< Mambo ya Walawi 25 >

1 Bwana akamwambia Mose katika Mlima Sinai,
and to speak: speak LORD to(wards) Moses in/on/with mountain: mount Sinai to/for to say
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapa ninyi, nchi yenyewe ni lazima ishike Sabato kwa ajili ya Bwana.
to speak: speak to(wards) son: descendant/people Israel and to say to(wards) them for to come (in): come to(wards) [the] land: country/planet which I to give: give to/for you and to keep [the] land: country/planet Sabbath to/for LORD
3 Kwa miaka sita mtapanda mazao katika mashamba yenu, nanyi kwa miaka sita mtaikata mizabibu yenu matawi na kuvuna mazao yake.
six year to sow land: country your and six year to prune vineyard your and to gather [obj] produce her
4 Lakini mwaka wa saba nchi lazima iwe na Sabato ya mapumziko, Sabato kwa Bwana. Msipande mbegu katika mashamba yenu, wala msikate mizabibu yenu matawi.
and in/on/with year [the] seventh Sabbath sabbath observance to be to/for land: country/planet Sabbath to/for LORD land: country your not to sow and vineyard your not to prune
5 Msivune na kuweka akiba kinachoota chenyewe, wala kuvuna na kusindika zabibu ambayo hamkuhudumia mashamba yake. Nchi lazima iwe na mwaka wa mapumziko.
[obj] aftergrowth harvest your not to reap and [obj] grape Nazirite your not to gather/restrain/fortify year sabbath observance to be to/for land: country/planet
6 Chochote nchi itoacho katika mwaka wa Sabato kitakuwa chakula chenu wenyewe, watumishi wenu wa kiume na wa kike, mfanyakazi aliyeajiriwa, na mkazi wa muda anayeishi miongoni mwenu,
and to be Sabbath [the] land: country/planet to/for you to/for food to/for you and to/for servant/slave your and to/for maidservant your and to/for hired your and to/for sojourner your [the] to sojourn with you
7 vilevile malisho ya mifugo yenu na wanyama pori katika nchi yenu. Chochote nchi itakachozalisha kinaweza kuliwa.
and to/for animal your and to/for living thing which in/on/with land: country/planet your to be all produce her to/for to eat
8 “‘Hesabu Sabato saba za miaka, yaani miaka saba mara saba, ili Sabato saba za miaka utakuwa muda wa miaka arobaini na tisa.
and to recount to/for you seven Sabbath year seven year seven beat and to be to/for you day seven Sabbath [the] year nine and forty year
9 Ndipo tarumbeta itapigwa kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho, piga tarumbeta katika nchi yako yote.
and to pass trumpet shout in/on/with month [the] seventh in/on/with ten to/for month in/on/with day [the] atonement to pass trumpet in/on/with all land: country/planet your
10 Mwaka wa hamsini mtauweka wakfu na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakazi wake wote. Itakuwa ni yubile kwenu; kila mmoja wenu atairudia mali ya jamaa yake, na kila mmoja kurudi kwenye ukoo wake.
and to consecrate: consecate [obj] year [the] fifty year and to call: call out liberty in/on/with land: country/planet to/for all to dwell her jubilee/horn he/she/it to be to/for you and to return: return man: anyone to(wards) possession his and man: anyone to(wards) family his to return: return
11 Mwaka wa hamsini utakuwa yubile kwenu, msipande wala msivune kile kiotacho chenyewe, au kuvuna zabibu zisizohudumiwa.
jubilee/horn he/she/it year [the] fifty year to be to/for you not to sow and not to reap [obj] aftergrowth her and not to gather/restrain/fortify [obj] Nazirite her
12 Kwa kuwa ni yubile, nayo itakuwa takatifu kwenu; mtakula tu kile kilichotoka moja kwa moja mashambani.
for jubilee/horn he/she/it holiness to be to/for you from [the] land: country to eat [obj] produce her
13 “‘Katika huu Mwaka wa Yubile, kila mmoja atarudi kwenye mali yake mwenyewe.
in/on/with year [the] jubilee/horn [the] this to return: return man: anyone to(wards) possession his
14 “‘Ikiwa utauza ardhi kwa mmoja wa wazawa wa nchi yako, au ukinunua ardhi kutoka kwake, mmoja asimpunje mwingine.
and for to sell sale to/for neighbor your or to buy from hand: to neighbor your not to oppress man: anyone [obj] brother: compatriot his
15 Utanunua ardhi kwa mzawa wa nchi yako kwa misingi ya hesabu ya miaka baada ya Yubile. Naye ataiuza kwako kwa misingi ya hesabu ya miaka iliyobaki kwa kuvuna mavuno.
in/on/with number year after [the] jubilee/horn to buy from with neighbor your in/on/with number year produce to sell to/for you
16 Miaka inapokuwa mingi, utaongeza bei, nayo miaka ikiwa michache, utapunguza bei, kwa sababu kile anachokuuzia kwa hakika ni hesabu ya mazao.
to/for lip: according abundance [the] year to multiply purchase his and to/for lip: according to diminish [the] year to diminish purchase his for number produce he/she/it to sell to/for you
17 Mmoja asimpunje mwingine, bali utamcha Mungu wako. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.
and not to oppress man: anyone [obj] neighbor his and to fear: revere from God your for I LORD God your
18 “‘Fuateni amri zangu, mwe waangalifu kutii amri zangu, nanyi mtaishi salama katika nchi.
and to make: do [obj] statute my and [obj] justice: judgement my to keep: obey and to make: do [obj] them and to dwell upon [the] land: country/planet to/for security
19 Kisha nchi itazaa matunda yake, nanyi mtakula na kushiba na kuishi humo kwa salama.
and to give: give [the] land: country/planet fruit her and to eat to/for satiety and to dwell to/for security upon her
20 Mwaweza kuuliza, “Tutakula nini katika mwaka wa saba ikiwa hatutapanda wala kuvuna mazao yetu?”
and for to say what? to eat in/on/with year [the] seventh look! not to sow and not to gather [obj] produce our
21 Nitawapelekeeni baraka ya pekee katika mwaka wa sita, kwamba nchi itazalisha mazao ya kutosha kwa miaka mitatu.
and to command [obj] blessing my to/for you in/on/with year [the] sixth and to make [obj] [the] produce to/for three [the] year
22 Mnapopanda mwaka wa nane, mtakula mavuno ya miaka iliyopita. Pia mtaendelea kuyala mazao hayo hadi mvune mavuno ya mwaka wa tisa.
and to sow [obj] [the] year [the] eighth and to eat from [the] produce old till [the] year [the] ninth till to come (in): come produce her to eat old
23 “‘Kamwe ardhi isiuzwe kwa mkataba wa kudumu, kwa sababu nchi ni mali yangu, nanyi ni wageni na wapangaji wangu.
and [the] land: country/planet not to sell to/for finality for to/for me [the] land: country/planet for sojourner and sojourner you(m. p.) with me me
24 Katika nchi yote mtakayoshika kuwa milki yenu, ni lazima mtoe ukombozi wa ardhi.
and in/on/with all land: country/planet possession your redemption to give: allow to/for land: country/planet
25 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini na akauza baadhi ya mali yake, ndugu yake wa karibu atakuja na kukomboa kile ndugu yako alichokiuza.
for be poor brother: compatriot your and to sell from possession his and to come (in): come to redeem: redeem his [the] near to(wards) him and to redeem: redeem [obj] sale brother: compatriot his
26 Iwapo mtu huyo hana jamaa wa karibu wa kukomboa mali hiyo kwa ajili yake, lakini yeye mwenyewe akafanikiwa na kupata mali itoshayo kuikomboa,
and man: anyone for not to be to/for him to redeem: redeem and to overtake hand: themselves his and to find like/as sufficiency redemption his
27 ataamua tena thamani yake kwa miaka tangu alipoiuza, na kurudisha kiasi kilichobaki cha thamani kwa mtu ambaye alikuwa amemuuzia mali hiyo, naye ataweza kuirudia mali yake.
and to devise: count [obj] year sale his and to return: return [obj] [the] to remain to/for man which to sell to/for him and to return: return to/for possession his
28 Lakini kama hatapata njia ya kumlipa mnunuzi, ile mali aliyouza itabaki kumilikiwa na mnunuzi mpaka Mwaka wa Yubile. Mali hiyo itarudishwa mwaka wa Yubile, naye ataweza kuirudia mali yake.
and if not to find hand: power his sufficiency to return: pay to/for him and to be sale his in/on/with hand: power [the] to buy [obj] him till year [the] jubilee/horn and to come out: send in/on/with jubilee/horn and to return: return to/for possession his
29 “‘Ikiwa mtu atauza nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta, yeye anayo haki ya kuikomboa mwaka mzima baada ya mauzo ya hiyo nyumba. Wakati huo anaweza kuikomboa.
and man: anyone for to sell house: home seat city wall and to be redemption his till to finish year sale his day: year to be redemption his
30 Ikiwa haikukombolewa kabla ya mwaka mmoja kamili kupita, nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya mnunuzi na wazao wake. Haitarudishwa mwaka wa Yubile.
and if not to redeem: redeem till to fill to/for him year unblemished: complete and to arise: establish [the] house: home which in/on/with city which (to/for him *Q(K)*) wall to/for finality to/for to buy [obj] him to/for generation his not to come out: send in/on/with jubilee/horn
31 Lakini nyumba zilizo vijijini bila ya kuwa na kuta zilizozizunguka zitahesabiwa kama mashamba. Zinaweza kukombolewa, nazo zirudishwe katika mwaka wa Yubile.
and house: home [the] village which nothing to/for them wall around upon land: country [the] land: country/planet to devise: count redemption to be to/for him and in/on/with jubilee/horn to come out: send
32 “‘Walawi siku zote wana haki ya kukomboa nyumba zao katika miji ya Walawi wanayoimiliki.
and city [the] Levi house: home city possession their redemption forever: any time to be to/for Levi
33 Kwa hiyo mali ya Mlawi inaweza kukombolewa, yaani nyumba iliyouzwa katika mji wowote wanaoushikilia itarudishwa mwaka wa Yubile, kwa sababu nyumba zilizo katika miji ya Walawi ni mali yao miongoni mwa Waisraeli.
and which to redeem: redeem from [the] Levi and to come out: send sale house: home and city possession his in/on/with jubilee/horn for house: home city [the] Levi he/she/it possession their in/on/with midst son: descendant/people Israel
34 Lakini nchi ya malisho iliyo mali ya miji yao kamwe isiuzwe, ni milki yao ya kudumu.
and land: country pasture city their not to sell for possession forever: enduring he/she/it to/for them
35 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini, naye akashindwa kujitegemeza mwenyewe katikati yako, msaidie kama vile ambavyo ungelimsaidia mgeni au kama mkazi wa muda, ili aweze kuendelea kuishi katikati yako.
and for be poor brother: compatriot your and to shake hand: themselves his with you and to strengthen: strengthen in/on/with him sojourner and sojourner and to live with you
36 Usichukue riba wala faida yoyote kutoka kwake, bali utamwogopa Mungu wako, ili mzawa wa nchi yako aweze kuendelea kuishi katikati yako.
not to take: take from with him interest and increment and to fear: revere from God your and to live brother: compatriot your with you
37 Usimkopeshe fedha ili alipe na riba, wala usimuuzie chakula kwa faida.
[obj] silver: money your not to give: give to/for him in/on/with interest and in/on/with greatness not to give: give food your
38 Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekuleta kutoka nchi ya Misri nikupe nchi ya Kanaani, nami niwe Mungu wako.
I LORD God your which to come out: send [obj] you from land: country/planet Egypt to/for to give: give to/for you [obj] land: country/planet Canaan to/for to be to/for you to/for God
39 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini katikati yako, naye akajiuza kwako, usimfanye atumike kama mtumwa.
and for be poor brother: compatriot your with you and to sell to/for you not to serve in/on/with him service servant/slave
40 Atatendewa kama mfanyakazi aliyeajiriwa, au kama mkazi wa muda katikati yako, naye atatumika mpaka Mwaka wa Yubile.
like/as hired like/as sojourner to be with you till year [the] jubilee/horn to serve with you
41 Ndipo yeye na watoto wake wataachiwa, naye atarudi kwa watu wa ukoo wake, na kwenye mali ya baba zake.
and to come out: come from from with you he/she/it and son: child his with him and to return: return to(wards) family his and to(wards) possession father his to return: return
42 Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu niliowaleta kutoka nchi ya Misri, kamwe wasiuzwe kama watumwa.
for servant/slave my they(masc.) which to come out: send [obj] them from land: country/planet Egypt not to sell sale servant/slave
43 Usiwatawale kwa ukatili, lakini utamcha Mungu wako.
not to rule in/on/with him in/on/with severity and to fear: revere from God your
44 “‘Watumwa wako wa kiume na wa kike watatoka katika mataifa yanayokuzunguka; kutoka kwao waweza kununua watumwa.
and servant/slave your and maidservant your which to be to/for you from with [the] nation which around you from them to buy servant/slave and maidservant
45 Pia waweza kununua baadhi ya wakazi wa muda wanaoishi katikati yako, na jamaa ya koo zao waliozaliwa katika nchi yako, nao watakuwa mali yako.
and also from son: descendant/people [the] sojourner [the] to sojourn with you from them to buy and from family their which with you which to beget in/on/with land: country/planet your and to be to/for you to/for possession
46 Hao waweza kuwarithisha watoto wako kuwa urithi wao, na wanaweza kuwafanya watumwa maisha yao yote, lakini usiwatawale ndugu zako Waisraeli kwa ukatili.
and to inherit [obj] them to/for son: child your after you to/for to possess: possess possession to/for forever: enduring in/on/with them to serve and in/on/with brother: male-sibling your son: descendant/people Israel man: anyone in/on/with brother: compatriot his not to rule in/on/with him in/on/with severity
47 “‘Ikiwa mgeni au mkazi wa muda katikati yako atakuwa tajiri, na mmoja wa wazawa wa nchi yako akawa maskini, naye akajiuza kwa yule mgeni anayeishi katikati yako, au kwa mmoja wa jamaa wa koo za wageni,
and for to overtake hand: themselves sojourner and sojourner with you and be poor brother: compatriot your with him and to sell to/for sojourner sojourner with you or to/for descendant family sojourner
48 anayo haki ya kukombolewa baada ya kujiuza. Mmoja wa jamaa zake aweza kumkomboa:
after to sell redemption to be to/for him one from brother: male-relative his to redeem: redeem him
49 Mjomba wake, au binamu yake, au yeyote aliye ndugu wa damu katika ukoo wake aweza kumkomboa. Au ikiwa atafanikiwa, anaweza kujikomboa mwenyewe.
or beloved: male relative his or son: descendant/people beloved: male relative his to redeem: redeem him or from flesh flesh his from family his to redeem: redeem him or to overtake hand: themselves his and to redeem: redeem
50 Yeye na huyo aliyemnunua watahesabu muda kuanzia mwaka aliojiuza hadi Mwaka wa Yubile. Mahali pa kuanzia bei ya kuachiwa kwake itakadiriwa kwa ujira unaolipwa mfanyakazi aliyeajiriwa kwa idadi ya hiyo miaka.
and to devise: count with to buy him from year to sell he to/for him till year [the] jubilee/horn and to be silver: price sale his in/on/with number year like/as day hired to be with him
51 Ikiwa imebaki miaka mingi, ni lazima atalipia ukombozi wake fungu kubwa la bei iliyolipwa kumnunua yeye.
if still many in/on/with year to/for lip: according their to return: pay redemption his from silver: price purchase his
52 Ikiwa miaka iliyobaki ni michache kufikia Mwaka wa Yubile, atafanya hesabu yake, naye atalipa malipo yanayostahili kwa ajili ya ukombozi wake.
and if little to remain in/on/with year till year [the] jubilee/horn and to devise: count to/for him like/as lip: according year his to return: pay [obj] redemption his
53 Atatendewa kama mtu wa kuajiriwa mwaka hadi mwaka; lazima uone kwamba yule aliyemnunua hamtawali kwa ukatili.
like/as hired year in/on/with year to be with him not to rule him in/on/with severity to/for eye: seeing your
54 “‘Hata ikiwa hakukombolewa kwa njia mojawapo ya hizi, yeye na watoto wake wataachiwa katika Mwaka wa Yubile,
and if not to redeem: redeem in/on/with these and to come out: send in/on/with year [the] jubilee/horn he/she/it and son: child his with him
55 kwa maana Waisraeli ni mali yangu kama watumishi. Wao ni watumishi wangu, niliowatoa kutoka nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.
for to/for me son: descendant/people Israel servant/slave servant/slave my they(masc.) which to come out: send [obj] them from land: country/planet Egypt I LORD God your

< Mambo ya Walawi 25 >