< Mambo ya Walawi 27 >

1 Bwana akamwambia Mose,
خداوند به موسی فرمود:
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kama mtu yeyote ataweka nadhiri maalum ili kuweka watu wakfu kwa Bwana, kwa kutoa kiasi cha thamani inayolingana,
«این دستورها را به قوم بنی‌اسرائیل بده: هرگاه شخصی به موجب نذری به خداوند وقف شود، می‌تواند مبلغ معینی بپردازد و خود را از وقف آزاد سازد.
3 thamani ya kukomboa mwanaume mwenye kati ya umri wa miaka ishirini na miaka sitini itakuwa shekeli hamsini za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu;
مردی که سنش بین بیست تا شصت سال باشد، پنجاه مثقال نقره برحسب مثقالِ عبادتگاه، بپردازد.
4 ikiwa ni mwanamke, weka thamani yake kwa shekeli thelathini.
زنی که سنش بین بیست تا شصت سال باشد سی مثقال نقره،
5 Kama ni mtu mwenye umri wa miaka kati ya mitano na ishirini, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli ishirini, na mwanamke shekeli kumi.
پسران پنج تا بیست ساله باید بیست مثقال نقره و دختران پنج تا بیست ساله باید ده مثقال نقره بپردازند.
6 Kama ni mtu mwenye umri kati ya mwezi mmoja na miaka mitano, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli tano za fedha, na ile ya mwanamke kuwa shekeli tatu za fedha.
برای پسر یک ماهه تا پنج ساله، پنج مثقال نقره و برای دختر یک ماهه تا پنج ساله، سه مثقال نقره پرداخت شود.
7 Kama ni mtu mwenye miaka sitini na zaidi, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli kumi na tano, na mwanamke shekeli kumi.
مرد از شصت سال به بالا باید پانزده مثقال نقره و زن از شصت سال به بالا باید ده مثقال نقره بپردازد.
8 Kama mtu yeyote anayeweka nadhiri ni maskini mno kuweza kulipa kiasi kilichowekwa, atampeleka huyo mtu kwa kuhani, ambaye ataweka thamani yake kulingana na kile mweka nadhiri anachoweza kulipa.
ولی اگر کسی فقیرتر از آن باشد که بتواند این مبلغ را بپردازد، نزد کاهن آورده شود و کاهن مبلغی را تعیین کند که او قادر به پرداخت آن باشد.
9 “‘Kama kile mtu alichokiwekea nadhiri ni mnyama anayekubalika kama sadaka kwa Bwana, mnyama wa namna hiyo aliyetolewa kwa Bwana anakuwa mtakatifu.
«اگر نذر او شامل دادن حیوانی است که به عنوان قربانی به خداوند تقدیم می‌شود، چنین هدیه‌ای به خداوند مقدّس خواهد بود.
10 Mtu haruhusiwi kumbadilisha au kutoa mnyama mzuri kwa mbaya, au mnyama mbaya kwa mzuri. Kama atatoa mnyama badala ya mwingine, wanyama wote wawili, yaani yule aliyetolewa na yule aliyebadiliwa, ni watakatifu.
نذرکننده تصمیم خود را در خصوص چیزی که برای خداوند نذر کرده است نباید تغییر دهد و خوب را با بد یا بد را با خوب عوض نکند. اگر چنین کند، اولی و دومی، هر دو از آن خداوند خواهند بود.
11 Kama alichokiwekea nadhiri ni mnyama aliye najisi kiibada, yaani yule asiye kubalika kuwa sadaka kwa Bwana, huyo mnyama lazima aletwe kwa kuhani,
ولی اگر حیوانی که برای خداوند نذر شده آن نوع حیوانی نیست که برای قربانی مجاز می‌باشد، صاحبش آن را نزد کاهن بیاورد
12 ambaye ataamua ubora wa mnyama huyo, kama ni mzuri au mbaya. Thamani yoyote atakayoweka kuhani, hivyo ndivyo itakavyokuwa.
تا قیمتش را تعیین کند و او باید آن مبلغ را هر قدر که باشد، بپردازد.
13 Kama mwenye mnyama atapenda kumkomboa mnyama huyo, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake.
اگر حیوان از نوعی است که می‌توان آن را به عنوان قربانی تقدیم نمود ولی صاحبش می‌خواهد آن را بازخرید نماید، در آن صورت علاوه بر قیمتی که کاهن تعیین می‌کند، باید یک پنجم قیمت آن را نیز اضافه بپردازد.
14 “‘Kama mtu ataweka nyumba yake wakfu kama kitu kitakatifu kwa Bwana, kuhani ataamua ubora wa nyumba hiyo, kama ni nzuri au mbaya. Thamani yoyote kuhani atakayoweka, basi hivyo ndivyo itakavyokuwa.
«اگر کسی خانهٔ خود را وقف خداوند کند، کاهن باید قیمت خانه را تعیین کند و نذرکننده، این مبلغ را هر قدر که باشد، بپردازد.
15 Kama mtu aliyeweka nyumba yake wakfu ataikomboa, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, nayo nyumba itakuwa yake tena.
اگر وقف کننده بخواهد خانۀ خود را بازخرید کند، باید یک پنجم بر قیمت آن اضافه کند، آنگاه خانه دوباره از آن خودش خواهد بود.
16 “‘Kama mtu anaweka sehemu ya ardhi ya jamaa yake wakfu kwa Bwana, thamani yake itawekwa kulingana na kiasi cha mbegu inayohitajiwa kupandwa katika ardhi hiyo, yaani homeri moja ya mbegu za shayiri kwa shekeli hamsini za fedha.
«اگر کسی قسمتی از زمین خود را وقف خداوند کند، ارزش آن به تناسب مقدار بذری که در آن می‌توان کاشت تعیین شود. قطعه زمینی که صد کیلو جو در آن پاشیده شود، پنجاه مثقال نقره ارزش دارد.
17 Kama akiweka shamba lake wakfu katika Mwaka wa Yubile, ile thamani iliyokwisha wekwa itakuwa iyo hiyo.
اگر شخصی در سال یوبیل مزرعهٔ خود را وقف خداوند کند، در آن صورت قیمت زمین برابر با قیمت محصول پنجاه سالهٔ آن خواهد بود.
18 Lakini kama akiweka shamba lake wakfu baada ya Yubile, kuhani ataweka thamani kulingana na idadi ya miaka iliyobaki kufikia Mwaka wa Yubile unaofuata, na thamani yake iliyoamuliwa itapunguzwa.
ولی اگر بعد از سال یوبیل باشد، آنگاه کاهن قیمت زمین را به تناسب تعداد سالهایی که به سال یوبیل بعدی باقی مانده است، تعیین خواهد کرد.
19 Kama mtu anayeweka wakfu shamba anataka kulikomboa, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, nalo shamba litakuwa lake tena.
اگر آن شخص تصمیم بگیرد آن مزرعه را بازخرید نماید، بایستی علاوه بر قیمتی که کاهن تعیین می‌نماید یک پنجم هم اضافه بپردازد و مزرعه دوباره مال خودش خواهد شد.
20 Kama pengine halikomboi shamba hilo, au kama ameliuza kwa mtu mwingine, kamwe haliwezi kukombolewa.
ولی اگر مزرعه را بدون اینکه بازخرید نموده باشد، به دیگری بفروشد، دیگر هرگز حق بازخرید آن را نخواهد داشت.
21 Shamba hilo litakapoachiwa mwaka wa Yubile, litakuwa takatifu, kama shamba lililotolewa kwa Bwana, nalo litakuwa mali ya makuhani.
وقتی که در سال یوبیل آن مزرعه آزاد شود، به عنوان موقوفه متعلق به خداوند خواهد بود و باید به کاهنان داده شود.
22 “‘Kama mtu ameweka wakfu kwa Bwana shamba alilonunua, ambalo si sehemu ya ardhi ya jamaa yake,
«اگر کسی مزرعه‌ای را که خریده است، وقف خداوند کند ولی آن مزرعه قسمتی از ملک خانوادگی او نباشد،
23 kuhani ataamua thamani yake hadi Mwaka wa Yubile, naye huyo mtu atalazimika kulipa thamani yake siku hiyo kama kitu kitakatifu kwa Bwana.
کاهن باید ارزش آن را به تناسب مقدار سالهایی که تا سال یوبیل مانده، تعیین کند، و او هم باید همان روز مبلغ تعیین شده را بپردازد. این مبلغ به خداوند تعلق دارد.
24 Katika Mwaka wa Yubile, shamba litarudishwa kwa mtu yule ambaye lilinunuliwa kutoka kwake, yule ambaye ardhi ilikuwa mali yake.
در سال یوبیل مزرعه به صاحب اصلی آن که از او خریداری شده، باز پس داده شود.
25 Kila thamani lazima iwekwe kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, gera ishirini kwa shekeli.
تمام قیمت‌گذاری‌ها باید برحسب مثقال عبادتگاه که معادل بیست قیراط است، باشد.
26 “‘Lakini hakuna mtu atakayeweka wakfu mzaliwa wa kwanza wa mnyama, kwa kuwa mzaliwa wa kwanza tayari ni mali ya Bwana; awe ngʼombe au kondoo, ni wa Bwana.
«نخست‌زادۀ هر حیوانی، خواه گاو و خواه گوسفند، متعلق به خداوند است، پس کسی نمی‌تواند آن را برای خداوند نذر کند.
27 Kama ni mmoja wa wanyama walio najisi, aweza kumnunua kwa bei iliyowekwa, akiongeza sehemu ya tano ya thamani yake. Kama hatamkomboa, mnyama huyo atauzwa kwa bei iliyowekwa.
اما نوزاد حیوان حرام گوشت را که نمی‌توان برای خداوند قربانی کرد، می‌توان با پرداخت قیمتی که کاهن برای آن تعیین می‌کند به اضافهٔ یک پنجم، بازخرید نمود. اگر صاحبش نخواهد آن را بازخرید کند، کاهن می‌تواند آن را به شخص دیگری بفروشد.
28 “‘Lakini chochote kile mtu alicho nacho na akakiweka wakfu kwa Bwana, iwe ni binadamu, au mnyama, au ardhi ya jamaa, hakiwezi kuuzwa au kukombolewa. Chochote kilichowekwa wakfu ni kitakatifu sana kwa Bwana.
«اما چیزی که تماماً وقف خداوند شده باشد، چه انسان، چه حیوان و چه مزرعهٔ خانوادگی، هرگز فروخته یا بازخرید نشود چون برای خداوند بسیار مقدّس است.
29 “‘Mtu yeyote aliyewekwa wakfu ili kuangamizwa, hawezi kukombolewa. Mtu kama huyo lazima auawe.
کسی که در دادگاه به مرگ محکوم شده باشد نمی‌تواند جان خود را بازخرید نماید، بلکه باید حتماً کشته شود.
30 “‘Zaka ya kila kitu kutoka shambani, iwe ni nafaka kutoka kwa ardhi, au tunda kutoka kwa miti, ni mali ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana.
«ده‌یک محصول زمین، چه از غله و چه از میوه، از آن خداوند است و مقدّس می‌باشد.
31 Kama mtu akikomboa chochote cha zaka yake, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake.
اگر کسی بخواهد این میوه یا غله را بازخرید نماید، باید یک پنجم به قیمت اصلی آن اضافه کند.
32 Zaka yote ya kundi la ngʼombe au la kondoo na mbuzi, kila mnyama wa kumi apitaye chini ya fimbo ya yule awachungaye, atakuwa mtakatifu kwa Bwana.
ده‌یک گله و رمه از آن خداوند است. وقتی حیوانات شمرده می‌شوند، هر دهمین حیوان متعلق به خداوند است.
33 Yule mnyama wa kumi hatachaguliwa kwa kigezo cha uzuri au ubaya, naye haruhusiwi kubadiliwa. Ikiwa atabadiliwa, basi mnyama yule wa kwanza na huyo aliyebadiliwa wote watahesabiwa kuwa watakatifu, na haiwezekani kuwakomboa.’”
صاحب گله نباید حیوانات را طوری قرار دهد که حیوانات بد برای خداوند جدا شوند و نباید جای حیوان خوب را با بد عوض کند. اگر چنین کند، هر دو حیوان متعلق به خداوند خواهند بود و دیگر هرگز حق بازخرید آنها را نخواهد داشت.»
34 Haya ndiyo maagizo Bwana aliyompa Mose juu ya Mlima Sinai kwa ajili ya Waisraeli.
این است دستورهایی که خداوند در کوه سینا توسط موسی به قوم اسرائیل داد.

< Mambo ya Walawi 27 >