< Mambo ya Walawi 3 >
1 “‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
"Jos hänen uhrilahjansa on yhteysuhri, tuokoon hän, jos hän tuo raavaskarjasta härän tai lehmän, virheettömän eläimen Herran eteen.
2 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
Ja hän laskekoon kätensä uhriteuraansa pään päälle ja teurastakoon sen ilmestysmajan ovella; ja papit, Aaronin pojat, vihmokoot veren alttarille ympärinsä.
3 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
Ja hän tuokoon yhteysuhrista uhrina Herralle sisälmyksiä peittävän rasvan ja kaiken sisälmysten rasvan
4 figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
ja molemmat munuaiset ynnä niiden päällä lantiolihaksissa olevan rasvan ja maksanlisäkkeen, joka on irroitettava munuaisten luota.
5 Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Ja Aaronin pojat polttakoot sen alttarilla polttouhrin päällä, joka on halkojen päällä tulessa, suloisesti tuoksuvana uhrina Herralle.
6 “‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
Mutta jos hän tuo uhrilahjanaan Herralle yhteysuhriksi pikkukarjasta urospuolen tai naaraspuolen, niin tuokoon virheettömän eläimen.
7 Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
Jos hän tuo uhrilahjanaan lampaan, niin tuokoon sen Herran eteen
8 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
ja laskekoon kätensä uhriteuraansa pään päälle ja teurastakoon sen ilmestysmajan ovella, ja Aaronin pojat vihmokoot sen veren alttarille ympärinsä.
9 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
Ja hän tuokoon yhteysuhrista uhrina Herralle sen rasvan, koko rasvahännän, joka on irroitettava häntänikamista, sisälmyksiä peittävän rasvan ja kaiken sisälmysten rasvan
10 figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
ja molemmat munuaiset ynnä niiden päällä lantiolihaksissa olevan rasvan ja maksanlisäkkeen, joka on irroitettava munuaisten luota.
11 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
Ja pappi polttakoon sen alttarilla uhriruokana Herralle.
12 “‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
Ja jos hänen uhrilahjansa on vuohi, tuokoon sen Herran eteen
13 Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
ja laskekoon kätensä sen pään päälle ja teurastakoon sen ilmestysmajan ovella; ja Aaronin pojat vihmokoot sen veren alttarille ympärinsä.
14 Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
Ja hän tuokoon siitä uhrilahjanaan Herralle uhriksi sisälmyksiä peittävän rasvan ja kaiken sisälmysten rasvan
15 figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
ja molemmat munuaiset ynnä niiden päällä lantiolihaksissa olevan rasvan ja maksanlisäkkeen, joka on irroitettava munuaisten luota.
16 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
Ja pappi polttakoon ne alttarilla uhriruokana, suloisesti tuoksuvana uhrina; kaikki rasva olkoon Herran oma.
17 “‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”
Tämä olkoon teille ikuinen säädös sukupolvesta sukupolveen, missä asuttekin: mitään rasvaa tai verta älkää syökö."