< Mambo ya Walawi 4 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Og HERREN talede til Moses og sagde:
2 “Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote afanyapo dhambi bila kukusudia na akatenda lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana:
Tal til Israeliterne og sig: Naar nogen af Vanvare forsynder sig mod noget af HERRENS Forbud og overtræder et af dem, da skal følgende iagttages:
3 “‘Ikiwa kuhani aliyetiwa mafuta amefanya dhambi na kuwaletea watu hatia, lazima alete kwa Bwana fahali mchanga asiye na dosari, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
Er det den salvede Præst, der forsynder sig, saa der paadrages Folket Skyld, skal han for den Synd, han har begaaet, bringe HERREN en lydefri ung Tyr som Syndoffer.
4 Atamkabidhi huyo fahali kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo fahali na kumchinja mbele za Bwana.
Han skal føre Tyren hen til Aabenbaringsteltets Indgang for HERRENS Aasyn og lægge sin Haand paa dens Hoved og slagte den for HERRENS Aasyn,
5 Kisha kuhani huyo aliyetiwa mafuta atachukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuileta katika Hema la Kukutania.
og den salvede Præst skal tage noget af Tyrens Blod og bringe det ind i Aabenbaringsteltet,
6 Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza sehemu yake mara saba mbele za Bwana mbele ya pazia la mahali patakatifu.
og Præsten skal dyppe sin Finger i Blodet og stænke det syv Gange for HERRENS Aasyn foran Helligdommens Forhæng;
7 Kisha kuhani atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu ya kufukizia uvumba wenye harufu nzuri iliyoko mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ya huyo fahali ataimwaga chini ya hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
og Præsten skal stryge noget af Blodet paa Røgelsealterets Horn for HERRENS Aasyn, det, som staar i Aabenbaringsteltet; Resten af Tyrens Blod skal han udgyde ved Foden af Brændofferalteret, som staar ved Indgangen til Aabenbaringsteltet.
8 Atayaondoa mafuta yote ya fahali huyo wa sadaka ya dhambi, mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani au zile zinazounganika nazo,
Men alt Syndoffertyrens Fedt skal han tage ud Fedtet, som dækker Indvoldene, og alt Fedtet paa Indvoldene,
9 figo zote mbili na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yale yanayofunika ini ambayo atayaondoa pamoja na figo zote,
begge Nyrerne med det Fedt, som sidder paa dem ved Lændemusklerne, og Leverlappen, som han skal skille fra ved Nyrerne,
10 kama vile mafuta yanayoondolewa kutoka kwenye maksai aliyetolewa sadaka ya amani. Kisha kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
paa samme Maade som det udtages af Takofferoksen. Og Præsten skal bringe det som Røgoffer paa Brændofferalteret.
11 Lakini ngozi ya huyo fahali na nyama zake zote, pamoja na kichwa na miguu yake, sehemu za ndani na matumbo,
Men Tyrens Hud og alt dens Kød tillige med dens Hoved, Skinneben, Indvolde og Skarn,
12 yaani sehemu nyingine zote zilizobaki za huyo fahali, lazima azitoe nje ya kambi mpaka mahali palipo safi kiibada, ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni zilizoko juu ya lundo la majivu.
hele Tyren skal han bringe uden for Lejren til et urent Sted, til Askedyngen, og brænde den paa et Baal af Brænde; oven paa Aske; dyngen skal den brændes.
13 “‘Ikiwa jumuiya yote ya Israeli watatenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, hata kama jumuiya haifahamu juu ya jambo hilo, wana hatia.
Men hvis det et hele Israels Menighed, der forser sig, uden at Forsamlingen ved af det, og de har overtraadt et af HERRENS Forbud og derved paadraget sig Skyld,
14 Wanapotambua kuhusu dhambi waliyoitenda, lazima kusanyiko lilete fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi na kuikabidhi mbele ya Hema la Kukutania.
da skal Forsamlingen, naar den Synd, de har begaaet mod Forbudet, bliver kendt, bringe en ung, lydefri Tyr som Syndoffer; de skal føre den hen foran Aabenbaringsteltet,
15 Wazee wa jumuiya wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo fahali aliye mbele za Bwana, naye fahali atachinjwa mbele za Bwana.
og Menighedens Ældste skal lægge deres Hænder paa Tyrens Hoved for HERRENS Aasyn, og man skal slagte den for HERRENS Aasyn.
16 Kisha kuhani aliyetiwa mafuta ataiingiza sehemu ya damu ya huyo fahali ndani ya Hema la Kukutania.
Derpaa skal den salvede Præst bringe noget af Tyrens Blod ind i Aabenbaringsteltet,
17 Atachovya kidole chake kwenye damu na kuinyunyiza mara saba mbele za Bwana mbele ya hilo pazia.
og Præsten skal dyppe sin Finger i Blodet og stænke det syv Gange for HERRENS Aasyn foran Forhænget;
18 Atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu yaliyo mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu ya kuteketezea sadaka, penye ingilio la Hema la Kukutania.
og han skal stryge noget af Blodet paa Hornene af Alteret, som staar for HERRENS Aasyn i Aabenbaringsteltet; Resten af Blodet skal han udgyde ved Foden af Brændofferalteret, som staar ved Indgangen til Aabenbaringsteltet,
19 Atayaondoa mafuta yote ya yule fahali na kuyateketeza juu ya madhabahu,
Men alt, Fedtet skal han tage ud og bringe det som Røgoffer paa Alteret.
20 naye atamfanyia fahali huyu kama alivyomfanyia yule fahali mwingine wa sadaka ya dhambi. Kwa njia hii kuhani atawafanyia watu upatanisho, nao watasamehewa.
Derpaa skal han gøre med Tyren paa samme Maade som med den før nævnte Syndoffertyr. Da skal Præsten skaffe dem Soning, saa de finder Tilgivelse.
21 Kisha atamchukua yule fahali nje ya kambi na kumteketeza kama alivyomteketeza yule wa kwanza. Hii ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya jumuiya.
Saa skal Tyren bringes uden for Lejren og brændes paa samme Maade som den før nævnte Tyr. Det er Menighedens Syndoffer.
22 “‘Wakati kiongozi ametenda dhambi bila kukusudia na kufanya yaliyokatazwa katika amri yoyote ya Bwana Mungu wake, ana hatia.
Men hvis det er en Øverste, der forsynder sig og af Vanvare overtræder et af HERRENS Forbud og derved paa drager sig Skyld,
23 Atakapofahamishwa dhambi aliyotenda, ni lazima alete mbuzi dume asiye na dosari kama sadaka yake.
og den Synd, han har begaaet, bliver ham vitterlig, saa skal den Offergave, han bringer, være en lydefri Gedebuk.
24 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha yule mbuzi na kumchinja mahali pale ambapo sadaka za kuteketezwa huchinjiwa mbele za Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
Han skal lægge sin Haand paa Bukkens Hoved og slagte den der, hvor Brændofferet slagtes for HERRENS Aasyn. Det er et Syndoffer.
25 Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketeza, na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
Præsten skal tage noget af Syndofferets Blod paa sin Finger og stryge det paa Brændofferalterets Horn, og Resten af Blodet skal han udgyde ved Brændofferalterets Fod.
26 Atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, kama alivyoteketeza mafuta ya sadaka ya amani. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho wa dhambi kwa ajili ya yule mtu, naye atasamehewa.
Og alt dets Fedt skal han bringe som Røgoffer paa Alteret ligesom Fedtet fra Takofferet. Da skal Præsten skaffe ham Soning for hans Synd, saa han finder Tilgivelse.
27 “‘Kama mtu katika jumuiya ametenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, yeye ana hatia.
Men hvis det er en af Almuen, der af Vanvare forsynder sig ved at overtræde et af HERRENS Forbud og derved paadrager sig Skyld,
28 Atakapofahamishwa dhambi yake aliyoitenda, ni lazima alete mbuzi jike asiye na dosari kama sadaka yake kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
og den Synd, han har begaaet, bliver ham vitterlig, saa skal Offergaven, han bringer for den Synd, han har begaaet, være en lydefri Ged.
29 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kumchinjia mahali pa kuteketezea sadaka.
Han skal lægge sin Haand paa Syndofferets Hoved og slagte Syndofferet der, hvor Brændofferet slagtes.
30 Kisha kuhani atachukua sehemu ya ile damu kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
Præsten skal tage noget af Gedens Blod paa sin Finger og stryge det paa Brændofferalterets Horn, og Resten af Blodet skal han udgyde ved Alterets Fod.
31 Atayaondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kwenye sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.
Og alt Fedtet skal han tage ud, paa samme Maade som Fedtet tages ud af Takofferet, og Præsten skal bringe det som Røgoffer paa Alteret til en liflig Duft for HERREN. Da skal Præsten skaffe ham Soning, saa han finder Tilgivelse.
32 “‘Ikiwa ataleta mwana-kondoo kama sadaka yake ya dhambi, atamleta jike asiye na dosari.
Men hvis den Offergave, han vil bringe som Syndoffer, er et Lam, da skal det være et lydefrit Hundyr, han bringer.
33 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo mwana-kondoo na kumchinja kwa ajili ya sadaka ya dhambi mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa.
Han skal lægge sin Haand paa Syndofferets Hoved og slagte det som Syndoffer der, hvor Brændofferet slagtes.
34 Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na ile damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu.
Og Præsten skal tage noget af Syndofferets Blod paa sin Finger og stryge det paa Brændofferalterets Horn, men Resten af Blodet skal han udgyde ved Alterets Fod,
35 Ataondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kutoka kwenye mwana-kondoo wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu juu ya zile sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.
og alt Fedtet skal han tage ud, paa samme Maade som Takofferlammets Fedt tages ud, og Præsten skal bringe det som Røgoffer paa Alteret oven paa HERRENS Ildofre. Da skal Præsten skaffe ham Soning for den Synd, han har begaaet, saa han finder Tilgivelse.

< Mambo ya Walawi 4 >