< Mambo ya Walawi 27 >
Un Tas Kungs runāja uz Mozu un sacīja:
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kama mtu yeyote ataweka nadhiri maalum ili kuweka watu wakfu kwa Bwana, kwa kutoa kiasi cha thamani inayolingana,
Runā uz Israēla bērniem un saki tiem: ja kas laban Tam Kungam sola īpašu solījumu, tad lai tā dvēsele Tam Kungam ir pēc tava sprieduma.
3 thamani ya kukomboa mwanaume mwenye kati ya umri wa miaka ishirini na miaka sitini itakuwa shekeli hamsini za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu;
Un tavs spriedums par vīrieti no divdesmit gadiem līdz sešdesmit gadiem lai ir tas spriedums: piecdesmit sudraba sēķeļi pēc svētās vietas sēķeļiem;
4 ikiwa ni mwanamke, weka thamani yake kwa shekeli thelathini.
Bet ja tā ir sieviete, tad lai ir tavs spriedums trīsdesmit sēķeļi.
5 Kama ni mtu mwenye umri wa miaka kati ya mitano na ishirini, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli ishirini, na mwanamke shekeli kumi.
Bet ja tas no pieci līdz divdesmit gadiem vecs, tad tavs spriedums par vīrieti lai ir divdesmit sēķeļi, bet par sievieti desmit sēķeļi.
6 Kama ni mtu mwenye umri kati ya mwezi mmoja na miaka mitano, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli tano za fedha, na ile ya mwanamke kuwa shekeli tatu za fedha.
Bet ja tas vienu mēnesi līdz pieci gadiem vecs, tad tavs spriedums par vīrieti lai ir pieci sudraba sēķeļi, un par sievieti trīs sudraba sēķeļi.
7 Kama ni mtu mwenye miaka sitini na zaidi, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli kumi na tano, na mwanamke shekeli kumi.
Bet ja tas sešdesmit gadus vecs un pāri, ja tas ir vīrs, tad lai ir tavs spriedums piecpadsmit sēķeļi, un ja ir sieva, desmit sēķeļi.
8 Kama mtu yeyote anayeweka nadhiri ni maskini mno kuweza kulipa kiasi kilichowekwa, atampeleka huyo mtu kwa kuhani, ambaye ataweka thamani yake kulingana na kile mweka nadhiri anachoweza kulipa.
Bet ja tam nav tik daudz pie rokas, kā tu viņam esi nospriedis, tad to būs vest pie priestera, un priesteris lai viņu apspriež; pēc tam, cik tā solītāja roka var pelnīt, lai priesteris viņam spriež.
9 “‘Kama kile mtu alichokiwekea nadhiri ni mnyama anayekubalika kama sadaka kwa Bwana, mnyama wa namna hiyo aliyetolewa kwa Bwana anakuwa mtakatifu.
Un ja tas ir lops, ko Tam Kungam var upurēt, tad viss lai ir svēts, ko no tā Tam Kungam dod.
10 Mtu haruhusiwi kumbadilisha au kutoa mnyama mzuri kwa mbaya, au mnyama mbaya kwa mzuri. Kama atatoa mnyama badala ya mwingine, wanyama wote wawili, yaani yule aliyetolewa na yule aliyebadiliwa, ni watakatifu.
To nebūs ne mīt, ne mainīt labu ar nelabu, vai nelabu ar labu, bet ja tomēr lopu pret lopu pārmīs, tad šis un arī tas, kas pārmīts, lai ir svēts Tam Kungam.
11 Kama alichokiwekea nadhiri ni mnyama aliye najisi kiibada, yaani yule asiye kubalika kuwa sadaka kwa Bwana, huyo mnyama lazima aletwe kwa kuhani,
Un ja tas ir kāds nešķīsts lops, ko Tam Kungam nedrīkst upurēt, tad to lopu būs vest pie priestera,
12 ambaye ataamua ubora wa mnyama huyo, kama ni mzuri au mbaya. Thamani yoyote atakayoweka kuhani, hivyo ndivyo itakavyokuwa.
Un priesterim to būs apspriest, cik labs vai nelabs tas ir, un kā priesteris ir spriedis, tā tam būs būt.
13 Kama mwenye mnyama atapenda kumkomboa mnyama huyo, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake.
Un ja kas to pērkot izpirks, tad piekto tiesu lai pieliek pie tā, kā tu esi apspriedis.
14 “‘Kama mtu ataweka nyumba yake wakfu kama kitu kitakatifu kwa Bwana, kuhani ataamua ubora wa nyumba hiyo, kama ni nzuri au mbaya. Thamani yoyote kuhani atakayoweka, basi hivyo ndivyo itakavyokuwa.
Un ja kas savu namu svētī, ka tas Tam Kungam lai ir svēts, tad priesterim to būs apspriest, cik labs vai nelabs tas ir: kā priesteris spriedis, tā tam būs būt.
15 Kama mtu aliyeweka nyumba yake wakfu ataikomboa, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, nayo nyumba itakuwa yake tena.
Un ja tas, kas savu namu ir svētījis, to grib izpirkt, tad viņam būs pielikt piekto naudas tiesu pie tā, ko tu esi spriedis; tad tas viņam piederēs.
16 “‘Kama mtu anaweka sehemu ya ardhi ya jamaa yake wakfu kwa Bwana, thamani yake itawekwa kulingana na kiasi cha mbegu inayohitajiwa kupandwa katika ardhi hiyo, yaani homeri moja ya mbegu za shayiri kwa shekeli hamsini za fedha.
Un ja kas no sava paša tīruma Tam Kungam ko laba svētīs, tad tavs spriedums lai ir pēc viņa sējuma; kur viens omers miežu top sēts, tā būs spriest uz piecdesmit sudraba sēķeļiem.
17 Kama akiweka shamba lake wakfu katika Mwaka wa Yubile, ile thamani iliyokwisha wekwa itakuwa iyo hiyo.
Ja viņš savu tīrumu svētīs no gaviles gada, tad viņa maksā būs pēc tava sprieduma.
18 Lakini kama akiweka shamba lake wakfu baada ya Yubile, kuhani ataweka thamani kulingana na idadi ya miaka iliyobaki kufikia Mwaka wa Yubile unaofuata, na thamani yake iliyoamuliwa itapunguzwa.
Bet ja viņš savu tīrumu svētīs pēc gaviles gada, tad priesterim to naudu būs apspriest pēc atliekamo gadu skaita līdz gaviles gadam, un jāatņem no tava sprieduma.
19 Kama mtu anayeweka wakfu shamba anataka kulikomboa, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, nalo shamba litakuwa lake tena.
Un ja viņš to tīrumu, ko viņš ir svētījis, pērkot izpirks, tad viņam būs pielikt piekto naudas tiesu pie tā, ko tu esi spriedis, - tad tas viņam piederēs.
20 Kama pengine halikomboi shamba hilo, au kama ameliuza kwa mtu mwingine, kamwe haliwezi kukombolewa.
Bet ja viņš to tīrumu neizpirks un ja to tīrumu citam pārdos, tad tam vairs nebūs tapt izpirktam.
21 Shamba hilo litakapoachiwa mwaka wa Yubile, litakuwa takatifu, kama shamba lililotolewa kwa Bwana, nalo litakuwa mali ya makuhani.
Bet tas tīrums, kad viņš nāk vaļā gaviles gadā, lai ir svēts Tam Kungam, tā kā pavisam nodots tīrums; tas priesterim būs par īpašumu.
22 “‘Kama mtu ameweka wakfu kwa Bwana shamba alilonunua, ambalo si sehemu ya ardhi ya jamaa yake,
Un ja viņš Tam Kungam tīrumu ir svētījis, ko viņš pircis, kas nav no viņa paša tīruma,
23 kuhani ataamua thamani yake hadi Mwaka wa Yubile, naye huyo mtu atalazimika kulipa thamani yake siku hiyo kama kitu kitakatifu kwa Bwana.
Tad priesterim būs spriest, kāda vērtība viņam līdz gaviles gadam, un viņam tai dienā būs dot, cik tu esi nospriedis, lai tas Tam Kungam ir svēts.
24 Katika Mwaka wa Yubile, shamba litarudishwa kwa mtu yule ambaye lilinunuliwa kutoka kwake, yule ambaye ardhi ilikuwa mali yake.
Gaviles gadā tam tīrumam atkal būs tam krist, no kā viņš bija pirkts, tam, kam tā zeme īpaši piederēja.
25 Kila thamani lazima iwekwe kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, gera ishirini kwa shekeli.
Visa tava spriešana lai notiek pēc svētās vietas sēķeļa, vienam sēķeļim ir divdesmit ģeri.
26 “‘Lakini hakuna mtu atakayeweka wakfu mzaliwa wa kwanza wa mnyama, kwa kuwa mzaliwa wa kwanza tayari ni mali ya Bwana; awe ngʼombe au kondoo, ni wa Bwana.
Bet pirmdzimto no lopiem, kas Tam Kungam pieder, nevienam nebūs svētīt, vai tas ir vērsis, vai avs; - tas pieder Tam Kungam.
27 Kama ni mmoja wa wanyama walio najisi, aweza kumnunua kwa bei iliyowekwa, akiongeza sehemu ya tano ya thamani yake. Kama hatamkomboa, mnyama huyo atauzwa kwa bei iliyowekwa.
Bet ja tas ir no nešķīsta lopa, tad viņam to pēc tava sprieduma būs izpirkt, un piekto tiesu pielikt klāt, un ja tas netop izpirkts, tad lai to pārdod pēc tava sprieduma.
28 “‘Lakini chochote kile mtu alicho nacho na akakiweka wakfu kwa Bwana, iwe ni binadamu, au mnyama, au ardhi ya jamaa, hakiwezi kuuzwa au kukombolewa. Chochote kilichowekwa wakfu ni kitakatifu sana kwa Bwana.
Bet visu, kas (pagalam) novēlēts, ko tas Tam Kungam (pagalam) novēlēs no visa, kas tam pieder, no cilvēkiem, vai no lopiem, vai no sava paša tīruma, no tā neko nebūs pārdot nedz izpirkt; viss, kas (pagalam) novēlēts, Tam Kungam ir augsti svēts.
29 “‘Mtu yeyote aliyewekwa wakfu ili kuangamizwa, hawezi kukombolewa. Mtu kama huyo lazima auawe.
Visam, kas Tam Kungam (pagalam) novēlēts no cilvēkiem, nebūs tapt izpirktam, bet nokautam.
30 “‘Zaka ya kila kitu kutoka shambani, iwe ni nafaka kutoka kwa ardhi, au tunda kutoka kwa miti, ni mali ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana.
Un visi zemes desmitie no zemes labības, no koku augļiem, pieder Tam Kungam, tie Tam Kungam ir svēti.
31 Kama mtu akikomboa chochote cha zaka yake, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake.
Bet ja kas no saviem desmitiem ko laba pircin izpirks, tam piekto tiesu būs pielikt klāt.
32 Zaka yote ya kundi la ngʼombe au la kondoo na mbuzi, kila mnyama wa kumi apitaye chini ya fimbo ya yule awachungaye, atakuwa mtakatifu kwa Bwana.
Un visi desmitie no lieliem un sīkiem lopiem, kas ar rīksti top noskaitīti, tie desmitie no visa būs Tam Kungam svēti.
33 Yule mnyama wa kumi hatachaguliwa kwa kigezo cha uzuri au ubaya, naye haruhusiwi kubadiliwa. Ikiwa atabadiliwa, basi mnyama yule wa kwanza na huyo aliyebadiliwa wote watahesabiwa kuwa watakatifu, na haiwezekani kuwakomboa.’”
Starp nelaba un laba nekādu izmeklēšanu nebūs turēt, nedz to pārmainīt; bet ja to pārmīs, tad šis un arī tas, kas ir izmīts, būs svēts; to nebūs izpirkt.
34 Haya ndiyo maagizo Bwana aliyompa Mose juu ya Mlima Sinai kwa ajili ya Waisraeli.
Tie ir tie baušļi, ko Tas Kungs Mozum pavēlējis priekš Israēla bērniem uz Sinaī kalna.