< Mambo ya Walawi 3 >
1 “‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
“And if his offering [is] a sacrifice of peace-offerings, if he is bringing near out of the herd, whether male or female, he brings a perfect one near before YHWH,
2 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
and he has laid his hand on the head of his offering, and has slaughtered it at the opening of the Tent of Meeting, and sons of Aaron, the priests, have sprinkled the blood around the altar.
3 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
And he has brought near from the sacrifice of the peace-offerings a fire-offering to YHWH, the fat which is covering the innards, and all the fat which [is] on the innards,
4 figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
and the two kidneys, and the fat which [is] on them, which [is] on the flanks, and the redundance on the liver above the kidneys—he turns it aside,
5 Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
and sons of Aaron have made it an incense on the altar, on the burnt-offering which [is] on the wood, which [is] on the fire, [as] a fire-offering of refreshing fragrance to YHWH.
6 “‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
And if his offering [is] out of the flock for a sacrifice of peace-offerings to YHWH, male or female, he brings a perfect one near;
7 Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
if he is bringing a sheep near [for] his offering, then he has brought it near before YHWH,
8 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
and has laid his hand on the head of his offering, and has slaughtered it before the Tent of Meeting, and sons of Aaron have sprinkled its blood around the altar.
9 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
And he has brought near from the sacrifice of the peace-offerings a fire-offering to YHWH, its fat, the whole fat tail close by the bone—he turns it aside, and the fat which is covering the innards, and all the fat which [is] on the innards,
10 figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
and the two kidneys, and the fat which [is] on them, which [is] on the flanks, and the redundance on the liver above the kidneys—he turns it aside,
11 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
and the priest has made it an incense on the altar [as] bread of a fire-offering to YHWH.
12 “‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
And if his offering [is] a goat, then he has brought it near before YHWH,
13 Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
and has laid his hand on its head, and has slaughtered it before the Tent of Meeting, and sons of Aaron have sprinkled its blood around the altar;
14 Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
and he has brought his offering near from it, a fire-offering to YHWH, the fat which is covering the innards, and all the fat which [is] on the innards,
15 figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
and the two kidneys, and the fat which [is] on them, which [is] on the flanks, and the redundance on the liver above the kidneys—he turns it aside,
16 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
and the priest has made them an incense on the altar [as] bread of a fire-offering, for refreshing fragrance; all the fat [is] YHWH’s.
17 “‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”
[This is] a continuous statute throughout your generations in all your dwellings: you do not eat any fat or any blood.”