< Mambo ya Walawi 3 >

1 “‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
But if his oblation will be a sacrifice of peace offerings, and he wishes to offer it from the oxen, whether male or female, he shall offer what is immaculate, in the sight of the Lord.
2 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
And he shall place his hand upon the head of his victim, which shall be immolated at the entrance of the tabernacle of the testimony. And the sons of Aaron, the priests, shall pour the blood all around the altar.
3 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
And they shall offer from the sacrifice of peace offerings, as an oblation to the Lord: the fat which covers the vital organs, and whatever fat is interior,
4 figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
the two kidneys with the fat that covers the sides, and the mesh of the liver with the two little kidneys.
5 Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
And they shall burn them upon the altar as a holocaust, placing fire under the wood, as an oblation of a most sweet odor to the Lord.
6 “‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
Yet truly, if his oblation and the sacrifice of peace offerings will be from the sheep, whether he will offer a male or a female, they shall be immaculate.
7 Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
If he will offer a lamb in the sight of the Lord,
8 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
he shall place his hand upon the head of the victim. And it shall be immolated at the vestibule of the tabernacle of the testimony. And the sons of Aaron shall pour its blood all around the altar.
9 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
And they shall offer from the victim of peace offerings, as a sacrifice to the Lord: the fat, and the entire rump
10 figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
with the kidneys, and the fat that covers the abdomen, and all the vital organs, and both the little kidneys with the fat that is near the sides, and the mesh of the liver with the little kidneys.
11 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And the priest shall burn them upon the altar, as fuel for the fire and as an oblation of the Lord.
12 “‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
If his oblation will be a goat, and he will offer it to the Lord,
13 Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
he shall place his hand upon its head, and he shall immolate it at the entrance of the tabernacle of the testimony. And the sons of Aaron shall pour its blood all around the altar.
14 Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
And they shall take from it, to feed the Lord’s fire: the fat which covers the abdomen, and that which covers all the vital organs,
15 figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
the two little kidneys with the mesh that is over them near the sides, and the fat of the liver with the little kidneys.
16 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
And the priest shall burn them upon the altar, as nourishment for the fire and as a most sweet odor. All the fat shall be for the Lord;
17 “‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”
by a perpetual law, in your generations and in all of your habitations, neither blood nor fat shall you eat at all.

< Mambo ya Walawi 3 >