< Mambo ya Walawi 3 >

1 “‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
And if his oblation be a sacrifice of peace-offering, if he offer it of the herds, whether it be a male or female, he shall offer it without blemish before the Lord.
2 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
And he shall lay his hand upon the head of his offering, and kill it at the door of the tabernacle of the congregation: and the sons of Aaron the priests shall sprinkle the blood upon the altar round about.
3 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
And he shall offer the sacrifice of the peace-offering, as a fire-offering unto the Lord, the fat that covereth the inwards, and all the fat that is upon the inwards,
4 figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
And the two kidneys, and the fat that is on them, which is on the flanks, and the midriff above the liver, with the kidneys, shall he remove it.
5 Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
And Aaron's sons shall burn it on the altar, upon the burnt-offering, which is upon the wood that is on the fire: it is an offering made by fire, of a sweet savor unto the Lord.
6 “‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
And if of the flocks be his offering for a sacrifice of peace-offering unto the Lord, male or female, without blemish, shall he offer it.
7 Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
If he offer a sheep for his offering, then shall he bring it near before the Lord.
8 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
And he shall lay his hand upon the head of his offering, and kill it before the tabernacle of the congregation: and the sons of Aaron shall sprinkle its blood upon the altar round about.
9 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
And he shall offer the sacrifice of the peace-offering, as a fire-offering unto the Lord, the best part thereof, the whole rump, hard by the backbone shall he take it off; and the fat that covereth the inwards, and all the fat that is upon the inwards;
10 figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
And the two kidneys, and the fat that is upon them, which is on the flanks, and the midriff above the liver, with the kidneys, shall he remove it.
11 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And the priest shall burn it upon the altar: it is the food of the offering made by fire unto the Lord.
12 “‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
And if a goat be his offering, then shall he bring it near before the Lord.
13 Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
And he shall lay his hand upon its head, and kill it before the tabernacle of the congregation: and the sons of Aaron shall sprinkle its blood upon the altar round about.
14 Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
And he shall offer thereof his offering, as a fire-offering unto the Lord, the fat that covereth the inwards, and all the fat that is upon the inwards.
15 figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
And the two kidneys, and the fat that is upon them, which is on the flanks, and the midriff above the liver, with the kidneys shall he remove it.
16 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
And the priest shall burn them upon the altar; as the food of the offering made by fire for a sweet savor, is all the fat unto the Lord.
17 “‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”
A perpetual statute shall it be for your generations throughout all your dwellings: no fat nor blood shall ye eat.

< Mambo ya Walawi 3 >