< Mambo ya Walawi 25 >

1 Bwana akamwambia Mose katika Mlima Sinai,
Et l'Éternel parla à Moïse sur le mont de Sinaï en ces termes:
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapa ninyi, nchi yenyewe ni lazima ishike Sabato kwa ajili ya Bwana.
Parle aux enfants d'Israël et leur dis: Quand vous serez entrés au pays que je vous donne, la terre chômera un sabbat en l'honneur de l'Éternel.
3 Kwa miaka sita mtapanda mazao katika mashamba yenu, nanyi kwa miaka sita mtaikata mizabibu yenu matawi na kuvuna mazao yake.
Six années tu ensemenceras ton champ, tu tailleras ta vigne et tu en feras rentrer les produits;
4 Lakini mwaka wa saba nchi lazima iwe na Sabato ya mapumziko, Sabato kwa Bwana. Msipande mbegu katika mashamba yenu, wala msikate mizabibu yenu matawi.
mais la septième année il y aura un sabbat solennel pour le pays, un sabbat en l'honneur de l'Éternel; tu n'ensemenceras point ton champ et ne tailleras, point ta vigne.
5 Msivune na kuweka akiba kinachoota chenyewe, wala kuvuna na kusindika zabibu ambayo hamkuhudumia mashamba yake. Nchi lazima iwe na mwaka wa mapumziko.
Tu ne moissonneras pas le recrû de tes blés et ne vendangeras point les raisins de ta vigne non taillée: ce sera une année de repos pour la terre.
6 Chochote nchi itoacho katika mwaka wa Sabato kitakuwa chakula chenu wenyewe, watumishi wenu wa kiume na wa kike, mfanyakazi aliyeajiriwa, na mkazi wa muda anayeishi miongoni mwenu,
Et vous aurez l'usage du produit de la terre qui se repose, pour t'en nourrir toi et ton serviteur et ta servante et ton mercenaire et ton étranger qui séjournent chez toi;
7 vilevile malisho ya mifugo yenu na wanyama pori katika nchi yenu. Chochote nchi itakachozalisha kinaweza kuliwa.
tout son produit servira à la nourriture de ton bétail et des animaux qui peuplent ton pays.
8 “‘Hesabu Sabato saba za miaka, yaani miaka saba mara saba, ili Sabato saba za miaka utakuwa muda wa miaka arobaini na tisa.
Puis tu compteras sept années sabbatiques, sept fois sept années: ce qui pour sept années sabbatiques te donnera une période de quarante-neuf années.
9 Ndipo tarumbeta itapigwa kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho, piga tarumbeta katika nchi yako yote.
Et tu sonneras de la trompette le septième mois, le dixième jour du mois; le jour des propitiations vous sonnerez de la trompette dans tout votre pays.
10 Mwaka wa hamsini mtauweka wakfu na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakazi wake wote. Itakuwa ni yubile kwenu; kila mmoja wenu atairudia mali ya jamaa yake, na kila mmoja kurudi kwenye ukoo wake.
Et vous consacrerez ainsi la cinquantième année et vous publierez l'affranchissement dans le pays pour tous ses habitants: ce sera pour vous un Jubilé, chacun de vous rentrant dans sa propriété, et chacun de vous rentrant dans sa famille.
11 Mwaka wa hamsini utakuwa yubile kwenu, msipande wala msivune kile kiotacho chenyewe, au kuvuna zabibu zisizohudumiwa.
Cette cinquantième année sera pour vous un Jubilé, vous ne sèmerez point et vous ne moissonnerez point son recrû, et ne vendangerez point la vigne alors non taillée.
12 Kwa kuwa ni yubile, nayo itakuwa takatifu kwenu; mtakula tu kile kilichotoka moja kwa moja mashambani.
Car c'est un Jubilé; il vous sera sacré, et vous tirerez de vos champs pour votre usage ce qu'ils rendront.
13 “‘Katika huu Mwaka wa Yubile, kila mmoja atarudi kwenye mali yake mwenyewe.
Dans cette année du Jubilé, chacun de vous rentrera dans sa propriété.
14 “‘Ikiwa utauza ardhi kwa mmoja wa wazawa wa nchi yako, au ukinunua ardhi kutoka kwake, mmoja asimpunje mwingine.
Et si vous vendez quelque chose à votre prochain ou achetez quelque chose de votre prochain, ne vous molestez pas l'un l'autre.
15 Utanunua ardhi kwa mzawa wa nchi yako kwa misingi ya hesabu ya miaka baada ya Yubile. Naye ataiuza kwako kwa misingi ya hesabu ya miaka iliyobaki kwa kuvuna mavuno.
Tu compteras les années à partir du Jubilé pour acheter de ton prochain, et il te vendra d'après le nombre des années de récoltes.
16 Miaka inapokuwa mingi, utaongeza bei, nayo miaka ikiwa michache, utapunguza bei, kwa sababu kile anachokuuzia kwa hakika ni hesabu ya mazao.
Plus il y aura d'années, plus ton prix d'achat sera élevé, et moins il y aura d'années, moindre aussi sera ton prix d'achat; car c'est le nombre des récoltes qu'il te vend.
17 Mmoja asimpunje mwingine, bali utamcha Mungu wako. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.
Qu'aucun de vous ne moleste son prochain, et aie la crainte de ton Dieu; car je suis l'Éternel, votre Dieu.
18 “‘Fuateni amri zangu, mwe waangalifu kutii amri zangu, nanyi mtaishi salama katika nchi.
Exécutez ainsi mes statuts et observez mes lois et les exécutez et vous habiterez votre pays en sécurité.
19 Kisha nchi itazaa matunda yake, nanyi mtakula na kushiba na kuishi humo kwa salama.
Et le pays donnera ses fruits, et vous mangerez à rassasiement, et vous l'habiterez en sécurité.
20 Mwaweza kuuliza, “Tutakula nini katika mwaka wa saba ikiwa hatutapanda wala kuvuna mazao yetu?”
Que si vous dites: Que mangerons-nous la septième année, si nous ne semons pas, et si nous ne récoltons pas nos produits?
21 Nitawapelekeeni baraka ya pekee katika mwaka wa sita, kwamba nchi itazalisha mazao ya kutosha kwa miaka mitatu.
voici, je vous dispenserai ma bénédiction dans la sixième année qui rendra des produits pour trois ans.
22 Mnapopanda mwaka wa nane, mtakula mavuno ya miaka iliyopita. Pia mtaendelea kuyala mazao hayo hadi mvune mavuno ya mwaka wa tisa.
Vous sèmerez donc la huitième année vous nourrissant des vieilles récoltes; jusqu'à la neuvième année, en attendant que vous en ayez les récoltes, vous mangerez les vieilles.
23 “‘Kamwe ardhi isiuzwe kwa mkataba wa kudumu, kwa sababu nchi ni mali yangu, nanyi ni wageni na wapangaji wangu.
Le pays ne sera point vendu de manière à être aliéné; car le pays m'appartient, car vous êtes des étrangers et des locataires chez moi.
24 Katika nchi yote mtakayoshika kuwa milki yenu, ni lazima mtoe ukombozi wa ardhi.
Et dans tout le pays dont vous aurez la possession, vous accorderez le droit de retrait pour les terres.
25 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini na akauza baadhi ya mali yake, ndugu yake wa karibu atakuja na kukomboa kile ndugu yako alichokiuza.
Si ton frère réduit à la pauvreté vend quelqu'une de ses possessions, et que se présente son plus proche parent qui a droit de retrait, que celui-ci puisse retraire ce qu'a vendu son frère.
26 Iwapo mtu huyo hana jamaa wa karibu wa kukomboa mali hiyo kwa ajili yake, lakini yeye mwenyewe akafanikiwa na kupata mali itoshayo kuikomboa,
Et si quelqu'un n'a personne pour faire le retrait, mais parvient à avoir et à trouver de quoi faire le retrait,
27 ataamua tena thamani yake kwa miaka tangu alipoiuza, na kurudisha kiasi kilichobaki cha thamani kwa mtu ambaye alikuwa amemuuzia mali hiyo, naye ataweza kuirudia mali yake.
il supputera les années à partir de sa vente et remboursera l'excédant à celui auquel il aura vendu, et il rentrera par là dans sa propriété.
28 Lakini kama hatapata njia ya kumlipa mnunuzi, ile mali aliyouza itabaki kumilikiwa na mnunuzi mpaka Mwaka wa Yubile. Mali hiyo itarudishwa mwaka wa Yubile, naye ataweza kuirudia mali yake.
Et s'il ne trouve pas de quoi le rembourser, ce qu'il aura vendu restera entre les mains de l'acheteur jusqu'à l'année du Jubilé, époque à laquelle celui-ci se dessaisira et l'autre rentrera dans sa propriété.
29 “‘Ikiwa mtu atauza nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta, yeye anayo haki ya kuikomboa mwaka mzima baada ya mauzo ya hiyo nyumba. Wakati huo anaweza kuikomboa.
Et si quelqu'un vend une maison d'habitation dans une ville murée, le retrait pourra s'en faire jusqu'à la fin de l'année où la vente aura eu lieu; ce sera l'espace de temps accordé pour le retrait.
30 Ikiwa haikukombolewa kabla ya mwaka mmoja kamili kupita, nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya mnunuzi na wazao wake. Haitarudishwa mwaka wa Yubile.
Mais si le retrait n'en est pas opéré avant la fin de l'année complète, la propriété de la maison sise dans une ville murée sera définitivement dévolue à l'acheteur et à ses descendants, et il ne s'en dessaisira pas au Jubilé.
31 Lakini nyumba zilizo vijijini bila ya kuwa na kuta zilizozizunguka zitahesabiwa kama mashamba. Zinaweza kukombolewa, nazo zirudishwe katika mwaka wa Yubile.
Mais les maisons des villages qui ne sont pas entourés d'un mur, seront considérées comme des champs; l'on pourra en faire le retrait, et au Jubilé elles seront libérées.
32 “‘Walawi siku zote wana haki ya kukomboa nyumba zao katika miji ya Walawi wanayoimiliki.
Quant aux villes des Lévites, aux maisons des villes qu'ils posséderont, il y aura pour les Lévites droit perpétuel de retrait.
33 Kwa hiyo mali ya Mlawi inaweza kukombolewa, yaani nyumba iliyouzwa katika mji wowote wanaoushikilia itarudishwa mwaka wa Yubile, kwa sababu nyumba zilizo katika miji ya Walawi ni mali yao miongoni mwa Waisraeli.
Et si un Lévite ne fait pas retrait l'année du Jubilé, ce qu'il aura vendu de la maison et de la ville qu'il possède lui reviendra, car les maisons des villes des Lévites sont leur propriété au milieu des enfants d'Israël.
34 Lakini nchi ya malisho iliyo mali ya miji yao kamwe isiuzwe, ni milki yao ya kudumu.
Et le terrain qui forme la banlieue de leurs villes ne doit point être vendu; ils en ont la possession perpétuelle.
35 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini, naye akashindwa kujitegemeza mwenyewe katikati yako, msaidie kama vile ambavyo ungelimsaidia mgeni au kama mkazi wa muda, ili aweze kuendelea kuishi katikati yako.
Et si ton frère devient pauvre et incapable de travail à côté de toi, soutiens-le, même étranger et d'une autre nation, afin qu'il puisse vivre à côté de toi.
36 Usichukue riba wala faida yoyote kutoka kwake, bali utamwogopa Mungu wako, ili mzawa wa nchi yako aweze kuendelea kuishi katikati yako.
Ne tire de lui ni intérêt, ni usure, et aie la crainte de ton Dieu, afin que ton frère puisse vivre à côté de toi.
37 Usimkopeshe fedha ili alipe na riba, wala usimuuzie chakula kwa faida.
Tu ne lui prêteras point ton argent à intérêt, ni tes denrées à usure.
38 Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekuleta kutoka nchi ya Misri nikupe nchi ya Kanaani, nami niwe Mungu wako.
Je suis l'Éternel, votre Dieu, qui vous ai tirés du pays d'Egypte pour vous donner le pays de Canaan, pour être votre Dieu.
39 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini katikati yako, naye akajiuza kwako, usimfanye atumike kama mtumwa.
Et si ton frère s'appauvrit à côté de toi, et se vend à toi, tu ne lui feras pas faire de service servile;
40 Atatendewa kama mfanyakazi aliyeajiriwa, au kama mkazi wa muda katikati yako, naye atatumika mpaka Mwaka wa Yubile.
il sera chez toi comme mercenaire et comme étranger; il sera à ton service jusqu'à l'année du Jubilé;
41 Ndipo yeye na watoto wake wataachiwa, naye atarudi kwa watu wa ukoo wake, na kwenye mali ya baba zake.
alors il sortira de chez toi, lui et ses fils avec lui, pour rentrer dans sa famille, pour rentrer dans la propriété de ses pères.
42 Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu niliowaleta kutoka nchi ya Misri, kamwe wasiuzwe kama watumwa.
Car ce sont mes serviteurs que j'ai tirés du pays d'Egypte; ils ne doivent point être vendus, comme on vend des esclaves.
43 Usiwatawale kwa ukatili, lakini utamcha Mungu wako.
Ne le gouverne pas avec dureté, mais aie la crainte de ton Dieu.
44 “‘Watumwa wako wa kiume na wa kike watatoka katika mataifa yanayokuzunguka; kutoka kwao waweza kununua watumwa.
Le serviteur et la servante qu'il t'est permis d'avoir, tu les prendras chez les nations qui t'environnent; c'est chez elles que vous pourrez acheter serviteur et servante.
45 Pia waweza kununua baadhi ya wakazi wa muda wanaoishi katikati yako, na jamaa ya koo zao waliozaliwa katika nchi yako, nao watakuwa mali yako.
De même des enfants des étrangers domiciliés chez vous, vous pouvez en acheter ainsi que de leurs familles établies chez vous, qu'ils auront engendrées dans votre pays, et les avoir en propriété,
46 Hao waweza kuwarithisha watoto wako kuwa urithi wao, na wanaweza kuwafanya watumwa maisha yao yote, lakini usiwatawale ndugu zako Waisraeli kwa ukatili.
et les transmettre par héritage à vos fils après vous comme une propriété, et les garder à perpétuité à votre service comme esclaves. Mais ne faites pas entre frères peser une dure autorité sur vos frères, les enfants d'Israël.
47 “‘Ikiwa mgeni au mkazi wa muda katikati yako atakuwa tajiri, na mmoja wa wazawa wa nchi yako akawa maskini, naye akajiuza kwa yule mgeni anayeishi katikati yako, au kwa mmoja wa jamaa wa koo za wageni,
Si à côté de toi un étranger ou un homme d'une autre nation parvient à avoir de l'aisance, et que à côté de lui ton frère s'appauvrisse et se vende à un étranger domicilié chez toi, ou au rejeton de la famille d'un étranger,
48 anayo haki ya kukombolewa baada ya kujiuza. Mmoja wa jamaa zake aweza kumkomboa:
on pourra, après qu'il aura été vendu, faire son rachat; c'est à l'un de ses frères à faire son rachat.
49 Mjomba wake, au binamu yake, au yeyote aliye ndugu wa damu katika ukoo wake aweza kumkomboa. Au ikiwa atafanikiwa, anaweza kujikomboa mwenyewe.
Le rachat sera fait soit par son oncle, soit par le fils de son oncle, ou un de ses plus proches consanguins de sa famille; ou bien s'il trouve des ressources, il se rachètera lui-même.
50 Yeye na huyo aliyemnunua watahesabu muda kuanzia mwaka aliojiuza hadi Mwaka wa Yubile. Mahali pa kuanzia bei ya kuachiwa kwake itakadiriwa kwa ujira unaolipwa mfanyakazi aliyeajiriwa kwa idadi ya hiyo miaka.
Et alors il comptera avec son acheteur à partir de l'année où il a été vendu jusqu'à l'année du Jubilé; et son prix de vente se réglera d'après le nombre des années, qui lui seront mises au taux des années d'un mercenaire.
51 Ikiwa imebaki miaka mingi, ni lazima atalipia ukombozi wake fungu kubwa la bei iliyolipwa kumnunua yeye.
S'il y a encore un grand nombre d'années, il paiera son rachat en raison de ces années avec l'argent qu'il possède;
52 Ikiwa miaka iliyobaki ni michache kufikia Mwaka wa Yubile, atafanya hesabu yake, naye atalipa malipo yanayostahili kwa ajili ya ukombozi wake.
et s'il ne reste que peu d'années jusqu'au Jubilé, on les lui comptera: il paiera son rachat à proportion de ses années.
53 Atatendewa kama mtu wa kuajiriwa mwaka hadi mwaka; lazima uone kwamba yule aliyemnunua hamtawali kwa ukatili.
Il sera chez lui comme un mercenaire à l'année. On ne le gouvernera pas avec dureté sous tes yeux.
54 “‘Hata ikiwa hakukombolewa kwa njia mojawapo ya hizi, yeye na watoto wake wataachiwa katika Mwaka wa Yubile,
Et s'il n'est pas racheté de la sorte, il sortira l'année du Jubilé, lui et ses fils avec lui.
55 kwa maana Waisraeli ni mali yangu kama watumishi. Wao ni watumishi wangu, niliowatoa kutoka nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.
Car les enfants d'Israël me sont des esclaves. Ils sont mes esclaves que j'ai tirés du pays d'Egypte. Je suis l'Éternel, votre Dieu.

< Mambo ya Walawi 25 >