< Mambo ya Walawi 3 >

1 “‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
Also if his oblation be a peace offering, if he will offer of the droue (whether it be male or female) he shall offer such as is without blemish, before the Lord,
2 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
And shall put his hande vpon the head of his offering, and kill it at the doore of the Tabernacle of the Congregation: and Aarons sonnes the Priestes shall sprinkle the blood vpon the altar rounde about.
3 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
So he shall offer part of the peace offerings as a sacrifice made by fire vnto the Lord, euen the fat that couereth the inwardes, and all the fat that is vpon the inwardes.
4 figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
He shall also take away the two kidneis, and the fat that is on them, and vpon the flankes, and the kall on the liuer with the kidneis.
5 Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
And Aarons sonnes shall burne it on the altar, with the burnt offering, which is vpon the wood, that is on the fire: this is a sacrifice made by fire for a sweete sauour vnto the Lord.
6 “‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
Also if his oblation be a peace offring vnto the Lord out of ye flocke, whether it be male or female, he shall offer it without blemish.
7 Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
If he offer a lambe for his oblation, then he shall bring it before the Lord,
8 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
And lay his hand vpon the head of his offring, and shall kill it before the Tabernacle of the Congregation, and Aarons sonnes shall sprinckle the blood thereof round about vpon the altar.
9 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
After, of the peace offrings he shall offer an offring made by fire vnto the Lord: he shall take away the fat therof, and the rump altogether, hard by the backe bone, and the fat that couereth the inwardes, and all the fat that is vpon the inwards.
10 figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
Also hee shall take away the two kidneis, with the fat that is vpon them, and vpon the flankes, and the kall vpon the liuer with the kidneis.
11 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
Then the Priest shall burne it vpon the altar, as the meat of an offring made by fire vnto the Lord.
12 “‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
Also if his offring be a goate, then shall he offer it before the Lord,
13 Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
And shall put his hande vpon the head of it, and kill it before the Tabernacle of the Congregation, and the sonnes of Aaron shall sprinkle the blood thereof vpon the altar round about.
14 Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
Then he shall offer thereof his offring, euen an offring made by fire vnto the Lord, the fat that couereth the inwardes, and all the fatte that is vpon the inwardes.
15 figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
Also hee shall take away the two kidneis, and the fat that is vpon them, and vpon ye flankes, and the kall vpon the liuer with the kidneis.
16 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
So the Priest shall burne them vpon the altar, as the meate of an offering made by fire for a sweete sauour: all the fatte is the Lordes.
17 “‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”
This shalbe a perpetual ordinance for your generations, throughout al your dwellings, so that ye shall eate neither fatte nor blood.

< Mambo ya Walawi 3 >