< Mambo ya Walawi 3 >

1 “‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
Lorsqu'un homme offrira un sacrifice pacifique, s'il offre du gros bétail, mâle ou femelle, il l'offrira sans défaut devant Yahweh.
2 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
Il posera sa main sur la tête de la victime et il l'égorgera à l'entrée de la tente de réunion, et les prêtres, fils d'Aaron, répandront le sang sur les parois de l'autel tout autour.
3 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
De ce sacrifice pacifique, il offrira en sacrifice par le feu à Yahweh: la graisse qui enveloppe les entrailles et toute la graisse qui est attachée aux entrailles;
4 figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
les deux rognons avec la graisse qui les recouvre et qui tient à la région lombaire; la taie du foie qu'il détachera près des rognons.
5 Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Les fils d'Aaron feront fumer cela sur l'autel, par-dessus l'holocauste placé sur le bois qui est sur le feu. C'est un sacrifice fait par le feu, d'une agréable odeur à Yahweh.
6 “‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
S'il offre du menu bétail, mâle ou femelle, en sacrifice pacifique à Yahweh, il l'offrira sans défaut.
7 Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
S'il offre en sacrifice un agneau, il le présentera devant Yahweh.
8 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
Il posera sa main sur la tête de la victime et il l'égorgera devant la tente de réunion, et les fils d'Aaron en répandront le sang sur les parois de l'autel tout autour.
9 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
De ce sacrifice pacifique, il offrira en sacrifice par le feu à Yahweh: sa graisse, la queue entière, coupée près de l'échine; la graisse qui enveloppe les entrailles et toute la graisse qui est attachée aux entrailles;
10 figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
les deux rognons, avec la graisse qui les recouvre et qui tient à la région lombaire; la taie du foie qu'il détachera près des rognons.
11 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
Le prêtre fera fumer cela sur l'autel: c'est l'aliment d'un sacrifice fait par le feu à Yahweh.
12 “‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
Si son offrande est une chèvre, il la présentera devant Yahweh.
13 Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
Il posera sa main sur la tête de la victime, et il l'égorgera devant la tente de réunion, et les fils d'Aaron en répandront le sang sur les parois de l'autel tout autour.
14 Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
De la victime, il offrira en sacrifice par le feu à Yahweh: la graisse qui enveloppe les entrailles et toute la graisse qui est attachée aux entrailles;
15 figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
les deux rognons, avec la graisse qui les recouvre et qui tient à la région lombaire; la taie du foie qu'il détachera près des rognons.
16 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
Le prêtre fera fumer cela sur l'autel: c'est l'aliment d'un sacrifice fait par le feu d'une agréable odeur. Toute graisse appartient à Yahweh.
17 “‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”
C'est ici une loi perpétuelle pour vos descendants, en quelque lieu que vous habitiez: vous ne mangerez ni graisse, ni sang. "

< Mambo ya Walawi 3 >