< Mambo ya Walawi 27 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Jahve reče Mojsiju:
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kama mtu yeyote ataweka nadhiri maalum ili kuweka watu wakfu kwa Bwana, kwa kutoa kiasi cha thamani inayolingana,
“Govori Izraelcima i reci im: 'Ako tko zaželi podmiriti Jahvi zavjet što vrijedi koliko čovjek,
3 thamani ya kukomboa mwanaume mwenye kati ya umri wa miaka ishirini na miaka sitini itakuwa shekeli hamsini za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu;
neka ti je mjerilo: muškarca od dvadeset do šezdeset godina starosti procijeni pedeset šekela u srebru, prema hramskom šekelu,
4 ikiwa ni mwanamke, weka thamani yake kwa shekeli thelathini.
a žensku procijeni trideset šekela.
5 Kama ni mtu mwenye umri wa miaka kati ya mitano na ishirini, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli ishirini, na mwanamke shekeli kumi.
A za dob od pet do dvadeset godina neka tvoja procjena bude: za muškarca dvadeset šekela, a za žensku deset šekela.
6 Kama ni mtu mwenye umri kati ya mwezi mmoja na miaka mitano, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli tano za fedha, na ile ya mwanamke kuwa shekeli tatu za fedha.
Je li dob od jednoga mjeseca do pet godina, neka ti je procjena: za muško pet šekela u srebru, a procjena za žensko tri šekela u srebru.
7 Kama ni mtu mwenye miaka sitini na zaidi, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli kumi na tano, na mwanamke shekeli kumi.
Bude li u starosti od šezdeset godina ili više, neka ti je procjena: za muškarca petnaest šekela, a za žensku deset šekela.
8 Kama mtu yeyote anayeweka nadhiri ni maskini mno kuweza kulipa kiasi kilichowekwa, atampeleka huyo mtu kwa kuhani, ambaye ataweka thamani yake kulingana na kile mweka nadhiri anachoweza kulipa.
Ali ako je tko siromašan te ne može platiti svoju cijenu, neka ga dovedu pred svećenika i neka ga svećenik procijeni. Ali neka svećenik procijeni prema onome što zavjetovalac može dati.
9 “‘Kama kile mtu alichokiwekea nadhiri ni mnyama anayekubalika kama sadaka kwa Bwana, mnyama wa namna hiyo aliyetolewa kwa Bwana anakuwa mtakatifu.
Ako zavjetovani prinos bude od životinja koje se mogu Jahvi prinositi, svaki takav prinos Jahvi bit će posvećena stvar.
10 Mtu haruhusiwi kumbadilisha au kutoa mnyama mzuri kwa mbaya, au mnyama mbaya kwa mzuri. Kama atatoa mnyama badala ya mwingine, wanyama wote wawili, yaani yule aliyetolewa na yule aliyebadiliwa, ni watakatifu.
Neka se ne nadomješta niti zamjenjuje za što drugo - bilo dobro za loše, bilo loše za dobro. Ako li se napravi zamjena jednoga živinčeta za drugo, onda će i zavjetovano i ono koje ga je zamijenilo biti posvećena stvar.
11 Kama alichokiwekea nadhiri ni mnyama aliye najisi kiibada, yaani yule asiye kubalika kuwa sadaka kwa Bwana, huyo mnyama lazima aletwe kwa kuhani,
Bude li zavjetovani prinos od nečiste životinje koja se ne može Jahvi prinositi, neka se takvo živinče dovede k svećeniku
12 ambaye ataamua ubora wa mnyama huyo, kama ni mzuri au mbaya. Thamani yoyote atakayoweka kuhani, hivyo ndivyo itakavyokuwa.
pa neka ga on procijeni. Bilo skupo, bilo jeftino, kako svećenik procijeni, neka tako bude.
13 Kama mwenye mnyama atapenda kumkomboa mnyama huyo, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake.
Zaželi li ga tko otkupiti, neka doda njegovoj procjeni jednu petinu.
14 “‘Kama mtu ataweka nyumba yake wakfu kama kitu kitakatifu kwa Bwana, kuhani ataamua ubora wa nyumba hiyo, kama ni nzuri au mbaya. Thamani yoyote kuhani atakayoweka, basi hivyo ndivyo itakavyokuwa.
Ako tko posveti svoju kuću zavjetovavši je Jahvi, neka svećenik procijeni da li je dobra ili loša. Kako svećenik prosudi, neka tako ostane.
15 Kama mtu aliyeweka nyumba yake wakfu ataikomboa, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, nayo nyumba itakuwa yake tena.
Ako onaj koji je svoju kuću zavjetovao zaželi da je otkupi, neka dometne jednu petinu svoti na koju je procijenjena pa neka bude njegova.
16 “‘Kama mtu anaweka sehemu ya ardhi ya jamaa yake wakfu kwa Bwana, thamani yake itawekwa kulingana na kiasi cha mbegu inayohitajiwa kupandwa katika ardhi hiyo, yaani homeri moja ya mbegu za shayiri kwa shekeli hamsini za fedha.
Ako tko zavjetuje Jahvi dio zemljišta od svoga vlasništva, procijeni ga prema njegovu usjevu: za jedan homer ječmena sjemena pedeset šekela u srebru.
17 Kama akiweka shamba lake wakfu katika Mwaka wa Yubile, ile thamani iliyokwisha wekwa itakuwa iyo hiyo.
Zavjetuje li zemljište za jubilejske godine, neka ostane prema ovoj procjeni.
18 Lakini kama akiweka shamba lake wakfu baada ya Yubile, kuhani ataweka thamani kulingana na idadi ya miaka iliyobaki kufikia Mwaka wa Yubile unaofuata, na thamani yake iliyoamuliwa itapunguzwa.
Ali ako zemljište zavjetuje poslije jubilejske godine, neka svećenik proračuna cijenu prema godinama što preostaju do jubilejske godine i prema tome smanji procjenu.
19 Kama mtu anayeweka wakfu shamba anataka kulikomboa, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, nalo shamba litakuwa lake tena.
Ako onaj tko je zemljište zavjetovao zaželi da ga otkupi, neka doda jednu petinu svoti na koju je procijenjeno pa neka mu ostane.
20 Kama pengine halikomboi shamba hilo, au kama ameliuza kwa mtu mwingine, kamwe haliwezi kukombolewa.
Ako zemljište ne otkupi nego ga proda drugome, ne može se više otkupiti.
21 Shamba hilo litakapoachiwa mwaka wa Yubile, litakuwa takatifu, kama shamba lililotolewa kwa Bwana, nalo litakuwa mali ya makuhani.
Kad zemljište bude oslobođeno u jubilejskoj godini, neka se posveti Jahvi kao zavjetovano zemljište i postane svećenikov posjed.
22 “‘Kama mtu ameweka wakfu kwa Bwana shamba alilonunua, ambalo si sehemu ya ardhi ya jamaa yake,
Zavjetuje li tko Jahvi kupljeno zemljište koje nije dio njegove očevine,
23 kuhani ataamua thamani yake hadi Mwaka wa Yubile, naye huyo mtu atalazimika kulipa thamani yake siku hiyo kama kitu kitakatifu kwa Bwana.
neka mu svećenik proračuna razmjernu procjenu do jubilejske godine. I toga istog dana neka isplati iznos kao stvar posvećenu Jahvi.
24 Katika Mwaka wa Yubile, shamba litarudishwa kwa mtu yule ambaye lilinunuliwa kutoka kwake, yule ambaye ardhi ilikuwa mali yake.
U jubilejskoj godini zemljište se ima vratiti onome od koga je kupljeno - kome pripada zemljišno vlasništvo.
25 Kila thamani lazima iwekwe kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, gera ishirini kwa shekeli.
Svaka procjena neka se vrši prema hramskom šekelu: dvadeset gera jedan šekel.
26 “‘Lakini hakuna mtu atakayeweka wakfu mzaliwa wa kwanza wa mnyama, kwa kuwa mzaliwa wa kwanza tayari ni mali ya Bwana; awe ngʼombe au kondoo, ni wa Bwana.
Ali neka nitko ne zavjetuje prvinu od stoke. TÓa prvina ionako pripada Jahvi - Jahvina je, pa bila od sitnoga bila od krupnoga blaga.
27 Kama ni mmoja wa wanyama walio najisi, aweza kumnunua kwa bei iliyowekwa, akiongeza sehemu ya tano ya thamani yake. Kama hatamkomboa, mnyama huyo atauzwa kwa bei iliyowekwa.
Bude li od nečiste stoke, može se otkupiti prema procjeni, dometnuvši petinu cijene. Ako se ne otkupi, neka se prema procjeni proda.
28 “‘Lakini chochote kile mtu alicho nacho na akakiweka wakfu kwa Bwana, iwe ni binadamu, au mnyama, au ardhi ya jamaa, hakiwezi kuuzwa au kukombolewa. Chochote kilichowekwa wakfu ni kitakatifu sana kwa Bwana.
Ali ništa od 'herema', od onog što je Jahvi izručeno, bio to čovjek ili živinče ili njegovo baštinjeno zemljište, ništa što je tko Jahvi zavjetom posvetio, ne može se niti prodati niti otkupiti. Svaka zavjetom posvećena stvar najveća je Jahvina svetinja.
29 “‘Mtu yeyote aliyewekwa wakfu ili kuangamizwa, hawezi kukombolewa. Mtu kama huyo lazima auawe.
Nijedno ljudsko biće koje bude 'heremom' - prokletstvom - udareno ne smije se otkupljivati: mora se smaknuti.
30 “‘Zaka ya kila kitu kutoka shambani, iwe ni nafaka kutoka kwa ardhi, au tunda kutoka kwa miti, ni mali ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana.
Svaka desetina sa zemljišta, bilo od poljskih usjeva bilo od plodova sa stabala, pripada Jahvi; to je Jahvi posvećeno.
31 Kama mtu akikomboa chochote cha zaka yake, lazima aongeze sehemu ya tano ya thamani yake.
Ako bi tko htio otkupiti koji dio svoje desetine, mora tome dodati jednu petinu cijene.
32 Zaka yote ya kundi la ngʼombe au la kondoo na mbuzi, kila mnyama wa kumi apitaye chini ya fimbo ya yule awachungaye, atakuwa mtakatifu kwa Bwana.
Svaka desetina od krupnoga i sitnoga blaga, to jest svako deseto od svega što prolazi ispod pastirskog štapa, neka bude posvećeno Jahvi.
33 Yule mnyama wa kumi hatachaguliwa kwa kigezo cha uzuri au ubaya, naye haruhusiwi kubadiliwa. Ikiwa atabadiliwa, basi mnyama yule wa kwanza na huyo aliyebadiliwa wote watahesabiwa kuwa watakatifu, na haiwezekani kuwakomboa.’”
Neka se ne gleda je li dobro ili rđavo; i neka se ne zamjenjuje. Ako se ipak zamijeni, neka je onda i jedno i drugo posvećeno i ne smije se otkupljivati.'”
34 Haya ndiyo maagizo Bwana aliyompa Mose juu ya Mlima Sinai kwa ajili ya Waisraeli.
To su zapovijedi koje je Jahve izdao Mojsiju za Izraelce na Sinajskome brdu.

< Mambo ya Walawi 27 >