of the commands of Jehovah [regarding things] which are not to be done, and hath done [something] against one of these —
3 “‘Ikiwa kuhani aliyetiwa mafuta amefanya dhambi na kuwaletea watu hatia, lazima alete kwa Bwana fahali mchanga asiye na dosari, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
'If the priest who is anointed doth sin according to the guilt of the people, then he hath brought near for his sin which he hath sinned a bullock, a son of the herd, a perfect one, to Jehovah, for a sin-offering,
4 Atamkabidhi huyo fahali kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo fahali na kumchinja mbele za Bwana.
and he hath brought in the bullock unto the opening of the tent of meeting before Jehovah, and hath laid his hand on the head of the bullock, and hath slaughtered the bullock before Jehovah.
5 Kisha kuhani huyo aliyetiwa mafuta atachukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuileta katika Hema la Kukutania.
'And the priest who is anointed hath taken of the blood of the bullock, and hath brought it in unto the tent of meeting,
6 Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza sehemu yake mara saba mbele za Bwana mbele ya pazia la mahali patakatifu.
and the priest hath dipped his finger in the blood, and sprinkled of the blood seven times before Jehovah, at the front of the vail of the sanctuary;
7 Kisha kuhani atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu ya kufukizia uvumba wenye harufu nzuri iliyoko mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ya huyo fahali ataimwaga chini ya hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
and the priest hath put of the blood on the horns of the altar of spice-perfume before Jehovah, which [is] in the tent of meeting, and all the blood of the bullock he doth pour out at the foundation of the altar of the burnt-offering, which [is] at the opening of the tent of meeting.
8 Atayaondoa mafuta yote ya fahali huyo wa sadaka ya dhambi, mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani au zile zinazounganika nazo,
'And all the fat of the bullock of the sin-offering he doth lift up from it, the fat which is covering over the inwards, and all the fat which [is] on the inwards,
9 figo zote mbili na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yale yanayofunika ini ambayo atayaondoa pamoja na figo zote,
and the two kidneys, and the fat which [is] on them, which [is] on the flanks, and the redundance above the liver, (beside the kidneys he doth turn it aside),
10 kama vile mafuta yanayoondolewa kutoka kwenye maksai aliyetolewa sadaka ya amani. Kisha kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
as it is lifted up from the ox of the sacrifice of the peace-offerings; and the priest hath made them a perfume on the altar of the burnt-offering.
11 Lakini ngozi ya huyo fahali na nyama zake zote, pamoja na kichwa na miguu yake, sehemu za ndani na matumbo,
'And the skin of the bullock, and all its flesh, besides its head, and besides its legs, and its inwards, and its dung —
12 yaani sehemu nyingine zote zilizobaki za huyo fahali, lazima azitoe nje ya kambi mpaka mahali palipo safi kiibada, ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni zilizoko juu ya lundo la majivu.
he hath even brought out the whole bullock unto the outside of the camp, unto a clean place, unto the place of the pouring out of the ashes, and he hath burnt it on the wood with fire; beside the place of the pouring out of the ashes it is burnt.
13 “‘Ikiwa jumuiya yote ya Israeli watatenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, hata kama jumuiya haifahamu juu ya jambo hilo, wana hatia.
'And if the whole company of Israel err ignorantly, and the thing hath been hidden from the eyes of the assembly, and they have done [something against] one of all the commands of Jehovah [concerning things] which are not to be done, and have been guilty;
14 Wanapotambua kuhusu dhambi waliyoitenda, lazima kusanyiko lilete fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi na kuikabidhi mbele ya Hema la Kukutania.
when the sin which they have sinned concerning it hath been known, then have the assembly brought near a bullock, a son of the herd, for a sin-offering, and they have brought it in before the tent of meeting;
15 Wazee wa jumuiya wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo fahali aliye mbele za Bwana, naye fahali atachinjwa mbele za Bwana.
and the elders of the company have laid their hands on the head of the bullock, before Jehovah, and [one] hath slaughtered the bullock before Jehovah.
16 Kisha kuhani aliyetiwa mafuta ataiingiza sehemu ya damu ya huyo fahali ndani ya Hema la Kukutania.
'And the priest who is anointed hath brought in of the blood of the bullock unto the tent of meeting,
17 Atachovya kidole chake kwenye damu na kuinyunyiza mara saba mbele za Bwana mbele ya hilo pazia.
and the priest hath dipped his finger in the blood, and hath sprinkled seven times before Jehovah at the front of the vail,
18 Atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu yaliyo mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu ya kuteketezea sadaka, penye ingilio la Hema la Kukutania.
and [some] of the blood he doth put on the horns of the altar which [is] before Jehovah, which [is] in the tent of meeting; and all the blood he doth pour out at the foundation of the altar of the burnt-offering, which [is] at the opening of the tent of meeting;
19 Atayaondoa mafuta yote ya yule fahali na kuyateketeza juu ya madhabahu,
and all its fat he doth lift up from it, and hath made perfume on the altar.
20 naye atamfanyia fahali huyu kama alivyomfanyia yule fahali mwingine wa sadaka ya dhambi. Kwa njia hii kuhani atawafanyia watu upatanisho, nao watasamehewa.
'And he hath done to the bullock as he hath done to the bullock of the sin-offering, so he doth to it; and the priest hath made atonement for them, and it hath been forgiven them;
21 Kisha atamchukua yule fahali nje ya kambi na kumteketeza kama alivyomteketeza yule wa kwanza. Hii ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya jumuiya.
and he hath brought out the bullock unto the outside of the camp, and hath burned it as he hath burned the first bullock; it [is] a sin-offering of the assembly.
22 “‘Wakati kiongozi ametenda dhambi bila kukusudia na kufanya yaliyokatazwa katika amri yoyote ya Bwana Mungu wake, ana hatia.
'When a prince doth sin, and hath done [something against] one of all the commands of Jehovah his God [regarding things] which are not to be done, through ignorance, and hath been guilty —
23 Atakapofahamishwa dhambi aliyotenda, ni lazima alete mbuzi dume asiye na dosari kama sadaka yake.
or his sin wherein he hath sinned hath been made known unto him, then he hath brought in his offering, a kid of the goats, a male, a perfect one,
24 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha yule mbuzi na kumchinja mahali pale ambapo sadaka za kuteketezwa huchinjiwa mbele za Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
and he hath laid his hand on the head of the goat, and hath slaughtered it in the place where he doth slaughter the burnt-offering before Jehovah; it [is] a sin-offering.
25 Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketeza, na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
'And the priest hath taken of the blood of the sin-offering with his finger, and hath put on the horns of the altar of the burnt-offering, and its blood he doth pour out at the foundation of the altar of the burnt-offering,
26 Atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, kama alivyoteketeza mafuta ya sadaka ya amani. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho wa dhambi kwa ajili ya yule mtu, naye atasamehewa.
and with all its fat he doth make perfume on the altar, as the fat of the sacrifice of the peace-offerings; and the priest hath made atonement for him because of his sin, and it hath been forgiven him.
27 “‘Kama mtu katika jumuiya ametenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, yeye ana hatia.
'And if any person of the people of the land sin through ignorance, by his doing [something against] one of the commands of Jehovah [regarding things] which are not to be done, and hath been guilty —
28 Atakapofahamishwa dhambi yake aliyoitenda, ni lazima alete mbuzi jike asiye na dosari kama sadaka yake kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
or his sin which he hath sinned hath been made known unto him, then he hath brought in his offering, a kid of the goats, a perfect one, a female, for his sin which he hath sinned,
29 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kumchinjia mahali pa kuteketezea sadaka.
and he hath laid his hand on the head of the sin-offering, and hath slaughtered the sin-offering in the place of the burnt-offering.
30 Kisha kuhani atachukua sehemu ya ile damu kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
'And the priest hath taken of its blood with his finger, and hath put on the horns of the altar of the burnt-offering, and all its blood he doth pour out at the foundation of the altar,
31 Atayaondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kwenye sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.
and all its fat he doth turn aside, as the fat hath been turned aside from off the sacrifice of the peace-offerings, and the priest hath made perfume on the altar, for sweet fragrance to Jehovah; and the priest hath made atonement for him, and it hath been forgiven him.
32 “‘Ikiwa ataleta mwana-kondoo kama sadaka yake ya dhambi, atamleta jike asiye na dosari.
'And if he bring in a sheep [for] his offering, for a sin-offering, a female, a perfect one, he doth bring in,
33 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo mwana-kondoo na kumchinja kwa ajili ya sadaka ya dhambi mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa.
and he hath laid his hand on the head of the sin-offering, and hath slaughtered it for a sin-offering in the place where he slaughtereth the burnt-offering.
34 Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na ile damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu.
'And the priest hath taken of the blood of the sin-offering with his finger, and hath put on the horns of the altar of the burnt-offering, and all its blood he poureth out at the foundation of the altar,
35 Ataondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kutoka kwenye mwana-kondoo wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu juu ya zile sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.
and all its fat he turneth aside, as the fat of the sheep is turned aside from the sacrifice of the peace-offerings, and the priest hath made them a perfume on the altar, according to the fire-offerings of Jehovah, and the priest hath made atonement for him, for his sin which he hath sinned, and it hath been forgiven him.

< Mambo ya Walawi 4 >