< Mambo ya Walawi 4 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh spoke to Moses, saying,
2 “Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote afanyapo dhambi bila kukusudia na akatenda lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana:
“Tell the people of Israel, 'When anyone sins without wanting to sin, doing any of the things that Yahweh has commanded not to be done, and if he does something that is prohibited, the following must be done.
3 “‘Ikiwa kuhani aliyetiwa mafuta amefanya dhambi na kuwaletea watu hatia, lazima alete kwa Bwana fahali mchanga asiye na dosari, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
If it is the high priest who sins so as to bring guilt on the people, then let him offer for his sin which he has committed a young bull without blemish to Yahweh as a sin offering.
4 Atamkabidhi huyo fahali kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo fahali na kumchinja mbele za Bwana.
He must bring the bull to the entrance of the tent of meeting before Yahweh, lay his hand on its head, and kill the bull before Yahweh.
5 Kisha kuhani huyo aliyetiwa mafuta atachukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuileta katika Hema la Kukutania.
The anointed priest will take some of the blood of the bull and take it to the tent of meeting.
6 Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza sehemu yake mara saba mbele za Bwana mbele ya pazia la mahali patakatifu.
The priest will dip his finger into the blood and sprinkle some of it seven times before Yahweh, before the curtain of the most holy place.
7 Kisha kuhani atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu ya kufukizia uvumba wenye harufu nzuri iliyoko mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ya huyo fahali ataimwaga chini ya hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
Then the priest will put some of the blood on the horns of the altar of fragrant incense before Yahweh, which is in the tent of meeting, and he will pour out all the rest of the blood of the bull at the base of the altar for burnt offerings, which is at the entrance of the tent of meeting.
8 Atayaondoa mafuta yote ya fahali huyo wa sadaka ya dhambi, mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani au zile zinazounganika nazo,
He will cut away all the fat of the bull of the sin offering; the fat that covers the inner parts, all the fat that is attached to the inner parts,
9 figo zote mbili na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yale yanayofunika ini ambayo atayaondoa pamoja na figo zote,
the two kidneys and the fat that is on them, which is by the loins, and the lobe of the liver, with the kidneys—he will cut away all this.
10 kama vile mafuta yanayoondolewa kutoka kwenye maksai aliyetolewa sadaka ya amani. Kisha kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
He will cut it all away, just as he cuts it off from the bull of the sacrifice of peace offerings. Then the priest will burn these parts on the altar for burnt offerings.
11 Lakini ngozi ya huyo fahali na nyama zake zote, pamoja na kichwa na miguu yake, sehemu za ndani na matumbo,
The skin of the bull and any remaining meat, with its head and with its legs and its inner parts and its dung,
12 yaani sehemu nyingine zote zilizobaki za huyo fahali, lazima azitoe nje ya kambi mpaka mahali palipo safi kiibada, ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni zilizoko juu ya lundo la majivu.
all the rest of the parts of the bull—he will carry all these parts outside the camp to a place that they have cleansed for me, where they pour out the ashes; they will burn those parts there on wood. They must burn those parts where they pour out the ashes.
13 “‘Ikiwa jumuiya yote ya Israeli watatenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, hata kama jumuiya haifahamu juu ya jambo hilo, wana hatia.
If the whole assembly of Israel sins without wanting to sin, and the assembly is unaware that they have sinned and done any of the things which Yahweh has commanded not to be done, and if they are guilty,
14 Wanapotambua kuhusu dhambi waliyoitenda, lazima kusanyiko lilete fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi na kuikabidhi mbele ya Hema la Kukutania.
then, when the sin they have committed becomes known, then the assembly must offer a young bull for a sin offering and bring it before the tent of meeting.
15 Wazee wa jumuiya wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo fahali aliye mbele za Bwana, naye fahali atachinjwa mbele za Bwana.
The elders of the assembly will lay their hands on the head of the bull before Yahweh, and the bull will be killed before Yahweh.
16 Kisha kuhani aliyetiwa mafuta ataiingiza sehemu ya damu ya huyo fahali ndani ya Hema la Kukutania.
The anointed priest will bring some of the blood of the bull to the tent of meeting,
17 Atachovya kidole chake kwenye damu na kuinyunyiza mara saba mbele za Bwana mbele ya hilo pazia.
and the priest will dip his finger in the blood and sprinkle it seven times before Yahweh, before the curtain.
18 Atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu yaliyo mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu ya kuteketezea sadaka, penye ingilio la Hema la Kukutania.
He will put some of the blood on the horns of the altar that is before Yahweh, which is in the tent of meeting, and he will pour out all the blood at the base of the altar for burnt offerings, which is at the entrance of the tent of meeting.
19 Atayaondoa mafuta yote ya yule fahali na kuyateketeza juu ya madhabahu,
He will cut off all the fat from it and burn it on the altar.
20 naye atamfanyia fahali huyu kama alivyomfanyia yule fahali mwingine wa sadaka ya dhambi. Kwa njia hii kuhani atawafanyia watu upatanisho, nao watasamehewa.
That is what he must do with the bull. Just as he did with the bull of the sin offering, so will he also do with this bull, and the priest will make atonement for the people, and they will be forgiven.
21 Kisha atamchukua yule fahali nje ya kambi na kumteketeza kama alivyomteketeza yule wa kwanza. Hii ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya jumuiya.
He will carry the bull outside the camp and burn it as he burned the first bull. This is the sin offering for the assembly.
22 “‘Wakati kiongozi ametenda dhambi bila kukusudia na kufanya yaliyokatazwa katika amri yoyote ya Bwana Mungu wake, ana hatia.
When a ruler sins without intending to sin, doing any one of all the things that Yahweh his God has commanded not to be done, and he is guilty,
23 Atakapofahamishwa dhambi aliyotenda, ni lazima alete mbuzi dume asiye na dosari kama sadaka yake.
then his sin which he has committed is made known to him, he must bring for his sacrifice a goat, a male without blemish.
24 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha yule mbuzi na kumchinja mahali pale ambapo sadaka za kuteketezwa huchinjiwa mbele za Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
He will lay his hand on the head of the goat and kill it in the place where they kill the burnt offering before Yahweh. This is a sin offering.
25 Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketeza, na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
The priest will take the blood of the sin offering with his finger and put it on the horns of the altar for burnt offerings, and he will pour out its blood at the base of the altar of burnt offering.
26 Atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, kama alivyoteketeza mafuta ya sadaka ya amani. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho wa dhambi kwa ajili ya yule mtu, naye atasamehewa.
He will burn all the fat on the altar, just like the fat of the sacrifice of peace offerings. The priest will make atonement for the ruler concerning his sin, and the ruler will be forgiven.
27 “‘Kama mtu katika jumuiya ametenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, yeye ana hatia.
If anyone of the common people sins without intending to sin, doing any of the things which Yahweh has commanded him not to be done, and when he realizes his guilt,
28 Atakapofahamishwa dhambi yake aliyoitenda, ni lazima alete mbuzi jike asiye na dosari kama sadaka yake kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
then his sin which he has committed is made known to him, then he will bring a goat for his sacrifice, a female without blemish, for the sin that he has committed.
29 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kumchinjia mahali pa kuteketezea sadaka.
He will lay his hand on the head of the sin offering and kill the sin offering at the place of burnt offering.
30 Kisha kuhani atachukua sehemu ya ile damu kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
The priest will take some of the blood with his finger and put it on the horns of the altar for burnt offerings. He will pour out all the rest of the blood at the base of the altar.
31 Atayaondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kwenye sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.
He will cut away all the fat, just as the fat is cut away from off the sacrifice of peace offerings. The priest will burn it on the altar to produce a sweet aroma for Yahweh. The priest will make atonement for the man, and he will be forgiven.
32 “‘Ikiwa ataleta mwana-kondoo kama sadaka yake ya dhambi, atamleta jike asiye na dosari.
If the man brings a lamb as his sacrifice for a sin offering, he will bring a female without blemish.
33 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo mwana-kondoo na kumchinja kwa ajili ya sadaka ya dhambi mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa.
He will lay his hand on the head of the sin offering and kill it for a sin offering at the place where they kill the burnt offering.
34 Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na ile damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu.
The priest will take some of the blood of the sin offering with his finger and put it on the horns of the altar for burnt offerings, and he will pour out all its blood at the base of the altar.
35 Ataondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kutoka kwenye mwana-kondoo wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu juu ya zile sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.
He will cut away all the fat, just as the fat of the lamb is cut away from the sacrifice of peace offerings, and the priest will burn it on the altar on top of the offerings of Yahweh made by fire. The priest will make atonement for him for the sin he has committed, and the man will be forgiven.

< Mambo ya Walawi 4 >