< Mambo ya Walawi 26 >

1 “‘Msijitengenezee sanamu au kusimamisha kinyago cha kuchonga, au mnara, wala jiwe la kuabudia, na pia msijiwekee jiwe lililochongwa katika nchi yenu na kusujudu mbele yake. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
Hina Gode da amane sia: i, “Dilia nodone sia: ne gadomusa: , loboga hamoi liligi, igiga hamoi golasu ifa agoane liligi amola osole dedei igi, amo mae hamoma. Bai Na da dilia Hina Gode!
2 “‘Zishikeni Sabato zangu na kuheshimu mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana.
Nama nodomusa: lolo Nasu gilisisu huluane noga: le dawa: ma amola Nama nodone sia: ne gadosu sogebi amo nodoma. Na da Hina Gode!
3 “‘Ikiwa mtafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii maagizo yangu,
Dilia da Na hamoma: ne sia: i amola Na sema amoma noga: le fa: no bobogesea,
4 nitawanyeshea mvua katika majira yake, nayo ardhi itatoa mazao yake, na miti ya mashambani itazaa matunda yake.
Na da dilima eso defele gibu imunu. Amasea, dilia sogega dilia da ha: i manu heda: lebe ba: mu, amola dilia ifa amoga fage legei dagoi ba: mu.
5 Kupura nafaka kwenu kutaendelea mpaka wakati wa kuvuna zabibu. Pia kuvuna zabibu kutaendelea mpaka wakati wa kupanda mbegu, nanyi mtakula na kushiba, na mtaishi salama katika nchi yenu.
Dilia ha: i manu faimu da bagadedafa ba: mu. Dilia da gagoma failalu, mae dagole waini fage faimu ba: mu. Amola dilia da waini fage failalu, bu gagoma hawa: bugima: ne eso da doaga: i dagoi ba: mu. Dilia da sadima: ne, ha: i manu bagade ba: mu amola dilia soge ganodini gaga: iwane esalumu.
6 “‘Nitawapa amani katika nchi, mpate kulala pasipo kutiwa hofu na yeyote. Nitawaondoa wanyama wakali watoke kwenye nchi, nao upanga hautapita katika nchi yenu.
Na da dilia soge ganodini dilima olofosu imunu. Amola dilia da enoba: le mae beda: iwane hahawane golamu. Na da gasonasu sigua ohe dilia soge ganodini mae misa: ne sefasimu, amola dilia da gegesu bu hame ba: mu.
7 Mtawafukuza adui zenu, nanyi mtawaua kwa upanga mbele yenu.
Dilia da dilia ha lai hasalimu.
8 Watu wenu watano watafukuza adui mia, watu wenu mia watafukuza adui elfu kumi, nao adui zenu wataanguka kwa upanga mbele yenu.
Dilia dunu biyale gala da ha lai dunu100 amo hasalimu. Amola dilia dunu100 da ha lai dunu10,000 hasalimu.
9 “‘Nitawaangalia kwa upendeleo na kuwafanya mzae na kuzidisha idadi yenu, nami nitalishika Agano langu na ninyi.
Na da dilima hahawane hamomu amola mano bagohame dilima imunu. Na da Na gousa: su dilima hamoi amo noga: le ouligimu.
10 Wakati wa kuvuna mtakuwa bado mnakula mavuno ya mwaka uliopita, na itawalazimu kuyaondoa ghalani ili mpate nafasi ya mavuno mapya.
Dilia da ha: i manu bagadedafa faimuba: le, dilia ha: i manu ode afaega defele ba: mu. Amasea, musa: fai ha: i manu da dialebeba: le, dilia da gaheabolo ha: i manu faisia, diasu ganodini legemusa: , musa: ha: i manu fai bagade dialebeba: le da ha: digimu agoai ba: mu.
11 Nitafanya makao yangu miongoni mwenu, nami sitawachukia.
Na da Na sema Abula Diasu ganodini, dilia fi dogoa esalumu. Amola Na da dili hame yolesimu.
12 Nitatembea katikati yenu niwe Mungu wenu, nanyi mtakuwa watu wangu.
Na amola da dili gilisili esalumu. Na da dilia Gode esalumu amola dilia da Na fidafa dunu esalumu.
13 Mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa katika nchi ya Misri ili msiendelee kuwa watumwa wa Wamisri, nikavunja kongwa lenu, na kuwawezesha kutembea mkiwa mmeinua vichwa vyenu juu.
Na, dilia Hina Gode, da dilia udigili hawa: hamosu dunu bu mae esaloma: ne, dili Idibidi sogega fisili masa: ne asunasi. Gasa bagade dunu da dili banenesi galu. Be dilia hahawane, dialuma mae fili sa: ili, gadili laloma: ne, Na da amo ilia gasa gugunufinisi dagoi.”
14 “‘Lakini kama hamtanisikiliza na kutimiza maagizo haya yote,
Hina Gode da amane sia: i, “Dilia da Na hamoma: ne sia: i hame nabasea, dilia da Na se iasu ba: mu.
15 nanyi kama mtazikataa amri zangu na kuzichukia sheria zangu, tena mkishindwa kutimiza amri zangu na hivyo mkavunja agano langu,
Dilia da higa: iba: le, Na hamoma: ne sia: i amola Na sema amoma hame fa: no bobogesea, amola gousa: su Na dilima hamoi amo wadela: sea,
16 ndipo nitakapowafanyia hili: Nitawaletea juu yenu hofu ya ghafula, magonjwa ya kufisha, na homa itakayopofusha macho yenu na kuwaondolea uhai wenu. Mtapanda mbegu bila mafanikio, kwa sababu adui zenu wataila.
Na da dilima se imunu. Na da gugunufinisisu liligi dilima iasimu. olo bagade amola asugi amo da dilia si wadela: mu amola dili da bogosu dilima madelai ba: mu. Dilia da ha: i manu hawa: bugimu be udigili bugimu. Bai dilia ha lai dunu da dilima hasalasili, dilia ha: i manu bugi huluane manu.
17 Nitauelekeza uso wangu dhidi yenu ili mshindwe na adui zenu; wale wanaowachukia watawatawala, nanyi mtakimbia ingawa hakuna mtu anayewafukuza.
Na da sinidigili dilima ha lai hamomu. Amaiba: le, dilia da enoga hasalasi dagoi ba: mu amola dilima higa: i dunu da dili ouligimu. Dilia da bagade beda: iba: le, dunu eno da dili hame sefasibi amomane dilia da udigili hobea: le masunu.
18 “‘Kama baada ya haya yote hamtanisikiliza, nitawaadhibu mara saba zaidi kwa ajili ya dhambi zenu.
Be amo se iasu ba: sea, dilia da Nama hame sinidigili nabasu hou hame hamosea, Na da fesuale agoane baligili dilima se imunu.
19 Nitakivunja kiburi chenu cha ukaidi na kuifanya anga iliyo juu yenu iwe kama chuma, na ardhi yenu kama shaba.
Na da dilia gasa fi hidasu hou amo gugunufinisisimu. Gibu da hame sa: imu amola dilia osobo da ga: nasi gula agoane hamomu.
20 Nguvu zenu zitatumika bila ya mafanikio, kwa sababu ardhi yenu haitawazalia mazao yake, wala miti ya nchi yenu haitazaa matunda yake.
Dilia gasa bagade hawa: hamosu da dilia hou hame fidimu. Bai dilia soge da ha: i manu hame legemu amola dilia ifa da fage hame legemu.
21 “‘Kama mtaendelea kuwa na uadui nami, na kukataa kunisikiliza, nitawazidishia mateso yenu mara saba zaidi, kama dhambi zenu zinavyostahili.
Amola dilia bu hame nabasu hou hamonanebe ba: sea, Na da bu dilia se iasu fesuale eno agoane imunu.
22 Nitawatuma wanyama mwitu dhidi yenu, nao watawaibieni watoto wenu, watawaangamiza ngʼombe wenu, na kuifanya idadi yenu kuwa ndogo, hivi kwamba barabara zenu zitakuwa hazina watu.
Na da medosu sigua ohe dilima asunasimu. Ilia da dilia mano medole legemu amola dilia lai gebo gugunufinisimu. Amola dilia bogogia: mubale, dunu bagahame fawane esalebe ba: mu. Logo huluane da dunu hame ahoanebeba: le, yaloi ba: mu.
23 “‘Ikiwa pamoja na mambo haya hamtakubali maonyo yangu lakini mkaendelea kuweka uadui nami,
Be dilia amo se iasu lai dagosea, bu Na hamoma: ne sia: i bu hame nabasea,
24 mimi mwenyewe nitaweka uadui nanyi, na kuwatesa kwa ajili ya dhambi zenu mara saba zaidi.
Na da sinidigili, se iasu fesuale eno agoane baligili dilima imunu.
25 Nitawaletea upanga juu yenu ili kuwapatiliza kwa kuvunja Agano langu. Mtakapokimbilia mijini mwenu, nitatuma tauni katikati yenu, nanyi mtatiwa mikononi mwa adui zenu.
Dilia da Na gousa: su wadela: lesiba: le, Na da dilima gegesu iasimu. Amola dilia moilai amo ganodini gagili salimusa: agoane gilisisia, Na da olo amo uhinisimu hamedei dilima imunu. Amasea, bu gegemu gogoleba: le, dilia da dilia ha lai ilima dili gagulaligima: ne amola fama: ne olemu.
26 Nitakapowaondolea upatikanaji wa mkate wenu, wanawake kumi wataoka mkate wenu katika tanuru moja, nao wataugawa mkate kidogo kwa kupima. Mtakula, lakini hamtashiba.
Na da dilia ha: i manu logo hedofamu. Amasea, uda nabuane gala da ilia agi ga: gi hamoma: ne, gobele nasu afae fawane defele ba: mu. Ilia fonobahadi fifili dilima imunu. Amola dilia huluane na dagosea, bu ha: i bagade ba: mu.
27 “‘Kama hata baada ya haya bado hamtanisikiliza lakini mkaendelea kuweka uadui nami,
Amalalu, dilia Nama halale Na hamoma: ne sia: i hame nabasea,
28 ndipo katika hasira yangu nitaweka uadui nanyi, nami mwenyewe nitawaadhibu mara saba kwa ajili ya dhambi zenu.
Na da ougili dilima gegene, se iasu fesuale eno baligili dilima imunu.
29 Mtakula nyama ya wana wenu na nyama ya binti zenu.
Dilia ha: i bagade nababeba: le, dilia manodafa amo hei manusa: dawa: mu.
30 Nitapaharibu mahali penu pa juu pa kuabudia miungu, nibomoe madhabahu zenu za kufukizia uvumba, na kuzilundika maiti zenu juu ya sanamu zenu zisizo na uhai, nami nitawachukia ninyi sana.
Dilia nodone sia: ne gadosu sogebi agologa diala amo Na da gugunufinisimu. Na da dilia gabusiga: manoma oloda amo mugulumu amola dilia bogoi da: i hodo amo dilia loboga hamoi ogogosu ‘gode’ dafai amo da: iya ha: digimu.
31 Nitaifanya miji yenu kuwa magofu, na kuharibu mahali patakatifu penu pa kuabudia, nami sitapendezwa na harufu nzuri ya sadaka zenu.
Na da dilima bagade higale, dilia moilai gugunufinisimu. Na da dilia nodone sia: ne gadosu sogebi gugunufinisimu amola dilia gobele salasu liligi hame lamu.
32 Nitaiharibu nchi, ili adui zenu watakaokuja kuishi humo washangae.
Na da dilia soge dafawanedafa gugunufinisimu. Amaiba: le, dilia ha lai da dilia soge gesowai, amo ba: sea, bagadewane fofogadigimu.
33 Nitawatawanya ninyi miongoni mwa mataifa, na kuufuta upanga wangu na kuwafuatia. Nchi yenu itaharibiwa, nayo miji yenu itakuwa magofu.
Na da gegesu dilima iasimu amola ga fifi asi gala ilia sogega dili afagogomu. Dilia soge da dunu hame esalebe ba: mu amola dilia moilai huluane mugululi gugunufinisi dagoi ba: mu.
34 Ndipo nchi itafurahia Sabato zake muda wote ule itakapokuwa ukiwa, nanyi mkiwa katika nchi ya adui zenu. Ndipo nchi itapumzika na kufurahia Sabato zake.
35 Wakati wote nchi itakapobaki ukiwa, itapumzika na kufurahia Sabato zake ambazo haikuzipata mlipokuwa mnaishi humo.
Amasea, Isala: ili soge da ode bagohame helefisu ba: mu (amo helefisu dilia da dilia sogega hame iasu). Soge da ouligisu dunu hamedene udigili dialumu. Dilia da mugululi asili, dilia ha lai dunu ilia soge ganodini esalea, soge da damunisi dialumu.
36 “‘Kwa habari ya wenzenu wale watakaobaki, nitaifanya mioyo yao kuwa na hofu kuu katika nchi za adui zao, kiasi kwamba sauti ya jani linalopeperushwa na upepo itawafanya wakimbie. Watakimbia kana kwamba wanakimbia upanga, nao wataanguka, ingawa hakuna anayewafukuza.
Na da hamobeba: le, dilia mugululi asi dunu da bagadewane beda: mu. Amasea, dilia da ifa lubi foga ahoa fane gulibagebe nabasea, hobea: mu. Dilia ha lai da gegesu ganodini dili sefasibi amo defele hobea: mu, amola ha lai da dilima gadenei ba: sea, dilia da udigili dafamu.
37 Watajikwaa mmoja juu ya mwingine kama wakimbiao upanga, hata ingawa hakuna anayewafuatia. Hivyo hamtaweza kusimama mbele ya adui zenu.
Ha lai da dili hame sefasisia, dilia da eno enoma legagala: le dafamu. Amola dilia ha lai ilima dabe gegemu hamedei ba: mu.
38 Mtaangamia katikati ya mataifa; nchi ya adui zenu itawala.
Dilia da mugululi asili, dilia ha lai ilia soge ganodini bogomu. Fedege agoane, dilia ha lai ilia sogega na dagoi ba: mu.
39 Wale wenu watakaobaki wataangamia katika nchi za adui zao kwa sababu ya dhambi zao; pia kwa sababu ya dhambi za baba zao wataangamia.
Dilia dunu afae afae dilia ha lai ilia soge ganodini hame bogoi esalebe, da da: i dione geloga: gia: mu. Bai dilia amola dilia aowalali da wadela: i hou hamosu.
40 “‘Lakini kama watatubu dhambi zao na dhambi za baba zao, udanganyifu wao dhidi yangu na uadui wao kwangu,
41 ambao ulinifanya niwe na uadui nao hata nikawapeleka katika nchi ya adui zao, wakati mioyo yao isiyotahiriwa itanyenyekea na kutubu dhambi yao,
Be diligaga fi ilia amola ilia aowalali (amo da Nama ha lai amola lelebeba: le, Na da ilima ha lale, ilia ha lai dunu sogega esaloma: ne, mugululi masa: ne sia: i) ilia wadela: i hou fofada: mu. Hobea, diligaga fi da ilia hou fonobosea, amola ilia wadela: i hou amola odoga: su hou amo ea dabe huluane ilia da hamoi dagosea, ilia da fofada: mu.
42 nami nitakumbuka agano langu na Yakobo, na agano langu na Isaki, na agano langu na Abrahamu, nami nitaikumbuka nchi.
Amasea, Na da Na gousa: su Na da Ya: igobe, Aisage amola A: ibalaha: me ilima hamoi, amo Na da bu dawa: mu. Na da Na fidafa ilima Isala: ili soge imunu ilegei, Na da bu gaheabolo ilegemu.
43 Kwa kuwa wataiacha nchi ukiwa, nayo itafurahia Sabato zake wakati itakuwa ukiwa bila wao. Wataadhibiwa kwa ajili ya dhambi zao, kwa sababu walizikataa sheria zangu na kuzichukia amri zangu.
Be hidadea, amo soge da hahawane damunisili, dunu hamedafa amo ganodini esalebe ba: mu. Amola Na fi dunu da Na hamoma: ne sia: i amola Na sema higale yolesiba: le, ilia amo dabe huluanedafa hamomu.
44 Lakini pamoja na hili, wakati watakuwa katika nchi ya adui zao, sitawakataa wala kuwachukia kiasi cha kuwaharibu kabisa na kuvunja agano langu nao. Mimi ndimi Bwana Mungu wao.
Be amo eso amolawane, ilia da ilia ha lai soge ganodini esalea, Na da Na fi dafawanedafa hame yolesimu amola dafawanedafa hame gugunufinisimu. Amai hamoi ganiaba, Na gousa: su da ilima dagolesila: loba. Be Na da ilia Hina Godedafa.
45 Lakini kwa ajili yao nitalikumbuka agano langu na baba zao, ambao niliwatoa Misri mbele ya mataifa ili niwe Mungu wao. Mimi ndimi Bwana.’”
Na da musa: Na fi amo Idibidi sogega fisili masa: ne asunasiba: le, Na da fifi asi gala huluane ilima Na gasa olelei. Amoha, Na da ilia aowalali ilima gousa: su hamoi. Amo gousa: su Na da bu gaheabolo ilegemu. Bai Na, Hina Gode, da ilia Godedafa esaloma: ne.”
46 Hizi ndizo amri, sheria na pia masharti ambazo Bwana alifanya kati yake mwenyewe na Waisraeli katika Mlima Sinai kupitia kwa Mose.
Amo dedei da sema amola Gode Ea hamoma: ne sia: i, amo Hina Gode da Sainai Goumia, Mousesema olelei, amo e da bu Isala: ili dunuma alofele ima: ne.

< Mambo ya Walawi 26 >