< Mambo ya Walawi 25 >

1 Bwana akamwambia Mose katika Mlima Sinai,
Og HERREN talede til Moses paa Sinaj Bjerg og sagde:
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapa ninyi, nchi yenyewe ni lazima ishike Sabato kwa ajili ya Bwana.
Tal til Israeliterne og sig til dem: Naar I kommer til det Land, jeg vil give eder, skal Landet holde Sabbatshvile for. HERREN.
3 Kwa miaka sita mtapanda mazao katika mashamba yenu, nanyi kwa miaka sita mtaikata mizabibu yenu matawi na kuvuna mazao yake.
Seks Aar skal du besaa din Mark, og seks Aar skal du beskære din Vingaard og indsamle Landets Afgrøde;
4 Lakini mwaka wa saba nchi lazima iwe na Sabato ya mapumziko, Sabato kwa Bwana. Msipande mbegu katika mashamba yenu, wala msikate mizabibu yenu matawi.
men i det syvende Aar skal Landet have en fuldkommen Sabbatshvile, en Sabbat for HERREN; din Mark maa du ikke besaa, og din Vingaard maa du ikke beskære.
5 Msivune na kuweka akiba kinachoota chenyewe, wala kuvuna na kusindika zabibu ambayo hamkuhudumia mashamba yake. Nchi lazima iwe na mwaka wa mapumziko.
Det selvgroede efter din Høst maa du ikke høste, og Druerne paa de ubeskaarne Vinstokke maa du ikke plukke; det skal være et Sabbatsaar for Landet.
6 Chochote nchi itoacho katika mwaka wa Sabato kitakuwa chakula chenu wenyewe, watumishi wenu wa kiume na wa kike, mfanyakazi aliyeajiriwa, na mkazi wa muda anayeishi miongoni mwenu,
Hvad der gror af sig selv, medens Landet holder Sabbat, skal tjene eder til Føde, dig selv, din Træl og din Trælkvinde, din Daglejer og den indvandrede hos dig, dem, der bor som fremmede hos dig;
7 vilevile malisho ya mifugo yenu na wanyama pori katika nchi yenu. Chochote nchi itakachozalisha kinaweza kuliwa.
dit Kvæg og de vilde Dyr i dit Land skal hele Afgrøden tjene til Føde.
8 “‘Hesabu Sabato saba za miaka, yaani miaka saba mara saba, ili Sabato saba za miaka utakuwa muda wa miaka arobaini na tisa.
Og du skal tælle dig syv Aarsabbater frem, syv Gange syv Aar, saa de syv Aarsabbater udgør et Tidsrum af ni og fyrretyve Aar.
9 Ndipo tarumbeta itapigwa kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho, piga tarumbeta katika nchi yako yote.
Saa skal du lade Alarmhornet lyde rundt om paa den tiende Dag i den syvende Maaned; paa Forsoningsdagen skal I lade Hornet lyde rundt om i hele eders Land.
10 Mwaka wa hamsini mtauweka wakfu na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakazi wake wote. Itakuwa ni yubile kwenu; kila mmoja wenu atairudia mali ya jamaa yake, na kila mmoja kurudi kwenye ukoo wake.
Og I skal hellige det halvtredsindstyvende Aar og udraabe Frigivelse i Landet for alle Indbyggerne; et Jubelaar skal det være eder; enhver af eder skal vende tilbage til sin Ejendom, og enhver af eder skal vende tilbage til sin Slægt;
11 Mwaka wa hamsini utakuwa yubile kwenu, msipande wala msivune kile kiotacho chenyewe, au kuvuna zabibu zisizohudumiwa.
et Jubelaar skal dette Aar, det halvtredsindstyvende, være eder; I maa ikke saa og ikke høste, hvad der gror af sig selv i det, eller plukke Druer af de ubeskaarne Vinstokke;
12 Kwa kuwa ni yubile, nayo itakuwa takatifu kwenu; mtakula tu kile kilichotoka moja kwa moja mashambani.
thi det er et Jubelaar, helligt skal det være eder; I skal spise, hvad Marken bærer af sig selv.
13 “‘Katika huu Mwaka wa Yubile, kila mmoja atarudi kwenye mali yake mwenyewe.
I Jubelaaret skal enhver af eder vende tilbage til sin Ejendom.
14 “‘Ikiwa utauza ardhi kwa mmoja wa wazawa wa nchi yako, au ukinunua ardhi kutoka kwake, mmoja asimpunje mwingine.
Naar du sælger din Næste noget eller køber noget af ham, maa I ikke forurette hinanden.
15 Utanunua ardhi kwa mzawa wa nchi yako kwa misingi ya hesabu ya miaka baada ya Yubile. Naye ataiuza kwako kwa misingi ya hesabu ya miaka iliyobaki kwa kuvuna mavuno.
Naar du køber noget af din Næste, skal der regnes med Aarene siden sidste Jubelaar; naar han sælger dig noget, skal der regnes med Afgrøderne indtil næste Jubelaar.
16 Miaka inapokuwa mingi, utaongeza bei, nayo miaka ikiwa michache, utapunguza bei, kwa sababu kile anachokuuzia kwa hakika ni hesabu ya mazao.
Jo flere Aar der er tilbage, des højere maa du sætte Prisen, jo færre, des lavere, thi hvad han sælger dig, er et vist Antal Afgrøder.
17 Mmoja asimpunje mwingine, bali utamcha Mungu wako. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.
Ingen af eder maa forurette sin Næste; du skal frygte din Gud, thi jeg er HERREN din Gud!
18 “‘Fuateni amri zangu, mwe waangalifu kutii amri zangu, nanyi mtaishi salama katika nchi.
I skal gøre efter mine Anordninger og holde mine Lovbud, saa I gør efter dem; saa skal I bo trygt i Landet,
19 Kisha nchi itazaa matunda yake, nanyi mtakula na kushiba na kuishi humo kwa salama.
og Landet skal give sin Frugt, saa I kan spise eder mætte og bo trygt deri.
20 Mwaweza kuuliza, “Tutakula nini katika mwaka wa saba ikiwa hatutapanda wala kuvuna mazao yetu?”
Men naar I siger: »Hvad skal vi da spise i det syvende Aar, naar vi hverken saar eller indsamler vor Afgrøde?«
21 Nitawapelekeeni baraka ya pekee katika mwaka wa sita, kwamba nchi itazalisha mazao ya kutosha kwa miaka mitatu.
saa vil jeg opbyde min Velsignelse til Bedste for eder i det sjette Aar, saa det bærer Afgrøde for de tre Aar;
22 Mnapopanda mwaka wa nane, mtakula mavuno ya miaka iliyopita. Pia mtaendelea kuyala mazao hayo hadi mvune mavuno ya mwaka wa tisa.
i det ottende Aar skal I saa, men I skal leve af gammelt Korn af den sidste Afgrøde indtil det niende Aar; indtil dets Afgrøde kommer, skal I leve af gammelt Korn.
23 “‘Kamwe ardhi isiuzwe kwa mkataba wa kudumu, kwa sababu nchi ni mali yangu, nanyi ni wageni na wapangaji wangu.
Jorden i Landet maa I ikke sælge uigenkaldeligt; thi mig tilhører Landet, I er kun fremmede og indvandrede hos mig;
24 Katika nchi yote mtakayoshika kuwa milki yenu, ni lazima mtoe ukombozi wa ardhi.
overalt i det Land, I faar i Eje, skal I sørge for, at Jorden kan indløses.
25 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini na akauza baadhi ya mali yake, ndugu yake wa karibu atakuja na kukomboa kile ndugu yako alichokiuza.
Naar din Broder kommer i Trang, saa han maa sælge noget af sin Ejendom, skal hans nærmeste Slægtning melde sig som Løser for ham og indløse, hvad hans Broder har solgt.
26 Iwapo mtu huyo hana jamaa wa karibu wa kukomboa mali hiyo kwa ajili yake, lakini yeye mwenyewe akafanikiwa na kupata mali itoshayo kuikomboa,
Hvis en ingen Løser har, men selv bliver i Stand til at skaffe den fornødne Løsesum,
27 ataamua tena thamani yake kwa miaka tangu alipoiuza, na kurudisha kiasi kilichobaki cha thamani kwa mtu ambaye alikuwa amemuuzia mali hiyo, naye ataweza kuirudia mali yake.
skal han udregne, hvor mange Aar der er gaaet siden Salget, og kun tilbagebetale Manden der købte det, for den Tid, der er tilbage, og derpaa igen overtage sin Ejendom.
28 Lakini kama hatapata njia ya kumlipa mnunuzi, ile mali aliyouza itabaki kumilikiwa na mnunuzi mpaka Mwaka wa Yubile. Mali hiyo itarudishwa mwaka wa Yubile, naye ataweza kuirudia mali yake.
Er han derimod ikke i Stand til at skaffe den fornødne Sum til Tilbagebetalingen, saa skal det, han har solgt, blive i Køberens Eje til Jubelaaret; men i Jubelaaret bliver det frit, saa han atter kan overtage sin Ejendom.
29 “‘Ikiwa mtu atauza nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta, yeye anayo haki ya kuikomboa mwaka mzima baada ya mauzo ya hiyo nyumba. Wakati huo anaweza kuikomboa.
Naar en Mand sælger et Beboelseshus i en By med Mure om, gælder hans Indløsningsret kun et fuldt Aar efter Salget; hans Indløsningsret gælder et Aar.
30 Ikiwa haikukombolewa kabla ya mwaka mmoja kamili kupita, nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya mnunuzi na wazao wake. Haitarudishwa mwaka wa Yubile.
Hvis derfor Indløsning ikke har fundet Sted, før et fuldt Aar er omme, gaar Huset i Byen med Mure om uigenkaldeligt over i Køberens og hans Efterkommeres Eje; det bliver ikke frit i Jubelaaret.
31 Lakini nyumba zilizo vijijini bila ya kuwa na kuta zilizozizunguka zitahesabiwa kama mashamba. Zinaweza kukombolewa, nazo zirudishwe katika mwaka wa Yubile.
Derimod henregnes Huse i Landsbyer, der ikke er omgivne af Mure, til Marklandet; for dem gælder Indløsningsretten, og i Jubelaaret bliver de fri.
32 “‘Walawi siku zote wana haki ya kukomboa nyumba zao katika miji ya Walawi wanayoimiliki.
Men med Hensyn til Leviternes Byer, Husene i de Byer, der tilhører dem, da gælder der en ubegrænset Indløsningsret for Leviterne;
33 Kwa hiyo mali ya Mlawi inaweza kukombolewa, yaani nyumba iliyouzwa katika mji wowote wanaoushikilia itarudishwa mwaka wa Yubile, kwa sababu nyumba zilizo katika miji ya Walawi ni mali yao miongoni mwa Waisraeli.
og naar en af Leviterne ikke gør sin Indløsningsret gældende, bliver Huset, han solgte, i de Byer, der tilhører dem, frit i Jubelaaret, thi Husene i Leviternes Byer er deres Ejendom blandt Israeliterne.
34 Lakini nchi ya malisho iliyo mali ya miji yao kamwe isiuzwe, ni milki yao ya kudumu.
Heller ikke maa Græsmarkerne, der hører til deres Byer, sælges, thi de tilhører dem som evigt Eje.
35 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini, naye akashindwa kujitegemeza mwenyewe katikati yako, msaidie kama vile ambavyo ungelimsaidia mgeni au kama mkazi wa muda, ili aweze kuendelea kuishi katikati yako.
Naar din Broder i dit Nabolag kommer i Trang og ikke kan bjærge Livet, skal du holde ham oppe; som fremmed og indvandret skal han leve hos dig.
36 Usichukue riba wala faida yoyote kutoka kwake, bali utamwogopa Mungu wako, ili mzawa wa nchi yako aweze kuendelea kuishi katikati yako.
Du maa ikke tage Rente eller Opgæld af ham, men du skal frygte din Gud og lade din Broder leve hos dig;
37 Usimkopeshe fedha ili alipe na riba, wala usimuuzie chakula kwa faida.
du maa ikke laane ham Penge mod Renter eller give ham af din Føde mod Opgæld.
38 Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekuleta kutoka nchi ya Misri nikupe nchi ya Kanaani, nami niwe Mungu wako.
Jeg er HERREN eders Gud, som førte eder ud af Ægypten for at give eder Kana'ans Land, for at være eders Gud.
39 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini katikati yako, naye akajiuza kwako, usimfanye atumike kama mtumwa.
Naar din Broder i dit Nabolag kommer i Trang og han maa sælge sig selv til dig, maa du ikke lade ham arbejde som Træl,
40 Atatendewa kama mfanyakazi aliyeajiriwa, au kama mkazi wa muda katikati yako, naye atatumika mpaka Mwaka wa Yubile.
men han skal være hos dig som Daglejer eller indvandret; han skal arbejde hos dig til Jubelaaret.
41 Ndipo yeye na watoto wake wataachiwa, naye atarudi kwa watu wa ukoo wake, na kwenye mali ya baba zake.
Da skal han gives fri sammen med sine Børn og vende tilbage til sin Slægt og sine Fædres Ejendom,
42 Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu niliowaleta kutoka nchi ya Misri, kamwe wasiuzwe kama watumwa.
thi mine Trælle er de, som jeg førte ud af Ægypten; de maa ikke sælges, som man sælger Trælle.
43 Usiwatawale kwa ukatili, lakini utamcha Mungu wako.
Du maa ikke bruge din Magt over ham med Haardhed; du skal flygte din Gud.
44 “‘Watumwa wako wa kiume na wa kike watatoka katika mataifa yanayokuzunguka; kutoka kwao waweza kununua watumwa.
Men har du Brug for Trælle og Trælkvinder, skal du købe dem af de Folkeslag, der bor rundt om eder;
45 Pia waweza kununua baadhi ya wakazi wa muda wanaoishi katikati yako, na jamaa ya koo zao waliozaliwa katika nchi yako, nao watakuwa mali yako.
ogsaa af Børnene efter de indvandrede, der bor som fremmede hos eder, maa I købe og af deres Familier, som er hos eder, og som de har avlet i eders Land; de maa blive eders Ejendom,
46 Hao waweza kuwarithisha watoto wako kuwa urithi wao, na wanaweza kuwafanya watumwa maisha yao yote, lakini usiwatawale ndugu zako Waisraeli kwa ukatili.
og dem maa I lade gaa i Arv og Eje til eders Børn efter eder; dem maa I bruge som Trælle paa Livstid; men over Israeliterne, eders Brødre, maa du ikke bruge din Magt med Haardhed, Broder over Broder.
47 “‘Ikiwa mgeni au mkazi wa muda katikati yako atakuwa tajiri, na mmoja wa wazawa wa nchi yako akawa maskini, naye akajiuza kwa yule mgeni anayeishi katikati yako, au kwa mmoja wa jamaa wa koo za wageni,
Naar en fremmed eller en indvandret hos dig kommer til Velstand, og en af dine Brødre i hans Nabolag kommer i Trang, og han maa sælge sig til den fremmede eller den indvandrede hos dig eller til en Efterkommer af en fremmeds Slægt,
48 anayo haki ya kukombolewa baada ya kujiuza. Mmoja wa jamaa zake aweza kumkomboa:
saa gælder Indløsningsretten for ham efter Salget; en af hans Brødre maa indløse ham,
49 Mjomba wake, au binamu yake, au yeyote aliye ndugu wa damu katika ukoo wake aweza kumkomboa. Au ikiwa atafanikiwa, anaweza kujikomboa mwenyewe.
eller ogsaa maa hans Farbroder eller Fætter eller en anden kødelig Slægtning af hans Familie indløse ham; han maa ogsaa indløse sig selv, hvis han faar Evne dertil.
50 Yeye na huyo aliyemnunua watahesabu muda kuanzia mwaka aliojiuza hadi Mwaka wa Yubile. Mahali pa kuanzia bei ya kuachiwa kwake itakadiriwa kwa ujira unaolipwa mfanyakazi aliyeajiriwa kwa idadi ya hiyo miaka.
Da skal han sammen med den, der købte ham, udregne Tiden fra det Aar, han solgte sig til ham, til Jubelaaret, og Købesummen skal svare til det Aaremaal; hans Arbejdstid hos ham skal regnes som en Daglejers.
51 Ikiwa imebaki miaka mingi, ni lazima atalipia ukombozi wake fungu kubwa la bei iliyolipwa kumnunua yeye.
Er der endnu mange Aar tilbage, skal han i Løsesum udrede den tilsvarende Del af Købesummen.
52 Ikiwa miaka iliyobaki ni michache kufikia Mwaka wa Yubile, atafanya hesabu yake, naye atalipa malipo yanayostahili kwa ajili ya ukombozi wake.
Og er der kun faa Aar tilbage til Jubelaaret, skal han regne dermed og udrede sin Løsesum i Forhold til de Aar, han har tilbage.
53 Atatendewa kama mtu wa kuajiriwa mwaka hadi mwaka; lazima uone kwamba yule aliyemnunua hamtawali kwa ukatili.
Som en Aar for Aar lejet Daglejer skal han være hos ham; du maa ikke roligt se paa, at Køberen bruger sin Magt over ham med Haardhed.
54 “‘Hata ikiwa hakukombolewa kwa njia mojawapo ya hizi, yeye na watoto wake wataachiwa katika Mwaka wa Yubile,
Men indløses han ikke paa en af disse Maader, skal han frigives i Jubelaaret, baade han selv og hans Børn.
55 kwa maana Waisraeli ni mali yangu kama watumishi. Wao ni watumishi wangu, niliowatoa kutoka nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.
Thi mig tilhører Israeliterne som Trælle; mine Trælle er de, thi jeg førte dem ud af Ægypten. Jeg er HERREN eders Gud!

< Mambo ya Walawi 25 >