< Mambo ya Walawi 25 >
1 Bwana akamwambia Mose katika Mlima Sinai,
Sinai mon dawk, BAWIPA ni Mosi koe, nang ni Isarel miphunnaw koe patuen bout na dei pouh hane teh,
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapa ninyi, nchi yenyewe ni lazima ishike Sabato kwa ajili ya Bwana.
Kai ni na poe e ram dawk na pha awh toteh, Hote ram ni BAWIPA hanlah sabbath ayâ han.
3 Kwa miaka sita mtapanda mazao katika mashamba yenu, nanyi kwa miaka sita mtaikata mizabibu yenu matawi na kuvuna mazao yake.
Kum taruk touh thung law hoi misur takha na sak awh vaiteh, apawhik na pâkhueng awh han.
4 Lakini mwaka wa saba nchi lazima iwe na Sabato ya mapumziko, Sabato kwa Bwana. Msipande mbegu katika mashamba yenu, wala msikate mizabibu yenu matawi.
Kum sarinae kum teh BAWIPA hanlah sabbath kum, ram thung kaawm e pueng kâhat vaiteh, sabbath yanae kum lah ao. Law na sak mahoeh. Misur takha hai na rasoun mahoeh.
5 Msivune na kuweka akiba kinachoota chenyewe, wala kuvuna na kusindika zabibu ambayo hamkuhudumia mashamba yake. Nchi lazima iwe na mwaka wa mapumziko.
Law dawk ama pouk kapâw e apawhik hai na khi mahoeh. Na rasoun hoeh e misur hai na khi mahoeh. Ram pueng kâhatnae kum lah ao.
6 Chochote nchi itoacho katika mwaka wa Sabato kitakuwa chakula chenu wenyewe, watumishi wenu wa kiume na wa kike, mfanyakazi aliyeajiriwa, na mkazi wa muda anayeishi miongoni mwenu,
Ram thung sabbath kum nah ka tâcawt e apawhik pueng teh namamouh, napui hoi tongpa, na thaw ka tawk e hoi, nang koe kaawm e imyinnaw hoi,
7 vilevile malisho ya mifugo yenu na wanyama pori katika nchi yenu. Chochote nchi itakachozalisha kinaweza kuliwa.
ram thung kaawm e saring pueng ni ca hane kawi lah ao han.
8 “‘Hesabu Sabato saba za miaka, yaani miaka saba mara saba, ili Sabato saba za miaka utakuwa muda wa miaka arobaini na tisa.
Sabbath kum, kum sari touh na parei vaiteh, kum sari vai sari touh tie kum 49 akuep hnukkhu,
9 Ndipo tarumbeta itapigwa kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho, piga tarumbeta katika nchi yako yote.
Tha sari, hnin 10, yonthanae hnin dawk mongka hah ram pueng dawk ueng sak han.
10 Mwaka wa hamsini mtauweka wakfu na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakazi wake wote. Itakuwa ni yubile kwenu; kila mmoja wenu atairudia mali ya jamaa yake, na kila mmoja kurudi kwenye ukoo wake.
Aruipanganae kum hah thoung sak vaiteh, ram pueng dawk khoca pueng koe hloutnae pathang han. Jubili kum lah ao dawkvah tami pueng amae talai, amae phun koe a ban han.
11 Mwaka wa hamsini utakuwa yubile kwenu, msipande wala msivune kile kiotacho chenyewe, au kuvuna zabibu zisizohudumiwa.
Hote aruipanganae kum teh Jubili kum lah ao dawkvah law na sak mahoeh. ama pouk kapâw e hai na a mahoeh. Rasoun hoeh e misur takha dawk e a paw hai na khi awh mahoeh.
12 Kwa kuwa ni yubile, nayo itakuwa takatifu kwenu; mtakula tu kile kilichotoka moja kwa moja mashambani.
Jubili kum teh kathounge kum lah ao dawkvah law dawk e apawhik dueng ca han.
13 “‘Katika huu Mwaka wa Yubile, kila mmoja atarudi kwenye mali yake mwenyewe.
Jubili kum nateh tami pueng ni amae khoram lah a ban awh han.
14 “‘Ikiwa utauza ardhi kwa mmoja wa wazawa wa nchi yako, au ukinunua ardhi kutoka kwake, mmoja asimpunje mwingine.
Nangmouh ni buet touh hoi buet touh yorannae na sak pawiteh buet touh hoi buet touh kâyue awh hanh.
15 Utanunua ardhi kwa mzawa wa nchi yako kwa misingi ya hesabu ya miaka baada ya Yubile. Naye ataiuza kwako kwa misingi ya hesabu ya miaka iliyobaki kwa kuvuna mavuno.
Jubili kum aloum teh a ngai rae kumnaw apawhik a paw nahan a kum parei vaiteh yorannae na sak han.
16 Miaka inapokuwa mingi, utaongeza bei, nayo miaka ikiwa michache, utapunguza bei, kwa sababu kile anachokuuzia kwa hakika ni hesabu ya mazao.
Hottelah, a paw paw na kum parei hoi yo e lah ao dawkvah, kum ayoun apap e patetlah aphu payoun, paluen lahoi yoran han.
17 Mmoja asimpunje mwingine, bali utamcha Mungu wako. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.
Nangmouh teh buet touh hoi buet touh kâyue awh hanh. Na Cathut taket awh. Kai teh nangmae BAWIPA Cathut lah ka o.
18 “‘Fuateni amri zangu, mwe waangalifu kutii amri zangu, nanyi mtaishi salama katika nchi.
Nangmouh ni ka phunglam hah na tarawi pawiteh hote ram dawk lungmawng lahoi kho na sak awh han.
19 Kisha nchi itazaa matunda yake, nanyi mtakula na kushiba na kuishi humo kwa salama.
Talai ni hai apawhik a tâco sak vaiteh, kaboumlah na ca awh vaiteh, lungmawng lah kho na sak awh han.
20 Mwaweza kuuliza, “Tutakula nini katika mwaka wa saba ikiwa hatutapanda wala kuvuna mazao yetu?”
Nangmouh ni hai asari kum nah, kaimouh ni bangtelamaw ka ca awh han. Law ka sak awh hoeh. Apawhik hai ka pâkhueng awh hoeh na tet awh pawiteh,
21 Nitawapelekeeni baraka ya pekee katika mwaka wa sita, kwamba nchi itazalisha mazao ya kutosha kwa miaka mitatu.
A kum taruk nah, nangmouh yawhawinae na poe vaiteh, hote kum dawk kum thum touh hane apawhik ka tâco sak han.
22 Mnapopanda mwaka wa nane, mtakula mavuno ya miaka iliyopita. Pia mtaendelea kuyala mazao hayo hadi mvune mavuno ya mwaka wa tisa.
nangmouh ni a kum taroe nah law na sak teh a kum tako nah apawhik pâkhuengnae totouh a karuem e apawhik na ca awh han.
23 “‘Kamwe ardhi isiuzwe kwa mkataba wa kudumu, kwa sababu nchi ni mali yangu, nanyi ni wageni na wapangaji wangu.
Talai hah ayâ pou tawn sak hanelah, yawt hanh. Talai teh Kaie doeh. Nangmouh teh Kai koe kârayen e imyin lah na o awh.
24 Katika nchi yote mtakayoshika kuwa milki yenu, ni lazima mtoe ukombozi wa ardhi.
Nangmouh ni talai na tawn a e hmuen pueng bout ratangnae kâ na poe awh han.
25 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini na akauza baadhi ya mali yake, ndugu yake wa karibu atakuja na kukomboa kile ndugu yako alichokiuza.
Na hmaunawnghanaw ni roedeng boilah a tawn e talai yawt pawiteh, kahnai e hmaunawngha ni a yo e talai hah bout ratangnae kâ ao han.
26 Iwapo mtu huyo hana jamaa wa karibu wa kukomboa mali hiyo kwa ajili yake, lakini yeye mwenyewe akafanikiwa na kupata mali itoshayo kuikomboa,
Hote talai hah ka ratang hane buet touh hai awm hoehpawiteh, ka tawn karuem ni ama ni bout ratang thai pawiteh,
27 ataamua tena thamani yake kwa miaka tangu alipoiuza, na kurudisha kiasi kilichobaki cha thamani kwa mtu ambaye alikuwa amemuuzia mali hiyo, naye ataweza kuirudia mali yake.
A yonae kum hah a touk vaiteh, aphu yit touh bout poe naseh. Hote talai teh bout a coe han.
28 Lakini kama hatapata njia ya kumlipa mnunuzi, ile mali aliyouza itabaki kumilikiwa na mnunuzi mpaka Mwaka wa Yubile. Mali hiyo itarudishwa mwaka wa Yubile, naye ataweza kuirudia mali yake.
Bout poe thai hoehpawiteh, a yo e hno hah Jubili kum totouh ka ran e kut dawk ao sak han. Jubili kum nah tha pawiteh, hmaloe e katawnkung e kut dawk bout a pha han.
29 “‘Ikiwa mtu atauza nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta, yeye anayo haki ya kuikomboa mwaka mzima baada ya mauzo ya hiyo nyumba. Wakati huo anaweza kuikomboa.
Khopui dawk e im hah imkung ni yawt pawiteh, kum touh thung ratang thainae kâ ao sak han.
30 Ikiwa haikukombolewa kabla ya mwaka mmoja kamili kupita, nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya mnunuzi na wazao wake. Haitarudishwa mwaka wa Yubile.
Kum touh thung ratang thai hoehpawiteh, hote im ka ran e catounnaw ni pou a tawn han. Jubili kum ka phat nakunghai tha pouh mahoeh toe.
31 Lakini nyumba zilizo vijijini bila ya kuwa na kuta zilizozizunguka zitahesabiwa kama mashamba. Zinaweza kukombolewa, nazo zirudishwe katika mwaka wa Yubile.
Rapan ka tawn hoeh e kho dawk kaawm e im hah law patetlah a pouk vaiteh, ratang thainae kâ ao. Jubili kum pha toteh a tha pouh han.
32 “‘Walawi siku zote wana haki ya kukomboa nyumba zao katika miji ya Walawi wanayoimiliki.
Hat navah, Levihnaw ni a tawn e khopui hoi khopui dawk e imnaw teh nâtuek hai thoseh, ratang thainae kâ ao.
33 Kwa hiyo mali ya Mlawi inaweza kukombolewa, yaani nyumba iliyouzwa katika mji wowote wanaoushikilia itarudishwa mwaka wa Yubile, kwa sababu nyumba zilizo katika miji ya Walawi ni mali yao miongoni mwa Waisraeli.
Levih ni a tawn e im hoi kho thoseh, ayâ ni ran pawiteh, Jubili kum a pha toteh a tha han. Bangkongtetpawiteh, Isarel miphun dawk Levihnaw teh ama onae kho hoi im hloilah alouke hno tawn hoeh.
34 Lakini nchi ya malisho iliyo mali ya miji yao kamwe isiuzwe, ni milki yao ya kudumu.
Hateiteh, Levih kho dawk kaawm e imlawnaw yawt mahoeh. Pou a tawn awh han.
35 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini, naye akashindwa kujitegemeza mwenyewe katikati yako, msaidie kama vile ambavyo ungelimsaidia mgeni au kama mkazi wa muda, ili aweze kuendelea kuishi katikati yako.
Nange na hmaunawngha ni a roedeng lawi, imyin patetlah tho pawiteh, nang koe o sak hanlah na kabawp han.
36 Usichukue riba wala faida yoyote kutoka kwake, bali utamwogopa Mungu wako, ili mzawa wa nchi yako aweze kuendelea kuishi katikati yako.
Ahni koe apung na cat mahoeh. Na hmaunawngha hah, nang koe o sak hanelah, na Cathut taket loe.
37 Usimkopeshe fedha ili alipe na riba, wala usimuuzie chakula kwa faida.
Apung ngaihawi lahoi ahni koe tangka thoseh, canei thoseh na cawi mahoeh.
38 Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekuleta kutoka nchi ya Misri nikupe nchi ya Kanaani, nami niwe Mungu wako.
Kai ni Kanaan ram na poe awh teh, nangmae Cathut lah ka o nahanlah nangmouh Izip ram hoi na ka tâcawtkhai e nangmae BAWIPA Cathut doeh.
39 “‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini katikati yako, naye akajiuza kwako, usimfanye atumike kama mtumwa.
Na hmaunawngha ni a roedeng dawkvah nang koe kâyawt pawiteh, san patetlah na hno mahoeh.
40 Atatendewa kama mfanyakazi aliyeajiriwa, au kama mkazi wa muda katikati yako, naye atatumika mpaka Mwaka wa Yubile.
Ahni teh hlai e patetlah thoseh, imyin patetlah thoseh, nang koe ao vaiteh, Jubili kum totouh na thaw a tawk han.
41 Ndipo yeye na watoto wake wataachiwa, naye atarudi kwa watu wa ukoo wake, na kwenye mali ya baba zake.
Hat navah, ahni teh a canaw hoi a tâco vaiteh amae a hmaunawngha, a mintoenaw e talai koe lah bout a ban han.
42 Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu niliowaleta kutoka nchi ya Misri, kamwe wasiuzwe kama watumwa.
Bangkongtetpawiteh, ahnimouh teh Izip ram hoi ka tâcokhai e ka thaw ka tawk e lah ao dawkvah san lah o hanelah na yawt mahoeh.
43 Usiwatawale kwa ukatili, lakini utamcha Mungu wako.
Ahni teh puenghoi na rektap mahoeh. Na Cathut hah taket.
44 “‘Watumwa wako wa kiume na wa kike watatoka katika mataifa yanayokuzunguka; kutoka kwao waweza kununua watumwa.
Nang ni na tawn hane sannu sanpa teh na tengpam kaawm e Jentelnaw koe na ran han.
45 Pia waweza kununua baadhi ya wakazi wa muda wanaoishi katikati yako, na jamaa ya koo zao waliozaliwa katika nchi yako, nao watakuwa mali yako.
Hothloilah, nangmouh koe kho ka sak e alouk ram e taminaw thoseh, na ram dawk a khe e a canaw thoseh, na ran vaiteh na tawn han.
46 Hao waweza kuwarithisha watoto wako kuwa urithi wao, na wanaweza kuwafanya watumwa maisha yao yote, lakini usiwatawale ndugu zako Waisraeli kwa ukatili.
Ahnimanaw teh san dawk hoi ka khe e lah ao teh, nang hoi na canaw ni râw lah na tawn han. Na hmaunawngha, Isarel miphun dawk e tho pawiteh, buet touh hoi buet touh puenghoi na rektap mahoeh.
47 “‘Ikiwa mgeni au mkazi wa muda katikati yako atakuwa tajiri, na mmoja wa wazawa wa nchi yako akawa maskini, naye akajiuza kwa yule mgeni anayeishi katikati yako, au kwa mmoja wa jamaa wa koo za wageni,
Nangmouh koe kho ka sak e alouke tami ni a tawnta ei teh, ahnie teng kho ka sak e na hmaunawngha a roedeng teh, nang koe kho ka sak e alouke ram e taminaw koe thoseh, a ca catounnaw koehai thoseh, kâyawt awh pawiteh,
48 anayo haki ya kukombolewa baada ya kujiuza. Mmoja wa jamaa zake aweza kumkomboa:
Yo hnukkhu, bout ratang thainae kâ ao han. A hmaunawngha lah kaawm e buetbuet touh ni a ratang han.
49 Mjomba wake, au binamu yake, au yeyote aliye ndugu wa damu katika ukoo wake aweza kumkomboa. Au ikiwa atafanikiwa, anaweza kujikomboa mwenyewe.
A na hma, a panga, a hmaunawngha koehoi rei ka tâcawt e imthung buetbuet touh ni a ratang han. Ama ni ratang thai pawiteh a ratang han.
50 Yeye na huyo aliyemnunua watahesabu muda kuanzia mwaka aliojiuza hadi Mwaka wa Yubile. Mahali pa kuanzia bei ya kuachiwa kwake itakadiriwa kwa ujira unaolipwa mfanyakazi aliyeajiriwa kwa idadi ya hiyo miaka.
Bawi hoi sannaw teh yorannae kum dawk hoi kamtawng vaiteh, Jubili kum totouh kum a parei hnukkhu, a kum ayoun apap e patetlah thoseh, a hlainae tueng khet lahoi thoseh, aphu teh to han.
51 Ikiwa imebaki miaka mingi, ni lazima atalipia ukombozi wake fungu kubwa la bei iliyolipwa kumnunua yeye.
Jubili kum a pha hoehnahlan a thawtawknae kum ayoun apap e parei vaiteh,
52 Ikiwa miaka iliyobaki ni michache kufikia Mwaka wa Yubile, atafanya hesabu yake, naye atalipa malipo yanayostahili kwa ajili ya ukombozi wake.
A ngai rae a kumtha ayoun apap e patetlah ratang nahane aphu hah rannae phu dawk hoi rayu vaiteh bout a pâban han.
53 Atatendewa kama mtu wa kuajiriwa mwaka hadi mwaka; lazima uone kwamba yule aliyemnunua hamtawali kwa ukatili.
Ahni teh kum touh hnukkhu, kum touh hlai e patetlah ao han. Na hmaitung vah rektap lah awm hanh naseh.
54 “‘Hata ikiwa hakukombolewa kwa njia mojawapo ya hizi, yeye na watoto wake wataachiwa katika Mwaka wa Yubile,
Hottelah hoi ratang thai hoehpawiteh, Jubili kum a pha toteh, ahni teh a canaw hoi bawi e kut dawk hoi a hlout han.
55 kwa maana Waisraeli ni mali yangu kama watumishi. Wao ni watumishi wangu, niliowatoa kutoka nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.
Bangkongtetpawiteh, Isarelnaw teh ka thaw ka tawk e lah ao awh. Izip ram hoi ka tâcokhai e ka thaw ka tawk e lah ao awh. Kai teh nangmae BAWIPA Cathut doeh.