< Mambo ya Walawi 4 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And Yahweh spake, unto Moses, saying:
2 “Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote afanyapo dhambi bila kukusudia na akatenda lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana:
Speak thou unto the sons of Israel, saying—When any person, shall sin by mistake, departing from any of the commandments of Yahweh, as to things which should not be done, and shall do any one of them, —
3 “‘Ikiwa kuhani aliyetiwa mafuta amefanya dhambi na kuwaletea watu hatia, lazima alete kwa Bwana fahali mchanga asiye na dosari, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
If, the anointed priest, shall sin, so as to bring guilt upon the people, then shall he bring near for his sin which he hath committed a choice young bullock without defect, unto Yahweh as a sin-bearer.
4 Atamkabidhi huyo fahali kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo fahali na kumchinja mbele za Bwana.
And he shall bring in the bullock unto the entrance of the tent of meeting, before Yahweh, —and shall lean his hand upon the head of the bullock, and shall slay the bullock before Yahweh.
5 Kisha kuhani huyo aliyetiwa mafuta atachukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuileta katika Hema la Kukutania.
And the anointed priest shall take of the blood of the bullock, —and bring it into the tent of meeting;
6 Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza sehemu yake mara saba mbele za Bwana mbele ya pazia la mahali patakatifu.
and the priest shall dip his finger in the blood, —and sprinkle of the blood seven times, before Yahweh, in front of the veil of the sanctuary.
7 Kisha kuhani atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu ya kufukizia uvumba wenye harufu nzuri iliyoko mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ya huyo fahali ataimwaga chini ya hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
Then shall the priest put of the blood upon the horns of the altar of fragrant incense before Yahweh, which is in the tent of meeting, —and, all the [remainder of the] blood of the bullock, shall he pour out at the base of the altar of ascending-sacrifice, which is at the entrance of the tent of meeting,
8 Atayaondoa mafuta yote ya fahali huyo wa sadaka ya dhambi, mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani au zile zinazounganika nazo,
And all the fat of the sin-bearing bullock, shall he heave up therefrom, —the fat that covereth over the inwards, and all the fat that is upon the inwards;
9 figo zote mbili na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yale yanayofunika ini ambayo atayaondoa pamoja na figo zote,
and the two kidneys, and the fat that is upon them which is upon the loins, —and as for the caul upon the liver, upon the kidneys, shall he remove it:
10 kama vile mafuta yanayoondolewa kutoka kwenye maksai aliyetolewa sadaka ya amani. Kisha kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
just as it is heaved up from the ox of the peace-offering, —and the priest shall make of them a perfume on the altar of ascending-sacrifice,
11 Lakini ngozi ya huyo fahali na nyama zake zote, pamoja na kichwa na miguu yake, sehemu za ndani na matumbo,
But, as for the skin of the bullock and all its flesh with its head and with its legs, —and its inwards, and its dung,
12 yaani sehemu nyingine zote zilizobaki za huyo fahali, lazima azitoe nje ya kambi mpaka mahali palipo safi kiibada, ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni zilizoko juu ya lundo la majivu.
he shall take forth the entire bullock—unto the outside of the camp, unto a clean place unto the outpoured heap of fat-ashes, and shall burn it up on wood in the fire, —upon the outpoured heap of fat-ashes, shall it be burned up.
13 “‘Ikiwa jumuiya yote ya Israeli watatenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, hata kama jumuiya haifahamu juu ya jambo hilo, wana hatia.
And, if the whole assembly of Israel, shall make a mistake, and a matter be hidden from the eyes of the convocation, —and so they do something, whereby they depart from any of the commandments of Yahweh as to things which should not be done, and become guilty;
14 Wanapotambua kuhusu dhambi waliyoitenda, lazima kusanyiko lilete fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi na kuikabidhi mbele ya Hema la Kukutania.
and the sin shall become known, which they have committed therein, then shall the convocation bring near a choice young bullock as a sin-bearer, yea they shall bring it in. before the tent of meeting;
15 Wazee wa jumuiya wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo fahali aliye mbele za Bwana, naye fahali atachinjwa mbele za Bwana.
and the elders of the assembly shall lean their hands upon the head of the bullock before Yahweh, —and shall slay the bullock, before Yahweh;
16 Kisha kuhani aliyetiwa mafuta ataiingiza sehemu ya damu ya huyo fahali ndani ya Hema la Kukutania.
and the anointed priest shall bring in of the blood of the bullock, —into the tent of meeting;
17 Atachovya kidole chake kwenye damu na kuinyunyiza mara saba mbele za Bwana mbele ya hilo pazia.
and the priest shall dip his finger in the blood, —and shall sprinkle of the blood seven times before Yahweh, upon the face of the veil;
18 Atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu yaliyo mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu ya kuteketezea sadaka, penye ingilio la Hema la Kukutania.
and, some of the blood, shall he put upon the horns of the altar which is before Yahweh, which is in the tent of meeting; and, all the [remainder of the] blood, shall he pour out at the base of the altar of ascending-sacrifice, which is at the entrance of the tent of meeting;
19 Atayaondoa mafuta yote ya yule fahali na kuyateketeza juu ya madhabahu,
and, as for all the fat thereof, he shall heave up therefrom, —and make a perfume at the altar.
20 naye atamfanyia fahali huyu kama alivyomfanyia yule fahali mwingine wa sadaka ya dhambi. Kwa njia hii kuhani atawafanyia watu upatanisho, nao watasamehewa.
And he shall do to the bullock, as he did to the [first] sin-bearing bullock, so shall he do with this, —and the priest shall put a propitiatory-covering over them, and it shall be forgiven them.
21 Kisha atamchukua yule fahali nje ya kambi na kumteketeza kama alivyomteketeza yule wa kwanza. Hii ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya jumuiya.
And he shall take forth the bullock unto the outside of the camp, and burn it up, just as he burned up the first bullock, —the sin-bearer of the convocation, it is.
22 “‘Wakati kiongozi ametenda dhambi bila kukusudia na kufanya yaliyokatazwa katika amri yoyote ya Bwana Mungu wake, ana hatia.
When a prince, shall sin, —and shall do something, departing from any of the commandments of Yahweh his God as to things which should not be done, by mistake and shall become aware of his guilt;
23 Atakapofahamishwa dhambi aliyotenda, ni lazima alete mbuzi dume asiye na dosari kama sadaka yake.
or his sin wherein he hath sinned be made known unto him, then shall he bring in. as his oblation a he-goat a male without defect;
24 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha yule mbuzi na kumchinja mahali pale ambapo sadaka za kuteketezwa huchinjiwa mbele za Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
and shall lean his hand upon the head of the goat, and shall slay it in the place where they slay the ascending-sacrifice before Yahweh, —a sin-bearer, it is.
25 Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketeza, na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
And the priest shall take of the blood of the sin-bearer with his finger, and put upon the horns of the altar of ascending-sacrifice; and, the [remainder of the] blood thereof, shall he pour out at the base of the altar of ascending-sacrifice;
26 Atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, kama alivyoteketeza mafuta ya sadaka ya amani. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho wa dhambi kwa ajili ya yule mtu, naye atasamehewa.
and with all the fat thereof, shall he make a perfume at the altar, as with the fat of the peace-offering, —so shall the priest put a propitiatory-covering over him because of his sin, and it shall be forgiven him.
27 “‘Kama mtu katika jumuiya ametenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, yeye ana hatia.
And, if, any person, shall sin, by mistake from among the people of the land, —by his doing anything departing from any of the commandments of Yahweh, as to things which should not be done, and shall become aware of his guilt;
28 Atakapofahamishwa dhambi yake aliyoitenda, ni lazima alete mbuzi jike asiye na dosari kama sadaka yake kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
or his sin which he hath committed shall be made known unto, him, then shall he bring in, as his oblation, a kid of the goats a female, without defect, for his sin which he hath committed;
29 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kumchinjia mahali pa kuteketezea sadaka.
and shall lean his hand upon the head of the sin-bearer, —and shall slay the sin-bearer in the place of the ascending-sacrifice.
30 Kisha kuhani atachukua sehemu ya ile damu kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
Then shall the priest take of the blood thereof with his finger, and put upon the horns of the altar of ascending-sacrifice, —and all the [remaining] blood thereof, shall he pour out, at the base of the altar;
31 Atayaondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kwenye sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.
and all the fat thereof, shall he remove as the fat from off the peace-offering was removed, and the priest shall make a perfume at the altar, for a satisfying odour unto Yahweh, —so shall the priest put a propitiatory-covering over him, and it shall be forgiven him.
32 “‘Ikiwa ataleta mwana-kondoo kama sadaka yake ya dhambi, atamleta jike asiye na dosari.
And, if a lamb, he bring in. as his oblation for a sin-bearer, a female without defect, shall he bring in;
33 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo mwana-kondoo na kumchinja kwa ajili ya sadaka ya dhambi mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa.
and shall lean his hand upon the head of the sin-bearer, —and shall slay it as a sin-bearer, in the place where they slay the ascending-sacrifice.
34 Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na ile damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu.
Then shall the priest take of the blood of the sin-bearer with his finger, and put upon the horns of the altar of ascending-sacrifice, —and all the [remaining] blood thereof, shall he pour out, at the base of the altar;
35 Ataondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kutoka kwenye mwana-kondoo wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu juu ya zile sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.
and all the fat thereof, shall he remove as the fat of the lamb is removed, from the peace-offering, and the priest shall make a perfume therewith at the altar, upon the altar-flames of Yahweh, —so shall the priest put a propitiatory-covering over him on account of his sin which he hath committed, and it shall be forgiven him.

< Mambo ya Walawi 4 >